Sakata la Mpina na Waziri Bashe, nilivyoelewa kwa Lugha Rahisi


MAJIBU YA MASWALI YAKO:
1. Sheria inaruhusu viwanda vyenye jukumu la uzalishaji sukari pekee ndivyo viagize nakisi ya sukari (Gap Sugar) ya kiasi chochote baada ya Bodi ya sukari kuhakiki upungufu huo...

2. Ukishajua kuwa umepeleka ushahidi wako kwa mtu ambaye una uhakika kabisa kuwa hawezi kukutendea haki, atachakachua ushahidi wako, tumia mbinu ya kivita kum - outsmart kabla hajaleta uharibifu wowote kwako. Spika Dr Tulia Ackson ni miongoni mwa wafaidika wa ufisadi huu. Ndiyo maana kashituka na kufadhaika sana kwa namna ambavyo Mbunge Luhaga Mpina alivyom outsmart. Huyu angetumiwa na serikali kupindisha ukweli. Lakini kwa alichofanya Luhaga Mpina kuwawahi na kuweka ushahidi hadharani kwenye public, hilo limewashitua, kuwakasirisha na kuwapanikisha. Angalia uso wa Spika wakati anasoma tamko lake. She looked embarrassed..!!

3. Spika Dr Tulia Ackson ni mbaya, hilo halina ubishi. Na kama wewe huoni ubaya wa Spika huyu, hilo ni shauri lako lakini the truth will always stand. Na ukweli wake ni kuwa, Spika Dr Tulia Ackson siku zote hayuko upande wa wananchi. Yeye siku zote hutetea ubaya na kila aina ya upuuzi wa serikali na chama chake CCM likiwemo hili la ufisadi huu ndiko anakoelekea...

4. Usidhani kuwa Luhaga Mpina(MB) hajui anachokifanya pamoja na matokeo yake. Usifikiri kuwa huyu mbunge hazijui hizo kanuni. Lakini kama nilivyosema hapo juu, kwenye vita yoyote ni lazima uwe some steps ahead ktk mbinu za kivita dhidi ya unayepambana naye. Ni wazi kuwa Luhaga Mpina alishaona kuwa ziko mbinu chafu za serikali kuu - manipulate ushahidi wake. Au wewe hujui kuwa katibu wa bunge ni mteule wa Rais? Unadhani angekubali boss wake (Rais) aliyemteua kupitia kwa waziri wake (Bashe) kuingia kwenye kashfa ya sukari (sugar scandal) kama ilivyotokeaga miaka ile wakati wa serikali ya Mkapa waziri wa kilimo akiwa Iddi Simba?

5. Huyu Spika wako unayemtetea, afanye mambo mawili tu: MOSI; Ashughulike na Luhaga Mpina kwenye masuala ya kikanuni. PILI; akumbuke kuwa pamoja na makosa ya kikanuni ya mbunge Luhaga Mpina, ufisadi na wizi wa mapato ya nchi kupitia skandali la importation ya nakisi ya sukari (gap sugar) uko palepale na ni lazima bunge lishughulike nao. Wakipiga chenga kama ilivyo kawaida yao kulindana na kuteteana kwenye rushwa, ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka, basi wanasubiriwa huku nje ili wapigwe spana za uhakika!!
 
Uko sahihi kwa upande wako ila unakosea
 
Jibu la kwanza ndio nimelipokea
 
Mkuu umegonga spana kweli kweli πŸ‘
 

Ni mpumbavu na mjinga tu ndiye anaweza eti kumlaumu Mpina kwa kuamua kuanika uovu hadharani.
Kwa hiyo mtu akiamua kufichua maovu ni makosa?
Ni watu wenye nia ovu ndio watamuona Mpina kwamba kakosea kuweka uovu hadharani
 
Umeiweka vizuri zaidi kwa kifupi. Tukiwa wakweli mtu mwenye mtaji wa milioni moja ni kweli ana uwezo wa kuagiza mzigo wa 6.6bn?
 
Hata spika katumia muda mwingi kumsema Luhaga Mpina badala ya kilichowasilishwa
Muhimu Spika akanushe ushahidi ulioshiba uliotolewa na Mpina badala ya kubadilisha topic na kusema vitu personal. Mpina kajikita zaidi kwenye maslahi ya Taifa.

Yeye anazungumzia anaheshimika duniani kuliko nani? Ila amelifanyia nini hili Taifa?
 
Katusanua mkuu au wewe umelionaje hili swala Ni dogo kwamba tulipuuzie au wewe una maoni gani apo?

Binafsi na simama na mpina katusanua na kawaumbua vibaya Sanaa ccm.
 
Haki ya kuichagua itel na kuinyima kampuni nyingine inakuwa ni nini , nasaba, ukaribu au mtaji, uwezo wa kuhifadhi, njia za kuisambaza hiyo bidhaa au
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…