Uchaguzi 2020 Sakata la Sheikh Ponda na "masheikh rasmi"

Sasa Mzee wangu, ikitokea Wakatoliki au walutheri au wakristo wote kwa ujumla wakatangaza kura ni kwa flani(upande tofauti na aliochagua sheikh wako)kama alivyofanya Sheikh Ponda unadhani nini kitatokea baada ya matokeo!?
Hao wakatoliki na walutheri ni wa Tanzania hii au nchi nyingine.Hivi Katika Tanzania kuna mtu au jamii ambayo haijapitia chungu ya shubiri ya Huyu mungu wa chato?
 
mnapiga kelele Bakwata je kipindi cha mrisho mbona hakuwapa hizo haki zenu kama mjumbe kutoka kwenu.?
Kheee!!!

Sasa suala la Mrisho linatokea wapi?!

Hapa wanaozungumziwa ni madhalimu ya CCM bila kujali Ikulu yupo Mristo au Mwislamu!!

Ni haya madhalimu ya CCM ndiyo yanapoka haki za makundi mbalimbali!!

Kwamba eti Zanzibar sijui mbona mwezi wa Ramadhani hivi, mara vile inaonesha tena hujui watu wanajadili nini!!!!

Uliwahi kumuona huyo Sheikh Ponda huko Zanzibar aki-deal na hao Wakristo?!

Na ni watu wa aina yenu ndio ambao hadi kesho mnadhani Sheikh Ponda ana matatizo na Wakristo lakini kwa wanaofahamu wanajua Sheikh Ponda always tatizo lake limekuwa dhidi ya Serikali, BAKWATA na CCM!!

Ni kutokana na hilo, ndio maana harakati zake huwa haziangalii Ikulu yupo nani tofauti na viongozi wengine wa dini ambao wakiona Ikulu kuna rais wa dini yao, wanapiga kimya, wakiona asiye wa dini yao, basi matamko hayaishi!!!
 
Hujui lolote, mzee ponda ni mnufaika wa mali za waislam, aliponyang’anywa (tena waliosimamia arejeshe hizo mali na waislam wenzie waliokuwa wanamtuhumu), sasa kabaki kutumia udhaifu wenu kupandikiza chuki, na magaidi wote wanatumia hiyo mbinu, si unakumbuka mlivyokuwa mnaunga mkono ugaidi?
 
Mzee Mohamed unamaanisha hiyo 'shura ya maimamu' anayoiongoza sheikh Ponda ndio inatakiwa kuchukua nafasi ya Bakwata?
Shuura ya maimamu haihitaji kuwa au kuchukua nafasi ya Bakwata na matendo ya Bakwata yatabaki kibakwatabakwata.
Kuna tatizo ambalo linafunikwa kwa kudhani kuwa mapambio yanasaidia kutuliza hali mbovu.
 
Mtazamo wangu Tanganyika Kuna waislamu wachache wengi wana majina ya kiarabu lakini si waislamu.
Hauwezi kuwa chini ya Bakwata ukajiita muislamu bali wewe umejengwa kwenye taasisi iliyojichimbia katika mhimili mkubwa wa Ccm serikali.
 
Najiuliza, hivi aka ka branch ka siri-kali (BAKWATA) kwanini bado kaliendelea kutamalaki ktk kipindi cha Mzee Ruksa na pia ktk kipindi cha Baba Riz?
Utajiuliza sana kwa sababu huitazami fisiemu ambayo ni mlezi na muasisi wa "hako ka branch" fullstop
 
Khalfan Mrisho huwezi kumuita muislamu, yeye ndio aliyewaweka ndani masheikh wa Uamsho.

Khalfan licha ya kuwa ni Billionaire hajawahi kitimiza nguzo za uislamu kwenda kuhiji Maka wakati pesa anazo.

Khalfan ni kafir tu, tena bora hata yule mnafki Lipumba nimeshamuona kwenye Umra.
 
Sheikh Mkuu wa JF nimekusoma

situpi tena kura yangu
 
Mkuu Maalim Sheikh Mohamed Said , poleni sana ndugu zetu Waislamu wa Tanzania, kwa madhila yaliyowakuta, tangu baada ya kuvunjwa kwa EAMWS na serikali mwaka wa 1968 na Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir kukamatwa na kufukuzwa nchini na serikali kuwaundia Waislam BAKWATA, Waislam wameishi na kinyongo miaka yote sasa inafika nusu karne.

Kwenye hili la kunyoosha kidole upande fulani na kusema kuna adui wa Waislamu na adui wa Uislamu, naomba tuwe wakweli, na ukweli wa kwanza, naomba utuelimishe kidogo kumhusu Mufti wa kwanza wa Tanganyika na baadaye Tanzania, Sheikh Hassan bin Ameir,
  1. alikuwa ni mtu wa wapi?.
  2. Alikamatiwa wapi?
  3. Kwa kosa gani?
  4. Alikuzwa nchini na serikali, na kufukuziwa wapi?.
Tuanzie hapo ili tufike mahali tumjue adui halisi wa Waislamu ni nani, tusije kunyoosheana vidole, tukawashawishi ndugu zetu Waislamu, kupiga kura za chuki, kutokana na vinyongo bandia, kwa kudhani adui yao ni fulani kumbe sio kweli, huku kutakuwa ni kuwatendesha Waislamu wa Tanzania, dhambi ya ubaguzi, hao Waislamu wanaoishi kwa kinyongo dhidi ya utawala kwa miaka mingi, naomba pia waambiwe ukweli kuwa wasipeleke kura zao upande fulani kwasababu ya kinyongo cha miaka mingi, kwasababu hata huko watakapopelekehizo kura zao, zitapotea bure, hivyo sio tuu kuendelea kuishi na kinyongo, wataishi na kihoro!.

Dawa ya madhila, sio kuishi kwa kinyongo, bali ni kwa kukaa chini na watawala na kuyazungumza, tuyajenge, tuwe kitu kimoja!.
Na kwa vile kwa sasa mimi pia ni kada, naomba kuchukua fursa hii kuwaomba kura Waislamu wote wa Tanzania, kura ni JPM, na CCM, ndio pakee anaweza kumaliza madhila yote ya Waislamu, na hapa tulipo, nitamuomba Mwenyekiti wetu, kesho Jumatatu, awaachie huru wale Masheikh wote wa Uamsho wanaoshikiliwa, ili Jumanne waungane na familia zao, na Jumatano, Waislamu wote kwa sauti moja, wamshukuru kwa vitendo, aliyewaachia masheikh wa uamsho.
P

P
 
Na wakati sahihi kwa waislamu wote kuinuka sasa na kuungana pamoja kudai haki zetu. Sheikh Ponda ameonyesha njia.
Bakwata ni mpango mahususi wa makafir kuwadidimiza waislamu hapa Tanzania.
Mkuu Zanzibar-ASP , ungeweza kujenga hoja yako bila kutumia lugha ya maudhi ya kuwaita watu makafir!. Kwa mujibu wa Waislamu, Kafir ni mtu asiye na dini, sasa kwa vile serikali yetu haina dini, ni haina dini kwa maana ya a secular state na sio haina dini kwa maana ni kafir, tena jina kasir lina bado connotation meaning ukisema kafiri, Wakiristo tunakasirika kama unamaanisha ni ya Mwenyeenzi Mungu ni Islam tuu, nje ya hapo, wote ni ma makafiri!.
This is not a fair comment!,
P
 
Swali nzuri kbs Kaka yngu Nina Imani Mzee Sheikh Mohamed Said atakuletea majibu ila nami naomba nisaidie kujibu maswali haya maana umekuwa unakwepa kuni jibu.
1.lile swali lako Ikulu kwa Mh Rais John Joseph Pombe Magufuli ilikuwa ni Usalama wa Taifa upo kazini au?
2.kinachoendelea nchini ni kweli ukioni au ukabila kwanza mengine Baadae
3...

Sent from my ANE-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Haki huinua Taifa, Amani ni Tunda la Haki, Amani yaweza tunzwa hata kibabe tu. Lkn Haki, Haki, Haki!!
 
Unaposema utamuomba kesho mwenyekiti awaachie mashehe wa uamusho kwani wako ndani kwa amri au utashi wa mwenyekiti? je mkiwaachia bila kuwafikisha mahakamani na hatimae mahakama ndo iamue iwapo wana hatia au la je,huoni mtahalalisha madai kwamba wako ndani kwa makosa ya kubumba? Je huoni kitendo cha kuwaachia sasa kitawaudhi zaidi waislamu maana wataamini ndugu zao waliwekwa ndani kwa hila,na hivyo badala ya kuwaongezea kura watawanyima kura kwa dhuluma hiyo?
 
Mkuu Rubawa ,
  1. litafute lile swali, lisikilize tena, kama akili yako inakuwa muulizaji swali ni mtu wa Tiss na hilo ni swali kutoka kwa Tiss kwenda kwa CinC, then I just feel sorry for you!. Mtu wa Tiss anaweza kupandisha humu bandiko kama hili hili. TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!
  2. Kinachoendelea nchini kwa sasa, ni kusubiria siku na saa tukatimize wajibu wetu, ni kishindo kile kile cha 90% +, and I'm sorry for you, najua hautapiga kura kwasababu hukujiandikisha, ila wahimize ndugu zako, wasifanye majaribio kwenye urais, tumpe mitano tena, JPM.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…