Sakata la Yusuph Kagoma kusaini timu mbili Klabu ya Simba kukatwa alama

Sakata la Yusuph Kagoma kusaini timu mbili Klabu ya Simba kukatwa alama

Simba roho juu, huwenda waka-katwa alama ishu ya mchezaji Yusuph Kagoma kusaini Yanga kisha kuwatosa na kuibukia mitaa ya Msimbazi.
Mchambuzi na expert wa mambo ya usajili, Hans Rafael amedai kuwa Kamati ya sheria na hadhi za wachezaji, Leo asubuhi imesikiliza kesi ya kiungo wa Simba Yusuph Kagoma, na kuamuru mchezaji huyo asimame haraka kuitumikia klabu hiyo.

Yanga wao wamethibitisha kuwa hawajamsamehe Kagoma, na wanataka haki ifuatwe.

Pia Yanga wanashinikiza Simba wapokwe pointi sita za ligi ambazo walizipata kwa kumtumia mchezaji batili (Kagoma) kwenye mechi dhidi ya Tabora na Fountain Gate.

Sakata hili pia lilimuibua mdau wa michezo na Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba na kuzungumza uhalisia wa namna anvyofahamu sakata hili la Kagoma kusaini pande zote mbili.

Swali la kujiuliza aliwezaje kucheza mechi kama usajili wake ulikuwa na utata kuitumikia Simba SC?

Soma ==>Mwigulu awaomba viongozi wa Yanga wapotezee suala la Kagoma ili aweze kucheza Simba
Yaani mpira wa bongo kwenye usajili, mikataba kuna sakarakasi nyingi sana,ujinga huu wanaulea TFF.
 
Simba roho juu, huwenda waka-katwa alama ishu ya mchezaji Yusuph Kagoma kusaini Yanga kisha kuwatosa na kuibukia mitaa ya Msimbazi.
Mchambuzi na expert wa mambo ya usajili, Hans Rafael amedai kuwa Kamati ya sheria na hadhi za wachezaji, Leo asubuhi imesikiliza kesi ya kiungo wa Simba Yusuph Kagoma, na kuamuru mchezaji huyo asimame haraka kuitumikia klabu hiyo.

Yanga wao wamethibitisha kuwa hawajamsamehe Kagoma, na wanataka haki ifuatwe.

Pia Yanga wanashinikiza Simba wapokwe pointi sita za ligi ambazo walizipata kwa kumtumia mchezaji batili (Kagoma) kwenye mechi dhidi ya Tabora na Fountain Gate.

Sakata hili pia lilimuibua mdau wa michezo na Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba na kuzungumza uhalisia wa namna anvyofahamu sakata hili la Kagoma kusaini pande zote mbili.

Swali la kujiuliza aliwezaje kucheza mechi kama usajili wake ulikuwa na utata kuitumikia Simba SC?

Soma ==>Mwigulu awaomba viongozi wa Yanga wapotezee suala la Kagoma ili aweze kucheza Simba
Yanga wanaleta upumbavu wa propaganda za nje ya uwanja, mwaka huu ni ubaya ubwela na wamegundua hivyo wanatumia siasa za kijinga za nje ya uwanja.

Walishindwa kumnunua huyo Kagoma Simba wakaja na ofa nzuri zaidi wakapita nae na wao inawauma haswa ukizingatia ni mchezaji wa Singida timu ya Mwigulu Nchemba,

Yanga ndio wanaofanya watu wengi haswa vijana wa kisasa waichukie CCM kwa mambo ya kipumbavu kama haya. Kudhani kwamba wao ndio kila kitu kwenye nchi hii.
 
Kwaiyo kama wamelalamika Awana haki ya kusikilizwa? Au mlitakaje labda? Kama wameona mchezaji kakiuka Sheria za Mpira lazima walalamike kwanini waache? Mamlaka za Mpira ndizo zitaamua kama wako sahihi ama lah na sio kuwaelekeza wafuate matakwa ya mtu kwa manufaa yake, uyo dogo ni mtu mzima na anayo menejiment yake walifanya vile kusaini sehemu mbili kwa sababu zipi?
Ni siasa nyepesi za propaganda, ni mambo ya kawaida kwenye mpira wa bongo. Kama Mwigulu aliwaambia Yanga wamsamehe hizi kelele zinatoka wapi?.
 
Mpira wa miguu unaendeshwa kwa kanuni na taratibu zake sasa kuna mashabiki humu hawajui kuhusu mpira wao wanajua mihemko isiyokua na sababu mpira sio mapenzi et nilikukataa na kuanzisha mahusiano na mwingine pindi anasaini klabu mbili tofauti hakujua kama ni kosa?
Kama kuna shida kamati ya sheria na hadhi ya wachezaji wataamua kwa kufuata sheria sio kwa maneno ya mashabiki maandazi et haitaki Yanga wakati alisaini mkataba na Yanga..
 
mashabiki maandazi et haitaki Yanga wakati alisaini mkataba na Yanga..
Anayesimamia hizo sheria ni nani? Jee Kangoma alicheza bila ya kuwa na leseni. Na kama alikuwa na leseni nani aliitoa hiyo leseni kama si TFF na Bodi ya Ligi?

Zaidi ya yote FIFA ilishaagiza mambo ya pointi za mezani ni MARUFUKU na ndiyo maana watu wa FA wanahimizwa kuhakikisha kuwa mambo ya usajili yapo sawa kabla ya kutoa leseni.
 
Muwe mnaacha mihemko ya kijinga, kwaiyo kama kamati ya Sheria na hadhi za wachezaji wameona tatizo wangeacha tu wakakaa kimya? Uyo mchezaji inawezekana kweli alisaini pande zote na ndio maana suala lake limekuwa gumu, pia ni kwanini Simba walimchezesha mchezaji ambae bado wanajua usajili wake una matatizo?
Sidhani kama viongozi wa yanga na kamati yenyewe Awana akili au awazijui Sheria mpaka wakomae na kagoma aiwezekani, kama alisaini kotekote basi Sheria ifate mkondo wake na sio busara ili kutoka onto kwa wachezaji wote Wenye tamaa za kipumbavu na Simba wapokwe point ambazo mchezaji alihusika kwenye mechi walizoshinda, akuna cha msalia mtume apo!
Mwaka huu ni ubaya ubwela tu hakuna namna .Na bado , mwaka huu kila tundu lililopo kwenye mwili wa Amfibia lazima litowe milio kama si pwiii basi ni fwii!
 
Hahahaaa mpwaaaaaa tushaanza kuagizaaa brian viongozi wajingaaa walee wacha wafundishwe sheria
Yanga hii inayobwagwa kila siku huko FIFA ndiyo iwe na viongozi wanaojua sheria za mpira kuliko viongozi wa simba?

Hizo ni propoganda za kizamani sana za kutaka kuwatoa tu simba kwenye reli . Lakini mwaka huu ni ubaya ubwela tu hakuna namna
 
Anayesimamia hizo sheria ni nani? Jee Kangoma alicheza bila ya kuwa na leseni. Na kama alikuwa na leseni nani aliitoa hiyo leseni kama si TFF na Bodi ya Ligi?

Zaidi ya yote FIFA ilishaagiza mambo ya pointi za mezani ni MARUFUKU na ndiyo maana watu wa FA wanahimizwa kuhakikisha kuwa mambo ya usajili yapo sawa kabla ya kutoa leseni.
Yanga mna mbwembwe sana.

Viongozi wenu wameshachachawa wewe unajifanya huna hofu.
Kwa taarifa Yako viongozi wa Simba ni mabingwa wa ku kiuka taratibu kwa kutegemea wata bebwa na kundi kubwa la Viongozi wenye vinasaba vya Simba pale Tff.
bahati mbaya Kuna makosa ya kikanuni yakifanyika ata ao viongozi Wana shindwa kuwa beba.

Walimtangaza Lamek Lawi kwenye Official page kabla usajili wake hauja kamilika Tff waka potezea,
Wakamtambulisha Valentinon Mashaka wakati Bado anamkataba na Geita Tff wakalizima juukwa juu.

Waka Mtambulisha Awesu Awesu wakati Bado anamkataba na KMC Tff waka wabeba Simba.

Bahati mbaya wame mchezesha Yusufu Kagoma ambaye Alisha ingia mkataba wa awali na Yanga na Tukumbuke mikataba yote ya awali uwa inapelekwa Tff kwa kumbukumbu ili kusije kutokea utata.

Mchezaji alikua anajua kabisa kama anafanya Double signing lakini viongozi wenu wakamwambia wewe Sign tu mengine tuachie sisi na Ligi utacheza, na aya ndio madhara yake.

Uko nyuma Simba alishawahi kunyang'anywa point 3 kwa kumchezesha Musa Mgosi na kukosa Ubingwa.
Kwasasa Simba imemchezesha mchezaji ambaye ana double signing sijui Tff watafunika kanuni au watakuja na Sarakasi zipi kuibeba Simba.
Kuna Muda Mbeleko huchanika, Ingawa Tff walipambana ku adjust ratiba ya Ligi ili Simba mechi za awali ianze na timu ambazo wachezaji wageni wanao toka nje ya Nchi hawaja kamilisha vibali na washinde ki urahisi
Bahati mbaya Simba wenyewe wametoboa mtumbwi kwa kumchezesha Kagoma.
Yaani Tff Wana changanyikiwa wa wabebe vipi!!

Tusibiri tuone.
 
Ushabiki mbaya Sana ndugu hivi unafikili Simba anaweza akapokonywa point Kwa ujinga wa Mchezaji mwenyewe na Nani alitoa kibali ili acheze na hata Shauli lililopo ni Kati ya Yanga na Mchezaji na si Simba
 
Back
Top Bottom