Salamu kwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji, Passport za Tanzania zinakimbilia mikononi mwa wageni kupitia viongozi waandamizi na askari

Salamu kwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji, Passport za Tanzania zinakimbilia mikononi mwa wageni kupitia viongozi waandamizi na askari

Tanzania imezungukwa na maadui wengi kuliko marafiki, Tanzania imezungukwa na nchi zisizo na amani kama taifa letu. Ulinzi wa Tanzania upo mikononi mwetu Watanzania. Tusiposema hakuna atakayesema Kesho Wala Kesho kutwa. Nchi yetu imevamiwa Sana na wageni wanaotaka kuifanya nchi hii ni Mali Yao. Naamini nisipomwambia Kamishna Mkuu kuhusu Hali hii ntakua simsaidii, nisipomwambia Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Hali ilivyo mtaani may be wataingia wabaya nchini na wataishambulia nchi nakuumiza hata ndugu zangu naomba niseme. Yawezekana ninayoyasema anayajua au ni mapya kwake ila yatasaidia Taifa.

Kabla sijasema nikiri kwamba Mimi ni mtoa huduma za kisheria, Katika kutoa huduma za kisheria ndipo nilipokutana na haya nitakayoyaeleza hapa ambayo naamini yanamsaada mkubwa Kwa ulinzi wa nchi yetu,ulinzi wa afrika mashariki na ulinzi wa Dunia Kwa ujumla wake. Hivyo naomba anaposoma Kamishna Mkuu wa Uhamiaji basi asisome peke yake wasome Watanzania wengi na watakapoona visa vya aina hii waweze kuripoti wahusika wakamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria. Hizi ni true stori ambazo zimepita mikononi mwangu na mikononi mwa watoa huduma ya kisheria wengine, hakuna aliyechukulia serious au kama walichukulia serious basi awakufikisha ujumbe panapohusika.
Kati ya mwaka 2015 Hadi Sasa nimetoa huduma Kwa wateja wengi nikianzia Mwanza, nikaenda Mbeya, nikahamia Dar na Sasa nipo Kilimanjaro. Kupitia huduma hizo naomba kueleza madhara ya huduma hizi kwa Taifa letu na kwa Mataifa mengine
1. Huduma ya utoaji wa kiapo Cha kuzaliwa: Hii huduma inatolewa na Mawakili wengi na ni huduma ipo kisheria lakini huduma hii usipoifanya Kwa uadilifu madhara yake ni makubwa sana. Mwaka 2016 alifika mteja anatafuta kiapo kwangu, Mteja huyo alikua na maneno machache Sana ya kiswahili na mengi ya kiingereza, alikua anatafuta kiapo Kwa ajili ya pasipoti; nilipomhoji kuhusu majina yake,majina ya wazazi na majina ya watakao shuhudia kiapo alionekana dhahiri kwamba anatunga majina hivyo kumtilia mashaka. Nilipombana zaidi na kumweleza umuhimu wa kusema ukweli alikiri yeye ni raia wa Kenya ila amakuja nchini kufuatilia pasipoti, familia waliyofikia wakiwa watu wanne wanawasaidia kupata pasipoti na kwamba wenzake wote wamepata yeye amekwama kiapo. Nilikataa kumpa huduma na kumwacha aondoke Kisha kuwasilisha taarifa zake na za Ndugu zake ambao alidai wanapasipoti Uhamiaji ya karibu nisingependa kutaja jina; baada ya kuwasilisha taarifa zile nakuchukua namba za simu za afisa Kwa ajili yakupeana taarifa zaidi nilikuja kubaini kwamba kesi Ile imeingiliwa na watu flani wakubwa wanaofanya kazi wizara ya mambo ya ndani hivyo suspects wakapata mtetezi kutoka juu. Kwanini nimeandika hii stori, nimeandika baada ya kukutana na Mteja yuleyule aliyekiri kwangu kwamba ni raia wa Kenya Uhamiaji Dar es salaam akiwa anafuatilia siyo pasipoti mpya tu bali anabadilisha apewe ya kielekroniki. Kibaya zaidi treatment yake ilikuwa ni VIP kwa sababu wakati wengine tunasubiri yyeye aliingia Moja Kwa Moja nakukamilisha huduma nikasikia anaelekezwa kwenda Kurasini means ana mtandao mkubwa. Nilitamani kuwajulisha maafisa wawe makini lakini nilisita kukwamishwa mimi yeye akapita na sikupenda kujipnyesha kwake. Kwa tafsiri nyingine yupo mtumishi wa serikali aliyezuia huyu bwana kuchunguzwa uraia wake, yupo wakili aliyemtengenezea kiapo na wapo Watanzania nyuma yake waliojitolea kumpokea na kuruhusu atumie majina ya familia Yao. Lakini je wakati haya yanafanyika nani anajua dhamira za wageni hawa kutafuta pasipoti za Tanzania? Kwanini wabadili majina? Wana athari gani kwa kesho ya Tanzania? Kamishna tulindie nchi yetu simu zenu wakubwa wakati mwingine zinapeperusha wahalifu

2. Nikiwa Arusha nilikuta kesi Moja ofisini ambayo wahusika walioomba msaada wa kisheria walikuwa Dar es salaam. Katika kuwasikiliza nilipobaini ukweli nilijitoa bila kusema Kwanini nimejitoa. Story Yao Kwa ufupi ipo hivi; Wana asili ya Somalia, baba na mama waliingia nchini miaka ya 1970 wakiwa na pasipoti za Somalia. Walipokelewa na kaka Yao ambaye pia alikuwa Msomali. Miaka ya 1980 wenyeji wao wakafanikiwa kupata pasipoti za Tanzania na kwenda Ulaya. Wao pia wakatafuta pasipoti na kupata pasipoti lazima wawe na cheti cha kuzaliwa. Nilisikitika kusikia waliweza kupenyeza rupia wakapata vyeti vya kuzaliwa wazazi na watoto kipindi hicho hicho wakiwa tayari wanaishi kwa karatasi za kufanya kazi za uhamiaji. Baadaye walifanikiwa kupata pasipoti na watoto wao, nusu wakaenda ulaya na nusu wakabaki Tanzania. Mwaka 1995 Mzee wao akakamatwa Kwa Tuhuma za kugushi na kujipatia nyaraka( means yupo mtu aliwatonya Uhamiaji kwamba familia Ile siyo Watanzania) wakapanchi wakafunga uchunguzi bila uchunguzi. Siku wanakabidhiwa kwangu nakueleza stori hii ndipo nikabaini mambo yafuatayo.
I. Familia hii tayari ilishaingiza nchini ndugu zao wengi na wote kupitia cheti cha kuzaliwa Cha mwaka 1980+ wamefanikiwa kujitanabaisha kama wazaliwa wa Tanzania. Kila wakitaka cheti wanatoa copy vile vyeti vya awali na kuambatisha Kisha RITA wanatoa vyeti kama wazaliwa wa Tanzania. Kwanini wakieleza ukweli? Ni kwa sababu katika Tuhuma zilizokuwa zinawakabili tayari mamlaka za uchunguzi zilikuwa na ushahidi wote kwamba familia nzima ilikuwa siyo Watanzania. Jambo jema zaidi ni kwamba taarifa hizi zilitokana na mgogoro wa familia hivyo wao hoja Kwa mwanasheria haikuwa kupingana na ukweli wa serikali Bali walitaka mwanasheria asaidie kufifisha ushahidi na wasichunguzwe Wala uraia wao kuguswa Bali waendelee kutambulika kama Watanzania. Naamini wapo wanasheria wengi wanakutana na kesi za aina hii ambazo ni wazi zinaonyesha nchi ipo Miko mwa wageni na tumekuwa tukizishughulikia kwa lengo lakupata Fedha na tunashiriki kuzima uchunguzi. Hawa watu tunajua malengo Yao? Kesho wamekulipa ukajenga ghorofa uone ipo siku watalipua ghorofa ukiwa ndani na familia Yako? Watanzania tusidharau Utanzania wetu, tuulinde.
Ii. Kupitia kesi hii nilibaini wapo wageni wametoroka mapigano Somalia nakuja Tanzania kujificha , Ili wasisumbuliwe wanautafuta utanzania wa magumashi ambao ndio huu wakurithishana makaratasi ya kuzaliwa ambayo nilipouliza cheti chakuzaliwa kinacost shs ngapi nikaambiwa wakala anapewa laki Hadi laki na nusu na wakati mwingine Kwa mfano familia hii Ina mtu maalumu ofisi za RITA anayepokea na kushughulikia. Kikubwa kinachofanyika wageni wanaachwa nyumbani Kwa sababu wakihojiwa watabaonika.
III. Kupitia stori za familia hii nilibaini ni rahisi Sana kwa mgeni mwenye fedha kupata kitambulisho Cha NIDA, wakipata cheti cha kuzaliwa wenyeji wao wanakwenda serikali za mtaa wanaandikiwa barua kisha wakienda NIDA wanapata ID ndani ya muda mfupi Sana. Wakati huo yupo mtanzania wakuzaliwa asikilizwi na apewi huduma. Kamishna sijui kama mbinu hizi unazijua na unajua zinavyochezwa.
iv. Nini kilitokea, Wakati kesi hii inaletwa tusaidie kudefend wakiomba istop kwenda mahakamani na wasivuliwe uraia na baada ya kujitoa kwa kuogopa kushiriki uharamia huu; zile pasipoti zilifutwa lakini sijui sheria ipoje, pasipoti zilizofutwa siyo za familia Bali ya mmoja aliyekuwa analalamikiwa Sana ila sasa waliofuta wakatoa kitu kinatwa restrictions passport Kwa miaka minne kupisha uchunguzi. Lakini baadaye kidogo wale waliobaki wakaendelea kupewa electronic Passport na yule aliyezuiwa aliomba tumwandikie kitu flani baada ya muda amepewa Tena electronic Passport. Naomba hapa Kamishna Mkuu uwasaidie Watanzania ni nani anayepewa pasipoti ya Tanzania? Hii kesi kwa upande wangu na namna ilivyofikiswa kwetu ilitutisha na nakumbuka one of our wakili ilibidi afike uhamiaji kuuliza madhara ya wakili kutoa huduma Kwa kutengeneza nyaraka Kwa watu kama Hawa ambao wanakiri wazi na nyaraka zipo wazi kwamba siyo Watanzania lakini wanataka bargaining wasipokonywe Uraia; lakini alitaka kujua ni katika mazingira Gani Raia wa Kigeni anapewa restrict pasipoti? Lakini pia tulichanganywa na Nani mhamaji haramu? Hii kesi imenifanya niandike kumwomba Kamishna Jenerali awaangalie watendaji wake, Hali ya Dunia hasa nchi maskini ipo hatarini na tishio kubwa la usalama ni binadamu. Hao maafisa wa chini wanapotoa hizi restric pasipoti wadhibitiwe, maana kila kesi ya mwenye pesa zinaishia aidha anatamkwa raia au anafutiwa pasipoti ya miaka kumi na kupewa ya muda kidogo na baada ya muda anaonga anapewa tena pasipoti kama Mtanzania. Kwa mawakili wenzetu kesi kama hizi vuteni mpunga lakini hakiiisheni mnachosaidia ni huyu mgeni kuishi kihalali au mtaftieni huyo mgeni nauli arudi kwao.


3. Kesi ya mwisho; kuna watu wanaomba msaada wa kisheria kama wakimbizi hasa kutoka huko Yemen na kwingine: Hawa watu mnashughulika nao baada ya mwaka wakiwa wanafuatilia ukimbizi unasikia wana pasipoti za Tanzania. Kwanini pasipoti za Tanzania wanasema wanakwenda Ulaya na pasipoti ya Tanzania ni dili. Nadhani hapa nchini zipo familia zinapokea wa siria na wayemeni na watu wa bara Hindi nakujifanya ni ndugu zao. Hii mbinu nafuatilia zaidi kwa sababu watu hawa sijakutana na anayetaka huduma ya nyaraka ila naaamini mawakili wenzangu wanakesi kama hizi wameletewa watengeneze nyaraka au kuthibitisha cheti ni Tru copy. Lakini uhamiaji si mnahoji, mnajua kwamba watu wanapachikwa kwenye familia? Kamishna Mkuu hapa napo fanyia utafiti ni vipi watu Hawa wanapata pasipoti? Mgeni ni mkimbizi lakini anapata pasipoti.

4. Kamishna Mkuu, Jambo nililolipenda kuhusu viongoozi wenzako lakini nilikuja kubaini mbinu hii inatumika vibaya; ukifika ofisi ya Kiongozi wa uhamiaji ukajitambulisha nakulalamikia Jambo hatua zinachukuliwa fasta, mwanzo kabla sijafunguka macho ilikuwa tukipata kesi tunakwenda Kwa wakubwa kuizima. Wakati nashighulikia kesi ya wasomali ndipo nikagundua huu ukarimu unaambatana na mlungula wakati mwingine. Siku Moja mmoja wa wateja kwenye kesi hiyo alitakiwa kwenda kuhojiwa na hakutaka kutoa maelezo it was around may, 2018. Alimpigia simu bwana mmoja jina tunalihifadhi akiomba msaada asihojiwe, what happened agent claimed apewe Milioni arobaini kuzima mahojiano, and finally alifanikiwa na ndipo masuala ya restric yalipozaliwa. Hivyo huu ukarimu wa watendaji waandamizi pls usiandamane na Rushwa, kama wanakarimu kwa kupewa rushwa bora wasikarimu.

Mwisho; ntaandika majina ya wahusika wote ambao naamini nimewahi kuwahudumia ila wana viashiria vya ugeni , ntakutumia pia hizo restric pasipot number uangalie ni namna gani kesi hii itasiadia kurise awareness kwa watendaji wako na kuwataadharisha kwamba ulimwengu huu umebadilika. Nimesoma south Africa naelewa namna corruption na tamaaa za watendaji zilivyopelekea kinachoutwa ubaguzi wa karne. Viongozi walikalia kutoa huduma mwisho wakasau kuwachuja wanaowapa huduma. Tuombe Mungu miongoni mwa hawa niliowaeleza wasiwe na nia mbaya, lakini wapo wangapi wanacheza na RIta ,NIDA, UHAMIAJI NA MIPAKANI kwa kutumia mbinu hizi?

Tuilinde Tanzania ,tuache Rushwa.

HUU SASA ndo uzalendo
 
Mleta mada asante sana. Kwa sasa keep low profile huku ukifuatilia kinachoendelea. Polepole kasema mambo manne ambayo wahuni wanaweza kukufanyia. Mleta mada bado tunakuhitaji. Tafadhali zingatia ushauri wangu.
 
Kati ya idara hovyo za serikali uhamiaji ni nambari moja.hiyo idara imeoza sana.wakubwa wengi sio raia wa nchi hii kwahiyo wanafaidika na udhaifu wa uhamiaji.
 
Tanzania imezungukwa na maadui wengi kuliko marafiki, Tanzania imezungukwa na nchi zisizo na amani kama taifa letu. Ulinzi wa Tanzania upo mikononi mwetu Watanzania. Tusiposema hakuna atakayesema Kesho Wala Kesho kutwa. Nchi yetu imevamiwa Sana na wageni wanaotaka kuifanya nchi hii ni Mali Yao. Naamini nisipomwambia Kamishna Mkuu kuhusu Hali hii ntakua simsaidii, nisipomwambia Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Hali ilivyo mtaani may be wataingia wabaya nchini na wataishambulia nchi nakuumiza hata ndugu zangu naomba niseme. Yawezekana ninayoyasema anayajua au ni mapya kwake ila yatasaidia Taifa.

Kabla sijasema nikiri kwamba Mimi ni mtoa huduma za kisheria, Katika kutoa huduma za kisheria ndipo nilipokutana na haya nitakayoyaeleza hapa ambayo naamini yanamsaada mkubwa Kwa ulinzi wa nchi yetu,ulinzi wa afrika mashariki na ulinzi wa Dunia Kwa ujumla wake. Hivyo naomba anaposoma Kamishna Mkuu wa Uhamiaji basi asisome peke yake wasome Watanzania wengi na watakapoona visa vya aina hii waweze kuripoti wahusika wakamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria. Hizi ni true stori ambazo zimepita mikononi mwangu na mikononi mwa watoa huduma ya kisheria wengine, hakuna aliyechukulia serious au kama walichukulia serious basi awakufikisha ujumbe panapohusika.
Kati ya mwaka 2015 Hadi Sasa nimetoa huduma Kwa wateja wengi nikianzia Mwanza, nikaenda Mbeya, nikahamia Dar na Sasa nipo Kilimanjaro. Kupitia huduma hizo naomba kueleza madhara ya huduma hizi kwa Taifa letu na kwa Mataifa mengine
1. Huduma ya utoaji wa kiapo Cha kuzaliwa: Hii huduma inatolewa na Mawakili wengi na ni huduma ipo kisheria lakini huduma hii usipoifanya Kwa uadilifu madhara yake ni makubwa sana. Mwaka 2016 alifika mteja anatafuta kiapo kwangu, Mteja huyo alikua na maneno machache Sana ya kiswahili na mengi ya kiingereza, alikua anatafuta kiapo Kwa ajili ya pasipoti; nilipomhoji kuhusu majina yake,majina ya wazazi na majina ya watakao shuhudia kiapo alionekana dhahiri kwamba anatunga majina hivyo kumtilia mashaka. Nilipombana zaidi na kumweleza umuhimu wa kusema ukweli alikiri yeye ni raia wa Kenya ila amakuja nchini kufuatilia pasipoti, familia waliyofikia wakiwa watu wanne wanawasaidia kupata pasipoti na kwamba wenzake wote wamepata yeye amekwama kiapo. Nilikataa kumpa huduma na kumwacha aondoke Kisha kuwasilisha taarifa zake na za Ndugu zake ambao alidai wanapasipoti Uhamiaji ya karibu nisingependa kutaja jina; baada ya kuwasilisha taarifa zile nakuchukua namba za simu za afisa Kwa ajili yakupeana taarifa zaidi nilikuja kubaini kwamba kesi Ile imeingiliwa na watu flani wakubwa wanaofanya kazi wizara ya mambo ya ndani hivyo suspects wakapata mtetezi kutoka juu. Kwanini nimeandika hii stori, nimeandika baada ya kukutana na Mteja yuleyule aliyekiri kwangu kwamba ni raia wa Kenya Uhamiaji Dar es salaam akiwa anafuatilia siyo pasipoti mpya tu bali anabadilisha apewe ya kielekroniki. Kibaya zaidi treatment yake ilikuwa ni VIP kwa sababu wakati wengine tunasubiri yyeye aliingia Moja Kwa Moja nakukamilisha huduma nikasikia anaelekezwa kwenda Kurasini means ana mtandao mkubwa. Nilitamani kuwajulisha maafisa wawe makini lakini nilisita kukwamishwa mimi yeye akapita na sikupenda kujipnyesha kwake. Kwa tafsiri nyingine yupo mtumishi wa serikali aliyezuia huyu bwana kuchunguzwa uraia wake, yupo wakili aliyemtengenezea kiapo na wapo Watanzania nyuma yake waliojitolea kumpokea na kuruhusu atumie majina ya familia Yao. Lakini je wakati haya yanafanyika nani anajua dhamira za wageni hawa kutafuta pasipoti za Tanzania? Kwanini wabadili majina? Wana athari gani kwa kesho ya Tanzania? Kamishna tulindie nchi yetu simu zenu wakubwa wakati mwingine zinapeperusha wahalifu

2. Nikiwa Arusha nilikuta kesi Moja ofisini ambayo wahusika walioomba msaada wa kisheria walikuwa Dar es salaam. Katika kuwasikiliza nilipobaini ukweli nilijitoa bila kusema Kwanini nimejitoa. Story Yao Kwa ufupi ipo hivi; Wana asili ya Somalia, baba na mama waliingia nchini miaka ya 1970 wakiwa na pasipoti za Somalia. Walipokelewa na kaka Yao ambaye pia alikuwa Msomali. Miaka ya 1980 wenyeji wao wakafanikiwa kupata pasipoti za Tanzania na kwenda Ulaya. Wao pia wakatafuta pasipoti na kupata pasipoti lazima wawe na cheti cha kuzaliwa. Nilisikitika kusikia waliweza kupenyeza rupia wakapata vyeti vya kuzaliwa wazazi na watoto kipindi hicho hicho wakiwa tayari wanaishi kwa karatasi za kufanya kazi za uhamiaji. Baadaye walifanikiwa kupata pasipoti na watoto wao, nusu wakaenda ulaya na nusu wakabaki Tanzania. Mwaka 1995 Mzee wao akakamatwa Kwa Tuhuma za kugushi na kujipatia nyaraka( means yupo mtu aliwatonya Uhamiaji kwamba familia Ile siyo Watanzania) wakapanchi wakafunga uchunguzi bila uchunguzi. Siku wanakabidhiwa kwangu nakueleza stori hii ndipo nikabaini mambo yafuatayo.
I. Familia hii tayari ilishaingiza nchini ndugu zao wengi na wote kupitia cheti cha kuzaliwa Cha mwaka 1980+ wamefanikiwa kujitanabaisha kama wazaliwa wa Tanzania. Kila wakitaka cheti wanatoa copy vile vyeti vya awali na kuambatisha Kisha RITA wanatoa vyeti kama wazaliwa wa Tanzania. Kwanini wakieleza ukweli? Ni kwa sababu katika Tuhuma zilizokuwa zinawakabili tayari mamlaka za uchunguzi zilikuwa na ushahidi wote kwamba familia nzima ilikuwa siyo Watanzania. Jambo jema zaidi ni kwamba taarifa hizi zilitokana na mgogoro wa familia hivyo wao hoja Kwa mwanasheria haikuwa kupingana na ukweli wa serikali Bali walitaka mwanasheria asaidie kufifisha ushahidi na wasichunguzwe Wala uraia wao kuguswa Bali waendelee kutambulika kama Watanzania. Naamini wapo wanasheria wengi wanakutana na kesi za aina hii ambazo ni wazi zinaonyesha nchi ipo Miko mwa wageni na tumekuwa tukizishughulikia kwa lengo lakupata Fedha na tunashiriki kuzima uchunguzi. Hawa watu tunajua malengo Yao? Kesho wamekulipa ukajenga ghorofa uone ipo siku watalipua ghorofa ukiwa ndani na familia Yako? Watanzania tusidharau Utanzania wetu, tuulinde.
Ii. Kupitia kesi hii nilibaini wapo wageni wametoroka mapigano Somalia nakuja Tanzania kujificha , Ili wasisumbuliwe wanautafuta utanzania wa magumashi ambao ndio huu wakurithishana makaratasi ya kuzaliwa ambayo nilipouliza cheti chakuzaliwa kinacost shs ngapi nikaambiwa wakala anapewa laki Hadi laki na nusu na wakati mwingine Kwa mfano familia hii Ina mtu maalumu ofisi za RITA anayepokea na kushughulikia. Kikubwa kinachofanyika wageni wanaachwa nyumbani Kwa sababu wakihojiwa watabaonika.
III. Kupitia stori za familia hii nilibaini ni rahisi Sana kwa mgeni mwenye fedha kupata kitambulisho Cha NIDA, wakipata cheti cha kuzaliwa wenyeji wao wanakwenda serikali za mtaa wanaandikiwa barua kisha wakienda NIDA wanapata ID ndani ya muda mfupi Sana. Wakati huo yupo mtanzania wakuzaliwa asikilizwi na apewi huduma. Kamishna sijui kama mbinu hizi unazijua na unajua zinavyochezwa.
iv. Nini kilitokea, Wakati kesi hii inaletwa tusaidie kudefend wakiomba istop kwenda mahakamani na wasivuliwe uraia na baada ya kujitoa kwa kuogopa kushiriki uharamia huu; zile pasipoti zilifutwa lakini sijui sheria ipoje, pasipoti zilizofutwa siyo za familia Bali ya mmoja aliyekuwa analalamikiwa Sana ila sasa waliofuta wakatoa kitu kinatwa restrictions passport Kwa miaka minne kupisha uchunguzi. Lakini baadaye kidogo wale waliobaki wakaendelea kupewa electronic Passport na yule aliyezuiwa aliomba tumwandikie kitu flani baada ya muda amepewa Tena electronic Passport. Naomba hapa Kamishna Mkuu uwasaidie Watanzania ni nani anayepewa pasipoti ya Tanzania? Hii kesi kwa upande wangu na namna ilivyofikiswa kwetu ilitutisha na nakumbuka one of our wakili ilibidi afike uhamiaji kuuliza madhara ya wakili kutoa huduma Kwa kutengeneza nyaraka Kwa watu kama Hawa ambao wanakiri wazi na nyaraka zipo wazi kwamba siyo Watanzania lakini wanataka bargaining wasipokonywe Uraia; lakini alitaka kujua ni katika mazingira Gani Raia wa Kigeni anapewa restrict pasipoti? Lakini pia tulichanganywa na Nani mhamaji haramu? Hii kesi imenifanya niandike kumwomba Kamishna Jenerali awaangalie watendaji wake, Hali ya Dunia hasa nchi maskini ipo hatarini na tishio kubwa la usalama ni binadamu. Hao maafisa wa chini wanapotoa hizi restric pasipoti wadhibitiwe, maana kila kesi ya mwenye pesa zinaishia aidha anatamkwa raia au anafutiwa pasipoti ya miaka kumi na kupewa ya muda kidogo na baada ya muda anaonga anapewa tena pasipoti kama Mtanzania. Kwa mawakili wenzetu kesi kama hizi vuteni mpunga lakini hakiiisheni mnachosaidia ni huyu mgeni kuishi kihalali au mtaftieni huyo mgeni nauli arudi kwao.


3. Kesi ya mwisho; kuna watu wanaomba msaada wa kisheria kama wakimbizi hasa kutoka huko Yemen na kwingine: Hawa watu mnashughulika nao baada ya mwaka wakiwa wanafuatilia ukimbizi unasikia wana pasipoti za Tanzania. Kwanini pasipoti za Tanzania wanasema wanakwenda Ulaya na pasipoti ya Tanzania ni dili. Nadhani hapa nchini zipo familia zinapokea wa siria na wayemeni na watu wa bara Hindi nakujifanya ni ndugu zao. Hii mbinu nafuatilia zaidi kwa sababu watu hawa sijakutana na anayetaka huduma ya nyaraka ila naaamini mawakili wenzangu wanakesi kama hizi wameletewa watengeneze nyaraka au kuthibitisha cheti ni Tru copy. Lakini uhamiaji si mnahoji, mnajua kwamba watu wanapachikwa kwenye familia? Kamishna Mkuu hapa napo fanyia utafiti ni vipi watu Hawa wanapata pasipoti? Mgeni ni mkimbizi lakini anapata pasipoti.

4. Kamishna Mkuu, Jambo nililolipenda kuhusu viongoozi wenzako lakini nilikuja kubaini mbinu hii inatumika vibaya; ukifika ofisi ya Kiongozi wa uhamiaji ukajitambulisha nakulalamikia Jambo hatua zinachukuliwa fasta, mwanzo kabla sijafunguka macho ilikuwa tukipata kesi tunakwenda Kwa wakubwa kuizima. Wakati nashighulikia kesi ya wasomali ndipo nikagundua huu ukarimu unaambatana na mlungula wakati mwingine. Siku Moja mmoja wa wateja kwenye kesi hiyo alitakiwa kwenda kuhojiwa na hakutaka kutoa maelezo it was around may, 2018. Alimpigia simu bwana mmoja jina tunalihifadhi akiomba msaada asihojiwe, what happened agent claimed apewe Milioni arobaini kuzima mahojiano, and finally alifanikiwa na ndipo masuala ya restric yalipozaliwa. Hivyo huu ukarimu wa watendaji waandamizi pls usiandamane na Rushwa, kama wanakarimu kwa kupewa rushwa bora wasikarimu.

Mwisho; ntaandika majina ya wahusika wote ambao naamini nimewahi kuwahudumia ila wana viashiria vya ugeni , ntakutumia pia hizo restric pasipot number uangalie ni namna gani kesi hii itasiadia kurise awareness kwa watendaji wako na kuwataadharisha kwamba ulimwengu huu umebadilika. Nimesoma south Africa naelewa namna corruption na tamaaa za watendaji zilivyopelekea kinachoutwa ubaguzi wa karne. Viongozi walikalia kutoa huduma mwisho wakasau kuwachuja wanaowapa huduma. Tuombe Mungu miongoni mwa hawa niliowaeleza wasiwe na nia mbaya, lakini wapo wangapi wanacheza na RIta ,NIDA, UHAMIAJI NA MIPAKANI kwa kutumia mbinu hizi?

Tuilinde Tanzania ,tuache Rushwa.
Duh! Shukurani sana kabisa!

Hili lifanyiwe kazi na mamlaka husika
 
Huyo mama kabebwa na gender tu hamna kitu pale, pia Magu alipenda watu ndio mzee yaani nyuma geuka tembea watu wa kupokea amri
 
Sijasoma yote Ila wewe jamaa inaonekana ni mzalendo kwerii kweriii.. kuna sehemu nilipita huko Kagera , wanyarwanda wamepata NIDA kibaoo, na wanajitambilisha kuwa wao ni watz wa kuzaliwa
True ni mzalendo ni nadra Sana kwa mtza kumripoti mgeni haramu sehemu husika labda tu kama wanagombea interest mfano wanawake, fitina za biashara nk.
 
Hongera mkuu kwa kuumizwa na utendaji wa uhamiaji! Mimi binafsi ningependa kamishna wa uhamiaji nchini APUMZISHWE! Naona kama anapwaya sana yule Madam! Mambo ya rushwa uhamiaji ni kama wimbo maarufu miaka yote.
 
Kati ya idara hovyo za serikali uhamiaji ni nambari moja.hiyo idara imeoza sana.wakubwa wengi sio raia wa nchi hii kwahiyo wanafaidika na udhaifu wa uhamiaji.
Yule mama haiwezi ile idara anachojua ni kusimamisha na kufukuza watumishi na sio kufanya maboresho au kutatua changamoto.
Alifukuza watoto wa watu 15 bila huruma eti kisa wapewa hela ya soda, sasa abiria vichenji vidogo elf 5 elf 10 anazipeleka wapi hali ategemei kurudi tena Bongo wala nchini kwake Hakuna bureau ya kubadili shilingi, mtu kapanda tax chenji imebaki, karidhika na huduma kaamua utakunywa soda chenji hio sirudi Bongo pia hata nikirudi nayo kwetu ni useless, wivu unamfukuza Kazi eti kisa kapewa soda bila kujali gharama ulizotumia kumtrain, mswahili hana roho mbaya sana akipata madaraka.

Ukimfukuza mtu Kazi haimaaishi utapewa mishahara yake.
 
Una lengo jema ila chukua tahadhari, usijaribu kuweka wazi your true id, waovu ni wengi kuliko wema na wapo kila pahala mpaka ndani ya nyumba za ibada.Rejea kilichompata amina etc.
 
Hongera mkuu kwa kuumizwa na utendaji wa uhamiaji! Mimi binafsi ningependa kamishna wa uhamiaji nchini APUMZISHWE! Naona kama anapwaya sana yule Madam! Mambo ya rushwa uhamiaji ni kama wimbo maarufu miaka yote
True kuwa na phd sio kuweza uongozi, uongozi ni inborn character, uongozi yafaa anapewa mtu anaeijua taasisi kama ni Waziri wa elimu yafaa aliyepanda madaraja ya ualimu so ni rahisi kujua maboresho ni yepi.
 
Hongera mkuu kwa kuumizwa na utendaji wa uhamiaji! Mimi binafsi ningependa kamishna wa uhamiaji nchini APUMZISHWE! Naona kama anapwaya sana yule Madam! Mambo ya rushwa uhamiaji ni kama wimbo maarufu miaka yote
Kiongozi rushwa haiwezi kuisha hata siku moja yeyote utakayweka hata ukiwekwa wewe. Kinachowezekana ni kupunguza tu na kama una ushauri namna ya kupunguza hiyo rushwa unaweza kutoa.
 
True kuwa na phd sio kuweza uongozi, uongozi ni inborn character, uongozi yafaa anapewa mtu anaeijua taasisi kama ni Waziri wa elimu yafaa aliyepanda madaraja ya ualimu so ni rahisi kujua maboresho ni yepi.
Sometime leaders are made and not born
 
Sisi kama taifa tunaelekea wapi, yaani unakuta passport ya Tanzania inauzwa kwa thamani ya bucket ya windhoek..

Mfumo ujitathiminj kwa hili na watendaji wale wakumbuke kile kiapo walichokula wakati wanakabidhiwa zile identity, the same goes to vipenyo wote ambao wako hapo Uhamiaji.
 
Hongera mkuu kwa kuumizwa na utendaji wa uhamiaji! Mimi binafsi ningependa kamishna wa uhamiaji nchini APUMZISHWE! Naona kama anapwaya sana yule Madam! Mambo ya rushwa uhamiaji ni kama wimbo maarufu miaka yote
Wanawake wanalindana hata kama ni dhaifu ukimbilia jenda.
 
Uhamiaji rushwa nje nje Hadi unashangaa tuko serious, Yani ukitaka passport ni hela yako tu, tena wageni huwa rahisi ukiwa na hela
 
Naomba kueleza lengo la taarifa hii

1. Nimeonyesha namna Mawakili na wanadheria wanavyoweza kuhatarisha usalama wa nchi Kwa kutotambua thamani ya mihuri waliyopewa. Mfano affidavit inagharamiwa elfu kumi au ishirini na 100,000+ kwenye firm ambazo Zina hadhi ya juu. Shilingi elfu kumi ya kiapo imekuwa ikitumiwa vibaya na Mawakili wengi binafsi na hata waliopo Serikalini, Mawakili wanashawishi wamtengenezee kiapo Mteja akiwepo au asiwepo. Nitato mfano eneo hili, baba zetu na ndugu zetu wapo vijijini lakini huku mjini kuna watu wanaghushi signature zao na kutumia majina yao kutengeneza viapo bila wao kujua. Huu ni uhalifu unaofanywa na wanasheria na hapa ndipo hizi affidavit za wageni wasio watanzania zinapotolewa. Mkenya anatafuta affidavit kama requirement ya kupata pasipoti au kadi ya NIDA, hivyo niombe awali UHAMIAJI waangalie umuhimu wa viapo na uhalali wa viapo wanavyopokea. Pili maongeze mahojiano na wateja.

2. Eneo la pili nilitaka kumweleza Kamishna Mkuu wa Uhamiaji kwamba Wapo viongoz wakubwa wanatumia vibaya madaraka na mishahara yao kutoa huduma. Badala wasimamie haki wamekuwa wepesi Sana kusikiliza laghai za wanasheria na mawakala nakutoa maelekezo yenye madhara kwenye hizo huduma zao. Mwanasheria anaingia mkataba wa Milioni let say ishirini kumtetea Mteja, then akiona kesi Katika ngazi ya chini Ina ugumu anakwenda kupakazia wakubwa kwamba Mteja wake anaoneo na maneno mengine, badala wakubwa wasimamie haki wanapindisha haki na hapa ndipo zinapopitia hizi pasipoti za wageni. Lakini pia Kuna wakati unakua engaged na Mteja kwenye kesi, unabaini mapungufu na unatamani kuisaidia Jamhuri mara Mteja anarudi kwako kwamba ameshamalizana na mkubwa na mkataba wenu unafungwa. Ukifuatilia unagundua a lot of money zimepitia mikononi mwa mtu wa Kati na wageni wamerejeshewa hati zao. Hapa sijui Hawa wakubwa wanafanya kwa upofu Gani.

3. Nimeleta Uzi huu kuwaomba watanzania tuulinde Utanzania wetu, naamini wapo watu wanachukizwa sisi kusema huu ukweli na niviongozi wakubwa ila ninachoomba kuwaeleza ni kwamba Hawa wageni wakiingilia soko la ajira, wakiingia magaidi, wakiingia watu wenye uchu na madaraka tukawapa nchi, wakijaa nchini wataanza kutuletea machafuko yaliyotokea Libya, watatuletea kubaguana kama south Afrika na kwingine. Wakati tunapigana Hawa wanaokula Rushwa Leo watakuwa wamestaafu wapo wamewekewa ulinzi makwao wanakula pensheni au wamekufa. Hivyo kwenye ya uadilifu na uraia wetu tusikubali kurudi nyuma, fedha tuchukue lakini tuwachome Viongozi wanatoa huduma Kwa wageni

4. Leo ukienda NIDA ukafuatili Kwa miezi sita wametoa vitambulisho kiasi Gani vya watu wenye rangi, wenye asili ya Mataifa ya nje utabaini ni wengi na walipewa huduma Kwa muda mfupi Sana lakini qapo Watanzania Wana miaka mitatu wanatumia namba. Kwanini Hawa watu wanapewa haraka nikwa sababu Hawana muda wakupoteza wanataka Pasipoti wavuke waende au wakwepe kusumbuliwa na dola

Mwisho; endapo tutachukilia Uzi huu kuwalaumu Uhamiaji tutakuwa tunakosea. Tatizo ni la Kitaifa kwa sababu Hawa watu wanasaidiwa na sisi wasomi na wasio soma. Wanakarimiwa na sisi na wanahudumiwa na maafisa wa serikali ambao ni watoto wetu. Tusaidie wageni wapokonywe pasipoti Taifa Liwe salama, tusaidie NIDA wafute vitambulisho Taifa Liwe salama.
Lakini pia tukumbuke serikali inataka uwe na kadi ya NIDA upate line ya simu, niambieni ni mgeni Gani unayemfahamu Kijiji au mjini Hana simu? Hiyo line kasajili Kwa namba zipi za NiDA? Tulione kama bomu na tunapolalamika ajira may be ajira nyingi wameshika wao. Tuanze kuchujana

Katika kuliangalia kisheria utabaini sheria ya Uhamiaji imekaa kuvutia wageni wahalifu, kama mtu anaweza kutoa Milioni ishirini kuweka wakili au kutoa Rushwa asishtakiwe au asichunguzwe atashindwaje kulipa fine laki Tano mahakamani? Kesi za Uhamiaji ukienda mahakamani unaenda na laki Tano unamaliza, lakini sheria ya pasipoti fine laki mbili sijui Hawa watu wanaiona pasipoti ya Tanzania ni kama hati isiyo na hadhi? Mtu adanganye apate pasipoti akose laki mbili?

Natamani watokee watu makini wachambue tatizo la uraia wa Tanzania kiusalama ikiwezekana ukikutwa na pasipoti kinyume Cha sheria iwe lazima kufikishwa mahakamani na huku iwe kifungo hata miaka 30 na viongozi wa Uhamiaji wasipewe Uhuru wakufanya administration procedure kama hizi zakutoa pasipoti ndogo au kufukuza. Mgeni akasote jela kwanza alime ndipo arejeshwe kwao utaona kama huu ujinga wakuweka Mawakili wakatetee usichunguzwe uraia kama utaendelea. Lakini pia itawasaidia Mawakili wa Tanzania kulipwa fedha nzito ambazo zitaendeleza uchumi wetu.

Tujadili bila kuwaona Uhamiaji kama tatizo, wanatekeleza wajibu wao ambao sisi pia ni wajibu wetu. Umetimiza wajibu wako? Tuwafichue Hawa wahuni wanaotaka kuliteka Taifa letu baada yakuvurugana kwao
 
Ukweli ni kwamba wahamiaji haramu huwa wa mwanzo kabisa kutafuta passport, vitambulisho vya taifa, ukaribu na viongozi , hati za umiliki wa ardhi na hata uongozi (zaidi sana kupitia chama tawala)

Hali hii ikikomaa sana, huweza kudhibiti idara nyeti za serikali, kupata uwaziri na hata urais.
 
Back
Top Bottom