Salome Mgaya (Mama Kibonge) akamatwa kwa ukwepaji Kodi za Mabilioni ya fedha Bandarini

Salome Mgaya (Mama Kibonge) akamatwa kwa ukwepaji Kodi za Mabilioni ya fedha Bandarini

Mi nadhani nyeupe isemwe nyeupe na nyeusi isemwe nyeusi ukwepwaji wa kodi kwa wafanyabiashara upo mwingi sana na hii haipingiki kupitia stoo inajulikana, kutoa risiti za mzigo pungufu kithamani nayo kawaida. Wafanyabiashara nchi hii si wazalendo yajulikana upande wa pili napo tatizo kuna vikodi vingi vingi na vya kipuuzi ambavyo mwisho wa siku mpaka upande wa pili wanapata sababu kuleta haya yaliyotokea.

Hitimisho: NANI AMVISHE PAKA KENGERE
 
Kwa Jinsi wafanyabiashara walivyoeleza ,ni wazi watendaji wanaweka kodi zisizolipika ili mradi watu watoe rushwa na wao wapate chao,kuna mfanyabiashar alitoa wazo ambalo kama mwigulu angelitekeleza serikali ingepata kodi mara mbili ya waliotarget wao lakini hawakusikiliza mawazo yao zaidi ya kuongeza tozo kutoka laki 8 hadi 2.4m
Mwigulu anashida ya kiburi
 
Mama kibonge ndo huyu
Screenshot_20230517-202009.jpg
 
Mama bonge...hajawah shindwa vita...na hii vita anapigwa na boss wa simba na mamluki kibao..kuna kaumafia fulan hivi kwenye hii biashara ya vitenge....kuna mmoja anataka kuwa supplyer na ni billionea na mzawa lakin kiwanda chake hakikidhi uhitaji wa bidhaa kwa hao wahitaji.,,na hapa ndio vita ilipoanzia tokea enz za Magu....

NB bil 5 kwa mama bonge...aah jaman mbona wanamchafua...pesa ya mandaz kabisa hyo...
Mama kibonge kashinda vita....
 
Yule wa container 15 na kudaiwa bilioni 30 mara 10 mara 3.5 ndiyo wa mapicha picha na mkubwa?
 
Ila tuacheni utani kodi TRA kubwa sana bila ujanja janja hakuna kutoboa.
Uwiano wa manunuzi katika uagizaji na tozo na kodi sio sawa.
Mfano ukiagiza gari,kodi na tozo ni sawa au zaidi ya thamani ya gharama ya kuagiza gari,(uagize gari kwa Tshs.milioni 10,kodi na tozo milioni 15,mpaka utoe bandari gharama jumla inakuwa Tshs.milioni 25 ).
PENDEKEZO:
1.TRA ibadilishe tafsiri ya kumiliki gari kuwa ni anasa,bali ni bidhaa muhimu katika kukuza uchumi wa taifa,kwani wamiliki wakiwa wengi watachangia kodi kwa kununua mafuta.
2.Kodi ya uagizaji magari ipunguzwe hasa "import duty".
 
Tunahangaika na kina Mama Kibonge pekee na kuwasahau / kujifanya hatuoni wanayoitafuna iliyoshakusanywa !!!!, Anyway hili limetupa Nishati nguvu za kusifia....,

By the way wamejuaje alikuwa anakwepa kwa muda mrefu ? Kwahio walikuwa wanamuona na kumfumbia macho ?
 
Mi nadhani nyeupe isemwe nyeupe na nyeusi isemwe nyeusi ukwepwaji wa kodi kwa wafanyabiashara upo mwingi sana na hii haipingiki kupitia stoo inajulikana, kutoa risiti za mzigo pungufu kithamani nayo kawaida. Wafanyabiashara nchi hii si wazalendo yajulikana upande wa pili napo tatizo kuna vikodi vingi vingi na vya kipuuzi ambavyo mwisho wa siku mpaka upande wa pili wanapata sababu kuleta haya yaliyotokea.

Hitimisho: NANI AMVISHE PAKA KENGERE
Siwezi watetea hao hata siku Moja ni wakwepaji Kodi wakubwa na hawatakiwi kuchelewa..

Pamoja na Changamoto za watu wa TRA ila kucheka na Hawa watu umekwisha,hakuna mfanyabishara anataka kulipa Kodi Kwa hiari hayupo hata Mimi Huwa silipi inavyotakiwa labda Kwa kubanwa.
 
Tunahangaika na kina Mama Kibonge pekee na kuwasahau / kujifanya hatuoni wanayoitafuna iliyoshakusanywa !!!!, Anyway hili limetupa Nishati nguvu za kusifia....,

By the way wamejuaje alikuwa anakwepa kwa muda mrefu ? Kwahio walikuwa wanamuona na kumfumbia macho ?
Tutimize wajibu kwanza ili tudai uwajibikaji.
 
Uwiano wa manunuzi katika uagizaji na tozo na kodi sio sawa.
Mfano ukiagiza gari,kodi na tozo ni sawa au zaidi ya thamani ya gharama ya kuagiza gari,(uagize gari kwa Tshs.milioni 10,kodi na tozo milioni 15,mpaka utoe bandari gharama jumla inakuwa Tshs.milioni 25 ).
PENDEKEZO:
1.TRA ibadilishe tafsiri ya kumiliki gari kuwa ni anasa,bali ni bidhaa muhimu katika kukuza uchumi wa taifa,kwani wamiliki wakiwa wengi watachangia kodi kwa kununua mafuta.
2.Kodi ya uagizaji magari ipunguzwe hasa "import duty".
Sera ya Tanzania Ina discourage magari used ndio maana unaona Iko hivyo.
 
Ona huyu amehama kutoka kwenye mada ya kero za kulipa Kodi amehamia kwenye siasa Kwa kudia Kodi inaliwa


Mpaka hapo huo unakuwa ni mgomo wenye msukumo wa Kisiasa.
 
Back
Top Bottom