Samaki, nyama, kuku na maharage kuliwa kama mboga ni dalilli ya umaskini?

Samaki, nyama, kuku na maharage kuliwa kama mboga ni dalilli ya umaskini?

Hayo nilishayazungumza kule juu yote.
Ni sawa unarejelea kilichozungumzwa.
Pia wewe unatakiwa utizame kwa umri wako na kazi ufanyayo na afya yako unahitaji zaidi aina ipi ya chakula kuliko kingine,na vilivyobaki ule kwa kiwango gani.
Nini maana ya Balanced ? Nadhani hapa tunaanza kwenda pengine wakati mimi nilisema neno moja tu kukujibu kwamba mlo muhimu kuliko yote katika siku ni Breakfast; hayo mengine sasa tunaanza kuingia kwenye technicality
 
Nini maana ya Balanced ? Nadhani hapa tunaanza kwenda pengine wakati mimi nilisema neno moja tu kukujibu kwamba mlo muhimu kuliko yote katika siku ni Breakfast; hayo mengine sasa tunaanza kuingia kwenye technicality
Aya umepatia mkuu mchana mwema.
 
kuna sehemu nilitaka kununuA nyama choma peke yake, nikaambiwa lazima ninunue na ugali
Au nenda kwenye haya mahoteli tunayokula tukisafiri kwa mabasi ya mikoani,halafu jifanye mjanja kuomba chips kavu peke yake.Hawataki,ni lazima ununue na nyama ya kuku,ng'ombe,samaki n.k
 
kuna sehemu nilitaka kununuA nyama choma peke yake, nikaambiwa lazima ninunue na ugali
Unaweza kwenda kwa mama ntilie ukaomba ununue maharage peke yake ? (Nadhani hapo kwa maneno mengine ni kwamba bei ya ugali na nyama choma na ugali pekee bei ni ileile labda wewe ungetoa pesa ya nyama choma na ugali alafu ukawaambia niwekee nyama peke yake watu kama nyie tukiwapa loophole hamchelewi kuomba mnunue chumvi mkapike nyumbani...
 
Kwenye hoteli kubwa zote, na nyingi za kati menu ya chakula kikuu huwa ni samaki, kuku, nyama ya ng'ombe, mbuzi kitimoto na nyinginezo halafu ndio unachagua utakula na nini ikiwa ni ugali, wali, viazi n.k

Kwenye hizi hoteli bei ya chakula inapimwa kwa samaki, kuku na nyama kisha (wanga) ambao ni ugali, wali, ndizi, viazi n.k inakuwa nyongeza tu, ina maana hata usipokula wanga utalipa bei ile ile tu ya nyama, kuku au samaki. Kama wewe sio mla nyama bei itabadilika.

Sasa kwa mama ntilie inakuwa kinyume chake, chakula kikuu ni wanga ambao ni ugali, wali, ndizi n.k halafu nyama, kuku, samaki inakuwa kama nyongeza tu. Halafu huwezi kusema unataka kula nyama, kuku au samaki tu, ukitaka hivyo huwezi kuuziwa chakula na inaweza kuzua hata ugomvi!

Na nyumba nyingi za Watanzania ulaji ni kama huo wa mama ntilie, hii inaweza kumaanisha uduni wa maisha japo tunajigamba kuwa na chakula kingi.
Dah ,,,,,too much thinking is harmful
 
Back
Top Bottom