Samaki, nyama, kuku na maharage kuliwa kama mboga ni dalilli ya umaskini?

Samaki, nyama, kuku na maharage kuliwa kama mboga ni dalilli ya umaskini?

Kikawaida asubuhi hutakiwi kula sana unatakiwa upate wanga kiasi kidogo na protini kiasi kidogo.
Mathalan chai,mkate wenye blue band ama jam na yai inatosha.
Mkate protein na blueband ina protein na fats yai lina protein.
Inatosha kwa hiko kiwango.
Breakfast is the most important meal of the day sababu una break the fast....
 
Kwenye hoteli kubwa zote, na nyingi za kati menu ya chakula kikuu huwa ni samaki, kuku, nyama ya ng'ombe, mbuzi kitimoto na nyinginezo halafu ndio unachagua utakula na nini ikiwa ni ugali, wali, viazi n.k

Kwenye hizi hoteli bei ya chakula inapimwa kwa samaki, kuku na nyama kisha (wanga) ambao ni ugali, wali, ndizi, viazi n.k inakuwa nyongeza tu, ina maana hata usipokula wanga utalipa bei ile ile tu ya nyama, kuku au samaki. Kama wewe sio mla nyama bei itabadilika.

Sasa kwa mama ntilie inakuwa kinyume chake, chakula kikuu ni wanga ambao ni ugali, wali, ndizi n.k halafu nyama, kuku, samaki inakuwa kama nyongeza tu. Halafu huwezi kusema unataka kula nyama, kuku au samaki tu, ukitaka hivyo huwezi kuuziwa chakula na inaweza kuzua hata ugomvi!

Na nyumba nyingi za Watanzania ulaji ni kama huo wa mama ntilie, hii inaweza kumaanisha uduni wa maisha japo tunajigamba kuwa na chakula kingi.
Kichwa cha thread kinauliza swali tofauti na contents za thread. Sasa wewe unataka tujibu nini wakati umetoa habari ya kuhabarisha tu? Ndio maana mnafeli vyuoni jamani.
 
Protein mzee,we ukitaka kula mboga tu ni wewe.
Mama ntilie hawezi kukupa samaki mzima 3000 yako ye atapata wapi faida.
Mfano.
Nilikula mama ntilie kwa kupenda tu.
Chakula sahani
Wali nazi mwingi tu.
Maharage na mchicha na hata tunda unapewa.
Kataka kuweka nyama nikawaachia wengine.
Nikaongeza kipaja choma kwa mwingine.
Total 3500 tu.
Nikatoka nimeshiba vibaya.
Okay nilimpa 5000 no change.
Toka hapo ikawa ni treatment km VIP.
Kwa Shilole ningekula same kwa 10000 mpk 15000 nusu kuku.
Same food,
karambezi,samaki samaki,
Etc 25 000-30 000.
Mtanzania gani anamudu bei hiyo kwa mlo mmoja tu.
 
Mazoea tu...
Kama vile wanavyopima wali au ugali na nyama mbili, kwani ukiwekewa kumi kuna shida gani...


Cc: Mahondaw
 
Pia unatakiwa ule kiafya sio kwa kulimbikiza vyakula tumboni.
Sasa kuna zaidi ya kiafya zaidi ya balanced diet ?

Pili inategemea unafanya kazi gani chakula ni nishati na maisha ya watu tofauti yana matumizi tofauti ya nishati Kwahio sio chakula tu bali unahitaji exercise ku-burn excess fat...
 
Sasa kuna zaidi ya kiafya zaidi ya balanced diet ?

Pili inategemea unafanya kazi gani chakula ni nishati na maisha ya watu tofauti yana matumizi tofauti ya nishati Kwahio sio chakula tu bali unahitaji exercise ku-burn excess fat...
Hayo nilishayazungumza kule juu yote.
Ni sawa unarejelea kilichozungumzwa.
Pia wewe unatakiwa utizame kwa umri wako na kazi ufanyayo na afya yako unahitaji zaidi aina ipi ya chakula kuliko kingine,na vilivyobaki ule kwa kiwango gani.
 
Back
Top Bottom