Samia hataki kabisa kusikia habari za urais 2025

MSAGA SUMU

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2015
Posts
6,661
Reaction score
21,656
Kutoka korido za CCM Chamwino, mama ameanza kuwaambia wandani wake kuwa habari za kugombea urais 2025 hataki kabisa kusikia, tena anadai Kama ingekuwa ni kitu chepesi basi angestaafu hata Jana. Madai yake makubwa ni jinsi kila Jambo analogusa linashindwa kabisa kufanyika.

Miradi iliyokuwa inaenda vizuri kabla ya yeye kushika usukani imekwama, Dar haina maji, nchi haina umeme. Watu wanajenga shade ya mlinzi kwa mil 11, watoto mikopo yao vyuoni haileweki, kwa mujibu wa ilani ya chama chake ilitakiwa vijiji vyote viwe na umeme lakini mpaka Sasa mambo yanasusua

Kitu kinachomuumiza mama akili ni jinsi gani anavyojitahidi kukopa lakini hela zikifika nyumbani hamna Cha maana kinachofanyika zaidi ya TRAB na TRAT.

Mama kaamua 2025 anarudi nyumbani kupumzika kulea wajukuu na kufanya majukumu mengine madogo madogo Kama ya usuluhishi wa kimataifa atakapochaguliwa na rais anayefuata.

Pia mama anataka legacy yake kubwa iwe ni rais pekee aliyejenga madarasa mengi kwa muda mfupi tangu tupate Uhuru.
 
Na iwe kweli uyasemayo
 
kama ni kweli watu wengi watafrahi
 
Mbona hilo lilifahamika kitambo sana !
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…