Saninu Laizer wa madini lipa pesa za watu. Ulituonyesha una madini ya mabilioni leo hii mchina anataka bilioni 8 zake

Saninu Laizer wa madini lipa pesa za watu. Ulituonyesha una madini ya mabilioni leo hii mchina anataka bilioni 8 zake

Huyu walimrusha rusha tu
Kaongezewa na masifuri
WakTi wakina manga waliuza mawe ya zaidi ya bln 20 na walikuwa kimya

Any way hyo lazier amlipe mchina wa watu hela yake

Ova
Alikumbwa na siasa za wakati ule
 
Lazier lipa bana atujazoea kuringishana huku tunadhulumu watu

ARUSHA: Mfanyabiashara Maarufu wa Madini ya Tanzanite katika Mji wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Saninu Laizer maarufu kwa jina la Bilionea wa Tanzanite amemwangukia Mwekezaji raia wa China, Jun Fang akiomba wakae mezani kutafuta suluhisho ya mgongano wa kimaslahi kati yao.

Bilionea Laizer ameyasema hayo Jijini Arusha baada Fang kutaka kutaka kuomba msaada wa Balozi wa China nchini ili apate haki yake ya fedha na mali vyenye thamani ya Sh bilioni 8.5 ambazo (Laizer) anadaiwa kuonesha dalili za kutaka kumdhurumu.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Arusha Laizer alikiri kuingia ubia na mwekezaji Fang toka mwaka 2011 hadi mwaka 2021 kwa mwekezaji huyo kumiliki hisa asilimia 70 na yeye kama mzawa kumiliki hisa asilimia 30 kwa makubaliano kuwa Fang kuleta vifaa vyote vya kisasa vya uchimbaji,mtaji na kulipa gharama zote za uendeshaji ikiwemo mishahara ya wafanyakazi na alifanya hivyo.

Alisema baada ya mkataba kumalizika mwaka 2021 alimtaka mwekezaji Fang kuingia makubaliano (MOU) ya awali ambayo hakuyataja lakini raia huyo wa China aligoma kusaini makubaliano hayo.

‘’Mimi niko tayari kufanya kazi na Mchina wakati wowote na aje mezani tutatue changamoto zilizopo na tufanye kazi ya uchimbaji madini ya Tanzanite katika kitalu D kama zamani’’alisema Laizer.

Picha na John Mhala
Una maoni usisite kutuandikia
-
#MwangwiwaUkarimu
#echoesofkindness
#HabarileoUPDATES

View attachment 2881674
Mabalaa yameanza kumwandama
 
ile ilikuwa ni mambo ya kisiasa tu, jamaa mgodi ulikuwa unaendeshwa na huyo mchina na washirika wengine, yale mawe waligawana na huyu mchina na washirika wengine
Mi nilihisi tu yale mawe yalikuwa ya watu wakubwa zile zilikuwa mbinu tu za kuyatoa Nje ya Geti pesa zitumike kwa mambo ya wakati ule.
 
Kuna maajabu yalitokea wakati wa Magufuli kwa sasa siyaoni kabisa.

1. Huyo Leizer aliibuka wakati Magu sasa hivi hoi

2. Chato ilikuwa na mwanafunzi wa kwanza kitaifa kwa sasa sijui watoto hawafundishwi huko?
kilio kwa waliowekeza chato wahurumieni tu [emoji16]

3. Mashirika ya uma yalitoa gawio sasa hivi CAG ndo anaonekana mnoko

4. Kigogo sasa hivi ni kinukta sijui hayupo duniani?

5. ATC sifa zilikuwa sijui nisemeje mnielewe!

6. Makonda alilia sasa hivi anatufokea [emoji16]

7.

8.

9.

10.

Sijui ilikuwa uhalisia? Ila maigizo yalikuwa mengi mno hiyo awamu Leizer pambana na hali yako.

Sasa tusubiri zam ya anaupiga mwingi huyu nae aking’atuka tu ndo mambo yatakuwa wazi hasa upande wa upigaji hela jiandae kuacha vinywa wazi nawahakikishia hamtamuona huku Lucas Mwashambwa na pambio zake hizi.

Let’s wait!
 
Bilionea chawa haijawahi kutokea. Alipe pesa ya watu kwanza ndio wakae wajadili mkataba mpya aache janjajanja. Mtu alipata chance nzuro akaishia kujiweka kwa media kama baba levo. Minyii
 
Back
Top Bottom