Sasa barabara ya Lusahunga – Rusumo yenye urefu wa kilomita 92, kujengwa kwa Bilioni 153

Sasa barabara ya Lusahunga – Rusumo yenye urefu wa kilomita 92, kujengwa kwa Bilioni 153

Waweke pia mizani za kutosha magari ya Burundi na Rwanda wao wanapakia mizigo ya kuzidi kulingana na barabara zao. Walime kuipunguza makali na kuitanua ile down ya machinjioni pale kuelekea Rusumo.
Hiyo ni component ya Lazima mzee
 
Waweke pia mizani za kutosha magari ya Burundi na Rwanda wao wanapakia mizigo ya kuzidi kulingana na barabara zao. Walime kuipunguza makali na kuitanua ile down ya machinjioni pale kuelekea Rusumo.
Pale machinjioni, nimeshuhudia Magari magubwa 84 yaliyoanguka. Pale Machinjioni jina lake halisi ni Msitu wa nyati. Ipo karibu na Magereza ya Rusumo.

Kipindi hicho nilikuwa nakaa line Magereza upande wa KMKM. Ukitoka bwawa la mzungu kamatendeli, machinjioni Kahaza unashuka Rest house Makaburi ya kibari kuelekea Rusumo boda.

Kuna watu barabara za zege wameziona kipindi cha mwendikasi, ila sisi tumeziona Rusumo tangu 1992 pale boda.
 
Mradi mwingine huu hapa huko Kagera View attachment 2523092
Zikikamilika hizo zote kagera itakuwa imeunganisha na lami wilaya zote...inabaki barabara za vijiji ambazo zimeanza kujengwa huko uhayani muleba, misenyi na bukoba vijijini...

Kagera sasa inaunganishwa na meli ya mv Victoria na mv mwanza...inaunganishwa na uwanja wa ndege wa bukoba na mwingine mpya unasubiriwa..


Bado reli tu...
 
Pale machinjioni, nimeshuhudia Magari magubwa 84 yaliyoanguka. Pale Machinjioni jina lake halisi ni Msitu wa nyati. Ipo karibu na Magereza ya Rusumo. Kipindi hicho nilikuwa nakaa line Magereza upande wa KMKM. Ukitoka bwawa la mzungu kamatendeli, machinjioni Kahaza unashuka Rest house Makaburi ya kibari kuelekea Rusumo boda. Kuna watu barabara za zege wameziona kipindi cha mwendikasi, ila sisi tumeziona Rusumo tangu 1992 pale boda.
Pa hovyo sana pale jamaa angu. Wanasema haipitagi wiki pale lazima truck zipige chini pale.
 
Sawa na kilomita 153 ,billion Moja hujenga kilomita Moja ya Barabara kiwango Cha Lami
ni kweli illa siku hizi ujenzi umeboreshwa sana, unaweza kuta gharama inaongezwa na pavements, madaraja makubwa na madogo, Taa za barabarani, mifereji, kiwango cha lami yenyewe, upana wa barabara so ni vigezo vingi vinaweza ongeza gharama ya barabara kwa kila kilomita
 
Acha uongo,Kila siku wanaeleza hivyo..
Mbona Huwa mnasema miradi ya Magufuli?
Jiwe was an ass-hole(he is still an ass-hole in the grave) yeye ndiyo muanzilishi wa huu upuuzi sasa kila mteuliwa anaona ya kwamba survival tactics kwenye nafasi aliyoteuliwa ni uchawa before anything else.
 
Jibu swali kama huna majibu unanyamaza, hiyo ramani inajieleza na kuna uzi humu unazungumzia switch kuwa installed Rwanda

Hilo bwawa kwani lishaisha kwani maana naona kila siku wanasema wapo hatua za mwisho
 
Jibu swali kama huna majibu unanyamaza, hiyo ramani inajieleza na kuna uzi humu unazungumzia switch kuwa installed Rwanda

Watu hawajui kuwa hata lile bwawa limejegwa upande ule , kutoka na eneo tuu.
Kwa TZ Kuna milima utajengaje bwawa.
Watu wanaongea bila fact.
Na kupisha
 
Serikali ya Tanzania imesaini mkataba wa ujenzi wa barabara ya Lusahunga – Rusumo yenye urefu wa kilomita 92 kwa kiwango cha lami mradi utakaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 153.

Akiongea na wananchi wa mkoa kagera katika hafla ya utiaji saini iliyofanyika katika mji wa Benaco wilayani Ngara, waziri wa ujenzi na uchukuzi Prof. Makame Mbarawa amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuiunganisha Tanzania na Nchi Jirani ili kuweza kuinua uchumi wa wanakagera na watanzania kwaujumla.

Waziri Mbarawa Ameongeza kuwa baada ya kusainiwa mkataba huu kati ya serikali na mkandarasi ajulikanae kama Chines Civil Engineering Company LTD, Mradi huu utatakiwa kuanza kutekelezwa ndani ya miezi mitatu.

Amesema lengo la kujenga barabara hii upya ni kuwaondolea wananchi adha kubwa ya usafiri na usafirishaji ikiwa ni kufungua fursa upya za biashara.

Aidha amesema kuwa barabara huyo ni muhimu kwa nchi za Africa Mashariki katika kusafirisha mazao ya kilimo na kuongeza kipato kwa watanzania wa maeneo haya.

Kwa upande wake mtendaji mkuu wa TANRODS Mhandisi Logatusi Mativila amesema kuwa mradi huo utatekelezwa kwa kipindi cha miezi 24 huku mbunge wa jimbo la Ngara Mhe. Ndaisaba George Ruholo akiomba vijana wa wilaya za Ngara na Biharamulo wapate ajira pindi mradi huo utakapoanza.

Pia, soma:

1). Kwa hilo la barabara ya Lusahunga hadi Rusumo Serikali inacheza na hatari!

2). Barabara Rusahunga Benaco haipitiki kwa nini Tanroads Biharamulo wasitumbuliwe?

3). Ushauri wa Bure kwa Polisi barabara ya Ngara - Isaka Kipande cha Benaco Nyakanazi
KUMBE ILIKUWA BADO, AISEE IMETAJWA KWA MUDA MREFU SANA.
 
Back
Top Bottom