Sasa hivi kupita mkesha/sikukuu bila ngumi imekuwa kawaida sana kitu ambacho miaka hiyo ilikuwa ni Nadra mno

Sasa hivi kupita mkesha/sikukuu bila ngumi imekuwa kawaida sana kitu ambacho miaka hiyo ilikuwa ni Nadra mno

Hii michezo hasa mpira wa miguu ilijaa ubabe sana. muda wowote ungeweza kutokea ugomvi mkubwa na mechi ikaishia hapohapo. baadhi ya marefa waliishia kukimbizwa kama wezi au hata kupata kichapo cha mbwa mwizi😆

kwa sababu hii baadhi yao walijihami kwa kuning'iniza silaha kama vile kisu kwenye upaja wakati anachezesha pale uwanjani. hii ilimjengea heshima refa huyu kwa wale wachezaji maana wanajua jamaa ana "moto"

na hii ilikuwa hata kwenye hii michezo ya ligi kuu mambo yalikuwa ivoivo. mambo yangeweza kubadilika muda wowote na mechi ikaishia hapo. refa akizingua anakula kichapo mechi inaishia hapo au anatafutwa refa mwingine mechi inaendelea kupigwa na wachezaji nao ni ivoivo wakizinguana zinachapwa mechi inaishia hapo.

sasa mambo yamebadilika sana.
 
Sijui ni kwamba watu wameokoka sana hata sielewi kabisa.Miaka ya nyuma mkienda kwenye mkesha ama sikukuu ilikuwa ni lazima ushuhudie ngumi za wanaume zikipigwa katikati ya senta .

Haikuwa sio ajabu kuona wala kusikia kuwa akina J n p jana walizipiga kwenye mkesha.Ni miaka sasa imepita bila kusikia wala kuona ngumi zikipigwa asee hadi najiuliza ama tiyari dunia imegeuka kuwa paradiso?

Leo hii hata ukienda club hadi unarudi hakuna ugomvi wowote utakao ushuhudia asee.Zamani hata mkesha wa disco wa darasa la saba tu tulikuwa tunashuhudia ngumi zikipigwa sana tu.Tena ilikuwa marufu kidato cha nne kukesha kwenye mahafari yao lakini kwa sasa imekuwa kawaida tu madogo wanakesha na walimu wana amani tele.

Kipindi hicho hakuna mwalimu yeyote angeweza kubali kurusu eti tukeshe kwenye mkesha wa kidato cha nne.Pamoja na kwamba sisi tulikuwa tunaanza disco saa4 asbh hadi saa12 jioni lakini bado ngumi zilipigwa tu.

Enzi hizo kulikuwa na mbabe wa mtaa mzima au hata kijiji kizima anafahamika kabisa kuwa flani ndo mbabe wa huu mtaa/kijiji. sasa hivi ni hamna. Nimemiss zana ubabe wa enzi hizo.

Baba mdogo aliwapiga migambo hadi wakapoteana na hapo walikuwa wanne leo hii mgambo mmoja tu anakuijia na anaenda kakupiga jeck njia yote na unatii au yeye anakuwa na baiskeli anakuswaga kama ng'ombe na unakubali tu.Kunakipindi mgambo na police mmoja mwenye siraha walikuja kukamata waunza gongo kipigo walichopata hawakurudia kuja tena kukamata walio bahatika kutokupigwa ni hawa walikuwa na police kwenye kukamata lakini wale waliojitenga wakiwa na marungu tu walipigika vibaya mno vile hata simu hazikuwepo walipigwa mno.

DJ alikuwa akibadilisha wimbo bila mpangilio lazima kipigo kimuhusu na ma DJ wa kipindi hicho walikuwa wababe. Kuna mkesha mmoja zilipigwa kanisani padri anaendelea na ubatizo kisa jamaa mmoja alijamba tu...
tukiwa tunaimba kwaya mara wazamiaji wa kwenye mkesha wakanzisha huko ikabidi ibada isimame.. jenerata ikazimwa makusudi na wababe kukawa giza zilipigwa ovyo ovyo yani unatembea huku unarusha ngumi kujiokoa wachache walikuwa na tochi walisaidia japo nao walikuwa wanamulika watoke mbio hakuna namna..

Finaly Mkong'oto nilioupata mimi kwa kuanzisha vanga ilikuwa mwaka 2011 mr chocolate(Bob junio) walikuwa wamekuja na bonge la nyau mahala fulani kufanya show. kwnye mida ya usiku kama saa7 wakatoka club likabaki la manyani sasa........ nilipigwa na jamaa niliyedhani na mu mudu asee masela wangu wote wakaniachia msala siku 3 uso umevimba sitoki nje masela wananiuguza japo walinikimbia asee.

MAMBO YANABADIRIKA SANA
sio hilo tu,ata vichaa wamekuwa wapole sana,ila machungaji wamekuwa wapigaji!!!
 
Zamani hakukua na bifu za wanaume peke ake hata wa kike..unakuta kuna mdada darasani anaeogopewa basi unakuta wadada wengine wanajipendekeza kwake nyie ambao hamna habari nae anatafuta visa tuu mpk mpigane ili upigwe...
 
Hii michezo hasa mpira wa miguu ilijaa ubabe sana. muda wowote ungeweza kutokea ugomvi mkubwa na mechi ikaishia hapohapo. baadhi ya marefa waliishia kukimbizwa kama wezi au hata kupata kichapo cha mbwa mwizi😆

kwa sababu hii baadhi yao walijihami kwa kuning'iniza silaha kama vile kisu kwenye upaja wakati anachezesha pale uwanjani. hii ilimjengea heshima refa huyu kwa wale wachezaji maana wanajua jamaa ana "moto"

na hii ilikuwa hata kwenye hii michezo ya ligi kuu mambo yalikuwa ivoivo. mambo yangeweza kubadilika muda wowote na mechi ikaishia hapo. refa akizingua anakula kichapo mechi inaishia hapo au anatafutwa refa mwingine mechi inaendelea kupigwa na wachezaji nao ni ivoivo wakizinguana zinachapwa mechi inaishia hapo.

sasa mambo yamebadilika sana.
Hii imekuja kuishia enzi za akina Ben mwalala,mwaikimba nk. siku ya daby kuisha bila ngumi uwanjani ilikuwa nadra sana
 
Zamani hakukua na bifu za wanaume peke ake hata wa kike..unakuta kuna mdada darasani anaeogopewa basi unakuta wadada wengine wanajipendekeza kwake nyie ambao hamna habari nae anatafuta visa tuu mpk mpigane ili upigwe...
Kweli kabisa zamani mwanamke alikuwa akisikia mme wake anatoka na fln hakuna kusuntana wala mipasho ni ngumi tu
 
Sema imepungua coz wameona usela vima umepitwa na wakati ,ila ukifatilia taarifa za polisi mkesha wa mwaka mpya masela wameuana sana ,kuna jamaa alikuwa BETO akakata kamba mkesha wa mwaka mpya.
 
Back
Top Bottom