Sasa wageni kununua dhamana za serikali

Sasa wageni kununua dhamana za serikali

Kwamba tumewaruhusu wageni kuja kuwekeza kwenye dhamana zetu ili nasi tupate sababu ya kwenda kuwekeza kwenye dhamana zao, sijui kama nchi zilizotajwa nao wanaruhusu hiki kitu.

Hatua hii ya serikali kwangu naona ni sawa na kuweka uchumi wetu rehani, itakuwa vipi hao wawekezaji wakiamua kuondoa dhamana zao bila serikali kujiandaa?

Hali hii naona inasababishwa na udogo wa uchumi wetu, tumekuwa tegemezi sana, kuanzia kuchukua mikopo kwenye mabenki ya biashara, hadi kwenye taasisi za kimataifa, na kwa vile wapo wanaoona kukopa ni sifa, basi tujiandae kudumaa zaidi.
Tuweni optimistic aisee!! Kwamba kuruhusu EAC au SADC kununua Hati fungani ndio kutegemea wageni?? Mbona ni reforms kote Africa mashariki why sisi ndio tuone tunaibiwa? Kwanini tusione ni fursa kununua Hati fungani za Burundi huko au Kenya??

Tujifunze kuaminiana, Sheria zile zile zinazotumika kwa Mtanzania zitatumika kwa wageni. Mbona hatuogopi waTanzania kuondoa dhamana zao ila tuogope wa nje? Hizi mentality za kwamba wageni ni wezi sio sahihi otherwise waTanzania wasingepewa ajira huko ulaya maana wangesema watahujumu nchi!!!
 
Kwamba tumewaruhusu wageni kuja kuwekeza kwenye dhamana zetu ili nasi tupate sababu ya kwenda kuwekeza kwenye dhamana zao, sijui kama nchi zilizotajwa nao wanaruhusu hiki kitu.

Hatua hii ya serikali kwangu naona ni sawa na kuweka uchumi wetu rehani, itakuwa vipi hao wawekezaji wakiamua kuondoa dhamana zao bila serikali kujiandaa?

Hali hii naona inasababishwa na udogo wa uchumi wetu, tumekuwa tegemezi sana, kuanzia kuchukua mikopo kwenye mabenki ya biashara, hadi kwenye taasisi za kimataifa, na kwa vile wapo wanaoona kukopa ni sifa, basi tujiandae kudumaa zaidi.
Siku zote tulikuwa hatujaruhusu wageni kununua dhamana za Serikali na tukafika hapo tulipofika. Sasa tunajaribu kudikiria nje ya sanduku kuwa "what if" tukiruhusu wageni nao washiriki minada ya dhamana za Serikali.

Personally naamini BOT wamefanya research na wameangalia nchi nyingine zinafanyaje na ndiyo wameona na sisi tujaribu. Naamini wame assess risk na kuweka mitigation measures.
 
Marekani kule kiboko

Ukinunua municipal bond ya dola laki tano unapewa green card na permanent resident permit

Bond wanatumia kuuza uraia
Ila siku ukiwekewa vikwazo na pesa zako zinakuwa 'frozen'
 
Kumpa mgeni haki sawa na mwenyeji ni makosa ambayo hakuna serikali inafanya hapa duniani.
Serekali nyingi zilizobaki Africa ni za Kibepari siyo za kijamaa tena, is all about mkwanja! Lolote lile linawezekana!!!
 
Mawazo ya kimaskini
Huu ndio ukweli.

Hizo hati fungani walizonunua Ma-oligarch wa Urusi huko Marekani na Ulaya zote zimepigwa kufuli na huenda zikataifishwa hapo baadae na kupewa Ukraine.
 
Kote duniani wananunua Kama hujui soma u humi ili ujue parameters za u humi. Mgeni kuwekeza kwenye bonds ni sawa na fdi yaani foregn direct investment ambapo Kuna risk zake na faida zake pia. Kwa hiyo unataka kusema tusiruhusu hata wawekezaji waje kwa sababu wanaweza kuondoka ghafla!! Sasa nini maana ya sheria za uwekezaji kuwekwa. Kuna kitu kinaitwa security policies ambazo ndo zinagovern uwekezaji huo.

Huo ni uninga wako tu kutoelewa Mambo. Soma hata certificate ya financial management au economics.
 
Navyoelewa mimi kuwekeza katika hati fungani mtu yeyote anaweza kuwekeza tu popote,yaani utoke hapa uende marekani,uingereza,Japan,au China au Australia ukawekeze kwenye hati fungani zao wakukataze hilo halipo.
Kimkakati inawezekana sana tu watu kuwekeza nchi yoyote kwenye hati fungani.
Zingatia Neno kimkakati.
Kwa hapa Tanzania wawekezaji wakubwa wa Hati fungani ukiachana na Tàasisi za kifedha kubwa kubwa na makampuni makubwa watu binafsi wengi tu wanawekeza hasa hasa wahindi,na hao hao ndio wanawekeza sana katika hati fungani nchi za nje hasa hasa Uingereza na Canada.
Kimkakati unawezaje kuwekeza nje ya Tanzania kwenye hati fungani?
Wao wanakwenda kufungua offshore companies huko nje alafu wanaweka mtaji katika hizo companies then hizo companies ndizo sasa kisheria zinaruhusiwa kuwekeza katika hati fungani katika nchi hizo za nje.
Na hata wao sasa wageni wengi hata kabla ya hii kanuni nao waliweza kufanya the same strategy ya kuja kuja na offshore companies ambazo zinanunua shares kwenye holdings companies za hapa bongo wakiwa shared na wabongo then wanaweka capital ambazo hizo holding companies za hapa bongo zinawekeza katika hati fungani za hapa.
Hizo ni international business strategies tu ambazo mara nyingi hata zinawafanya wasilipe kodi nyingi sana kwenye uwekezaji wao.
Mimi naona hii notisi ni kama kutia chachu tu kwa investors wa ndani na nje hasa residents kutoka sadc and east Africa member countries kuja kuwekeza sana kwenye hati fungani zetu.
Ila practically hata pasipo hiyo notisi pia mimi kama mimi kama nina capital yangu kubwa sihitaji kanuni ya bank of Tanzania inipe approval nikawekeze kwenye treasury Bonds za Kenya,Japan,UK,Canada,USA popote pale.

It is possible.

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
Huyu mleta Mada asipokuelewa tena, bora basi tu
 
Kwamba tumewaruhusu wageni kuja kuwekeza kwenye dhamana zetu ili nasi tupate sababu ya kwenda kuwekeza kwenye dhamana zao, sijui kama nchi zilizotajwa nao wanaruhusu hiki kitu.

Hatua hii ya serikali kwangu naona ni sawa na kuweka uchumi wetu rehani, itakuwa vipi hao wawekezaji wakiamua kuondoa dhamana zao bila serikali kujiandaa?

Hali hii naona inasababishwa na udogo wa uchumi wetu, tumekuwa tegemezi sana, kuanzia kuchukua mikopo kwenye mabenki ya biashara, hadi kwenye taasisi za kimataifa, na kwa vile wapo wanaoona kukopa ni sifa, basi tujiandae kudumaa zaidi
Watanzania tuache uvivu
Umeambiwa hata wewe unaweza kufanya kwa nchi zingine za Afrika Mashariki na Jumuiya ya kusini mwa jangwa la Sahara hii SERA sio ya Tz pekee yake ni makubaliano ya nchi zote hizo.
Kama mtanzania una vigezo kanunue pia Rwanda Kenya Uganda n.k
 
Hati fungani means treasury bonds, Unawekeza fedha zako kwa lengo ili upate faida kwa uwekezaji wako, risk yake ipo wapi hapa? Mtaji wako unakuwa umeshikwa na Bot, kwa kipindi maalumu,huku ukilipwa percentage zako,
BINAFSI SIONI UHATARI WAKE
Kitaalamu ni Risk free investment, watu inabidi wasome mambo ya bond and bills kidogo kutanua knowledge maana mtu anaona kama ametekwa kumbe yeye ndo kateka [emoji1787]
 
Nchi zote tajiri duniani ndio zinavyokopa ivyo kwa kuuza hati fungani kwa yeyote mwenye uwezo wa kununua duniani. Be it wanunuzi wakubwa ni pension funds zenye mitaji mikubwa, mabank, other investment institutions na serikali ya China.

Nchi maskini hazina uwezo wa kuuza kwenye soko la dunia, ideally kila mtu angependa kuuza huko ni kukopa kwa mtindo wa kujipangia interest za deni mwenyewe.

Huko na kwenyewe kuna rating agencies wenye majina kama ‘Moody’s’, Fitch na ‘Standard and Poor’ wenye kuliambia soko huyu AAA anauewezo wa kulipa deni kirahisi, na huyu ana credit CCC una mkopa at your own perils.

View attachment 2255845

Tanzania ipo ranked kwenye number 15 last time we tried to get access into international market. Sasa kama kuanzia number 5 kupata mkopo kutoka makampuni makubwa utata ukiwa number 15 sahau kabisa.

Kwa ivyo nadhani lengo ni kukopeshana wenyewe kwa wenyewe ndani ya jumuiya ni jambo zuri, ila bond zetu zina interest kubwa sana kwa sababu ya poor credit rating. Otherwise tumechelewa.
Chief wabongo wengi bado wana mawazo km nyerere ya kijamaa hawaelewi uchumi wa wa kisasa unavyoendeshwa kwa kifupi wana mawazo mgando, ya kijima hawataki mawazo mapya....na izo bond zipo miaka na miaka na walikuwa hawanunui. Leo hii zimewekwa sokoni kila mmoja anunue imekuwa nongwa.
 
Back
Top Bottom