Tetesi: Saudi Arabia yapewa haki ya umiliki na uendeshaji wa bandari ya Bagamoyo kama sehemu ya mradi wa East Gate

🚮🚮
 
We are not interested na kumjua mmiliki wa kampuni, kampuni Huwa Zina Wana hisa wengi ,tunachotaka kuona ni urasimj unakwisha bandarini na Mapato yanaongezeka full stop.

Kwa sasa hata watu wetu wasiojulikana mnasema hamna haja ya kuwajua lakini Karma hua haiongopi mkuu . Kumbuka rasilimali za asili zimewekwa na Mungu na sio familia ya mtu .
Viwanda na ugunduzi na teknolojia kama ya wajapani au wakorea zile sio rasilimali za umma.

Rasilimali za umma ni mali ya umma . Tutamjua na siku inakuja na sio Mbali .
Historia inajirudia na mabadliko pia yanajirudia .
Yanayotokea huko Afrika ya Kati na magharibi yatasambaa Afrika nzima .
Kizazi hiki kinachokuja hakijui mambo ya imani za wageni na kuona wageni wakistawi huku wenyeji wakiwa watumwa wao.

Bandari haina tija yoyote kubwa .Ni Rushwa ndiyo inayowapogusha macho tu.

Hivi mtu anakusanya mil. 100 halafu 40 % anazipeleka Uarabuni 60 % inabaki wakati aliyeijenga bandari ni sisi wenyewe . Au tumejenga wenyewe halafu Watanganyika wenzetu wanakusanya mil. 100 wanakula kwa urefu wa kamba yao humu humu nchini na kusaidia familia na ndugu zetu humu na kujenga humu humu ,wanaona na kualewa humu humu ,wansomesha watoto na ndugu zao humu humu halafu inabaki wanakula 40 % na kupeleka serikalini 60% kipi ni bora tukiachana na ushabiki na chuki za kusema wale ni waarabu .

Lakini pia Wazawa waliharibu tuna mamlaka ya kuwafukuza kazi na kufilisi mali zao na hata kuwafunga . Kwa nini tunaacha kuwawajibisha au ni kutaka kuwafurahisha waliowaweka ndugu zao . ?Mbona akija mgani ni waafrika wale wale ndio wanaofanya kazi na yeye amekaa tu ofisini ?
Watu wetu wanauwezo tatizo ni siasa na chuki .
 

Mkopo wa kuongeza kina ili Ro-Ro barth ijengwe kupitia DMPG mkataba umesainiwa 2017 na Magufuli. Bado na barth zingine pia zilikuwa zinaongezewa kina.

Hilo limepunguza muda wa kushusha Magari na demurrage charges za bandari.


Gantry Cranes zilizopo hapo leo kanunua Magufuli ambazo zimepunguza meli kusubiri kutoka wastani wa siku 21+, mpaka siku tano leo.


Kabla Magufuli ajaona faida ya cranes mpya wala Ro-Ro, bandari ilitoa gawio la tsh 700 billion.

Imagine leo kuna Ro-Ro, Gantry Cranes, Idadi ya meli imeongezeka, demurrage charge zimepungua; lakini mapato yalishuka mpaka tsh 200 billion.

Halafu unaenda gawa port bure kabisa ambayo, ambapo kiongozi angekuwa mkali si ajabu sasa hivi mapato ni zaidi ya tsh 1.5 trillion.

Nchi ya pwagu na pwaguzi.
 
Yaan sijui mtu mweusi atashituka lini kwamba hakuna mtu mweupe au so called mwekezaji atatufanyia kazi sisi afu eti tutajirike haipo hiyo.ivi haiwezekani kabisa sisi kuendesha bandari na sekta zingine bila msaada wa mzungu au mwarabu???Mungu aingilie kati haya yote na atufanyie wepesi kama nchi
 
Mkataba wa hili jambo nao ni Siri? Vipengele tunaweza kuviona vya namna watakavyotumia haki ya kumiliki?
Haijafikia hiyo stage,ilifika mtaarifiwa.

Mikataba yote ni Siri au wewe u ajua mkataba gani ulio wazi?
 
Hiyo 60% ni kubwa zaidi kuliko wakati mpo.

Si mlikuwepo hapo kabla ya wawekezaji,Kuna jipya na ufanisi upi mlileta?

Swala la kujengwa Bandari ni sawa na kujenga reli na kuwapa watu kuendesha au.kujenga epz na kuita wawekezaji au kujenga nyumba na kumpa mpangaji
 

View: https://www.instagram.com/p/DGCn_EIIY12/?igsh=YzY2OGQ4eXc0ZGpq
 
Hii siyo sawa. For national security reasons, kuna vitu ambavyo havipaswi kuwa controlled na foreigner. Bandari ni moja ya hivyo vitu!
Especially kama hakuna ulazima . Na kwa sasa tupo vizuri kwenye uchumi unless tumeshirutishwa
 
Hebu tupe inefficieny ya bandari chini ya mwekezaji mpya
 
Hoja ya haraka ipelekwe bungeni Dodoma , sera hii ya serikali ya CCM kugawa mapande ya nchi ya Tanganyika Ihojiwe kwa kina

14 February 2025
Lilongwe, Malawi

STATE OF THE NATIONS ADDRESS (SONA) BY HIS EXCELLENCE DR LAZARUS CHAKWERA THE PRESIDENT OF MALAWI


View: https://m.youtube.com/watch?v=e2ZaPb4-Y5A
All is set for the opening of the 51st Session of Parliament in Lilongwe.President Dr Lazarus Chakwera is expected to open the 51st Session at the Parliament Building in Lilongwe this morning.According to communication from the office of the Speaker of the National Assembly, President Chakwera is expected to start delivering

CHAWA WAKIWA WAMEJITOKEZA BUNGENI MJINI LILONGWE MALAWI KUSHANGILIA HOTUBA

View: https://m.youtube.com/watch?v=BOivc33JFGYYote yamepangwa kwa ajili ya ufunguzi wa Mkutano wa 51 wa Bunge mjini Lilongwe. Rais Dk Lazarus Chakwera anatarajiwa kufungua Mkutano wa 51 katika Jengo la Bunge mjini Lilongwe leo asubuhi. Kwa mujibu wa mawasiliano kutoka ofisi ya Spika wa Bunge,Rais Chakwera anatarajiwa kuanza kuwasilisha hotuba kuhusu muelekeo wa nchi pamoja na mustakhabali wa muda mfupi hadi mrefu kufikia malengo
 
Binafsi mimi huwa najiulizaga sana.

Hili taifa sasa lina miaka zaidi ya 60 tangu lipate uhuru na hatujawahi kupitia civil war yoyote ile, tafsiri yake ni kwamba tumekuwa na zaidi ya mirongo sita ya kujijenga sisi wenyewe straight bila bugudha yoyote ile.

Taifa hili lina idadi ya watu 61m na miongoni mwao kuna wasomi,wabobezi na wataalamu wa fani fani mbali mbali hata kama sio kwa uwingi.

Sasa tunashindwa vipi kupata waatalamu wazawa wale ambao ni vichwa kabisa wa kutuendeshea hizi sectors zetu muhimu kama bandari kwa ufanisi zaidi? Yaani kwamba kwa miaka yote hiyo hatujaandaa kabisa wataalamu wa kutuendeshea vyanzo vya mapato kwa uwezo kiwango sawa na hao wageni tunaowakaribisha?

Kuna watanzania ambao wamegraduate vyuo vikubwa na vyenye hadhi ya juu kabisa hapa duniani kama Oxford,Princeton,Colombia na Havard... hao wakishagraduate huwa wanaenda wapi? Au wanaenda kuyatumia maarifa yao wapi?

Staki kabisa kuamini eti taifa hili halina watu wenye waledi kiasi cha kutuendeshea sector zetu za kiuchumi kwa ufanisi sawa na hao wawekezaji tunaowakabidhi watuendeshe.
 

View: https://www.instagram.com/p/DGDHss_CQxV/?igsh=OTd4anRwcW1ucnh4
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…