SAUT yafuta degree za Madaktari wa Afya 162 waliohitimu Chuo cha Mt. Francis

SAUT yafuta degree za Madaktari wa Afya 162 waliohitimu Chuo cha Mt. Francis

Ndo madhara ya kusoma chuo cha kata, badala ya kuwaadhibu waliotoa hivyo vyeti bila kipitishwa na seneti wanaadhibiwa wanafunzi

Wawarudishie na Tution Fee zao
 
kwani nikipewa elimu au maarifa chuoni me c na-bakinayo wanaichukuaje hatakama wakiondoka na makaratasi yao
Ndiyo wametangaza hadharani sasa,assume ulikuwa umeajiriwa pale Kitengule Hospital si ajira ndiyo inakoma hapo hapo japo una maarifa yako kichwani? Nani ataendelea kukuajiri wakati huna cheti?
 
Wapi utatumia maarifa yako hayo bila cheti? Utasimama mahakama gani kama wakili bila cheti? Utatibu hospitali gani kwa kutumia maarifa bila cheti?
Mkuu, hivi mtu mwenye elimu ya afya na uzoefu wa utendaji ukichukua cheti chake akaamua kufungua zahanati hiyo elimu haitamsaidia?
 
Ndiyo wametangaza hadharani sasa,assume ulikuwa umeajiriwa pale Kitengule Hospital si ajira ndiyo inakoma hapo hapo japo una maarifa yako kichwani? Nani ataendelea kukuajiri wakati huna cheti?
Boss tukumbuke kuna utofauti wa elimu, cheti na kipato. Cheti kinakupa access ya ajira ikiwa ni njia mojawapo ya kuitumia elimu kupata kipato, wamenyang'anywa ila elimu bado wanayo ubongoni kwao na kuna access nyingine za kuitumia hiyo elimu ikakusaidia kutengeneza kipato kwa njia mbadala.
 
Mkuu, hivi mtu mwenye elimu ya afya na uzoefu wa utendaji ukichukua cheti chake akaamua kufungua zahanati hiyo elimu haitamsaidia?
Itamsaidia lakini kwa gharama kubwa sana,atalazimika kutumia mngongo wa mwingine kuendesha Zahanati kwa kulipia cheti tofauti na angekuwa na Cheti chake ambacho kakisotea darasani.

Kwa darasa la saba,kwake kuingia gharama ya kulipia cheti ni sawa kwakuwa hakuwahi kukaa darasani kusotea cheti na alishajiandaa kisaikolojia kuwa lazima atalazimika kuingia hizo garama
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Kutorudisha nakala za masomo......
Naomba mtu anieleweshe hapo kosa lipo wapi? Na ina maana chuo inazo orijino lakini inadai nakala (copy) walizonazo wahitimu zirudishwe.

Je kitaaluma imekaaje hii
Suala ni:
1: Kuna nakala inayoendana na matokeo
2: Kuna nakala isiyoendana na matokeo, ilitokaje??

Unaambiwa rudisha hiyo isiyoendane upate inayoendana na hali halisi, unapiga kimwa, unakumbushwa x...
Unapiga kimya.
 
Waliokuwa wanawapa transcript hizo ni akina nani, why hazikuhizinishwa mbona miaka mingi sana 2015- 2019.?
Halafu degree ni karatasi au kilichomo kichwani?Kwani hizo transcripts si chuo waprinti, wazisaini.wawatumie wahusika...wao si wana-access na taarifa zote???
Hilo baraza la seneti nao wanashida....usikute walipiga kura, kumbe kuna issue sio za kura bali ni reasoning tu
 
Mkuu, hivi mtu mwenye elimu ya afya na uzoefu wa utendaji ukichukua cheti chake akaamua kufungua zahanati hiyo elimu haitamsaidia?
Anapaswa awe na leseni. Zahanati hata kama ni ya kwako kama huna cheti huruhusiwi kufanya matibabu yoyote
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Boss tukumbuke kuna utofauti wa elimu, cheti na kipato. Cheti kinakupa access ya ajira ikiwa ni njia mojawapo ya kuitumia elimu kupata kipato, wamenyang'anywa ila elimu bado wanayo ubongoni kwao na kuna access nyingine za kuitumia hiyo elimu ikakusaidia kutengeneza kipato kwa njia mbadala.
Na tukubaliane si wote wenye hiyo akili/uwezo wa kutumia njia nyingine kujipatia kipato nnje ya formal ajira inayohitaji upresent cheti chako kwa mwajiri.Wapo watakao venture na kufanikiwa lakini ni wachache.Majority wataathirika
 
Mwisho wa siku katika maisha jambo la muhimu ni " UTUPE MKATE WETU WA KILA SIKU" hii sentensi haina uhusiano na karatasi la degree.
Siku wakikudaka wakaguzi ndo utajua mkate unaweza geuka shubiriii 😀 😀 😀
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Hizo nakala za masomo hao watahiniwa walipewa vipi bila ufahamu na uidhinishaji wa seneti, ina maana zilitolewa kinyemela?

Kuna mtu alikula pesa hapo, naamini atakuwa alishapoteza kazi muda mrefu, ila kama yupo ofisini itakuwa ni maajabu..

Na hao watahiniwa ni kama hawaamini walitoka salama, wanaonekana hawajiamini, ndio maana wameingia mitini wasijezirudisha waambiwe walifeli masomo mawili wanatakiwa kuyarudia.
Kabisa itabid waliokula rushwa
 
Itamsaidia lakini kwa gharama kubwa sana,atalazimika kutumia mngongo wa mwingine kuendesha Zahanati kwa kulipia cheti tofauti na angekuwa na Cheti chake ambacho kakisotea darasani.

Kwa darasa la saba,kwake kuingia gharama ya kulipia cheti ni sawa kwakuwa hakuwahi kukaa darasani kusotea cheti na alishajiandaa kisaikolojia kuwa lazima atalazimika kuingia hizo garama
As long as hiyo elimu itamsaidia basi hajanyang'anywa bado anayo ila Amenyang'anywa access ya ajira kupitia cheti. Maisha yataendelea na huenda kwa uzuri kuliko walivyokuwa na cheti. Wasikate tamaa.
 
Boss tukumbuke kuna utofauti wa elimu, cheti na kipato. Cheti kinakupa access ya ajira ikiwa ni njia mojawapo ya kuitumia elimu kupata kipato, wamenyang'anywa ila elimu bado wanayo ubongoni kwao na kuna access nyingine za kuitumia hiyo elimu ikakusaidia kutengeneza kipato kwa njia mbadala.
Utafanya kimazabe sana labda kwa kujiajiri huko pembezoni sana na ukiingia kwenye 18 za watu ur done. Kwani usajili wako utakuwa umesitishwa. Atakaekuajiri naye ??
 
Kama hapakuwa na ujanja wowote, kwanini wanaogopa kuzirudisha?
Hawa wana lao jambo... sio kuwaita wakoloni
 

Chuo kikuu cha St. Augustine kimebatilisha shahada ilizotoa kwa madaktari 162 waliohitimu chuo cha udaktari cha St. Franscis kuanzia mwaka 2015-2019.

St. Augustine imechapisha tangazo kwenye gazeti la Daily news ikitoa notisi kubatilisha shahada za wanafunzi hao 162 ambao inadai wamegoma kurejesha nyaraka ya matokeo(Transcripts) ambazo walipewa bila baraza la senete la chuo kuwa na taarifa na kuziidhinisha.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na mwenyekiti wa seneti ya chuo hicho, balozi Prof Costa Mahalu imesema maamuzi hayo yamefikiwa baada ya mkutano wa senet ilioketi mwezi wa pili.

===

Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT) kimewafutia shahada Madaktari 162 waliohitimu Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha St Francis (SFUCHAS) kuanzia mwaka 2015-2019.

Notisi kwa Umma iliyochapishwa katika Gazeti la Daily mnamo Jumatatu (27 Machi, 2023), ilisema wahitimu 162 walikataa kimakusudi kurudisha nakala za masomo, 'Transcript' walizopewa bila ufahamu na uidhinishaji wa seneti ya chuo kikuu licha ya kukumbushwa kwa muda mrefu.

Taarifa hiyo iliyotiwa saini na Mwenyekiti wa seneti ya SAUT Balozi Prof. Costa Mahalu inaeleza uamuzi wa kuondoa shahada hiyo umekuja baada ya kikao cha Seneti cha Chuo Kikuu kilichofanyika Februari mwaka huu.

"SAUT kupitia Seneti ya Chuo Kikuu katika Seneti yake ya 54 isiyo ya kawaida, mkutano uliofanyika tarehe 25 Februari 2023 katika chuo kikuu cha SAUT na kwa mujibu wa Kifungu cha 47(1) & (2) cha Sheria ya Vyuo Vikuu, Sheria Na. 7 ya 2005 ikisomwa pamoja na Vifungu. 6(3)(ii), 7,8 na Kanuni ya 29 (1) ya Mkataba wa SAUT GN. HAPANA. 580 ya 2020 ilifuta shahada walizopewa wahitimu 162 wa Madaktari wa Udaktari wa SFUCHAS kuanzia 2015 -2019,” inasomeka taarifa hiyo.

Source: Daily News
Janga hili....tunafanya masihara na mambo muhimu....upuuzi huu
 
Back
Top Bottom