Seba aliyeandika meseji kwa rafiki yake amtunzie mwanae na anakata roho kwenye ghorofa ya Kariakoo lililoanguka, akutwa amefariki

Seba aliyeandika meseji kwa rafiki yake amtunzie mwanae na anakata roho kwenye ghorofa ya Kariakoo lililoanguka, akutwa amefariki

Bado nalia na serikali,hili ni fundisho,wahusika wa uzembe wowote ule utakao onekana wachukuliwe hatua bila ya kumuonea mtu,ukaguzi ufanyike kuanzia sasa kwa majengo mengine ili kusitokee baya lingine pengine kuliko hili.Kuna wakati ni lazima tuonyeshe ukali kidogo,japo kuna watakao umia lakini itasadidia kuepusha madhara zaidi baadaye...
 
Hawa vijana wanajifanya wako busy kwa mambo ya Yanga na Simba huku wakiunda vikundi vya kijinga vya kuombea mikopo ya Samia wanavuna ujinga wao
Nchi inaliwa na watawala wao huungana kuwasifu watawala badala ya kulikomboa Taifa lao .
 
Majanga kama haya hayana mbabe mkuu, kumbuka tetemeko la uturuki, ghorofa la floors kumi unadhani watafanyaje ili kuharakisha uokozi?
Hilo jengo la Kariakoo halijaporomoka kutokana na sababu za kuwepo kwa tetemeko la Ardhi..
Anyway, Ukweli unabaki kuwa Serikali inapaswa kuwa na taasisi imara na madhubuti kabisa za kuweza kupambana na majanga mbalimbali kama haya. Taasisi hizo zinapaswa kuwezeshwa kikamilifu kwa Mafunzo ya Utayari wa Kupambana na Majanga sambamba na kuwezeshwa kwa Vifaa vya Uokozi kwa ajili ya utayari wa kupambana na majanga mbalimbali.

Wananchi nao pia wapewe mafunzo ya utayari wa kuweza kupambana au mafunzo ya mbinu za kuweza kujihami na majanga mbalimbali, Mamlaka zinazohusika na masuala ya kupambana na majanga ziwe zinatoa mafunzo ya namna hii kwa umma.

Aidha, Watu wote waliozembea na kusababisha ajali hii huko Kariakoo wanapaswa kuwajibishwa kwa kufikishwa Mahakamani kwa makosa ya kusababisha vifo vya Watu kwa makusudi. Uwazi unatakiwa sana kwenye suala hili. Wahusika wafikishwe Mahakamani na wawajibishwe. Wafuatao ni Watu wa kuanza nao:-
1.Mmiliki wa Jengo.
2. Mhandisi wa Ujenzi Manispaa ya Ilala, pamoja na Maafisa wengine wote kabisa waliohusika na mchakato wa Kutoa Kibali cha Ujenzi na/au Ukaguzi wa Jengo.
3. Contractor.
4. Consultant.
5. Wahusika wa Usalama Mahali pa kazi (OSHA).,n.k, n.k.
 
Uzembe wa serikali umesababisha kuua watu.wanapitisha vibali vya ujenzi holela visivyofuata usalama wa jengo.kamati ya uokoaji ikiwemo jeshi la uokoaji na zima moto hayana msaada kabisa.yaani jengo Moja tu wiki nzima Bado mnahangaika tu lakini ingekuwa maandamano ya chadema wangeyamaliza siku Moja tu.
 
Huyu alikuwa hai na alikuwa na uwezo wa kuwasiliana na jamaa zake leo kaopolewa maiti, sasa tujiulize wale walibanwa vibaya zaidi kama watakuwa na uhai hadi sasa.

Nadhani hili jengo litakuwa limepora uhai wa watu wengi sana.
 
Back
Top Bottom