Sekondari za Vipaji maalum takribani miaka 40 tangu kuanzishwa kwake umaalum wake uko kwenye nini? Hatuoni ubunifu wowote

Sekondari za Vipaji maalum takribani miaka 40 tangu kuanzishwa kwake umaalum wake uko kwenye nini? Hatuoni ubunifu wowote

Mleta mada..
Naomba kufahamu kama umesoma special school?
Kama ulipata alama za kukokoteza huwezi soma huko.
 
Tumejionea wenyewe kule chini na mahala pengine kama ulaya Watoto wadogo wanaandaliwa kiwa Wanasayansi na mainjinia wabobezi. Watoto hao wanasukwa na kufinyangwa kiasi kwamba wanaanza kubuni na kuvumbua Mitambo na teknolojia za kipekee zenye mchango mkubwa ktk maendeleo ya kiuchumi kwenye nchi zao.

Hapa Tanzania mfumo wa Shule za Vipaji maalum umekuwepo kwa miaka mingi sasa.

Binafsi sikuwa na bahati ya Kujiunga na shule hizo hivyo nilitarajia pia kunufaika na Ubunifu/ innovations kutokana na kundi hili kubwa wenye vipaji Maalum/ special inteligence.

Tuna sekondari nyingi kama
1. Ilboru Arusha
2. Msalato Girls Morogoro
3.Mzumbe Boys Morogoro
4.Kibaha Boys Pwani
5. Tabora girls na Tabora Boys.

Ndio kusema Maelfu kwa Maelfu ya Wanafunzi waliopita humo hakuna hata wawili watatu walioonesha Ukipaji wao?

Tuseme basi Mtaji ni Mkubwa ku invest, hata Basi Kuwa Social influencer/ matumizi ya tech zilizopo je?

Tunaona Watu wenye elimu kiasi tu ndio wanaofaidi matumizi ya Technolojia na kunufaika na kuitangaza Tanzania.
Watu kama akina Maulid Kitenge, Kipanya, Zembwela, Diamond, Millard Ayo, Mwijaku, Baba Levo, Mobeto.

Angalau hawa hawakugundua chochote kama walivyo wale wa vipaji maalum ispokuwa wameweza kugundua matumizi sahihi ya teknolojia iliyopo.

Vipaji maalumu katika sekondari hizo ni vya mchongo au tunakwama Wapi?

Bonjour, Je M'apelle Bush Dokta habité à Makerere universite.

Bonvenué de discusio reun̈ion
Zilikua zinasaidia kutoa top 10 tu. Baada ya hapo hakuna jipya .
 
Hii mada inarudiwa Kila baada ya muda humu.

Hoja hii ni Sawa na ile inayojengwa na Dotto Magari kuwa degree hazina maana yeyote kwakuwa wenye degree hawana hela!

Trust me, 80% za PhD Tanzania zimetoka shule hizo. 80% ya policy makers wamepita shule hizo!

Lakini liangalie kwenye context ya uchumi wa nchi husika! Tuna nuclear scientists Tanzania Mfano Mohammed Gharib Bilal aliyekuwa makamo wa RAIS, je wamegundua Nini kwenye nishati ya nuclear?
 
Hao ndo wanakuendeshea maisha mkuu,

Wamejaa mawizara yote, wamejaa mataasisi yote makubwa,

Kama haujui Hao ndo muhimili wa watanzania, sio wote ila like 20% wanafanya vzr na wanazibeba saana taasisi wanazozifanyia kazi
Watu concentration yao ipo kwa wakina chief godlove na show off zao mitandaoni. Kwaiyo wanafikiri wasomi wote ni useless
 
Hizo ni shule maalumu kwa waliopata alama za juu tu.
Nafikiri jina sahihi ni shule maalumu/special schools kama ulivyoandika na si vipaji maalumu.

Wazee wa mongwe wanywa nyuka na wenzao wa mkoani Arusha, Pwani, Dodoma na Tabora wanaelewa hivyo. Sema mtaani watu walikuza mambo na kutoa sifa ambazo hata wao hawakuzipenda wala kutaka waitwe vipaji maalum
 
Hakuna elimu ya maana zaidi ya kuzalisha majobless wenye matokeo makubwa kila mwaka na hizi ndio ndoto zao wanasiasa, yaani serikali haina maono yoyote wao furaha yao kuona kila mtoto anapata Masomo A zote, division 1, na GPA ya kutisha, masuala ya kazi na baada ya shule wao hayawahusu.

Upuuzi wa hali ya juu karne hii kukomalia katika matokeo ya ufaulu badala ya matokeo yanayohusu vitendo vya uzalishaji wa nguvu kazi ktk matumizi sahihi ya rasilimali, ubunifu na solution kwa changamoto za kiafya, kijamii, kiuchumi, yaani tupo tupo kupigana na walimu wafaulishe matokeo makubwa ambayo hayana impacts yoyote.

Elimu ya form5+6 ni takataka haina maana wala faida kwa sasa lakini bado tumekomalia huu upuuzi, baadhi ya masomo na topics hazina maana wala faida lakini bado tumekomalia kukalilisha watoto upuuzi usio na maana.
Matokeo ya kuongozwa na serikali isiyo na vision ndio haya bado tungali gizani.
 
Tumejionea wenyewe kule chini na mahala pengine kama ulaya Watoto wadogo wanaandaliwa kiwa Wanasayansi na mainjinia wabobezi. Watoto hao wanasukwa na kufinyangwa kiasi kwamba wanaanza kubuni na kuvumbua Mitambo na teknolojia za kipekee zenye mchango mkubwa ktk maendeleo ya kiuchumi kwenye nchi zao.

Hapa Tanzania mfumo wa Shule za Vipaji maalum umekuwepo kwa miaka mingi sasa.

Binafsi sikuwa na bahati ya Kujiunga na shule hizo hivyo nilitarajia pia kunufaika na Ubunifu/ innovations kutokana na kundi hili kubwa wenye vipaji Maalum/ special inteligence.

Tuna sekondari nyingi kama
1. Ilboru Arusha
2. Msalato Girls Morogoro
3.Mzumbe Boys Morogoro
4.Kibaha Boys Pwani
5. Tabora girls na Tabora Boys.

Ndio kusema Maelfu kwa Maelfu ya Wanafunzi waliopita humo hakuna hata wawili watatu walioonesha Ukipaji wao?

Tuseme basi Mtaji ni Mkubwa ku invest, hata Basi Kuwa Social influencer/ matumizi ya tech zilizopo je?

Tunaona Watu wenye elimu kiasi tu ndio wanaofaidi matumizi ya Technolojia na kunufaika na kuitangaza Tanzania.
Watu kama akina Maulid Kitenge, Kipanya, Zembwela, Diamond, Millard Ayo, Mwijaku, Baba Levo, Mobeto.

Angalau hawa hawakugundua chochote kama walivyo wale wa vipaji maalum ispokuwa wameweza kugundua matumizi sahihi ya teknolojia iliyopo.

Vipaji maalumu katika sekondari hizo ni vya mchongo au tunakwama Wapi?

Bonjour, Je M'apelle Bush Dokta habité à Makerere universite.

Bonvenué de discusio reun̈ion
Vipaji maalum weru ni div one

Which is a veeybwrong factor yw kuwa special student
 
Nikiwa m1 wa waliopita special schools, itoshe kusema kule ni kusoma sana, kukariri na kugombania u TO.

Ila kuna ka hype fulani kusoma special schools. Tchaos.

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
Utakubaliana na mimi hizi special schools wengi wanafaulu kwa uwezo wao maana hata walimu ni wa kawaida sana kuliko hata wanafunzi.

Ukitaka kuona uwezo wao peleka huduma zote zilipo Fedha schools halafu uone watakachofanya. Huko kuna vichwa kwelikweli sio mchezo. Kuyaelewa masimple pendulum inahitaji ubongo tulivu kwelikweli. Hata sasa matokeo ya shule hizi ni mazuri sana.
 
Kukariri kipaji pia usifanye mchezo kukariri,kwanini wao waweze kukariri halafu wengine washindwe?
Uko kukalili Kuna faida gani kwa mwanafunzi na taifa? Nyie ndio wale ambao bado mko gizani mnadhani elimu ni kupata marks za juu wakati huo mkishamaliza hiyo shule mnarudi mtaani hata kujiajiri hamuwezi wala kubadili hiyo elimu kutatua changamoto hamuwezi mnasubiri ajira za kugombania.

Mjifunze kwa hao waliowaandikia hiyo mifumo ya elimu, wao walishaachana na huo upuuzi wenu wa kugombania marks za kukalili ambazo hazina impacts
 
Mada nzuri.
Kwa kuwa ume declear kuwa hukubahatika kuchaguliwa shule hizo basi moja kwa moja umekiri wengi huwajui na hujawahi wafuatilia.

BInafsi nawatambua vijana kadhaa waliopita shule hizo na wana mchango mkubwa kwa taifa katika nyanja mbalimbali.

Mfumo wa elimu zetu hazikutuwezesha kufanya gunduzi mbalimbali kwa sababu ya mazingira na vifaa. Lakini pia ugunduzi si mpaka urushe ndege. Matumizi sahii ya akili yako yanaweza kuleta matokeo chanya katika jamii.

Mfano juzi tumeona wanafunzi wa kibaha wakiwekeza mfumo wao wa kupiga kura kidigitali na kufanya uchaguzi.

Vipaji maalumu wengi walivyofika chuo wameendelea katika taaluma mbali mbali na pia wengi wapo na kampuni kadhaa....

Naweza kukutajia mbili tu. Anayeendesha AI ya kiswahili ni kipaji maalumu. Aliyeandika code za kampuni moja ya mawasiliano ni kipaji maalumu.

Nyerere ni kipaji maalumu n.k

Kwa namna ulivyotaja hao influencer wako ni dhahiri wewe ni mtu wa social media unayedanganywa na mafanikio ya picha.
Tatzo la watanzania wengi hudhania mafanikio ni hela nyingi au umaarufu.

Mimi nikuhakikishie tu. Kusanyiko la vilaza sio sawasawa na kusanyiko la vipaji maalumu. Kuna tofauti tu mtaonyesha kwenye kufikiri na kwenye kuamua.

Leo form 1 failure anaweza kutamba kuwa ana hela kuliko aliyesoma chuo. Lakini anasahau kuna watu behind walioweka mifumo imara inayofanya yeye apate hela.

Uvivu wa kufikiri unafanya tunakuwa na jamii isiyo na misingi imara na iliyokosa fikra timamu. Leo mtu mzima ana praise wauza uchi na machawa kuwa ndio wenye mafanikio. Huu ni ugonjwa wa akili.
Pia mifumo mingi ya IT wako hao wanaopuuzwa, watendaji wakuu wa wizara na taasisi za umma wako hao special schools alumni. Sehemu pekee ambako wako wachache ni kwenye siasa ndio unawapata wachache.
 
Vipaji maalum weru ni div one

Which is a veeybwrong factor yw kuwa special student
Watu wanatafuta sana sababu za kuwashusha hadhi waliosoma kama vile wao hawakutaka au walikatazwa kufaulu vizuri. Mimi nilipomaliza shule ya msingi ni peke angu nilipiga flat A ikiwemo hesabu nilipiga 50/50 nikapangiwa kwenda kuendelea form azania sekondary.

Wanafunzi wengine sio kwamba hawakutaka au walikatazwa kufaulu kama mimi, isipokua uwezo wao ulikua mdogo. Hao sasa wakiyabahatisha maisha ndio hawa wakina dotto magari, kutwa kuwapopoa wasomi wakati ajui kwamba takwimu zinaonesha illiteracy people wenzake ndio population kubwa zaidi ya watu wanaoishi maisha ya dhiki
 
Zote ni njia za kutafuta hela sio u maalum wa pekee tu. Tunategemea mwanafunzi akishajifunza katika shule hizo anakuwa bora zaidi katika masomo ya amali na vilevile tunapata madaktari bingwa ambao ni wepesi kuelewa katika masomo yao.
 
Utakubaliana na mimi hizi special schools wengi wanafaulu kwa uwezo wao maana hata walimu ni wa kawaida sana kuliko hata wanafunzi.

Ukitaka kuona uwezo wao peleka huduma zote zilipo Fedha schools halafu uone watakachofanya. Huko kuna vichwa kwelikweli sio mchezo. Kuyaelewa masimple pendulum inahitaji ubongo tulivu kwelikweli. Hata sasa matokeo ya shule hizi ni mazuri sana.
Ni kweli matokeo yao yako poa. How about Innovations?
 
Tumejionea wenyewe kule chini na mahala pengine kama ulaya Watoto wadogo wanaandaliwa kiwa Wanasayansi na mainjinia wabobezi. Watoto hao wanasukwa na kufinyangwa kiasi kwamba wanaanza kubuni na kuvumbua Mitambo na teknolojia za kipekee zenye mchango mkubwa ktk maendeleo ya kiuchumi kwenye nchi zao.

Hapa Tanzania mfumo wa Shule za Vipaji maalum umekuwepo kwa miaka mingi sasa.

Binafsi sikuwa na bahati ya Kujiunga na shule hizo hivyo nilitarajia pia kunufaika na Ubunifu/ innovations kutokana na kundi hili kubwa wenye vipaji Maalum/ special inteligence.

Tuna sekondari nyingi kama
1. Ilboru Arusha
2. Msalato Girls Morogoro
3.Mzumbe Boys Morogoro
4.Kibaha Boys Pwani
5. Tabora girls na Tabora Boys.

Ndio kusema Maelfu kwa Maelfu ya Wanafunzi waliopita humo hakuna hata wawili watatu walioonesha Ukipaji wao?

Tuseme basi Mtaji ni Mkubwa ku invest, hata Basi Kuwa Social influencer/ matumizi ya tech zilizopo je?

Tunaona Watu wenye elimu kiasi tu ndio wanaofaidi matumizi ya Technolojia na kunufaika na kuitangaza Tanzania.
Watu kama akina Maulid Kitenge, Kipanya, Zembwela, Diamond, Millard Ayo, Mwijaku, Baba Levo, Mobeto.

Angalau hawa hawakugundua chochote kama walivyo wale wa vipaji maalum ispokuwa wameweza kugundua matumizi sahihi ya teknolojia iliyopo.

Vipaji maalumu katika sekondari hizo ni vya mchongo au tunakwama Wapi?

Bonjour, Je M'apelle Bush Dokta habité à Makerere universite.

Bonvenué de discusio reun̈ion
Swali lako ni sawa na mtu kuuliza faida ya misikiti na makanisa ni zipi ...jibu ni hakuna faida yoyote ya maana
 
Tatizo sio shule bali waliozianzisha ndio ambao akili zao zinatia mashaka .
Huwezi kuanzisha vipaji maalumu bila kulenga ugunduzi na teknolojia .
Tulitegemea pawe na shule za Vipaji maalumu zenye Maabara na workshop za ufundi na masuala ya ugunduzi na vipaji maalumu katika ubunifu na Computer.

Cha ajabu shule hizi ni za kukariri tu hesabu na sio vipaji vya ugunduzi . Wengi wao hawawezi hata kuchunga mwiko au hata kutengeneza jiko la mkaa achilia mbali Kutengeneza masufuria kama wazee wetu wa zamani .
Hata kufinyanga chungu hawawezi lakini wanauwezo wa kukariri na kupata alama A zote.

Shule za Vipaji maalumu zilitakiwa ziwe ni vipaji vya kuzaliwa na sio kukariri kama Koran tu.
Walitakiwa wapimwe kwa ujuzi usio wa kawaida na uelewa wa kuzaliwa kabla hata ya kuingia kwenye mitihani. Mfano mtoto mwenye uwezo wa kufanya hesabu ngumu kwa kichwa bila kuandika n.k.
Lakini hii ya ufaulu wa A haitatuletea Wagunduzi hata wa baiskeli achilia mbali Cherehani za Kidigitali.
Una point nzuri sana ila nafikiri kwa watu ule shule za msingi hazikuandaa kutambua vipaji vya watoto ili wanapokwenda sekondari waende kutokana na vipaji vyao. Angalau majeshi enzi za Nyerere na mwinyi watu waliingia kutokana na walichonacho. Kuna wazee waliingia jeshi kwa kusakata kabumbu, riaza, ufundi, kuimba na vipaji vingine.

Hizi shule zingine kigezo ilikuwa uwezo kuelewa. Sikubaliani na wazo la kukariri. Serikali ndio haikuweka mifumo mizuri ya kuhakikisha wanatumika kugundua vitu na hata wakigundua au wakibuni wanawekewa vikwazo. Na wengi wamechukuliwa na mataifa yaliyoendelea ili wakanufaishe nchi zao. Wachache serikali huamua kuwarudisha nchini ingawa mazingira huwa magumu kwao
 
Niliwahi kusikia waligundua Namba ya Panya kugundua Magonjwa ya TB kwenye Sample za Makohozi. Hadi leo sijajua imefikia wapi ile project
Na pia kutegua mabomu kule Afghanistan na kwingineko kwenye vita, panya mtaalamu alikufa,baadae tukasikia alipata warithi wake,sijui hadi sasa waliishia wapi!!?
 
Utakubaliana na mimi hizi special schools wengi wanafaulu kwa uwezo wao maana hata walimu ni wa kawaida sana kuliko hata wanafunzi.

Ukitaka kuona uwezo wao peleka huduma zote zilipo Fedha schools halafu uone watakachofanya. Huko kuna vichwa kwelikweli sio mchezo. Kuyaelewa masimple pendulum inahitaji ubongo tulivu kwelikweli. Hata sasa matokeo ya shule hizi ni mazuri sana.
Ni kweli matokeo yao yako poa. How about Innovations?
 
Well
Zote ni njia za kutafuta hela sio u maalum wa pekee tu. Tunategemea mwanafunzi akishajifunza katika shule hizo anakuwa bora zaidi katika masomo ya amali na vilevile tunapata madaktari bingwa ambao ni wepesi kuelewa katika masomo yao.
 
Kwenye izo izo fani zao kuna ubunifu wanaufanya. Taarifa zao hatuna kwa sababu hatuna utaratibu mzuri wa kufuatilia watu wetu uko nje wanafanya nini, labda mpaka wanapokutana na changamoto mbaya ndio tunaamka.

Mfano mzuri nemes raymond tarimo, mtanzania mwenzetu aliekufa kwenye vita ya ukraine na urusi. Yule ni mshkaji wangu kitambo na alipata scholarship ya kusoma IT kule urusi si ajabu hata mamlaka hazikua zinajua uwepo wake kule. Kama asingekutana na yaliyomkita isingejulikana uwepo wake kule.

Kitu kingine huwa hawa vipaji maalumu ambao wengi wao ni diaspora huwa hawapendi kujitokeza kwa sababu wanakwepa siasa za afrika.

Kuna mshkaji wangu mmoja ambae ni kama broo angu alinitangulia madarasa mawili pale azania, jamaa anaishi canada na yupo vizuri, katika kuwasiliana nikamuuliza kwanini asije kuwekeza bongo? aliniambia huku kuna masuala ya uraia pacha yanakwamisha, na usipokua puppet wa wanasiasa unafanyiwa vigisu sasa kwa mtu ambae hawezi kuwa chawa ni changamoto.


Trust me mzee baba, hawa finnest wa vipaji maalumu wapo uko google, nasa, harvard n.k wanafanya mambo makubwa tu
Umeeleza vizuri boss. Hawa vipaji maalumu wapo na wanatumika kwenye mataifa yaliyoendelea. Sera za nchi haziwapi nafasi ya kutumia uwezo walio nao. Wakigundulika na mataifa mengine wanabebwa nankupotelea huko. Nawafahamu wengi hawapo nchini wako ughaibuni.
 
Back
Top Bottom