Sekretariet ya ajira katika utumishi wa umma kuendesha usaili siku ya ibada Jumapili

Sekretariet ya ajira katika utumishi wa umma kuendesha usaili siku ya ibada Jumapili

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Huku ni KUPITILIZA na tunasema HAIKUBALIKI KABISA. Haiingii akilini watu na akili zao kuamua kutokuheshimu kwa makusudi imani ya watu ambao wanapaswa kuwa kwenye ibada KANISANI na kuipanga siku hiyo kuwa ni siku ya kuwasaili waombaji wa ajira.

Ina maana wanaoendesha usaili huu kama ni wakristo watakuwa wamedhulumiwa haki na uhuru wao wa kuabudu. Ina maana pia waombaji wa ajira walio wakristo watakuwa wamedhulumiwa haki na uhuru wao wa kuabudu. Hili tunalikataa kwa nguvu zetu zote!!

Tarehe 18/06/2022 siku ya JUMAMOSI (SIKU YA IBADA KWA WASABATO), na tarehe 19/06/2022 siku ya JUMAPILI (SIKU YA IBADA KWA WAKRISTO) zimetangazwa kuwa ni moja ya siku ambazo usaili wa waombaji wa ajira utafanyika. Kwanza jumamosi na jumapili siyo siku za kazi, kwa nini hawa sekretarieti ya ajira wameamua kuzifanya kuwa siku za kazi? Hii JEURI WANAIPATA WAPI? Ushahidi upo kwenye tovuti yao- www.ajira.go.tz na ninatupia kipande hapa:

KADA: ASSISTANT VOCATIONAL TEACHER – ELECTRICAL INSTALLATION MWAJIRI: MAMLAKA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI (VETA) TAREHE YA USAILI WA VITENDO: (1-37) 18 JUNI, 2022 (38-74) 19 JUNI, 2022 MAHALI: VETA DODOMA TAREHE YA USAILI WA MAHOJIANO: 22 JUNI, 2022 MUDA: SAA 1:00 KAMILI ASUBUHI. MAHALI: OFISI YA RAIS SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA ZILIZOPO MAJENGO YA DKT. ASHA ROSE MIGIRO, UDOM - DODOMA.

Ninamwomba waziri mwenye dhamana na sekretarieti hii kufanya mambo yafuatayo kwa dharula:
1. Kubatilisha hizo tarehe haraka na kagiza zipangwe tarehe zingine.
2. Kuwawajibisha wote waliofanya ujeuri huu wa kuleta utaratibu unaoashiria UDINI kwenye nchi yetu.
 
Nakumbuka chuoni walimu walikuwa wanapenda Sana kutoa test siku ya jumamosi au jumapili wasabato wakawa wanalalamika walimu wakawa wanasema sawa msije ila mtafanya test ya kwenu j3 ,tukawa tunashanga hao wasabato tunawaona jumamosi ndio nikajua dini ni kichaka tu
 
Dini ni ugonjwa mbaya sana wa akili kuwahi kuikumba dunia.

Anyway wamekusikia naamini wata reschedule ili wafia dini mfanye kwa uhuru.

#MaendeleoHayanaChama
Siyo suala la kuwa mfia dini, bali ni suala la watu kuheshimu ibada ya watu wengine> Hivi haujaona hata hotuba za kitaifa kusitishwa kwa muda kupisha muda wa ADHANA? Wakristo na Wasabato wanaheshimu siku yao ya ibada na serikali ITAMBUE HIVYO na hapo HAKUNA MJADALA.
 
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa Maarifa....

Umasikini wa Namna hii ni mbaya kuliko umasikini wa Fedha...
 
Nakumbuka chuoni walimu walikuwa wanapenda Sana kutoa test siku ya jumamosi au jumapili wasabato wakawa wanalalamika walimu wakawa wanasema sawa msije ila mtafanya test ya kwenu j3 ,tukawa tunashanga hao wasabato tunawaona jumamosi ndio nikajua dini ni kichaka tu
Huo ndio unyanyasaji wa kidini kwa kutumia uhitaji wake na shida yake na hiyo ni mbaya sana.
 
Inajulikana JUMAMOSI NA JUMAPILI SIYO SIKU ZA KAZI kwa nini uzipangie shughuli muhimu kama usaili kama siyo kuwa UNA AJENDA YA SIRI!!
 
Mkuu kwani wewe kila Jumamosi uanenda kwenye usahili? Ile sio shule ni single day activity tana ni chini ya lisaa limoja na nusu. Mbona majeshini na hospitali watu wana attend ratiba zao za kazi wakipangiwa siku hiyo.

Mimi nafikiri ulipaswa kumshukuru Mungu kuwa usahili umeangukia siku ya ibada yako na Mungu awe upande wako ufaulu, ukalitumikie taifa lako upate na matoleo ya sadaka kwaajili ya kazi ya Mungu.
 
Kwa hiyo hata Ijumaa isiwe siku ya kazi kwa sababu kuna wengine wanatakiwa kuwa kwenye ibada sio? Au huu UDINI unauona upande moja tuu?
Tayari JUMAMOSI na JUMAPILI si SIKU za kazi. Huwezi kuzipangia majukumu ya kiserikali bila kuvunja sheria. Dini yao HAIJAWAHI kudai kuwa ni HARAMU kufanya kazi siku ya IJUMAA isipokuwa ni yale masaa ya ibada tu, na serikali ilishaliheshimu hilo. Hotuba husitishwa kupisha ADHANA, na mashuleni masomo huisha baada ya break time na wanafunzi kuruhusiwa kwenda ibadani.
 
Wewe na hao waliotangaza hizo siku mnatofauti gani ...mbona na wewe umewabagua waislamu na siku yao ya kuabudu ya Ijumaa! usilopenda kutendewa wewe..usiwatendee pia wenzio!
 
Mkuu kwani wewe kila Jumamosi uanenda kwenye usahili? Ile sio shule ni single day activity tana ni chini ya lisaa limoja na nusu. Mbona majeshini na hospitali watu wana attend ratiba zao za kazi wakipangiwa siku hiyo.

Mimi nafikiri ulipaswa kumshukuru Mungu kuwa usahili umeangukia siku ya ibada yako na Mungu awe upande wako ufaulu, ukalitumikie taifa lako upate na matoleo ya sadaka kwaajili ya kazi ya Mungu.
HAIWEZEKANI!! SIKU NZIMA (bila kupinguza hata sekunde moja) imewekwa WAKFU kwa BWANA!! Hiyo ni imani ya watu na lazima IHESHIMIWE!! Vinginevyo, mchakato mzima utapingwa na kubatilishwa MAHAKAMANI kama wahusika wasipolipa uzito suala hili. Hii ni nchi yetu wote!!
 
Tayari JUMAMOSI na JUMAPILI si SIKU za kazi. Huwezi kuzipangia majukumu ya kiserikali bila kuvunja sheria. Dini yao HAIJAWAHI kudai kuwa ni HARAMU kufanya kazi siku ya IJUMAA isipokuwa ni yale masaa ya ibada tu, na serikali ilishaliheshimu hilo. Hotuba husitishwa kupisha ADHANA, na mashuleni masomo huisha baada ya break time na wanafunzi kuruhusiwa kwenda ibadani.
Nioneshe mstari wa Biblia uliosema kufanya kazi siku ya Jumamosi au Jumapili ni haramu! biblia imesema tu "Ikumbukwe siku ya saba na itakaswe" wasabato wanatafsiri kuwa siku hiyo hutakiwi kufanya kazi, wanaosali Jumapili hakuna sehemu inayosema wasifanye kazi...na mwisho kazi ni nini kwa tafsiri ya kisayansi au hata ya dini? halafu tujiulize je usahili unafit kiasi gani kwa "definition" hiyo ya kazi?
 
HAIWEZEKANI!! SIKU NZIMA (bila kupinguza hata sekunde moja) imewekwa WAKFU kwa BWANA!! Hiyo ni imani ya watu na lazima IHESHIMIWE!! Vinginevyo, mchakato mzima utapingwa na kubatilishwa MAHAKAMANI kama wahusika wasipolipa uzito suala hili. Hii ni nchi yetu wote!!
Basi achana nao huo usahili Mkuu....Yesu aliponya mtu siku ya Sabato wakaja watu hodari kuzidi wewe kuhoji, walipopigwa swali kama punda zao na mifugo zao hazipo katika malisho walipiga kimya.

Ila kimsingi wewe ukiitwa Jumamosi wakomoe usiende.
 
Siyo suala la kuwa mfia dini, bali ni suala la watu kuheshimu ibada ya watu wengine> Hivi haujaona hata hotuba za kitaifa kusitishwa kwa muda kupisha muda wa ADHANA? Wakristo na Wasabato wanaheshimu siku yao ya ibada na serikali ITAMBUE HIVYO na hapo HAKUNA MJADALA.
Pole sana mreta maada,kuabudi haitakiwi kuzidi nusu saa au saa moja,na unaendelea na kazi zako kama kawaida,hiyo ya kupumzika siku nzima ni utamaduni wa Kiroma,naomba unipe kifungu kutoka kwenye biblia kinachosema jmapili watu wapumzike?
 
Wewe na hao waliotangaza hizo siku mnatofauti gani ...mbona na wewe umewabagua waislamu na siku yao ya kuabudu ya Ijumaa! usilopenda kutendewa wewe..usiwatendee pia wenzio!
Hawajawahi kubaguliwa! Wametimiziwa matakwa yao kwa kadri walivyoyahitaji. Waislamu hawajawahi kudai kuwa hawapaswi kufanya kazi siku ya Ijumaa wala msahafu wao haujawataka hivyo. ILA muda wa sala ukifika serikali imewapa ruhusa ya kusali. Shule zote humaliza program zao mapema siku ya ijumaa ili kuwapa nafasi wanafunzi na watumishi kuabudu kwa mujibu wa imani yao.
 
Huku ni KUPITILIZA na tunasema HAIKUBALIKI KABISA. Haiingii akilini watu na akili zao kuamua kutokuheshimu kwa makusudi imani ya watu ambao wanapaswa kuwa kwenye ibada KANISANI na kuipanga siku hiyo kuwa ni siku ya kuwasaili waombaji wa ajira.
Mkuu, mbona ijumaa ni siku ya kazi na waislam hawajalalamika? Cha muhimu hapo ni kuomba au kwenda kanisani mapema ili uwahi usaili. Serikali yetu haina dini!
 
Back
Top Bottom