Sekretariet ya ajira katika utumishi wa umma kuendesha usaili siku ya ibada Jumapili

Sekretariet ya ajira katika utumishi wa umma kuendesha usaili siku ya ibada Jumapili

Ulitaka ufanyike weekdays sio na hizo venue hao wanachuo wasisome? Mbona una kaubinafsi ndani yako?
Kwa bahati mbaya unaandika bila ufahamu wa ndani. Usaili unafanyika tarehe weekdays pia. Kwa hiyo sababu yako haiingii hapa.
 
Ni haki ya kila aliyeitwa kwenye usaili kufanya usaili. Huwezi ukafukuza watu kwa kuwawekea mtego wa kufanya usaili siku ya ibada. haikubaliki na PATACHIMBIKA!! Hii nchi inaendeshwa kwa kufuata utawala wa sheria. Sheria imekiukwa kupanga usaili siku ya mapumziko ya shughuli zote za serikali. Usaili siyo dharula!!
Hivi ukienda kusali kisha ukaenda kwenye usahili...kuna kitu kitaharibika?
 
( يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نُودِيَ لِلصَّلَاةِ مِن يَوْمِ الْجُمُعَةِ فَاسْعَوْا إِلَىٰ ذِكْرِ اللَّهِ وَذَرُوا الْبَيْعَ ۚ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ )

الجمعة (9) Al-Jumu'a

Enyi mlio amini! Ikiadhiniwa Sala siku ya Ijumaa, nendeni upesi kwenye dhikri ya Mwenyezi Mungu, na wacheni biashara. Hayo ni bora kwenu, lau kama mnajua.

( فَإِذَا قُضِيَتِ الصَّلَاةُ فَانتَشِرُوا فِي الْأَرْضِ وَابْتَغُوا مِن فَضْلِ اللَّهِ وَاذْكُرُوا اللَّهَ كَثِيرًا لَّعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ )

الجمعة (10) Al-Jumu'a

Na itakapo kwisha Sala, tawanyikeni katika nchi mtafute fadhila za Mwenyezi Mungu, na mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi ili mpate kufanikiwa.
Safi sana. Kumbe mara baada ya sala wanatakiwa wachachalike kufanya kazi kutafuta fadhila!! Na serikali haijawahi kuwaingilia katika muda wao wa ibada!!
 
Wapi kwenye biblia panasema kuwa kuabudu Jumapili lazima uende kanisani.
Wewe amka siku ya Jumapili, tenga nusu saa yako au saa nzima sali na abudu in private hapo nyumbani kwako kisha kapige usaili.

Au wakati unasubiri usaili nenda jitenge na watu pembeni kule kaabudu kisha rudi kafanye usaili.
 
Dini ni ugonjwa mbaya sana wa akili kuwahi kuikumba dunia.

Anyway wamekusikia naamini wata reschedule ili wafia dini mfanye kwa uhuru.

#MaendeleoHayanaChama
Zaidi ya kansa,Yaani huyo jamaa,Usikute hata Usaili haumhusu!!
 
Hivi ukienda kusali kisha ukaenda kwenye usahili...kuna kitu kitaharibika?
Kutoka 20:8-11. "Ikumbuke siku ya saba uitakase, siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote, lakini siku ya saba ni sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo USIFANYE KAZI NYOYOTE, wewe wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana kwa siku sita BWANA alifanya mbingu na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba, kwa hiyo Bwana akaibarikia siku ya sabato akaitakasa".
Kama lengo lako ni kutaka kuelewa bila shaka umeelewa.
 
kutoka 20:8-11. "Ikumbuke siku ya saba uitakase, siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote, lakini siku ya saba ni sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo USIFANYE KAZI NYOYOTE, wewe wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana kwa siku sita BWANA alifanya mbingu na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba, kwa hiyo Bwana akaibarikia siku ya sabato akaitakasa".
Kama lengo lako ni kutaka kuelewa bila shaka umeelewa.
Asante sasa nimeelewa kuhusu kumpumzika kwamba ni takwa la maandiko matakatifu na ni haki yenu kabisa hapo sina ubishi....kama ulivyonifafanulia hili naomba pia unifafanulie kwa kati ya Jumamosi na Jumapili ni siku ipi imelengwa na andiko hili?
 
Hii sio inchi ya kidini afu usipangie serikali kitu cha kufanya hutaki kufanya usaili usiendee sio lazima kuna watu mna vitu vya ajabu
 
Hatokujibu huyo Wa mchongo tuu!
Si haramu kwa mwislamu kufanya kazi siku ya ijumaa na hakuna aya yoyote kwenye msahafu wao unaowazuia kufanya kazi siku ya ijumaa. Ila waislamu huruhusiwa kwenda kwenye ibada masaa ya ibada yakifika siku ya ijumaa.
 
Hatuongei kibinafsi, bali tunaongea kisera! Unataka kuniambia wakristo WOTE hawahusiki na usaili huo?
Serikali ilisema Haina Dini kwa Ajili ya watu km Ninyi,Kila kitu Dini...Kwa hiyo waislamu nao wasiende kazini Ijumaa au hawana haki.
 
Huku ni KUPITILIZA na tunasema HAIKUBALIKI KABISA. Haiingii akilini watu na akili zao kuamua kutokuheshimu kwa makusudi imani ya watu ambao wanapaswa kuwa kwenye ibada KANISANI na kuipanga siku hiyo kuwa ni siku ya kuwasaili waombaji wa ajira.

Ina maana wanaoendesha usaili huu kama ni wakristo watakuwa wamedhulumiwa haki na uhuru wao wa kuabudu. Ina maana pia waombaji wa ajira walio wakristo watakuwa wamedhulumiwa haki na uhuru wao wa kuabudu. Hili tunalikataa kwa nguvu zetu zote!!

Tarehe 18/06/2022 siku ya JUMAMOSI (SIKU YA IBADA KWA WASABATO), na tarehe 19/06/2022 siku ya JUMAPILI (SIKU YA IBADA KWA WAKRISTO) zimetangazwa kuwa ni moja ya siku ambazo usaili wa waombaji wa ajira utafanyika. Kwanza jumamosi na jumapili siyo siku za kazi, kwa nini hawa sekretarieti ya ajira wameamua kuzifanya kuwa siku za kazi? Hii JEURI WANAIPATA WAPI? Ushahidi upo kwenye tovuti yao- www.ajira.go.tz na ninatupia kipande hapa:

KADA: ASSISTANT VOCATIONAL TEACHER – ELECTRICAL INSTALLATION MWAJIRI: MAMLAKA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI (VETA) TAREHE YA USAILI WA VITENDO: (1-37) 18 JUNI, 2022 (38-74) 19 JUNI, 2022 MAHALI: VETA DODOMA TAREHE YA USAILI WA MAHOJIANO: 22 JUNI, 2022 MUDA: SAA 1:00 KAMILI ASUBUHI. MAHALI: OFISI YA RAIS SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA ZILIZOPO MAJENGO YA DKT. ASHA ROSE MIGIRO, UDOM - DODOMA.

Ninamwomba waziri mwenye dhamana na sekretarieti hii kufanya mambo yafuatayo kwa dharula:
1. Kubatilisha hizo tarehe haraka na kagiza zipangwe tarehe zingine.
2. Kuwawajibisha wote waliofanya ujeuri huu wa kuleta utaratibu unaoashiria UDINI kwenye nchi yetu.
Hiyo ni mojawapo ya usaili.Kama vipi usiende.
 
Kuwakomoa tusiende
Lazima wabatilishe hiyo siku, vinginevyo matokeo ya usaili yatabatilishwa mahakamani maana yamefanyika kwa kuwabagua baadhi ya watu!! Hakuna namna LAZIMA wabatilishe na LAZIMA waliopanga hivyo WAWAJIBISHWE>
 
Huku ni KUPITILIZA na tunasema HAIKUBALIKI KABISA. Haiingii akilini watu na akili zao kuamua kutokuheshimu kwa makusudi imani ya watu ambao wanapaswa kuwa kwenye ibada KANISANI na kuipanga siku hiyo kuwa ni siku ya kuwasaili waombaji wa ajira.

Ina maana wanaoendesha usaili huu kama ni wakristo watakuwa wamedhulumiwa haki na uhuru wao wa kuabudu. Ina maana pia waombaji wa ajira walio wakristo watakuwa wamedhulumiwa haki na uhuru wao wa kuabudu. Hili tunalikataa kwa nguvu zetu zote!!

Tarehe 18/06/2022 siku ya JUMAMOSI (SIKU YA IBADA KWA WASABATO), na tarehe 19/06/2022 siku ya JUMAPILI (SIKU YA IBADA KWA WAKRISTO) zimetangazwa kuwa ni moja ya siku ambazo usaili wa waombaji wa ajira utafanyika. Kwanza jumamosi na jumapili siyo siku za kazi, kwa nini hawa sekretarieti ya ajira wameamua kuzifanya kuwa siku za kazi? Hii JEURI WANAIPATA WAPI? Ushahidi upo kwenye tovuti yao- www.ajira.go.tz na ninatupia kipande hapa:

KADA: ASSISTANT VOCATIONAL TEACHER – ELECTRICAL INSTALLATION MWAJIRI: MAMLAKA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI (VETA) TAREHE YA USAILI WA VITENDO: (1-37) 18 JUNI, 2022 (38-74) 19 JUNI, 2022 MAHALI: VETA DODOMA TAREHE YA USAILI WA MAHOJIANO: 22 JUNI, 2022 MUDA: SAA 1:00 KAMILI ASUBUHI. MAHALI: OFISI YA RAIS SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA ZILIZOPO MAJENGO YA DKT. ASHA ROSE MIGIRO, UDOM - DODOMA.

Ninamwomba waziri mwenye dhamana na sekretarieti hii kufanya mambo yafuatayo kwa dharula:
1. Kubatilisha hizo tarehe haraka na kagiza zipangwe tarehe zingine.
2. Kuwawajibisha wote waliofanya ujeuri huu wa kuleta utaratibu unaoashiria UDINI kwenye nchi yetu.
We mzee hivi kweli hili jambo nilakumsumbua waziri aache kufanya jambo la msingi ashughurike na hizi tarehe kwanii yaani??

Mungu yupo kila siku bhana nenda kwenye usaili au hata kabla ya huo usaili wako fanya ibada muombe mungu utakavyo nenda kwenye usaili sio lazima saana kuwepo na mtukati kati yako na mungu kwa ajili yakukuombea.


Achana na hizi lalamalama ambazo hazina maana,

Si tunapambania hizi saili zifanyike kwa zonal,, maana huko dodoma yaani nikama vile ishakuwa mbinu yakwanza kushortlist watu daaaaa!

Hivi hawaoni hili au makusudi yao tu jamanii nina shortlisted nyingi kwenye portal Ila naziangalia tu yaani.
 
Si haramu kwa mwislamu kufanya kazi siku ya ijumaa na hakuna aya yoyote kwenye msahafu wao unaowazuia kufanya kazi siku ya ijumaa. Ila waislamu huruhusiwa kwenda kwenye ibada masaa ya ibada yakifika siku ya ijumaa.
Kwani Mungu na Usaili kipi bora!! Wewe km Una imani kweli,Achana na Usaili nenda kanisani.
 
Serikali ilisema Haina Dini kwa Ajili ya watu km Ninyi,Kila kitu Dini...Kwa hiyo waislamu nao wasiende kazini Ijumaa au hawana haki.
Si haramu kwa mwislamu kufanya kazi siku ya ijumaa na hakuna aya yoyote kwenye msahafu wao unaowazuia kufanya kazi siku ya ijumaa. Ila waislamu huruhusiwa kwenda kwenye ibada masaa ya ibada yakifika siku ya ijumaa.
 
We mzee hivi kweli hili jambo nilakumsumbua waziri aache kufanya jambo la msingi ashughurike na hizi tarehe kwanii yaani??

Mungu yupo kila siku bhana nenda kwenye usaili au hata kabla ya huo usaili wako fanya ibada muombe mungu utakavyo nenda kwenye usaili sio lazima saana kuwepo na mtukati kati yako na mungu kwa ajili yakukuombea.


Achana na hizi lalamalama ambazo hazina maana,

Si tunapambania hizi saili zifanyike kwa zonal,, maana huko dodoma yaani nikama vile ishakuwa mbinu yakwanza kushortlist watu daaaaa!

Hivi hawaoni hili au makusudi yao tu jamanii nina shortlisted nyingi kwenye portal Ila naziangalia tu yaani.
Hili jambo limepangwa hivyo kimkakati ili kubagua baadhi ya watanzania. Kama unafikiri kuwa jambo hili ni dogo subiri na ulifuatilie jinsi litakavyoishia jambo hili!! Suala hili litaenda hadi mahakama ya juu kabisa kama akithubutu mtu kulishughulikia kivyepesi vyepesi!!
 
Lazima wabatilishe hiyo siku, vinginevyo matokeo ya usaili yatabalishwa mahakamani maana yamefanyika kwa kuwabagua baadhi ya watu!! Hakuna namna LAZIMA wabatilishe na LAZIMA waliopanga hivyo WAWAJIBISHWE>
Hahahaha ndo maana sipendagi kwenda kwenye makanisa ya ovyo ovyo yanaondoa ubongo wako kabisa
 
Back
Top Bottom