Uchaguzi 2020 Sera ya majimbo itaua utaifa na uzalendo

Uchaguzi 2020 Sera ya majimbo itaua utaifa na uzalendo

Mbana hata Sasa maeneo yenye rasilimali nyingi hayana maendeleo Huku dar es Salam ikiwa ndyo unaonekana inaendelea zaidi kwani Ina rasilimali nyingi
 
Geita ilipo chato unajua kuna migodi ya dhahabu mikubwa inayoingizia nchi Mabilioni ya pesa za kigeni ? Au unadhani chato ni singida wanakotegemea mauzo ya alizeti
Singida nasi tutabuni vyanzo vyetu vya mapato, tatamtoza pesa inayolingana na nauli kamili kila abiria anayekatiza Singida kwenda sijui kaskazini, kanda ya ziwa au kuelekea Dom. Mbona tutaombana pooo!
 
Maana yake halisi ni kuwa watu wenyewe kwenye maeneo yao, yawe mikoa au wilaya, ndio wawe wanachagua au kuwateua viongozi wao, kama wakuu wa mikoa, wilaya na halmashauri.

Pia maeneo hayo, pamoja na Bunge, viongezewe madaraka ya kuamua badala ya Rais pekee.
Pigia mstari *maeneo yao*! Nikuulize maaeneo ya wasukumu ni wapi? Lakini leo wapo mpaka Lindi hadi katavi japo siyo "maeneo yao*. Nikuulize wachaga maeneo yao ni yapi? Leo tazama wachaga walivyotapakaa nchi nzima. Nikuulize maeneo ya wapemba ni wapi? Leo mpemba yupo Singida analima vitunguu.
Kwa mfumo wa akili za mtz mweusi, ujue fika mtu atakapokosa cha kufanya ndani ya *maeneo yao* hawataweza kutoka nje ya *maeneo yao*, hata walioko nje ya *maeneo yao* watarudishwa kwa lazima kwenye *maeoneo yao*. Tafakari acha ushabiki maandazi.
 
Pigia mstari *maeneo yao*! Nikuulize maaeneo ya wasukumu ni wapi? Lakini leo wapo mpaka Lindi hadi katavi japo siyo "maeneo yao*. Nikuulize wachaga maeneo yao ni yapi? Leo tazama wachaga walivyotapakaa nchi nzima. Nikuulize maeneo ya wapemba ni wapi? Leo mpemba yupo Singida analima vitunguu.
Kwa mfumo wa akili za mtz mweusi, ujue fika mtu atakapokosa cha kufanya ndani ya *maeneo yao* hawataweza kutoka nje ya *maeneo yao*, hata walioko nje ya *maeneo yao* watarudishwa kwa lazima kwenye *maeoneo yao*. Tafakari acha ushabiki maandazi.
Maeneo yao maana yake ni maeneo waliko wananchi, si makabila. Huko huko walikochanganyika. Swala ni kwamba maamuzi yasifanywe na Rais pekee. Yeye kapigiwa kura, ni halali kufanya maamuzi lakini asihodhi madaraka yote. Lakini mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya, mkurugenzi wa halmashauri, wote hawa wana maamuzi makubwa kwenye 'maeneo yao', na hawachaguliwi wala kuteuliwa na wananchi wa maeneo hayo. Sera ya majimbo pengine CHADEMA wameipa jina linalotisha, lakini ina mantiki kubwa. Tuondoe upotoshaji, tujadili maana yake ya kweli.
 
Sera ya majimbo inakuwa applied sana kwenye nchi zenye eneo kubwa mfano mzuri Marekani,uchina,urusi na india wanatumia huu mfumo hata congo pia kwa mbaali unaona kama wanamajombo lakini kwetu autakuwa na maana ingawaje kwa kenya naona wanao lakini kuongeza gharama tu
 
SWALI NI: JE, MFUMO WA MAJIMBO UTALETA UKABILA NA KUFANYA BAADHI YA SEHEMU TANZANIA KUTOKUWA NA MAENDELEO?

Amani iwe nanyi wadau!

Leo napenda kuwajibu wana CCM wanaosema mfumo wa Majimbo utachochea ukabila na kusababisha baadhi ya maeneo kutokuwa na maendeleo,

Ukweli ni kuwa kamwe mfumo wa majimbo hautaleta ukabila na kamwe hautoleta kudumaa kwa maendeleo kwenye baadhi ya sehemu kama propaganda za CCM zinavyosema! Hii ni kwa sababu zifuatazo;

1. Jimbo la Kati- Mikoa ya Dodoma, Singida na Tabora na Morogoro.
Mikoa hii ina utajiri mkubwa wa mazao kama Tumbaku, Zabibu, Alizeti, Karanga, Asali na Mtama, Mpunga,Ndizi na Mahindi(vya mkoa wa Morogoro) Haya mazao tukipata viongozi wenye akili sio hawa wa CCM yataendelezwa vizuri na kuingiza mapato makubwa kwenye jimbo hili la kati.

Kuna uhitaji mkubwa sana wa Karanga na Asali kwenye masoko ya Asia na Ulaya. Haya mazao yakiendelezwa kisasa na kibiashara jimbo hili litanyanyuka mno kiuchumi. Hata viwanda vya mvinyo tu Dodoma vikiendelezwa na kutangazwa vizuri na mvinyo ukitengenezwa mzuri mapato

Pia kwenye jimbo hili kuna maliasili mbalimbali za wanyama kutokana na mapori ya akiba kama swagaswaga, manyoni na mapori ya Tabora ambayo pia yana tembo wengi na mbao nyingi. Hivi vitu vikiendelezwa na kutangazwa vizuri vitakuwa source kubwa ya mapato kutokana na uwindaji na utalii. Haya pia ni mapato makubwa sana.

Mkoa wa Morogoro una mbuga za wanyama kama mikumi, udzungwa na nyingine nyingi ambazo pia zitaleta mapato ya utalii.

Pia Kuna madini Kama dhahabu mikoa ya Tabora na Singida na Morogoro ambayo yakiendelezwa vizuri yataketa mapato makubwa sana kwenye maeneo haya. Hapo sijaweka biashara za mifugo, wanyama na viwanda ambavyo navyo vipo na vitakuwepo kwenye jimbo hili.

Kwa hiyo dhana ya Jimbo la Kati kuwa masikini si kweli.

2. Jimbo la Mashariki- Mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Pwani
Jimbo hili chanzo kikuu cha Maputo kitakuwa Bandari, Viwanda na Biashara. Kodi nyingi itakusannywa kutoka maeneo haya na kwa kweli itaendeleza kweli jimbo hili.

3. Jimbo la Kusini- Mikoa ya LINDI, Mtwara na Ruvuma
Jimbo hili lina utajiri mkubwa wa gesi na mazao ya korosho na mbaazi bila kusahau viwanda, bandari na uvuvi. - Hili jimbo litakuwa na na mapato makubwa sana ambayo yatajenga shule bora, hospitali, madawa, kujenga barabara nzuri na makazi bora.

Pia jimbo hili litakuwa na mapato ya utalii kutokana na hifadhi ya Selous na mapori ya akiba ya mkoa wa Ruvuma.

4. Jimbo la Nyanda za Juu kusini- Mikoa ya Iringa, Njombe,Songwe na Mbeya
Jimbo hili ndo mzalishaji mkuu wa chakula kinacholisha Tanzania, Afrika ya kati na Afrika mashariki. Kilimo na Biashara ya Chakula kitaingiza mapato makubwa sana kwenye jimbo hili. Biashara pia ya mbao na utalii kutokana na hifadhi za kipengele, Ruaha, Kitulo na Rungwe vitaingiza mapato makubwa sana kwenye jimbo hili.

Mipaka ya Zambia na Malawi pia itaingiza mapato makubwa kutokana na biashara bila kusahau viwanda na kilimo cha mashamba makubwa ya mpunga, maparachichi, nyanya, chai na miti.

5. Jimbo la Magharibi- Mikoa ya Katavi, Rukwa, Kigoma na Kagera- Mikoa hii ina utajili wa kilimo hasa cha mazao ya mahindi, tumbaku, mawese, miwa pamoja na miti pia. Pia ina uvuvi wa maziwa ya Tanganyika na Victoria.

Mikoa hii pia ina utalii wa mbuga za wanyama kama hifadhi za Gombe, Kimisi, Katavi, Mto Maragarasi pamoja na biashara kubwa na kodi katika mipaka ya nchi za Congo( Bandari) , Burundi, Rwanda na Uganda! Itoshe tu kusema kuwa jimbo hili pia litakuwa na mapato mengi sana ambayo yataboresha miondombinu ya barabara, hospitali , mashule na huduma za Maji safi na salama!!

6. Jimbo la Kaskazini- Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Mara.
Jimbo hili litakuwa na na chanjo kikuu cha mapato ambacho ni utalii na pia madini ya mikoa ya Arusha, Manyara na Mara. Utalii wa mbuga za kilimanjaro, Ngorongoro, Serengeti na Manyara utaingiza pesa nyingi sana za kuboresha miondombinu na huduma za msingi

Biashara pia na kodi kwenye mipaka ya Kenya kwa sehemu za holili,Silali na Arusha italeta mapato mengi Sana. Na hapa hujaweka kilimo cha ndizi, tangawizi na mifugo bila kusahau viwanda.

7. Jimbo la Kanda ya Ziwa (Victoria)- Mikoa ya Simiyu, Geita, Shinyanga na Mwanza.
Jimbo hili ndo kitovu cha madini Tanzania. Pia lina mbuga na mapori ya akiba mengi bila kusahau viwanda na biashara ambavyo vitaingiza napata mengi sana na kuleta impact kubwa sana kwenye uchumi. Uvuvi pia utaleta mapato mengi sana.

Dhana ya ukabila haiwezi kupata nguvu kwenye mfumo huu kwa sababu Kuna mchanganyo mkubwa wa makabila kwenye majimbo haya!

Pia chini ya mfumo huu kila mwananchi atawajibika kufanya kazi halali na kujituma kwa sababu atajua bila kufanya kazi hawezi endelea na sehemu yake haiwezi kufanya vizuri katika huduma za msingi.

Chini ya mfumo huu pia hakutakuwa na unyanyasaji wa wananchi kwa sababu wananchi watakuwa wanajua kuwa Mapato yao ndio yatakayowaletea maendeleo!

Viongozi pia watawajibika moja kwa moja kwa wananchi na kamwe hawatofuja mali kwa wananchi wala kuwagawa kwa misingi ya kikabila au kichama kwenye maendeleo.
kuanzisha kanda za uchumi Tanzania hicho ndio kitu bora zaidi kuliko kuanza na kanda za majimbo
 
Maeneo yao maana yake ni maeneo waliko wananchi, si makabila. Huko huko walikochanganyika. Swala ni kwamba maamuzi yasifanywe na Rais pekee. Yeye kapigiwa kura, ni halali kufanya maamuzi lakini asihodhi madaraka yote. Lakini mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya, mkurugenzi wa halmashauri, wote hawa wana maamuzi makubwa kwenye 'maeneo yao', na hawachaguliwi wala kuteuliwa na wananchi wa maeneo hayo. Sera ya majimbo pengine CHADEMA wameipa jina linalotisha, lakini ina mantiki kubwa. Tuondoe upotoshaji, tujadili maana yake ya kweli.
Hatufanyi upotoshaji, ndo uhalisia wa nchi yetu. Nimekaa Dar, Arusha, Moshi, Mwanza na Mbeya. Mjini watu wanachanganyikana poa tu, ila ukisogea maeneo ya pembezoni kidogo mgeni unabandikwa jina Fulani hivi amazing kuonyesha kuwa siyo wa kwao. Ubaguzi utangezeka maradufu katika mfumo wa majimbo.
 
Singida nasi tutabuni vyanzo vyetu vya mapato, tatamtoza pesa inayolingana na nauli kamili kila abiria anayekatiza Singida kwenda sijui kaskazini, kanda ya ziwa au kuelekea Dom. Mbona tutaombana pooo!
Umenena vyema mkuu ila sera ya majimbo si yakukomoana maana umejuwa na hasira ghafla.
 
Kenya enzi ya KANU ilikuwa nchi ya kijinga kwelikweli ila baada ya mabadiliko ya katiba Kenya unaiona sasa ilipo? Yani khaya mazimwi yoooteee yameondoka sisi tumebaki na hili la CCM tumeling'ang'ania.
Wacha uongo! Baada ya KANU kuondoka madarakani nini kimefanyika kikubwa Kenya zaidi rushwa kuhalalishwa na rasilimali za nchi kushikiliwa na familia chache huku ukabila ukiendelea kutamalaki kila kona? Waliolilia katiba mpya kenya wameipata na shida zipo palepale.
Wananchi maskini wanabaki kusoma hadithi za enzi zile za maziwa ya nyayo tuu

Maendeleo ni action sio blah blah
 
Nimekakuta mahali
Screenshot_20200923-103547.jpg
 
Itakuaje kila jimbo lisimamie rasilimali zake, kila mtu aajiriwe au kufanya biashara kwenye jimbo tuu
Natafakari
Dada ungeomba ueleweshwe majimbo yanafanyaje kazi. Sikiliza clip ya Lissu jana akiwa Kagera
 
Umenena vyema mkuu ila sera ya majimbo si yakukomoana maana umejuwa na hasira ghafla.
Si mnasema Singida tunategemea alizeti tu, ndo nawapa sasa vyanzo vya mapato vyetu. Wana jimbo tutakuwa huru vyanzo vyetu vya mapato na namna ya kutumia mapato hayo. Kama mdau alivyotoa mfano wa majimbo ya Marekani kugomea bomba la mafuta hivyo hivyo Sindiga tutagomea magari mabovu mabovu kukatiza anga zetu kwani yanatuchafulia mazingira. Haya majimbo yaje tu tuoneshane makali.
 
Back
Top Bottom