Serikali iachane na malipo kwa masikini wa TASAF bali ianze kuwalipa pesa walemavu wote wasio na ajira

Katika vitu vya kitahira huwa naona Serikali inafanya ni huu ujinga wa TASAF... Yaani kama wanataka kuwasaidia ni Bora wangekuwa wanawapa Ng'ombe au Mbuzi wafuge...
 
Kwani hizo pesa za TASAF ni zetu mpaka tuzipangie matumizi?
Mleta mada una wazo zuri ila kama fedha ni za wahisani basi itafanya vile wahisani wanavyotaka
 
Hizo hela za TASAF zinazokuuma ni kodi zako, wenye kodi zao ndio wanataka ziende huko unataka kuwapangia matumizi...
 
Hizo hela za TASAF zinazokuuma ni kodi zako, wenye kodi zao ndio wanataka ziende huko unataka kuwapangia matumizi...
Endelea kuamini hivyohivyo mkuu, usilolijua ni usiku wa giza.
 
Wanaewa fedha baada ya kufanya kazi mfano uchimbaji mfereji, bwawa nk.

Sasa mlemavu ataweza kuchimba bwawa?
 
Hizo hela za TASAF zinazokuuma ni kodi zako, wenye kodi zao ndio wanataka ziende huko unataka kuwapangia matumizi...
Sasa kuna ulazima gani wa serikali kukubali kupewa msaada au mkopo wenye masharti ambayo haitawasaidia wananchi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…