Serikali: Idadi ya wagonjwa wa Corona nchini Tanzania imeongezeka na kufikia Sita(6)

indigenous tupo na strong immunity exotic breeds zina sumbuliwa sana na hili dudu

Muda si mda, utaanza kuwa kama yule mwanasayansi wa Hitler aliyekuwa anapima ukubwa wa vichwa na bongo za watu akitafuta ushahidi wa kuwa weupe (wakidhaniwa kuwa na ubongo mkubwa) kuliko weusi, kwamba ndio sababu mhimu ya weupe kuwa 'superior' zaidi ya hawa wengine.

Nikuulize sasa, nawe tukuite mwanasayansi wa-------------.

Sitaki kumtaja jina.
 
Naamini huu ugonjwa (Covid 19) utapata chanjo muda sio mrefu, kwa sababu inavyo onekana hawa virusi hawabadiliki badiliki kwa haraka kama virusi wengine ambao unaweza kutengeza chanjo ndani ya miezi mitatu haifai tena.

NAOMBA TUELIMISHANE HUKO MITAANI NAMNA YA KUJIKINGA na sio watu kujitahidi kuwa wa kwanza kuandika kuwa wagonjwa wameongezeka .....idadi pekee haitusaidii sana.
Natamani na magonjwa mengine hatari kama Ukimwi, Malaria, nk yapate the same publicity...
 
Hii mijitu mixenge sana,kwani lazima msafiri kwenda hizo nchi zenye Corona?
 
Praying wont take away CORONA, if we can't take precautions sereously by ourselves and by government apparatus we will all die, if this comedy by government continues for any single minute we shall all die
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanapopima hizo symptoms mbona hawatengwi? Baada ya kuwa nazo

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimesema hivi: Wanapima joto la mwili tu. Na kuna watu wengi tu wenye virus lakini joto la mwili liko sawa. Hebu fikiria: Kama mtu ameambukizwa leo mchana na akasafiri jioni bila shaka kesho akipimwa joto la mwili wake litakuwa tu sawa kwani anakuwa bado hajaanza kuugua. Sasa mtu wa aina hiyo pale airport bila shaka ataruhusiwa kupita lakini akija kukaa eg siku 5 akianza kuwa na dalili basi linaweza kuwa juu. Hizi ndiyo cases kama za hawa wanaojitangaza kuwa wana virus wakati walipowasili na kupima walionekana hawana shida.
 
March 19, 2020

Mahojiano Live: Coronavirus: Tanzania latest

Taarifa sahihi ya serikali kwa umma

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile azungumzia Covid-19 (coronavirus)


Naibu Waziri ambaye kitaaluma ni mtabibu aliyehitimu masomo ya udaktari wa binadamu katika vyuo vikuu vya Muhimbili MUCHS Tanzania na ngazi ya masters huko Afrika ya Kusini leo kwa faida ya umma anazungumza na Ayo TV.
 
Pale mjinga anapotaka kuondoa tatizo la ujinga.
 
Kwelii kabsaa mkuu Ni ugonjwa hatari ila wameukuza sana. Sijui Nini Kiko nyuma ya pazia.

Ndugu zanguni chukueni tahadhari, huu ugonjwa haujakuzwa kwani ni zaidi ya ulivyoeleza kama hujapambana nao kwa asilimia 110. Ngoja nikupe TAKWIMU ZA LEO HUKO CHINA NA ULAYA:
  • ITALY mpaka leo 19/3/2020 waliofariki kwa corona ni watu 3405. masaa 24 (alhamisi) yaliyopita wamefariki watu 427, ikiwa ongezeko la 14%. walioambukizwa mpaka leo ni 41000. Hivyo mpaka leo Italy imeipita China ilipokuwa kwenye pick.
  • Uispania mpaka leo waliofariki ni 767. alhamisi peke yake wamefariki watu 209. Walioambukizwa na corona ni mpaka leo ni 17100. Jumatano tu walioambukizwa walikuwa 13700. Kwa siku moja tu wameambukizwa watu 17100 - 13700 = 3400.
Na hawa wenzetu wana nyenzo kabambe,. vipimo hupata majibu baada ya masaa 8 tu na vipo kila mji. Wamezuia karibu kila biashara na usafiri toka nje- magari na ndege. Hygine yao ni nzuri- sprit anayo kila mmoja mfukoni n.k

Iran wana hali mbaya.

Ninachotaka kusema ni kuwa tusicheze na huu ugonjwa, tukifanya mchezo na ukatuvamia kama ulivyowavamia wenzetu hakuna wa kupona. Tuchukue tahadhari sasa hivi.

Daktari wa Italy amesema hivi: Hajawahi kuona ugonjwa unaoshambulia mapafu na virus kuingia ndani zaidi ya mapafu na kuwa agresive na kushambulia kwa kasi sana kama huu.

Kwa juhudi za CHINA mpaka leo hakuna mgonjwa hata mmoja aliyekutikana na virusi vya corona ambaye ni mkazi wa china. Wanne wamepatikana lakini ni wageni walioingia kwa ndege toka nchi nyingine. Hongera China!!!!.

Hivyo ndivyo Tanzania tunatakiwa kuwa makini kabla maambukizi hayajakolea.
 
sasa si u update kuwa ni zaidi ya 6 au unapigaje hesabu?



Waziri mkuu Majaliwa athibitisha kwa kusema “Tuna ongezeko la wagonjwa wawili ambao ....

=====

Watu 2 kutoka Zanzibar na Dar wenye asili ya Kijerumani, Kimarekani wagundulika na virusi vya Corona Dar na Zanzibar.....
Moja ya wagonjwa wa leo ni Mwana FA na Meneja wa Diamond.[/CENTER][/QUOTE]



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nafikiria.

Shule zote za msingi, sekondari na vyuo wametangaziwa kusitisha masomo kwa siku 30. Ni katika harakati za kuepusha maambukizi na kusambaa kwa virusi vya Corona.

Ni wazo zuri sana ila bado napata ukakasi katika haya

1: Wanafunzi wa shule za bweni na vyuo watalazimika kusafiri, tayari maambukizi yamethibitishwa yapo Tanzania, endapo kuna mtu/watu m/wenye maambukizi inamaanisha anaweza kusambaza kwa wengi zaidi.

2: Mipaka ya nchi kuwa wazi kwa wanaoingia na kuzuia kutoka. Hili naona wamefanya kinyume, ni rahisi sana kudhibiti kusambaa kwa virusi wagonjwa wachache waliotambulika mpaka sasa hivi endapo mipaka itafungwa kwa wageni wanaokuja. Ila kwa wanalolifanya naona kama wanakaribisha mlipuko.

3: Uchache wa vituo vya kufanyia vipimo. Je endapo ikitokea maambukizi ktk mikoa ambayo haina vituo madhubuti kwa ajili ya upimaji, nini hatma ya wananchi !?

NB: Kuna vituo vilivyotajwa katika kanda eg Mawenzi, Mount Meru, Rufaa Mbeya, Bugando na Mloganzila n.k

Swali la kizushi.
Waliowekwa karantini Arusha, gharama za chakula, malazi, vinywaji nani anagharamia!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pesa za utalii zinalipia mshahara. Zikiondoka utaona kama mishahara haijasitishwa.

Biashara zimekufa, mapato tunayoambiwa ya ndani yameporomoka, waliokuwa wanatuokoa tumewatukana na kuwafukuza, zaidi tukawaambia waje watuombe sisi msaada, eti tumekuwa dona kantri.

Tumeingia kwenye projects zinazohitaji pesa nyingi na continuous flow kwa miaka kama mitatu hivi ndipo tuweze kuanza kupata mapato.

Kwa mwendo huo, hata ukiambiwa wanaokuja wana corona %100 utaweza kuwazuia? Pesa zao ndizo zinawezesha mkono uende kinywani.
 
Haya ndio tulikuwa tunayataka maana tungefunga mipaka bado mapema yasingetokea haya toka mgonjwa (1) mpka sita 6 hii inatisha.
 
Nafikiri tungetumia muda mwingi zaidi kuelimishana hapa jukwaani namna nzuri za kujiepusha tusiambukizwe, na pia wenye mawazo mbadala ya kusaidia matibabu kama wapo; Nafikiri kulaumiana na
KUTUMIA MUDA MWINGI KUSHABIKIA IDADI YA WAGONJWA au KUJITAHIDI KUWA WA KWANZA KUPOST IDADI YA WAGONJWA haitusaidii badala yake hufanya watu waonekane wameelimika ila hawana maarifa!
 
ngachoooookaaa kapisaaaa woiii

sasa tunapoelekea msishangae Pdidy naupata 1 Apr foolishday najitangaza na mimi sitaki ujinga

Hivi wanaotangaza ni Wizara ama wagonjwa wenyewe. Tukiruhusu hili msishangae wachagaa wote wanarudi Moshi kablà ya Pasaka kuogopa Corona na ndio wanatuongezea uchumi wa nchi hapa dar tutaliaa

tuache kabisaa hayamamboo kujitangaza OVYO
 
Italy sasa yaipiku China kwa vifo vya wagonjwa wa Covid19
Familia zote Katika miji ya Italy yawekwa kwenye self isolation, hakuna mtu kutoka nje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…