Serikali imetoa Bilioni 150 Kujenga Barabara ya Lusahunga - Rusumo

Serikali imetoa Bilioni 150 Kujenga Barabara ya Lusahunga - Rusumo

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

RAIS SAMIA AMETOA BILIONI 150 KUJENGA BARABARA YA LUSAHUNGA - RUSUMO

Mbunge wa Jimbo La Ngara Mhe. Ndaisaba Ruholo Amemupongeza Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan Kwa Kutoa Bilioni Mia Moja na Hamsin (150)Katika Mradi Wa Barabara ya Lusahunga Mpaka Rusumo Yenye Kilometa Tisini na Mbili (92)

Akiongea na Baadhi ya Wananchi Katika Mkutano Wa Hadhara Uliondaliwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kagera Mhe. Oliver Semuguruka Amesema Kuwa Ilikuwepo Changamoto ya Barabara hiyo Ambayo Ilikuwa Imeanza Kuchakaa na Kusema Kuwa anampongeza Mhe. Rais Kwa Kutoa Pesa Hiyo.

Amesema Kuwa Jimbo La Ngara Ni Miongoni wa Majimbo Ambayo Yamepokea Pesa Nyingi za Maendeleo na Kusema Kuwa Chama Cha Mapinduzi Kipo Tayari Kutekeleza Miradi Ya Maendeleo Kwa Wananchi.
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2024-07-21 at 16.45.59.mp4
    44.7 MB
Anamahela mengi.

Akumbuke na Barabara za mkoa wa Geita. Mkoa wa dhahabu Barabara za tope kama zizi la ng'ombe.
 
Ni maajabu kipande muhimu kabisa km hicho kimekaa katika hali ya uchakavu kwa muda mrefu sana kuzidi hata miaka 10, ngoja tusubiri utekelezaji
 
Swali Kwa Mhe
Mbunge na Mwandishi habari.Kwa kuwa Pesa hizi ni za walipakodi,Ni lini mtaanza kuwapongeza wananchi Kwa Kulipia Ujenzi wa hizi Barabara Kupitia Kodi wanazolipa??
 
Back
Top Bottom