CCM imekufa vipande vipande, mambo yote anafanya Magufuli.
Wabunge wa CCM Mpya mtajibeba, chama siyo muhimu ndiyo falsafa ya wakuja ndani ya CCM iliyo na kina Dr. Bashiru Ally, Humphrey Polepole ndo maana "sifa zote zinakwenda kwa bwana yule asiyetajwa jina" - in Bernard Membe voice na CCM si lolote sasa mtu mmoja ndiyo kila kitu.
Ndiyo maana fedha zote zinaelekezwa ktk Maendeleo ya Vitu kama SGR reli, Stiegler's Gorge, Bombadier , Madaraja ya baharini, Flyovers, Stendi Mpya za Mabasi ukubwa wa Airport ya Dar es Salaam kona nyingi za Tanzania... kwa kifupi miradi ya fahari ya macho...
Lakini Maendeleo ya Watu kama kulipa wakulima haki zao za korosho, mishahara kwa watumishi kama waalimu, kujenga hospitali kubwa kama ile ya Bugando Mwanza kila wilaya za Tanganyika ikiwa imejazwa vifaa-tiba, madaktari, wafamasia, Nuclear-Imaging-Radiology staffs, manesi.... siyo kipaumbele cha CCM hii Mpya.
Polepole : " Wewe Si Kitu Mbele ya Hiki Chama"