Serikali imuondoe Paul Makonda haraka kabla mambo hayajaharibika. Tamko lijalo linaweza kuathiri nchi pakubwa

USA huwa wanadeal na mtu specific ndiyo maana ameguswa yeye
Kama huwa wanadeal na mtu specific iweje wazuie raia wasio na hatia kucheza bahati nasibu ya green card lottery!? Hawa raia wana kosa gani?.
 
Jibuni hoja ya wamarekani .kwani wewe wangekupa URC. Wa DSM.vyombo vyote vya ulinzi vyako ungeshindwa dhibiti madawa ya kulevya? Jibuni hoja kimkakati!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukifuatilia vizuri utaona Magufuli plan zake zote toka mwanzoni zinalead sehemu moja tu, anataka Tanzania igeuke kua kama China under communist party. One man controls the party, one man controls the entire country, anareplace mtu yeyote ambaye anapinga kitu chochote regardless anachopinga ni sahihi au la anaweka watu ambao kazi yao ni kusifia 24/7 hata kama hawafit kazi wanayopewa. So far his plan is working perfectly.
 
Mbona huandiki na wangapi wamepoteza maisha kwa sababu yake? Usijitie macho kumchuzi kuona upande mmoja tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani mnataka kutuaminisha kuwa Makonda ni One man army?? Hao wenzake ni kina nani?? Tulieni tu jamani mambo haya yatakwisha ni upepo wa kisulisuli tu utapita
Nigeria na Elitrea wamezuiliwa nchini nzima wao wafamyeje?
 
Uhitaji kuwa mtalii ili ujue siri za nchi social media ni good source ya information yeyeto ya nchi yeyeto uitakayo.Sasa mtalii ajui lugha,pia Simu zote kumbuka zinarekodiwa jiulize kwanin Osama alikuwa atumii Simu.Kama wanawezayanasa mawasiliano ya siri ya magaidi sembuse ya washamba.
Kikwazo cha utumbuzi ndie mbeba siri,na TV bila remote haitowezawaka
 

Bandiko Murua kabisa hili. Watanzania wengi wana good will na JPM. Swali gumu labda ni kama haiwezekani kufanya yoooote anayoyafanya bila kuhangaishana na wakosoaji wake. Kwa mwenye akili anajua.....Raia 55 million hatuwezi kuwa na fikra sawa. Never! Kuandika yasipoandika magazeti ya ndani..ya nje yataandika. Na hiyo ndo mbaya Zaidi.

JPM asiporudi nyuma aka-focus kwenye agenda zake akaacha kukimbizana na wapinzani na wakosoaji wake..he will fail na historia itamkumbuka kwa mabaya..wakati miradi mikubwa kama SGR ingemuweka kwenye sehemu sahihi ya historia ya nchi yetu.

Huwezi kuendesha nchi kubwa kama Tanzania kama mtu mmoja na marafiki wajinga wachache kama akina Makonda. Lazima ukubali hulka ya binadamu ni tofauti. Haiko hivyo. Tumeumbwa kuhoji. Tumeumbwa kuudhi. Tumeumbwa na madhaifu mengi sana. Kikubwa usitoke kwenye reli. Ukisema uwapige risasi kwa sababu ya kuudhi..utawapiga wangapi??? ukisema uwafunge, utawafunga wangapi?

Eti Umuue Zitto kwa faida ipi? Risasi za Lissu zitaendelea kuwa kwenye doa jeusi kwa awamu hii. Was it worth it? Not sure!
 
CCM wanamtegemea huyu Makonda, nyie mnataka atoke.
Ataenda wapi?!

Mkimvua madaraka simtamuua kama kibaka?!

Huyo nchi hii hatosalimika akiachwa bila ulinzi atauwawa labda akatunzwe mahabusu au magereza for a long time.
 
Marekani imesema: Makonda ni mkandamizaji wa haki za kibinaadamu ikiwemo haki ya kuishi (kwa tafsiri isiyo rasmi ni kuwa anahusika na mauaji ya raia); haki ya kidemokrasia na nyinginezo. Anapaswa kuwekwa kando haraka!

Marekani imetega mtego usio na magego. Mtego mkali. Mtego wao unaanzia kwenye swali la kiudadisi: Makonda amefikiaje kukandamiza haki za kibinaadamu hadi kupigwa marufuku ya kuingia Marekani akiwa amezungukwa na wakuu wake(ukiwemo Mwenyekiti wangu) waliopaswa kumdhibiti?

Marekani imeamua kukusaidia kujitenga na Makonda. Marekani imekutega Rais na Mwenyekiti wangu Dr. John Pombe Magufuli. Imekusaidia na kukupa nafasi adhimu. Jitenge na Makonda kabla ya mambo mrama kwenda!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…