Serikali inapaswa kuona umuhimu wa kuweka sheria na utaratibu mzuri kwaajili ya watanzania wote wanaofanya kazi viwandani ili kuwalinda na ukatili

Serikali inapaswa kuona umuhimu wa kuweka sheria na utaratibu mzuri kwaajili ya watanzania wote wanaofanya kazi viwandani ili kuwalinda na ukatili

Genius Man

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2024
Posts
1,012
Reaction score
2,317
Watanzania maskini wengi wao wamekuwa wakipitia wakati mgumu na manyanyaso wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto wanaofanya kazi viwandani hali hii haikubaliki na inaminya haki za msingi za binadamu.

kuna ushahidi mkubwa kuwa kuna watanzania wengi wananyanyasika viwandani na kufanyishwa kazi kama mifugo kwa masaa 24 bila kupewa nafasi ya kupumzika huu ni ukoloni na unyama na wala sio sawa wala haki hao ni wanadamu sio mifugo.

lakini pia licha ya kufanyishwa kazi kwa masaa 24 bado malipo yao ni madogo na sio ya uhakika kuna siku nyengine hawalipwi chochote hatuwezi kwenda hivi sisi kama nchi kwani wanaoteswa ni watanzania wenzetu hivyo serikali inapaswa kuliangalia suala hili na kuona namna ya kukomesha vitendo vyovyote vya unyanyasaji kwenye maeneo hayo ikiwemo kuweka sheria na utaratibu mzuri ili kuwalinda watanzania wote na ukatili wanaofanya kazi huko.

Nashauri itungwe sheria na tuweke utaratibu mzuri ili kuwalinda watanzania wote wanaofanya kazi huko ikiwemo wanawake na watoto, hii ni pamoja na kuweka ukomo wa muda maalum wa watanzania kufanya kazi ili kuwalinda na kufanyishwa kazi kupita kiasi kama mifugo kwa muda mrefu, pia nashauri serikali kuangalia na kuweka kiasi maalum kama malipo sio watu wafanyishwe kazi masaa 24 alafu walipwe fedha kidogo mfano elfu 1000.

lakini pia nashauri serikali kuweka muda maalum wa kufanyika malipo hayo kwa wafanyakazi wote kwasababu kumekuwa hakuna utaratibu wa malipo hali inayoweza kupelekea watanzania wasilipwe malipo yao baada ya kazi, kwahiyo nashauri serikali kuweka muda maalum wa kufanyika malipo hayo kwa wakati ili kuhakikisha watanzania wanapata haki yao.

pia nashauri serikali kuweka sheria ili kuwalinda watoto wanaofanyishwa kazi viwandani ikiwemo kuweka ukomo wa umri wa watu wanaopaswa kufanya kazi huko, hii itasaidia kuwalinda watoto wetu kwani kwa sasa hakuna utaratibu mzuri wa kuwalinda watoto na ukatili hasa maeneo ya viwandani, nashauri serikali kuliangalia suala hili.
 
Sheria zipo, wametunga wenyewe, na kwa kuanzia tu ni nzuri, kisha maboresho yangefanyika kadiri ya mahitaji kutokana na wakati.

Tatizo linaanza kwenye usimamjzi wa sheria na taratibu!

Hakuna mwenye kiwanda au mtu yeyote atakayeweza kumnyanyasa raia anayelindwa na serikali yake. Serikali ni watu, na ndo hao wanaopewa bahasha ili watwana wanyanyasike.

Anza na OSHA, ukienda kila kiwanda kuna mabandiko yao kuonesha wanafuatilia na wako makini; ukiwaangalia watumishi wa hapo hapo kiwandani, hutodhani kama kuna OSHA au hata HR eneo husika.
  • Kazi za hatari
  • Vifaa vya kazi hamna
  • Vikingia ajali hakuna

Unakuta mtu kavaa mitambala miguuni, anacheza na moto bila apron, miwani, gloves etc. Na nyuma yake kasimama Nyapara akihakikisha kazi inafanywa sawia.
- Mtu huyo asiye kingwa, akikutwa amesinzia, kesi yake ni kubwa...kufukuzwa ni jambo la kawaida.

Sasa mamlaka imeshindwa kuwalinda raia wake kwasababu ya UROHO na UBINAFSI, ikaundwa VYAMA VYA WAFANYAKAZI VIWANDANI, watetee maslahi na mazingira bora ya kazi makazini....ndo hopeless kabisaaa!

Centra Gvt, inapaswa kuweka benchmark na kuhakikisha wmabwanyenye wanaelewa hiyo mark, kwa yeyote atakaye cross, hakuna swalia mtume!

Ni kama kudhani, pamoja na kuwa ni utawala wa kiimani, ukadhani kule uarabuni mamlaka hazijui ni jinsi gani WEUSI wanavyonyanyasika na kutwezwa utu wao, mamlaka ndo hao hao watu wanaofanya huo unyanyasaji majumbani, wakifika kwenye viti vya kiutawala watawalinda raia(wao wenyewe) dhidi ya tuhuma zozote zile na kuwasafisha popote pale!

Sio mageni hayo, kuna yule aliyempiga risasi dereva daladala, wakasema ilifyatuka bahati mbaya...vipi kuhusu safety lock, risasi kuingia kwenye chamber? Shabaha?

Au ile iliyokata kona angani ikarudi chini vertically kisha ikatafuta straight line horizontally na kumuondoa binti kwenye daladala.

Mwaka wa ngapi huu MAMLAKA imeshindwa kum-unfold ASIYEJULIKANA?

Au kwanini mtu wa kaliba ya Lisu, anasema tu kwa mdomo na kutuhumu watu waliompiga risasi ilhali anajua kabisa bila USHAHIDI usiotia shaka HUWEZI kumtuhumu mtu hadharani?

Serikali ya SA imeshikwa na Boers, wenye mashamba ni Boers, wenye kumiliki uchumi wa nchi ni Boers.
  • Weusi wanataka ujira kwa siku huki mashambani upandishwe kulingana na gharama za maisha.
  • Serikali haifanyi chochote wala kujali kwakuwa ndio hao hao wanaopaswa kulipa hao vibarua!
  • Matokeo yake, immigrants wao wako radhi kufanya kwa chochote kitu ilimradi aishi UGENINI.
  • Wenyeji wanachukua hatua ya kupambana na wanaokubaliana na MABWANYENYE ambao ndio waliokalia viti serikalini.

Xenophobia, dunia nzima inaambiwa BLACKS hamna kitu, wanapambana wenyewe kwa wenyewe.
  • Serikali ina deploy law enforcers kwenda kupiga risasi raia.
  • Raia wanarudi nyuma, wanakubaliana na ujira mdogo walioukataa, UNYANYASI umeshika hatamu kwa baraka ya WATAWALA.
 
Sheria zipo, wametunga wenyewe, na kwa kuanzia tu ni nzuri, kisha maboresho yangefanyika kadiri ya mahitaji kutokana na wakati.

Tatizo linaanza kwenye usimamjzi wa sheria na taratibu!

Hakuna mwenye kiwanda au mtu yeyote atakayeweza kumnyanyasa raia anayelindwa na serikali yake. Serikali ni watu, na ndo hao wanaopewa bahasha ili watwana wanyanyasike.

Anza na OSHA, ukienda kila kiwanda kuna mabandiko yao kuonesha wanafuatilia na wako makini; ukiwaangalia watumishi wa hapo hapo kiwandani, hutodhani kama kuna OSHA au hata HR eneo husika.
  • Kazi za hatari
  • Vifaa vya kazi hamna
  • Vikingia ajali hakuna

Unakuta mtu kavaa mitambala miguuni, anacheza na moto bila apron, miwani, gloves etc. Na nyuma yake kasimama Nyapara akihakikisha kazi inafanywa sawia.
- Mtu huyo asiye kingwa, akikutwa amesinzia, kesi yake ni kubwa...kufukuzwa ni jambo la kawaida.

Sasa mamlaka imeshindwa kuwalinda raia wake kwasababu ya UROHO na UBINAFSI, ikaundwa VYAMA VYA WAFANYAKAZI VIWANDANI, watetee maslahi na mazingira bora ya kazi makazini....ndo hopeless kabisaaa!

Centra Gvt, inapaswa kuweka benchmark na kuhakikisha wmabwanyenye wanaelewa hiyo mark, kwa yeyote atakaye cross, hakuna swalia mtume!

Ni kama kudhani, pamoja na kuwa ni utawala wa kiimani, ukadhani kule uarabuni mamlaka hazijui ni jinsi gani WEUSI wanavyonyanyasika na kutwezwa utu wao, mamlaka ndo hao hao watu wanaofanya huo unyanyasaji majumbani, wakifika kwenye viti vya kiutawala watawalinda raia(wao wenyewe) dhidi ya tuhuma zozote zile na kuwasafisha popote pale!

Sio mageni hayo, kuna yule aliyempiga risasi dereva daladala, wakasema ilifyatuka bahati mbaya...vipi kuhusu safety lock, risasi kuingia kwenye chamber? Shabaha?

Au ile iliyokata kona angani ikarudi chini vertically kisha ikatafuta straight line horizontally na kumuondoa binti kwenye daladala.

Mwaka wa ngapi huu MAMLAKA imeshindwa kum-unfold ASIYEJULIKANA?

Au kwanini mtu wa kaliba ya Lisu, anasema tu kwa mdomo na kutuhumu watu waliompiga risasi ilhali anajua kabisa bila USHAHIDI usiotia shaka HUWEZI kumtuhumu mtu hadharani?

Serikali ya SA imeshikwa na Boers, wenye mashamba ni Boers, wenye kumiliki uchumi wa nchi ni Boers.
  • Weusi wanataka ujira kwa siku huki mashambani upandishwe kulingana na gharama za maisha.
  • Serikali haifanyi chochote wala kujali kwakuwa ndio hao hao wanaopaswa kulipa hao vibarua!
  • Matokeo yake, immigrants wao wako radhi kufanya kwa chochote kitu ilimradi aishi UGENINI.
  • Wenyeji wanachukua hatua ya kupambana na wanaokubaliana na MABWANYENYE ambao ndio waliokalia viti serikalini.

Xenophobia, dunia nzima inaambiwa BLACKS hamna kitu, wanapambana wenyewe kwa wenyewe.
  • Serikali ina deploy law enforcers kwenda kupiga risasi raia.
  • Raia wanarudi nyuma, wanakubaliana na ujira mdogo walioukataa, UNYANYASI umeshika hatamu kwa baraka ya WATAWALA.
sheria zilizopo zinaonesha watu wanapaswa kufanya kazi kwa muda gani na wanapaswa kulipwa kwa muda gani na kiwango elekezi cha malipo ni kiasi gani ?
 
Siamini kama mtu mmoja anafanya kazi masaa 24 bila kupumzika

Labda kama unamaanisha watu wawili ama watatu wanapishana shift ili kukamilisha hayo masaa 24
 
sheria zilizopo zinaonesha watu wanapaswa kufanya kazi kwa muda gani na wanapaswa kulipwa kwa muda gani ?
Sina ujuvi wa sheria ila najua kuwa mwisho wa saa za kazi ni saa 45 kwa wiki.
- Saa za ziada zisizidi 50 kwa mwezi

Kibarua akifanyishwa kazi zaidi ya miezi mitatu mfululizo, inapaswa kupewa ajira eneo husika.

Malipo ya saa, siku, wiki, mwezi yanakubalika.
- Unakopesha nguvu, unalipwa baadae!
 
Siamini kama mtu mmoja anafanya kazi masaa 24 bila kupumzika

Labda kama unamaanisha watu wawili ama watatu wanapishana shift ili kukamilisha hayo masaa 24
Hakuna utaratibu maalum huko kwasababu hakuna utaratibu mzuri hii inawaweka watu wengi katika hatari ya kufanyishwa kazi kupita kiasi na wasimamizi wasio waaminifu hivyo bado kuna umuhimu wa kuweka muda maalum na unao weza kutekelezeka
 
Sina ujuvi wa sheria ila najua kuwa mwisho wa saa za kazi ni saa 45 kwa wiki.
- Saa za ziada zisizidi 50 kwa mwezi

Kibarua akifanyishwa kazi zaidi ya miezi mitatu mfululizo, inapaswa kupewa ajira eneo husika.

Malipo ya saa, siku, wiki, mwezi yanakubalika.
- Unakopesha nguvu, unalipwa baadae!
hizi sheria za jumla jumla sizani kama zinaweza kuleta mabadiliko kwenye upande wa viwandani labda kwa wa ofisini ni vyema kuwe na sheria maalum zinazonesha utaratibu wa kazi za viwandani zifanyike kwa malipo gani na muda gani
 
Back
Top Bottom