Serikali ingilieni kati, huu mfumo wa elimu utasababisha watoto waanze kuichukia shule

Serikali ingilieni kati, huu mfumo wa elimu utasababisha watoto waanze kuichukia shule

Mr mutuu

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2023
Posts
2,869
Reaction score
14,501
Nimerudi nyumbani kutoka mahali ninapofanyia shughuli zangu, nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana.

Mwanangu wa kwanza (4yrs old) alikuwa anapenda shule sana, mwaka jana alikuwa anasoma shule si mbali sana na hapa, walikuwa wanatoka saa 6 mchana, sasa mwaka huu nikaona nimtafutie nursery bora angalau hata mwakani aanze la kwanza.

Aisee sasa hivi ndio nimekaa nyumbani, yapata muda kidogo wife alinambia siku hizi dogo hapendi shule, nikamwambia labda hajapata marafiki hiyo shule mpya!

Sasa hawa watoto wa nursery wanaamka saa 11:30 saa 12 gari lipo getini, kutoka shule saa 12, homework kibao, mtoto muda wote namuona kachoka.

Leo kaamshwa kwenda shule mtoto analia tu, yaani hawa watoto wana ratiba ngumu kuliko hata watumishi, hivi kweli nursery mkiwaachia saa 7 kuna tatizo gani? Wanacheza na kurelax saa ngapi hawa watoto?

Leo naenda kukiwasha shuleni, mwanangu mwisho saa 8 atakua anakuja kuchukuliwa anapelekwa nyumbani, kama hawataki poa tu nitatafuta shule nyingine, uzuri private zipo kama utitiri.

Serikali wekeni miongozo ya elimu, hwa watoto wana ratiba ngumu hata physiological sidhani kama wanafurahia shule kama miaka yetu ile.

Elimu yenyewe hii ya kuja kukutana na mishahara ya laki 4 ukitoka chuo, upuuzi tu!
 
Nimerudi nyumbani kutoka Mahali napofanyia shughuli zangu nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana

Mwanangu wa kwanza(4yrs old) alikua anapenda shule sana, mwaka Jana alikua anasoma shule si mbali sana na hapa
Naunga mkono hoja.
 
Nimerudi nyumbani kutoka Mahali napofanyia shughuli zangu nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana

Mwanangu wa kwanza(4yrs old) alikua anapenda shule sana, mwaka Jana alikua anasoma shule si mbali sana na hapa walikua wanatoka saa 6 mchana, sasa mwaka huu nikaona nimtafutie nursery Bora angalau hata mwakani aanze la kwanza

Aisee sa ivi ndo nimekaa nyumbani yapata muda kidogo wife alinambia siku izi dogo hapendi shule nikamwambia labda hajapata marafiki Hio shule mpya! Sasa Hawa watoto wa nursery wanaamka sa 11:30 saa 12 gari lipo getini, kutoka shule saa 12, homework kibao mtoto muda wote namuona kachoka

Leo kaamshwa kwenda shule mtoto analia tu yaani Hawa watoto Wana ratiba ngumu kuliko hata watumishi, hivi kweli nursery mkiwaachia saa 7 Kuna tatizo Gani? Wanacheza na kurelax saa ngapi Hawa watoto??

Leo naenda kukiwasha shuleni mwanangu mwisho saa 8 atakua anakuja kuchukuliwa anapelekwa nyumbani, kama hawataki poa tu ntatafta shule nyingine uzuri private zipo kama utitiri

Serikali wekeni miongozo ya elimu Hawa watoto Wana ratiba ngumu hata physiological sidhani kama wanafurahia shule kama miaka yetu ile

Elimu yenyewe hii ya kuja Kukutana na mishahara ya laki 4 ukitoka chuo, upuuzi tu!!
Kuna kipind nilikua namgonjwa muhimbili sasa ikabid niwe nampelekea mahitaji asubuhi sababu kuona wagonjwa muhimbili ni saa 12 mpaka saa moja

Ikabid niwe naamka saa 10:40 ili niweze kuwahi sasa kwenye mwendokas saa 11 nakutana na watoto wadogo ukipiga hesabu wameamka saa 10 nikawa najiuliza inamaana kimara au mbezi hakuna shule mpaka waje wasome olympio na shule nyingine ambozo zipo ukanda wa posta na upanga niliwaonea huruma
 
Ila hapo mzazi ndo wakulaumiwa, shule hazina tatizo, wanaopeleka watoto ndo wana tatizo

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Serikali kupitia wizara ya elimu hawawezi kuja na miongozo kwani? Wanakula Kodi zetu afu wanashindwa kusimamia vitu vidogo kama hivi, anyway kwa kutambua nchi yangu ni kichwa Cha mwendawazimu Leo saa 10 naenda kukiwasha, wakikataa nakubali hasara namuhamishia shule nyingine

Kipindi natafuta shule nilipewa recommendation tu na mtu wangu wa karibu wife ndo alienda tulifanya kosa kutojua ratiba zao

Ila kwa huu upuuzi mi mwanangu hapana aisee
 
Kuna muda unaona Hawa Wana afadhali, akili nayo ikichoshwa sana haifai, tutazalisha kizazi Cha watu wa ajabu
Mlete dumu fagio aje awe anabishana Kuhusu Simba na Yanga

Kiufupi shule za private zipo vizuri katika kuamua destiny ya mtoto huko baadae Mimi shule za serikali nazichukia sipendi mtoto wangu asome huko dumu fagio ni uchafu Sana .
 
Serikali kupitia wizara ya elimu hawawezi kuja na miongozo kwani? Wanakula Kodi zetu afu wanashindwa kusimamia vitu vidogo kama hivi, anyway kwa kutambua nchi yangu ni kichwa Cha mwendawazimu Leo saa 10 naenda kukiwasha, wakikataa nakubali hasara namuhamishia shule nyingine

Kipindi natafuta shule nilipewa recommendation tu na mtu wangu wa karibu wife ndo alienda tulifanya kosa kutojua ratiba zao

Ila kwa huu upuuzi mi mwanangu hapana aisee
Na watoto wanatoka wamekula chakula cha hovyo sana wakati gharama kubwa.


Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Nimerudi nyumbani kutoka mahali ninapofanyia shughuli zangu, nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana.



Elimu yenyewe hii ya kuja kukutana na mishahara ya laki 4 ukitoka chuo, upuuzi tu!
Ety nae mzazi anasema mtoto wa miaka 4 unamuamsha SAA 11 alfajil kumuandaa aende shule kweli uko serious??? Huyo mwanao mkuu mtoto wa jirani four years old siku wazazi hatutaki kulea watoto tunataka walimu ndo watulelee poah
 
Nimerudi nyumbani kutoka mahali ninapofanyia shughuli zangu, nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana.

Mwanangu wa kwanza (4yrs old) alikuwa anapenda shule sana, mwaka jana alikuwa anasoma shule si mbali sana na hapa, walikuwa wanatoka saa 6 mchana, sasa mwaka huu nikaona nimtafutie nursery bora angalau hata mwakani aanze
Mkuu upo sahihi.

Waalimu watussidie hapa. Hii kumkaririsha mtoto mpaka namba 1,000 shule ya awali inakuwaje kwani?
 
Ety nae mzazi anasema mtoto wa miaka 4 unamuamsha SAA 11 alfajil kumuandaa aende shule kweli uko serious??? Huyo mwanao mkuu mtoto wa jirani four years old siku wazazi hatutaki kulea watoto tunataka walimu ndo watulelee poah
Basi linapita saa 12 we ulitaka aamshwe saa ngap
 
Nimerudi nyumbani kutoka mahali ninapofanyia shughuli zangu, nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana.

Mwanangu wa kwanza (4yrs old) alikuwa anapenda shule sana, mwaka jana alikuwa anasoma shule si mbali sana na hapa, walikuwa wanatoka saa 6 mchana, sasa mwaka huu nikaona nimtafutie nursery bora angalau hata mwakani aanze la kwanza.

Aisee sasa hivi ndio nimekaa nyumbani, yapata muda kidogo wife alinambia siku hizi dogo hapendi shule, nikamwambia labda hajapata marafiki hiyo shule mpya!

Sasa hawa watoto wa nursery wanaamka saa 11:30 saa 12 gari lipo getini, kutoka shule saa 12, homework kibao, mtoto muda wote namuona kachoka.

Leo kaamshwa kwenda shule mtoto analia tu, yaani hawa watoto wana ratiba ngumu kuliko hata watumishi, hivi kweli nursery mkiwaachia saa 7 kuna tatizo gani? Wanacheza na kurelax saa ngapi hawa watoto?

Leo naenda kukiwasha shuleni, mwanangu mwisho saa 8 atakua anakuja kuchukuliwa anapelekwa nyumbani, kama hawataki poa tu nitatafuta shule nyingine, uzuri private zipo kama utitiri.

Serikali wekeni miongozo ya elimu, hwa watoto wana ratiba ngumu hata physiological sidhani kama wanafurahia shule kama miaka yetu ile.

Elimu yenyewe hii ya kuja kukutana na mishahara ya laki 4 ukitoka chuo, upuuzi tu!
Bado hapo hawajaanza bebeshwa macounterbook.
 
Nimerudi nyumbani kutoka mahali ninapofanyia shughuli zangu, nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana.

Mwanangu wa kwanza (4yrs old) alikuwa anapenda shule sana, mwaka jana alikuwa anasoma shule si mbali sana na hapa, walikuwa wanatoka saa 6 mchana, sasa mwaka huu nikaona nimtafutie nursery bora angalau hata mwakani aanze la kwanza.

Aisee sasa hivi ndio nimekaa nyumbani, yapata muda kidogo wife alinambia siku hizi dogo hapendi shule, nikamwambia labda hajapata marafiki hiyo shule mpya!

Sasa hawa watoto wa nursery wanaamka saa 11:30 saa 12 gari lipo getini, kutoka shule saa 12, homework kibao, mtoto muda wote namuona kachoka.

Leo kaamshwa kwenda shule mtoto analia tu, yaani hawa watoto wana ratiba ngumu kuliko hata watumishi, hivi kweli nursery mkiwaachia saa 7 kuna tatizo gani? Wanacheza na kurelax saa ngapi hawa watoto?

Leo naenda kukiwasha shuleni, mwanangu mwisho saa 8 atakua anakuja kuchukuliwa anapelekwa nyumbani, kama hawataki poa tu nitatafuta shule nyingine, uzuri private zipo kama utitiri.

Serikali wekeni miongozo ya elimu, hwa watoto wana ratiba ngumu hata physiological sidhani kama wanafurahia shule kama miaka yetu ile.

Elimu yenyewe hii ya kuja kukutana na mishahara ya laki 4 ukitoka chuo, upuuzi tu!
Sasa kwanini ulimpeleka shule ya mbali na nyumbani na unajua changamoto za Dar ?
 
Nimerudi nyumbani kutoka mahali ninapofanyia shughuli zangu, nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana.

Mwanangu wa kwanza (4yrs old) alikuwa anapenda shule sana, mwaka jana alikuwa anasoma shule si mbali sana na hapa, walikuwa wanatoka saa 6 mchana, sasa mwaka huu nikaona nimtafutie nursery bora angalau hata mwakani aanze la kwanza.

Aisee sasa hivi ndio nimekaa nyumbani, yapata muda kidogo wife alinambia siku hizi dogo hapendi shule, nikamwambia labda hajapata marafiki hiyo shule mpya!

Sasa hawa watoto wa nursery wanaamka saa 11:30 saa 12 gari lipo getini, kutoka shule saa 12, homework kibao, mtoto muda wote namuona kachoka.

Leo kaamshwa kwenda shule mtoto analia tu, yaani hawa watoto wana ratiba ngumu kuliko hata watumishi, hivi kweli nursery mkiwaachia saa 7 kuna tatizo gani? Wanacheza na kurelax saa ngapi hawa watoto?

Leo naenda kukiwasha shuleni, mwanangu mwisho saa 8 atakua anakuja kuchukuliwa anapelekwa nyumbani, kama hawataki poa tu nitatafuta shule nyingine, uzuri private zipo kama utitiri.

Serikali wekeni miongozo ya elimu, hwa watoto wana ratiba ngumu hata physiological sidhani kama wanafurahia shule kama miaka yetu ile.

Elimu yenyewe hii ya kuja kukutana na mishahara ya laki 4 ukitoka chuo, upuuzi tu!
Mtoto wa miaka minne homework ya nini? Hao walimu kweli ni wa nursery?

Amandla...
 
Labda wanaamini wazazi wengi muda wa saa 7 wanakuwa wako kazini kwahiyo wanawachelewesha ili wakutane jioni.
Hiyo ni kwa sababu wapo wazazi huwapeleka watoto nursery kama kumtunza tu(huku alison's) wakati yeye akiwa kazini.
 
Back
Top Bottom