Serikali inunue umeme Ethiopia, tatizo ni kubwa mno. Pole Biteko

Serikali inunue umeme Ethiopia, tatizo ni kubwa mno. Pole Biteko

Tik

Toka Magu aondoke hujui matumizi ya Umeme yameongezeka, TANESCO Wameunga zaidi ya wateja laki 3, Sasa unategemea Nini.

Nimesema Umeme unakatika kwasababu mbili, uzalishaji mdogo na ubovu wa miundombinu, ukinunua utakuwa umetatua tatizo la uzalishaji, halaf unapambana na la ubovu,
Ukinunua- utanunuaje na hauna dolla? Ethiopia hawataki dolla?

Halafu unaongelea Ethiopia - Tanzania, hiyo load ya umeme itakuwa remote? Wireless? High Tension Transmission kutoka Ethiopia hadi Dar nani atagharimia? Kwa nini hizo pesa zisimalizie miundo mbinu ya kwetu?
 
Biteko anawaambia TANESCO kuwa wananchi wanataka umeme, wananchi hawataki kusikia sijui kuna mipango na porojo gani kama alivyokuwa anasema Makamba, lakini hata akiwaambia wananchi wanataka umeme huo umeme utatoka wapi? Kwanini wananchi tusiwapime CCM kwa kutumia umeme?

Jinsi na kadiri siku zinavyoenda tatizo la upatikanaji umeme linazidi kwasababu;

1. Mahitaji ya umeme kwa wananchi yameongezeka kwasababu ya kujua kiuchumi, mahitaji ambayo uzalishaji uliopo umefeli. Ndio maana toka Makamba ameingi mpaka leo Biteko yupo mgao wa umeme upo kila siku.

2. TPDC wana uhaba mkubwa wa gesi, hivyo kupelekea baadhi ya mitambo ya gesi mara kwa mara kuwa nje, ila TPDS wamejaa kimya ili hali wanajua kuna uhaba na upungufu wa gesi, na uwezo wa kutatua tatizo hawana mpaka wazungu waingilie kati.

3. Maji ni shida kwenye mabwawa, uzalishaji wa mabwawa hautoshelezi, na nashangaa kwanini mama amemtoa Kalemani, kamtoa Makamba, kaja Biteko lakini kwa tatizo hili ya umeme nchi hii halitakuwa rahisi kwake.

4. Makamba kasaini mikataba ya trilioni 1.9 kuimarisha upatikanaji wa umeme ambao haupo, pamoja na fedha nyingi kutolewa matatizo ya umeme bado ni makubwa, umeme unakatika katika, kwasababu ya ubovu wa miundombinu na uzalishaji usiojitosheleza.

Lengo la uzi huu ni kuiomba Serikali Sasa ifikirie njia rahisi ya kutatua tatizo la umeme Kwa kununua umeme kutoka Ethiopia kupitia Kenya, kwani Ethiopia wana umeme mwingi wa bwawa la grand.

Kwakuwa upungufu wa Dolla utasababisha Stiglers kuchelewa kukamilika basi tufanye mpango tununue umeme Ethiopia. Japo serikali imeishiwa fedha za kumaliza mradi wa njia kubwa kilo volt 400 kutoka namanga kwenda Arusha, Babati, basi ikakope na tuhakikishe tunajenga miundombinu ya kununua umeme Ethiopia, hizi shida za mgao hazivumiliki.
Kama tatizo la umeme ,lipo kwenyelevel za Kalemani, Makamba, au Dotto basi tunashida kubwa ( whichi is obvious) Kam Taifa!
 
Biteko anawaambia TANESCO kuwa wananchi wanataka umeme, wananchi hawataki kusikia sijui kuna mipango na porojo gani kama alivyokuwa anasema Makamba, lakini hata akiwaambia wananchi wanataka umeme huo umeme utatoka wapi? Kwanini wananchi tusiwapime CCM kwa kutumia umeme?

Jinsi na kadiri siku zinavyoenda tatizo la upatikanaji umeme linazidi kwasababu;

1. Mahitaji ya umeme kwa wananchi yameongezeka kwasababu ya kujua kiuchumi, mahitaji ambayo uzalishaji uliopo umefeli. Ndio maana toka Makamba ameingi mpaka leo Biteko yupo mgao wa umeme upo kila siku.

2. TPDC wana uhaba mkubwa wa gesi, hivyo kupelekea baadhi ya mitambo ya gesi mara kwa mara kuwa nje, ila TPDS wamejaa kimya ili hali wanajua kuna uhaba na upungufu wa gesi, na uwezo wa kutatua tatizo hawana mpaka wazungu waingilie kati.

3. Maji ni shida kwenye mabwawa, uzalishaji wa mabwawa hautoshelezi, na nashangaa kwanini mama amemtoa Kalemani, kamtoa Makamba, kaja Biteko lakini kwa tatizo hili ya umeme nchi hii halitakuwa rahisi kwake.

4. Makamba kasaini mikataba ya trilioni 1.9 kuimarisha upatikanaji wa umeme ambao haupo, pamoja na fedha nyingi kutolewa matatizo ya umeme bado ni makubwa, umeme unakatika katika, kwasababu ya ubovu wa miundombinu na uzalishaji usiojitosheleza.

Lengo la uzi huu ni kuiomba Serikali Sasa ifikirie njia rahisi ya kutatua tatizo la umeme Kwa kununua umeme kutoka Ethiopia kupitia Kenya, kwani Ethiopia wana umeme mwingi wa bwawa la grand.

Kwakuwa upungufu wa Dolla utasababisha Stiglers kuchelewa kukamilika basi tufanye mpango tununue umeme Ethiopia. Japo serikali imeishiwa fedha za kumaliza mradi wa njia kubwa kilo volt 400 kutoka namanga kwenda Arusha, Babati, basi ikakope na tuhakikishe tunajenga miundombinu ya kununua umeme Ethiopia, hizi shida za mgao hazivumiliki
Kwani huyo makamba alikopa hizo trilioni zifanye kazi ya umeme au ilikuwa kupitishia tu huko katika namna ya kuiba?
Wazo lako ni kununua umeme kutoka Ethiopia
 
Biteko anawaambia TANESCO kuwa wananchi wanataka umeme, wananchi hawataki kusikia sijui kuna mipango na porojo gani kama alivyokuwa anasema Makamba, lakini hata akiwaambia wananchi wanataka umeme huo umeme utatoka wapi? Kwanini wananchi tusiwapime CCM kwa kutumia umeme?

Jinsi na kadiri siku zinavyoenda tatizo la upatikanaji umeme linazidi kwasababu;

1. Mahitaji ya umeme kwa wananchi yameongezeka kwasababu ya kujua kiuchumi, mahitaji ambayo uzalishaji uliopo umefeli. Ndio maana toka Makamba ameingi mpaka leo Biteko yupo mgao wa umeme upo kila siku.

2. TPDC wana uhaba mkubwa wa gesi, hivyo kupelekea baadhi ya mitambo ya gesi mara kwa mara kuwa nje, ila TPDS wamejaa kimya ili hali wanajua kuna uhaba na upungufu wa gesi, na uwezo wa kutatua tatizo hawana mpaka wazungu waingilie kati.

3. Maji ni shida kwenye mabwawa, uzalishaji wa mabwawa hautoshelezi, na nashangaa kwanini mama amemtoa Kalemani, kamtoa Makamba, kaja Biteko lakini kwa tatizo hili ya umeme nchi hii halitakuwa rahisi kwake.

4. Makamba kasaini mikataba ya trilioni 1.9 kuimarisha upatikanaji wa umeme ambao haupo, pamoja na fedha nyingi kutolewa matatizo ya umeme bado ni makubwa, umeme unakatika katika, kwasababu ya ubovu wa miundombinu na uzalishaji usiojitosheleza.

Lengo la uzi huu ni kuiomba Serikali Sasa ifikirie njia rahisi ya kutatua tatizo la umeme Kwa kununua umeme kutoka Ethiopia kupitia Kenya, kwani Ethiopia wana umeme mwingi wa bwawa la grand.

Kwakuwa upungufu wa Dolla utasababisha Stiglers kuchelewa kukamilika basi tufanye mpango tununue umeme Ethiopia. Japo serikali imeishiwa fedha za kumaliza mradi wa njia kubwa kilo volt 400 kutoka namanga kwenda Arusha, Babati, basi ikakope na tuhakikishe tunajenga miundombinu ya kununua umeme Ethiopia, hizi shida za mgao hazivumiliki.
Hizo gharama za kununua umeme Ethiopia ni upuuz na sio sustainable na viable kiuchumi ,kuna gharama kubwa za kujenga power transmission lines na miundombinu ,wakati tungeweza kutumia pesa hizo na kuongezea kiasi ili kujenga kinu cha nuclear kufua umeme na kuanza kuvuna Uranium yetu pale Dodoma kwa ajili ya uzalishaji wa nishati ya umeme ,kitu ambacho ni sustainable in the future ,
Ukizingatia hata mabadiliko ya hali ya hewa yanaongezeka hivyo hata kufua umeme kwa kutumia maji sio sustainable in the future kwani maji yanapungua kwenye vyanzo vya maji .

Pia tungeweza kuwekeza kwa kujenga vinu vipya vya kufua umeme kwa kutumia makaa ya mawe ,tuna reserve kubwa ya makaa ya mawe nchi hii kule Songea ,Mbeya ,Njombe , Rukwa nk .na huu ndio mfumo wa bei rahisi kabisa wa kufua umeme ,cost za kujenga hivi vinu vya kufua umeme kwa joto (thermal power plant ) ni cheapest kabisa ukilinganisha na njia nyingine za kufua umeme ,
Why tumeshindwa hilo ? ,Kila siku tunaleta visingizio vya kipuuz ,
 
Tatizo la umeme katika nchi yenye mito, gesi, volcano, makaa ya mawe, upepo na jua ni ya kujitakia.
Tunaongozwa na watu wenye akili finyu ,that's all .Nchi yoyote yenye watu wenye akili ,public utilities hasa umeme na nishati kiujumla sio kitu cha kuleta masikhara kabisa .
Ni nchi wapumbavu kama hii ndio utakuta mambo kama haya
 
Kila mradi mkubwa unapoanzishwa Huwa tunaambiwa bei itashuka. Mradi ukiisha Bei ya umeme inapapnda. Tuliambiwa umeme wa gas ya Mtwara ndiyo kila kitu na bei ingeshuka sana matokeo yake bei inapanda kila mwaka. Hilo bwawala Nyerere nalo likikamilika umeme utapanda tu kwakuwa sasa hivi wameamua kupandisha Bei kwa njia ya tozo. Hakuna nafuu yoyote ya umeme itakayotokea katika Tanganyika
Halafu hawa wapumbavu TANESCO si ndio walisamehe deni la bilioni 60 walilokuwa wanaodai serikali ya Zanzibar ?
Pumbavu sana
 
Magu aliunganisha wsteja wengi kuliko awamu zote, hatukuona umeme ukikatika,
Ngoja niwaeleze
Umeme unakatika, maji yanakatika, mafuta yanakatia, bei zinapaaa usiku na mchana.
Tuacheni kuongea siasa hawa ccm nchi imewashinda
Huyo hajielewi tu
 
Suala la dollar limeumiza sana makampuni ya kigeni hasa ya mafuta, uendeshaji umekuwa mgumu sana kwenye shughuli zao za kila siku na serikali ipo kimya wala hawana mpango wa namna ya kutatua hili tatizo la kukosekana kwa dollar
 
Biteko anawaambia TANESCO kuwa wananchi wanataka umeme, wananchi hawataki kusikia sijui kuna mipango na porojo gani kama alivyokuwa anasema Makamba, lakini hata akiwaambia wananchi wanataka umeme huo umeme utatoka wapi? Kwanini wananchi tusiwapime CCM kwa kutumia umeme?

Jinsi na kadiri siku zinavyoenda tatizo la upatikanaji umeme linazidi kwasababu;

1. Mahitaji ya umeme kwa wananchi yameongezeka kwasababu ya kujua kiuchumi, mahitaji ambayo uzalishaji uliopo umefeli. Ndio maana toka Makamba ameingi mpaka leo Biteko yupo mgao wa umeme upo kila siku.

2. TPDC wana uhaba mkubwa wa gesi, hivyo kupelekea baadhi ya mitambo ya gesi mara kwa mara kuwa nje, ila TPDS wamejaa kimya ili hali wanajua kuna uhaba na upungufu wa gesi, na uwezo wa kutatua tatizo hawana mpaka wazungu waingilie kati.

3. Maji ni shida kwenye mabwawa, uzalishaji wa mabwawa hautoshelezi, na nashangaa kwanini mama amemtoa Kalemani, kamtoa Makamba, kaja Biteko lakini kwa tatizo hili ya umeme nchi hii halitakuwa rahisi kwake.

4. Makamba kasaini mikataba ya trilioni 1.9 kuimarisha upatikanaji wa umeme ambao haupo, pamoja na fedha nyingi kutolewa matatizo ya umeme bado ni makubwa, umeme unakatika katika, kwasababu ya ubovu wa miundombinu na uzalishaji usiojitosheleza.

Lengo la uzi huu ni kuiomba Serikali Sasa ifikirie njia rahisi ya kutatua tatizo la umeme Kwa kununua umeme kutoka Ethiopia kupitia Kenya, kwani Ethiopia wana umeme mwingi wa bwawa la grand.

Kwakuwa upungufu wa Dolla utasababisha Stiglers kuchelewa kukamilika basi tufanye mpango tununue umeme Ethiopia. Japo serikali imeishiwa fedha za kumaliza mradi wa njia kubwa kilo volt 400 kutoka namanga kwenda Arusha, Babati, basi ikakope na tuhakikishe tunajenga miundombinu ya kununua umeme Ethiopia, hizi shida za mgao hazivumiliki.
Na huku bwawa la stigler gorge limeanza kutoa nyufa, wabongo sijui tunakwama wapi.
 
Kwani hamna nishati ya Geothermal(mvuke)hapo bongo ilhali mpo kwenye eneo la bonde la ufa?
Hapa Kenya tunaujuzi wa kuvua Geothermal miaka za kutosha tu na kupelekea hata Uhabeshi kukodisha kampuni yetu ya kiserikali (KenGen) kuwavunia nishati hiyo.
Nishati hutafutwa na njia zote,iwe upepo,maji,nyuklia,mvuke(geothermal),jua,mkaa na kadhalika.
Mpo wengi kutuzidi labda sijui tu kiasi Cha matumizi yenu lakini pia mkumbuke mna mradi wa treni za umeme.
Kwa hivyo msijisahaulishe kuwa majuto ni mjukuu,huja kinyumenyume.
Hata hivyo nafahamu mna gesi ya kumwaga labda mnahitaji tu subira.
Mtaarifuni mama.
 
Anasema
Wananchi wataka umeme na bodi aliyenayo ileile ,mkurugenzi yuleyule
 
Kila mradi mkubwa unapoanzishwa Huwa tunaambiwa bei itashuka. Mradi ukiisha Bei ya umeme inapapnda. Tuliambiwa umeme wa gas ya Mtwara ndiyo kila kitu na bei ingeshuka sana matokeo yake bei inapanda kila mwaka. Hilo bwawala Nyerere nalo likikamilika umeme utapanda tu kwakuwa sasa hivi wameamua kupandisha Bei kwa njia ya tozo. Hakuna nafuu yoyote ya umeme itakayotokea katika Tanganyika
Bei itapungua tutakapokuwa na uwezo wa kujenga miradi wenyewe kwa kutumia wataalamu wetu.
Kwa sasa miradi yote mikubwa ni kuendeleza mataifa yaliyotuletea contractors, kuanzia barabara, maji, reli tunaoendeleza China. Hata bwawa la Nyerere mchina amefanya kazi ya kujenga tuta kuu. Hivyo pesa yetu imepitia Misri kwenda China. SGR imeenda Uturuki.
Hizi hadithi za wanasiasa wetu kwamba ni maendeleo kujengewa barabara zote na miradi mikubwa ya maji baada ya miaka 60 ya uhuru ni za kupuuzwa, kizazi kipya kijenge uwezo wa ndani ili kupata maendeleo ya kweli na endelevu.
 
Back
Top Bottom