Serikali itunge sheria kuhusu uzazi wa mpango angalau watoto wawili kila familia maana kasi ya uzazi Tanzania inatisha

Uhakika wa soko hautokani na kuzaliana bali kipato cha wato, hata mkizaliana kama kumbikumbi kama ni mafukara hakuna chochote cha maana kitafanyika zaidi ya uharibifu wa nchi.
Nimekuelewa mtaalam.Asante.
 
Wanafunzi kuwa wachache eneo hilo sio kwa sababu watoto ni wachache bali ni kukimbia shule au utoro. Sehemu kubwa ya Tanzania watoto wamelundikana madarasani,walimu wana mzigo wa wakufundisha madarasa yaliyojaa kupita kiasi.
 
Kama hauna mbegu za kuzalisha wapishe wenye nazo tafadhali, kwani umeombwa msaada wa kuwasaidia hao wenye watoto wengi?
Ndio, mimi kila siku naombwa na wengi sana.
 
Watu wanazaa kama kuku, na maisha yenyewe ndo haya. Serikali iamrishe mwisho watoto wawili kama china. Zaidi ya hapo faini. Maana hata watoto wa mitaani wataisha kabisa na kazi zitakua nyingi kulingana na idadi ya watu waliomo
Sahihi kabisa
 
Kama mmeshindwa ongoza Nchi na kuweka mipango bora kaeni kimiya , acha tuzae, Mambo gani tena Sasa .
 
Kama mmeshindwa ongoza Nchi na kuweka mipango bora kaeni kimiya , acha tuzae, Mambo gani tena Sasa .
Mnaweza kuwahudumia na kuwapa maisha bora yanayomstahili binadamu hao mnaowazaa kama kumbikumbi?
 
Wanafunzi kuwa wachache eneo hilo sio kwa sababu watoto ni wachache bali ni kukimbia shule au utoro. Sehemu kubwa ya Tanzania watoto wamelundikana madarasani,walimu wana mzigo wa wakufundisha madarasa yaliyojaa kupita kiasi.
Mimi ni mdau Wa elimu ndugu na. Tanzania nimeizunguka sana best ukerewe ni kisiwa platform ni ndogo huko niliko kutajia eneo LA machame Masama hakuna utoro ingekuwa kuwa kama eneo LA rungwa Singida mpaka ni na chunya au mwamagembe. Ningekukukubalia ila kutokana na aridhi UA. Tanzania bado population ni ndogo wewe shauri serikali waongeze shule kila sehemu yenyewe idadi kubwa ya watu kama eneo hilo nililotolea mfano urefu Wa kilometa mbili sehemu hiyo INA shule za msingi tano(5) na vituo viwilo Vya afya hivyo kila eneo serikali ingejenga hivyo wala kusingikuwa na high population and no congested hamasisha serikali kujenga shule za kutosha
 
Kwa ujumla Tanzania ina wanafunzi wengi kuliko vyumba vya madarasa, madawati, matundu ya choo, walimu na vitabu vinavyohitajika.Huko kwenu Masama hakuwakilishi Tanzania pana.
 
Ndugu ,inaonekana umekalili theory za wazungu,zilizoshindwa.Biblia inasema zaeni mkaongezeke.Angalia Canada,Sweden na nchi nyingi za ulaya.Walikataa kuzaa na sasa hawana nguvu kazi.Wanaagiza watu kutoka Africa.CHINA walizaa sana.Na sasa watu wanafanya kazi na uchumi upo juu.Acha watu wazae ,ndio soko hilo.
 
Ila unapo kuwa na watu wengi ambao ni jobless si mtaji tena ni hasara kwa taifa
 
Unashangaza kufananisha uzaaji wa china na nchi kama tanzania na yawezekana huna taarifa sahihi za china
 
Unashangaza kufananisha uzaaji wa china na nchi kama tanzania na yawezekana huna taarifa sahihi za china
Ndugu ,unapofanya argument, uwe na twakwimu za kutosha.Usilete vitu vya kukalili vya wazungu.
 
Umeangalia idadi ya vifo pia?
 
Kama tulishakuomba pesa ya kulisha familia zetu una haki ya kutupangia.
 
Pimbi, mi mpaka wafike 10
 
Ndugu ,unapofanya argument, uwe na twakwimu za kutosha.Usilete vitu vya kukalili vya wazungu.
Kwani aliye ongea habari za china ni mimi au wewe ? Nani alikudanganya kwamba china hawana mpango wa uzazi? Nani aliye kalili hapa?
 
Kama tulishakuomba pesa ya kulisha familia zetu una haki ya kutupangia.
Kwa hiyo mnapo tozwa tozo msilalamike kwa sababu hao wama mnao watia mimba hovyo wanatibiwa vituo vya afya vya serikali na hawazalii sebleni kwako

Hapo ukiambiwa tu na mtendaji kata wako changia Tsh.3000/= za kujenga madarasa kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa basi mtalalamika hapo hadi mnafunga na kuomba mtendaji kata afe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…