Serikali itunge sheria kuhusu uzazi wa mpango angalau watoto wawili kila familia maana kasi ya uzazi Tanzania inatisha

Serikali itunge sheria kuhusu uzazi wa mpango angalau watoto wawili kila familia maana kasi ya uzazi Tanzania inatisha

@Mathanzua na @safuher mnakubaliana
Nikushukuru sana kwa kunitag hapa,naomba na mimi nitoe maoni yangu kwa kuhoji kama ifuatavyo
Fikiria Kijiji kina shule mbili za msingi lakini bado shule zimezidiwa na wanafunzi. Hizi shule unakuta shule Ina hadi watoto mia Saba hadi mia tisa.
Mkuu mimi nadhani tatizo sio kwq.ba 2atoto ni wengi hapana,ila tatizo ni kwamba shule chache.

Kwa hiyo tukisema tusolve tatizo maana yake tuongeze shule,na sio tuache kuzaa kwa sababu kuzaa sio tatizo halisi.
Kama hali hii isipodhibitiwa na wizara ya afya basi huko mbeleni kazi ya serikali itakua kujenga madarasa na hospitals
Sasa unatakiwa ujue kwamba ni jukumu la serikali kuweka miundombinu sasa hivi ya madarasa na vituo vya afya kabla ya wakati wa mahitajio ya vitu kufika.

Tunatakiwa tutengeneze miundombinu kabla watumiaji hawajafika,na sio wameshafika ndio unaanza miundombinu.

Hao watoto unaowaona wengi mashuleni ni kwa sababu hawakuandaliwa miundombinu kabla hawajaja,tatizo sio watoto.
Australia nchi yenye maendeleo makubwa Ina watu ambao wahazidi million Saba
China nchi yenye maendeleo makubwa ina watu zaidi ya Bilioni moja pia.

Urusi nchi yenye maendeleo ina watu zaidi ya milioni 145(zaidi ya mara mbili ya idadi ya watz)

Uwingi wa watu sio kikwqzo cha maendeleo,bali usimamiaji na usambazaji wa rasilimali ndio tatizo kubwa,

so tutatue tatizo,tusitatue jambo ambalo sio tatizo,matatizo hayaishi kwa sababu tunatatua mambo ambayo sio tatizo kama umavyotaka kufanya mtoa mada.
 
Ndugu zangu kasi ya Watanzania kuzaliana inatisha Sana. Juzi nilikua wilayani Ukerewe nimeshangaa vijiji vya hii wilaya Yaani Kila Kijiji kina shule za msingi mbilimbili lakini bado hazitoshi

Fikiria Kijiji kina shule mbili za msingi lakini bado shule zimezidiwa na wanafunzi. Hizi shule unakuta shule Ina hadi watoto mia Saba hadi mia tisa.

Nimeitolea Ukerewe kama mfano lakini najua hata sehemu nyinginezo za nchi yetu hali iko hivyo. Kama hali hii isipodhibitiwa na wizara ya afya basi huko mbeleni kazi ya serikali itakua kujenga madarasa na hospitals badala ya kufanya miradi ya maendeleo.

Australia nchi yenye maendeleo makubwa Ina watu ambao wahazidi million Saba Sasa ukija Tanzania Hali inatisha. Uzazi wa mpango utungiwe sheria ili tuweze kuwaletea Wananchi wetu maendeleo maana kasi ya uzazi ni kubwa kuliko ukuaji wa uchumi.

Asanteni.
Unataka tupunguze wapiga kura?
 
Katika watu vilaza unashika namba za juu sana. Hiyo hela ya kujenga madarasa unayoisema kutoka kwa serikali inatoka wapi kama sio population?? Umeshuhudia makato ya tozo kutoka kwenye population ndani ya mwezi tu yanaenda kujenga madarasa 500+ na vutuo vya afya vya kumwaga. Unafikiri mkizaa hao watoto wawili wawili hiyo population ya kutosha kufanya maendeleo mtaiotoa wapi??


Watu ndio mtaji wa kwanza kiuchumi (kama taifa hakitaingiliwa na mataifa makubwa kwa vita, magonjwa ya kutengeneza,n.k). Angalia nchi zote zilizopiga hatua kubwa kiuchumi duniani mfano China, USA, India, Nigeria na nyingine zina watu wengi sana. Wewe unadanganywa na akina Bill Gates ambao wanajua wanachokitafuta wanapokwambia watu wakiwa wengi hali itakuwa mbaya.


Acha upopoma. Mtuache tuzae. Bila kuwa na watu hayo maendeleo ni ya nini??
Mtz ukimwambia uzazi wa mpango ana sala kama mbogo huzani kwamba unamzuia asipige mashine😁
 
Yaani inaonesha bado haujatembea Tanzania nenda machame eneo LA tarafa ya Masama nilitembelea shule za msingi. Na kata idadi ya wanafunzi ni ndogo sana mfano shule ya sekondari sawe form one wako 16 tu shule ya msingi. Nkwakinini shule nzima wanafunzi hawafiki. Mia walimu wanadai watoto hakuna na Hao watu wamejenga shule karibu karibu mfano nilitembea toka shule. Iliyopo kwenye kituo cha afya cha kirani hadi kituo cha. Masama umbali km 2 mbili hapo kàtikati kuna shule za msingi 4 na vituo viwili Vya. Afya na wazazi wana mwamko. Wa nyota ya kijani cha msingi siyo kupunguza kuzaa shule zijengwe. Za. Kutosha aridhi yetu bado kubwa sana
Wale watu hawazaliani kama uyoga na wako vizuri kiuchumi kuanzia family level.

Ktk kusoma kwangu enzi zangu sijawahi kukutana na rafiki anayetoma kanda hizo akaniambia kuwa kwao ni watoto saba au 10. Sana sana utasikia siai kwetu ni watoto 3 wakiwa wengi ni wa nne. Na kila mtoto amesoma vizuri au kaka au Dada ana nyazifa nzuri kielimu na kiuchumi.

Sisi akina kajamba nani ambao wazazi walikuqa kwenye ligi ya kuzaa hata boom tu la chuo ndilo lilikuwa linatumika kusomesha wadogo zetu na kutibia wengine wakiumwa huko vijijini.

Ukishindwa kupangilia Idadi ya familia kuoingana na uwezo wako basi umepanga kuwa maskini maiaha yako yoote.
 
Mwanzo 1:28

"Mungu akawabariki na kuwaambia, “Zaeni muongezeke, mkaijaze nchi na kuimiliki; muwatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kitembeacho duniani.”

Kuzaliana kwa wingi ndiyo mojawapo ya majukumu ambayo mwanadamu alipewa na Muumba wake. Wewe ebu jaribu kuangalia, Yesu akiwa hapa duniani kwa mama yake mzazi Maria alikuwa na wadogo zake wa kiume wanne na wakike pia (maumbu zake).

Tukirejea katika maandiko matakatifu, nukuu kutoka katika vitabu vya injili Mathayo 12:46, Luka 8:19, na Marko 3:31 inathibitisha kwamba Yesu alikuwa na ndugu wanne wa kiume na majina yao ni Yakobo, Yusufu, Simioni na Yuda, ingawaje majina ya dada zake hayakutajwa (Mathayo 13:55).
Watoto wa Adamu walikuwa wangapi? Nuhu? Ibrahimu, Yakobo? vipi watoto wa Isaka? wewe ndio unaelewa sana bibilia kuliko Adamu aliyeambiwa uso kwa uso na Mungu?
 
Kuna mtoto wa jirani anakuja kuchukua ada kwako?

Vipi serikali yenu ya mtaa imepitisha sheria ya mtu mmoja kuruhusiwa kula nyumba yoyote?

Kwani wanaozaa watoto wengi wamelalamika kuwa wanaonewa na Serikali?

Nchi ina rasilimali lukuki, hata Watanzania tungekuwa bilioni moja kama serikali ingeweza kusimamia rasilimali zetu ziwe productive kila familia ingekuwa na maisha bora.

Serikali isikwepe jukumu lake, serikali ndio mmiliki wa kila kitu Tanzania ikiwemo ardhi. Hata leo chini ya kitanda chako ikigundulika dhahabu utatimuliwa kama mbwa ukikataa kutimuliwa kistaarabu.
Rasilimali lukuki na umaskink huu?? Unadhani kisa cha kulalamikia lita ta mafuta 3000 kinatokana na nini?
 
Kuna mtoto wa jirani anakuja kuchukua ada kwako?

Vipi serikali yenu ya mtaa imepitisha sheria ya mtu mmoja kuruhusiwa kula nyumba yoyote?

Kwani wanaozaa watoto wengi wamelalamika kuwa wanaonewa na Serikali?

Nchi ina rasilimali lukuki, hata Watanzania tungekuwa bilioni moja kama serikali ingeweza kusimamia rasilimali zetu ziwe productive kila familia ingekuwa na maisha bora.

Serikali isikwepe jukumu lake, serikali ndio mmiliki wa kila kitu Tanzania ikiwemo ardhi. Hata leo chini ya kitanda chako ikigundulika dhahabu utatimuliwa kama mbwa ukikataa kutimuliwa kistaarabu.
Mkuu serikali inalisha watoto wako?
 
Umesema kweli mkuu,shule nyingi za msingi maeneo ya machame hazina wanafunzi kabisa. Kuna moja darasa la saba walikuwa sita tu.
Unadhani ni kwa sababu wamezalina sana?? Fikiria Machame darasa moja wanafunzi 40. Ukerewe darasa moja wanafunzi 200.

Chagua mwenyewe kuishi kama kilaza au kama mwenye akili.
 
Unadhani ni kwa sababu wamezalina sana?? Fikiria Machame darasa moja wanafunzi 40. Ukerewe darasa moja wanafunzi 200.

Chagua mwenyewe kuishi kama kilaza au kama mwenye akili.
Sasa hivi vilaza wako vijijini na familia zao wanakula vyakula vya asili, wanamiliki rasilimali wakati "wenye" akili wako mtaani wanalialia na ukosefu wa ajira na upungufu wa nguvu za kiume.
 
Hakuna mtu anayasema watu wasizae, hapa jambo linalozungumziwa ni kupunguza idadi ya watoto watu wanaozaa.

Serikali haiwezi tu kuwa ina kazi ya kujenga shule kila siku, sasa hivi kuna shule zaidi ya moja karibia kila kata lakini bado halizitoshi, au unataka kuwepo na shule kila baada ya nyumba kumi? Bado maabara, vituo vya afya, hospitali, barabara, maji, umeme n.k Hospitali zetu kubwa ukifika zina msongamano wa hatari na zinakatisha tamaa kwa wagonjwa.

Tujizuie tuzae watoto wasiozidi wawili ili Tutengeneze kwanza miondombinu na huduma za msingi za kijamii ziwe nzuri kisha tutarudi kufyatua hata 10,Sera ya Uzazi wa mpango wa mtoto 1 ya China miaka ya 1980 hadi 2015 ilikuwa ni ya lazima na ilitekelezwa kikatili sana, sisi serikali sio lazima itumie nguvu na ukatili kuna sera nyingi mbadala inaweza kutumia kufanikisha hilo.

Russia ni nchi mojawapo yenye population ndogo sana, hao watu milioni 150 wanaishi kwenye eneo la km za mraba million 17.
Nikushukuru sana kwa kunitag hapa,naomba na mimi nitoe maoni yangu kwa kuhoji kama ifuatavyo

Mkuu mimi nadhani tatizo sio kwq.ba 2atoto ni wengi hapana,ila tatizo ni kwamba shule chache.

Kwa hiyo tukisema tusolve tatizo maana yake tuongeze shule,na sio tuache kuzaa kwa sababu kuzaa sio tatizo halisi.

Sasa unatakiwa ujue kwamba ni jukumu la serikali kuweka miundombinu sasa hivi ya madarasa na vituo vya afya kabla ya wakati wa mahitajio ya vitu kufika.

Tunatakiwa tutengeneze miundombinu kabla watumiaji hawajafika,na sio wameshafika ndio unaanza miundombinu.

Hao watoto unaowaona wengi mashuleni ni kwa sababu hawakuandaliwa miundombinu kabla hawajaja,tatizo sio watoto.

China nchi yenye maendeleo makubwa ina watu zaidi ya Bilioni moja pia.

Urusi nchi yenye maendeleo ina watu zaidi ya milioni 145(zaidi ya mara mbili ya idadi ya watz)

Uwingi wa watu sio kikwqzo cha maendeleo,bali usimamiaji na usambazaji wa rasilimali ndio tatizo kubwa,

so tutatue tatizo,tusitatue jambo ambalo sio tatizo,matatizo hayaishi kwa sababu tunatatua mambo ambayo sio tatizo kama umavyotaka kufanya mtoa mada.
 
Sasa hivi vilaza wako vijijini na familia zao wanakula vyakula vya asili, wanamiliki rasilimali wakati "wenye" akili wako mtaani wanalialia na ukosefu wa ajira na upungufu wa nguvu za kiume.
😆😆😆😁😁😄😃😃😀
 
Unafahamu watoto wengi wa vijijini ndio wanaongoza kwa udumavu na kwashakoo??
Hizo stories zenu za maisha kijijini ni kama peponi huwa mnazitoa wapi? Nchi hii maisha ni magumu zaidi vijijini kuliko mijini na umaskini mkubwa uko vijijini zaidi.
Sasa hivi vilaza wako vijijini na familia zao wanakula vyakula vya asili, wanamiliki rasilimali wakati "wenye" akili wako mtaani wanalialia na ukosefu wa ajira na upungufu wa nguvu za kiume.
 
Na kulingana na hayo maandiko wakati huo dunia ilikuwa ni hiyo familia moja tu.
Watoto wa Adamu walikuwa wangapi? Nuhu? Ibrahimu, Yakobo? vipi watoto wa Isaka? wewe ndio unaelewa sana bibilia kuliko Adamu aliyeambiwa uso kwa uso na Mungu?
 
[emoji23]
Serikali na asasi za kiraia zinatakiwa zitoe elimu ya uzazi mpango na Serikali iwaondoe hofu watu wa aina hiyo, iwahakikishie wataendelea kupiga mashine vizuri tu.
Mtz ukimwambia uzazi wa mpango ana sala kama mbogo huzani kwamba unamzuia asipige mashine[emoji16]
 
[emoji23]
Serikali na asasi za kiraia zinatakiwa zitoe elimu ya uzazi mpango na Serikali iwaondoe hofu watu wa aina hiyo, iwahakikishie wataendelea kupiga mashine vizuri tu.
😁😁😁mtu maskini ni maskini hadi kwenye ubongo
 
Ninao wanne na bado natamani miaka irudi nyuma ili niongeze watoto
 
Back
Top Bottom