BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 525
- 1,257
Habari, poleni na majukumu ya kazi wana JF na ahsanteni kwa habari nzuri na kutupasha Watanzania na wasio Watanzania.
Nimekuja kwenu tunaomba mtupazie sauti sisi ni wakazi wa Kigogo Mbuyuni, Dar es Salaam, toka upande wa Bonde la Msimbazi.
Huku kwetu kuna Mradi wa Bonde la Mto Msimbazi kwa hiyo kuna baadhi ya nyumba zinatakiwa kuvunjwa kupitisha huo mradi.
Kilio chetu ni kuhusu malipo yaliyotoka ni madogo sana kulingana na thamani ya nyumba zetu.
Kuna nyumba zaidi ya 450, kati ya hizo ambazo zimepangiwa kupata karibia Tsh. Milioni 50 hazifiki nyumba 5, nyingine nyingi ni chini ya hapo, mfano Tsh. Milioni 30, 20, 15 na nyingine hadi Milioni 4.
Mfano kuna vyumba ambazo vyoo waliofanya tathimini wanasema thamani ni Tsh. Laki nne, unaweza kujiuliza choo ambacho kuchimba tu gharama yake ni Ths. Laki mbili then mtu anakwambia thamani ya choo chote ni laki moja.
Siyo kwamba watu hatutaki kuhama lakini thamani ya nyumba zinazotakiwa kubomolewa na thamani ya fedha zinazolipwa ni ndogo, nyumba nyingi thamani iliyotajwa ni Tsh. Milioni 15, hapo ni zile ambazo zina sebule, vyumba vitatu au viwili.
Wanaofanya tathimini walipita hawakusema kuhusu masuala ya fedha, lakini wiki mbili zilizopita tulivyoenda kwenye mkutano mwanzoni mwa mwezi huu Machi 2023 ndio wakaanza kutuambia licha ya kuwa tathimin ilifanyika Mwaka 2022 au 2021 kama sijakosea.
Mbunge wetu Abbas Tarimba alikuja kwenye makazi yetu tukamlalamikia shida zetu na malalamiko yetu, akashauri kuwa tukubali kusaini tu wakati huo yeye anapeleka malalamiko hayo kwa uongozi wa juu Serikalini lakini tunajua hizo ni siasa na kutufanya tutulie.
Asilimia kubwa watu wengi wamesaini nyaraka za kuwa wapo tayari kupokea fedha kwa hofu kwa kuwa wanajua wanaweza kuacha kusaini na wakakosa vyote, nyumba na fedha.
Hivyo, wito wetu kwa Serikali iangalie inawezaje kutusaidia sisi wakati wa Kigogo kwa kuwa hatuna mpango wa kukataa kuhama ila thamani ya nyumba ndio changamoto.
Nimekuja kwenu tunaomba mtupazie sauti sisi ni wakazi wa Kigogo Mbuyuni, Dar es Salaam, toka upande wa Bonde la Msimbazi.
Huku kwetu kuna Mradi wa Bonde la Mto Msimbazi kwa hiyo kuna baadhi ya nyumba zinatakiwa kuvunjwa kupitisha huo mradi.
Kilio chetu ni kuhusu malipo yaliyotoka ni madogo sana kulingana na thamani ya nyumba zetu.
Kuna nyumba zaidi ya 450, kati ya hizo ambazo zimepangiwa kupata karibia Tsh. Milioni 50 hazifiki nyumba 5, nyingine nyingi ni chini ya hapo, mfano Tsh. Milioni 30, 20, 15 na nyingine hadi Milioni 4.
Mfano kuna vyumba ambazo vyoo waliofanya tathimini wanasema thamani ni Tsh. Laki nne, unaweza kujiuliza choo ambacho kuchimba tu gharama yake ni Ths. Laki mbili then mtu anakwambia thamani ya choo chote ni laki moja.
Siyo kwamba watu hatutaki kuhama lakini thamani ya nyumba zinazotakiwa kubomolewa na thamani ya fedha zinazolipwa ni ndogo, nyumba nyingi thamani iliyotajwa ni Tsh. Milioni 15, hapo ni zile ambazo zina sebule, vyumba vitatu au viwili.
Wanaofanya tathimini walipita hawakusema kuhusu masuala ya fedha, lakini wiki mbili zilizopita tulivyoenda kwenye mkutano mwanzoni mwa mwezi huu Machi 2023 ndio wakaanza kutuambia licha ya kuwa tathimin ilifanyika Mwaka 2022 au 2021 kama sijakosea.
Mbunge wetu Abbas Tarimba alikuja kwenye makazi yetu tukamlalamikia shida zetu na malalamiko yetu, akashauri kuwa tukubali kusaini tu wakati huo yeye anapeleka malalamiko hayo kwa uongozi wa juu Serikalini lakini tunajua hizo ni siasa na kutufanya tutulie.
Asilimia kubwa watu wengi wamesaini nyaraka za kuwa wapo tayari kupokea fedha kwa hofu kwa kuwa wanajua wanaweza kuacha kusaini na wakakosa vyote, nyumba na fedha.
Hivyo, wito wetu kwa Serikali iangalie inawezaje kutusaidia sisi wakati wa Kigogo kwa kuwa hatuna mpango wa kukataa kuhama ila thamani ya nyumba ndio changamoto.