Serikali iwajibike kwa Ajali za barabarani zinazomaliza watanzania

Serikali iwajibike kwa Ajali za barabarani zinazomaliza watanzania

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
Matukio ya ajali za barabarani yanaonekana kushamiri maeneo mbalimbali nchini huku watanzania wenzetu wasio na hatia wakipoteza maisha na wengine kubaki na ulemavu wa kudumu.

Hivi ni kweli amekosekana mtu wa kuwajibika kwenye hili la ajali za barabarani?
  • MTWARA watoto wa shule wameoteza maisha
  • Shinyanga
  • Simiyu
  • Morogoro
  • Mbeya
Na maeneo mengine nchini kila siku watanzania wenzetu wanapoteza maisha tatizo liko wapi?
 
Madereva wapo wachache sana Tanzania wengi ni waendesha vyombo vya moto ambao wao wanachojua zaidi wawapo barabarani ni kukanyaga mafuta na kupiga honi nyingi sana !! Mara nyingi hao wanaosababisha hizo ajali ni wenye umri chini ya miaka 40. Hapo ndipo pa kuanzia kufanya uchunguzi wa kina je ni matatizo ya akili au ni nini?
 
Matukio ya ajali za barabarani yanaonekana kushamiri maeneo mbalimbali nchini huku watanzania wenzetu wasio na hatia wakipoteza maisha na wengine kubaki na ulemavu wa kudumu...

Sasa ndugu yangu gari limeferi break Nani anawajibika hapo?

Utaonea watu tu
 
20220801_073423.jpg
 
Wamiliki wa magari wameongezeka na wengi hawana mafunzo ni km tu walivyo boda boda mtu ananunua gar leo wki ijayo dreva tayari na anataka asafiri umbali mrefu na iyo gar

Mafunzo ya udereva yasiyo bora unakuta mwalimu wa udereva hajui sheria za barabarani wala hana daraja la kua mwalimu wa udereva

Upungufu wa asikal barabarani
Rushwa
 
KWENYE HIZI AJALI NIT WANAYO KAZI (ROLE) YA KUFANYA KUSAIDIA KUZIPUNGUZA KUPITIA MAFUNZO WANAYOTOA

Sote tunafahamu kuwa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (National Institute of transport) yaani NIT, ndicho tunaweza kusema Chuo Kikuu pekee cha Madereva nchini Tanzania ambacho kinafundisha wataalamu katika Nyanja ya Usafiri na Mawasiliano katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati. Ni kwa kutambua umuhimu huu, Serikali ikakipa mamlaka Chuo hiki kufundisha madereva wanaotaka kuendesha mabasi ya abiria(PSV) na hata yale ya mizigo, hata hivyo kimekuwa maarufu sana kwa kufundisha madereva wetu.

Bila shaka kabisa ubora wa bidhaa inayotolewa na Chuo hiki lazima itafsirike sio tu kwenye matokeo ya mitihani bali pia matokeo ya kivitendo barabarani. Iwapo tafiti zetu kwa mfano zitasema, ajali nyingi zinatokea barabarani kutokana na makosa ya dereva ambapo inahusisha upungufu wa mafunzo au ujuzi duni basi, bila shaka NIT watahusika kabisaa pamoja na wale watahini wa Polisi (Driver examiners) ambao wao ndio wenye kazi ya kumuaminisha TRA kwamba huyu mwombaji wa Leseni Pingilinene Mfupi, ana sifa na ujuzi unaotakiwa kuendesha gari katika mazingira yote barabarani, hivyo apewe daraja C.

Chuo chetu cha NIT, kwa namna yoyote ile kinahusika katika kuhakikisha usalama barabarani unaimarika. Hakiwezi kujitoa kamwe kwa kusema tu, chenyewe kazi yake ni kufundisha tu, lazima kiende mbele kuhakikisha inatoa mchango katika kupunguza janga la ajali nchini. Kwa nini? Kwa sababu:
1. Chenyewe ndicho kinachofundisha madereva wanaoenda kuendesha magari ya abiria
2. Chenyewe ndicho kinawafundisha wakaguzi wa magari ambao baadae ndio wanakuwa watahini wa madereva (driver examiners) kule Polisi na pia wakaguzi wa magari (vehicle inspectors).

Ina maana Chuo hiki kikimtoa mkaguzi wa magari ambaye hajaiva vizuri, tafsiri yake ni kwamba huyo mkaguzi wa magari anaenda kuruhusu magari mabovu yaendeshwe barabarani, lakini sio hivyo tu, bali pia anaenda kuruhusu madereva wasio na sifa kuingia barabarani. Kwani, kwa mujibu wa sheria, TRA hawezi kumpa mtu leseni kama Mtahini wa madereva hajasema huyu mpe huyu usimpe. Ndio kusema kwamba Polisi wanapolalamika “madereva wa siku hizi wabovu kweli kweli, kimsingi wanakuwa wanajisema wenyewe kwamba sisi tunaowapitisha siku hizi na sisi ni wabovu kweli kweli.

SASA kwa upande wa NIT, mchango wao kwenye kuzuia ajali au kupunguza vifo na majeruhi ukoje? Maswali yafuatayo, yanalenga kuibua mjadala au kufikirisha tu jinsi ambavyo NIT wanaweza kuwa na nafasi katika kuzuia ajali:
1. Je, kwenye hizi ajali zinazotokea wenzetu NIT wanajifunza nini? Je huwa wanaenda kufanya tafiti kuhusu hivi vyanzo na kuona ni namna gani matokeo ya tafiti hizo yatasaidia kuwanoa madereva? Je, wanatumia picha na video za ajali hizo kama mifano ya kufundishia?

2. Je, wenzetu NIT wana jitihada zozote za kuhakikisha wanapata taarifa na kusoma kwa kina aina zote za mabasi au malori yanayoletwa nchini na taratibu za uendeshaji wake, ili dereva anayepita pale kwa kozi ya PSV au HGV aweze sio tu kujua Scania 9XYZ bali ajue pia Zhongtong au Asia Star bus yenye engine ya PXW inaendeshwaje?

3. Je, NIT wamejaribu kutengeneza taratibu mbalimbali za msingi (standard operating procedures) za ukaguzi magari kabla hayajaondoka (pre-departure inspection procedures) ili kuwasaidia madereva au wamiliki kuzitumia, au taratibu mbalimbali za uendeshaji wa magari katika mazingira tofauti tofauti? Mfano, katika mazingira Fulani dereva aendeshaje? Ikipasuka tairi afanyeje nk? Maana vitu vingine tunaambizana mtaani tu.

4. Lakini je, NIT wanafanya tafiti kujua ubora wa madereva wao baada ya kuwa wamehitimu pale? Kwa kufuatilia takwimu za ajali kwa mfano na kufahamu, je madereva wangapi waliopita mikononi mwao walipata ajali na ni ajali za namna gani kwa mwaka au kipindi cha miaka mitatu. ili kusudi wajue wanaboresha nini katika mitaala yao? Na kama zipo je ni nani mlaji wa taarifa hizo? Zinachapishwa wapi? Kama ni kwenye machapisho ya kingereza je, zinatusaidia vipi sisi walaji ambao ni wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili? Maana nchini hapa wengi waliojaliwa hela hawakufanikiwa kwenda vidato sana. Na hata idadi kubwa ya madereva wetu ni shule ya msingi na sekondari zetu za kawaida tu.

5. Je, ni kwa kiasi gani NIT wanatumia uzoefu wa madereva wakongwe katika kufundisha madereva pale ili kupata uzoefu wa barabarani kila siku? Kwa maana ya kuoanisha nadharia na vitendo au uhalisia ulioko barabarani? Je, kwenye kozi za PSV kule NIT madereva wanafundishwa uendeshaji wa usiku? Au wale walimu wao wenyewe washaendesha magari usiku au katika hali tofauti tofauti za hewa na miundo ya barabara?

6. Lakini pia Serikali inakitumiaje Chuo hiki katika kuvikuza na kuvisimamia vyuo vingine vidogo vinavyofundisha udereva wa awali ili kuhakikisha ubora wa madereva hao, ili hata baada ya miaka 3 wakifika huko NIT isiwe kwamba ndio kama wanaanza kujifunza na moja? Labda kwenye hili pia kuna kazi ya kufanya.

7. Je, NIT wanafundisha somo la usalama barabarani au ni ule udereva tu wa kujua kulimudu gari na alama za barabarani? Kwa msingi huo, madereva wetu wanajua dhana nzima ya road safety?

Ndugu zangu, kwa leo tuishie hapa tu kwa haya maswali fikirishi yenye kulenga kuibua mjadala. Karibu wale mliopita katika chuo hicho lakini pia NIT wenyewe tulionao humu.

C&P
Usalama Barabarani ni Jukumu Letu Sote
17/08/2022
 
Matukio ya ajali za barabarani yanaonekana kushamiri maeneo mbalimbali nchini huku watanzania wenzetu wasio na hatia wakipoteza maisha na wengine kubaki na ulemavu wa kudumu.

Hivi ni kweli amekosekana mtu wa kuwajibika kwenye hili la ajali za barabarani?

MTWARA watoto wa shule wameoteza maisha
Shinyanga
Simiyu
Morogoro
Mbeya
Na maeneo mengine nchini kila siku watanzania wenzetu wanapoteza maisha tatizo liko wapi?
Hii nchi haipo serious hata kidogo. Askari wa barabarani ni wala RUSHWA sana
Hili ndio tatizo hapo
 
Matukio ya ajali za barabarani yanaonekana kushamiri maeneo mbalimbali nchini huku watanzania wenzetu wasio na hatia wakipoteza maisha na wengine kubaki na ulemavu wa kudumu.

Hivi ni kweli amekosekana mtu wa kuwajibika kwenye hili la ajali za barabarani?

MTWARA watoto wa shule wameoteza maisha
Shinyanga
Simiyu
Morogoro
Mbeya
Na maeneo mengine nchini kila siku watanzania wenzetu wanapoteza maisha tatizo liko wapi?
Tukiacha wataalam wafanye kazi zao pasipo kuingiliwa na wanasiasa suluhisho la ajali lipo
Mfano
Uwepo wa sheria na adhabu kali kwa wakiukaji wa sheria za usalama barabarani
Kuacha kuuza leseni za udereva kama njugu badala madereva wetu kosomea taaaluma za udereva
Uwepo wa mifumo thabiti ya kiudhibiti kwenye magari yetu kama vile gavana na VTS
Maboresho ya miundo mbinu ya barabara
Uwepo wa sera madhubuti zilizojengewa sheria na kanuni sahihi
Usimamizi wa uingizwaji nchini magari bora salama na madhubuti
Kuwa wakali sana kwenye RUSHWA narudia tena kuwa wakali sana kwenye RUSHWA
YAPO MENGI LAKINI NIISHIE HAPO
 
miundombinu haiendani na wingi wa magari. bila kusahau udereva wa kujifunzia viwanja vya shule.
 
Tukiacha wataalam wafanye kazi zao pasipo kuingiliwa na wanasiasa suluhisho la ajali lipo
Mfano
Uwepo wa sheria na adhabu kali kwa wakiukaji wa sheria za usalama barabarani
Kuacha kuuza leseni za udereva kama njugu badala madereva wetu kosomea taaaluma za udereva
Uwepo wa mifumo thabiti ya kiudhibiti kwenye magari yetu kama vile gavana na VTS
Maboresho ya miundo mbinu ya barabara
Uwepo wa sera madhubuti zilizojengewa sheria na kanuni sahihi
Usimamizi wa uingizwaji nchini magari bora salama na madhubuti
Kuwa wakali sana kwenye RUSHWA narudia tena kuwa wakali sana kwenye RUSHWA
YAPO MENGI LAKINI NIISHIE HAPO
Haya yanawezakana kwa Jamii iliyo civilized.Nje ya hapo sheria ni fursa kwa wasimamizi wa Sheria.
Speed gavana ni ngumu ilifeli hii,mafundi walicheza na adjustment ya pedal ya accelerator. Bora wajaze askari barabarani KILA baada ya kilometa Ili ukijifanya kichwa ngumu unazo pesa tuone kama utaweza honga wote toka dar hadi mwanza na hata ukihonga jumla pesa yote bora upande ndege.
 
Dereva wa TANZANIA ni SAwa SAwa na mbuzi bila kuwachungwa ni lazima mazao. Angalia tu rafu za daladala na bodaboda mijini. KILA mmoja anataka awahi kisha wanaenda mbele kujiblock
 
Back
Top Bottom