Serikali kama imeshindwa kutengeneza ajira kwa vijana, ijiandae kujenga magereza mengi

Serikali kama imeshindwa kutengeneza ajira kwa vijana, ijiandae kujenga magereza mengi

Kiukweli vijana wanapitia changamoto nyingi sana mpaka huruma.
Nikikumbuka niliyopitia mimi ndani ya miaka sita bila ajira da mwingine hawezi.
Nimefanya vitu vingi nimelima ,nimekata mkaa, nimeuza dagaa ,nimesaidia fundi, nimeuza vyuma yaani naokota mtaani naenda kuuza.,nimetembeza njegere dar kwa kichwa, nimeuza ndizi natoa mabibo nakuja kuuza mbagara nadhani kuna baadhi humu wanaweza kunifahamu.

Hasa wale wanaoishi kongowe ya kuelekea vikindu,mbagala kibondemaji huko nimeuza sana ndizi mbichi natembeza kichwani, mitaa ya kurasini mji mpya kwa tesha, kiburugwa na mitaa mingi tu hapo dar.

Ila nimechojifunza vijana tusichague kazi na wala tusikate tamaa. Ipo siku mungu atawakumbuka.
Amen
 
Inawezekana changamoto kubwa ya umasikini inaanzia kwa wazazi. Wanamuandaaje kina na wao
Ndiyo, wazazi wengi wanafanya kazi kwaajili ya pesa hawana ujuzi wa kufanya pesa iwafanyie wao kazi yaani jinsi ya kutumia pesa kuzalisha pesa laiti wangekuwa na ujuzi huu umasikini ungepungua.
 
Life doesn't follow the blueprint of a syllabus.

If one does not know to which port one is sailing, no wind is favorable.

Maisha yamebadilisha kitasa, Elimu sio ufunguo tena.
Mbaya zaidi kuna kundi linaamini bila kufanya kazi haramu hutoboi, wengine wanaamini bila ushirikina hutoboi. Hali ni mbaya sana mitaani
 
Unakuta kijana ana miaka 30+, ametumia miaka 28 au zaidi shuleni hadi kuhitimu shahada yake ya udaktari.

Anarudi nyumbani bila ajira. Hana mtaji na hana ujuzi zaidi ya alichosomea. Wazazi nao hawakuwa na ajira rasmi, walikuwa wanaungaunga tu ili mtoto wao apate elimu aje kuwaokoa. Kijana anaamka anakuta baba na mama hawana nguvu tena ya kumsapoti na yeye hana nguvu ya kuwasapoti. Kila akiwaangalia wazazi anapata stress.

Kijana huyo akienda kwenye vibarua vya kusaidia mafundi anaonekana hajui lolote hivyo watu wanamkwepa.

Akisema aende mjini kama kariakoo, kutafuta cha kufanya. Anaishia kuzurula na anakosa hata 500 ya maji. Anaishia kutamani hata kuomba maji kwa mtu.

Hawezi kuuza simu ili aanze biashara maana kwenye simu ndipo ajira zinatangazwa. Na kuna muda anapitwa na fursa kwasababu ya kukosa bando.

Siku akipata elfu 1 yake anunue kifurushi, anakutana na kelele za motivational speaker wakimwambia kuwa kukaa kutegemea ajira ni uzembe. Utakufa masikini.
Anazidi kuchanganyikiwa.

Kijana huyu alikuwa na girlfriend wake, lakini ameachwa kwasababu future yake haionekani. Kijana huyu anahisia na mwili wake pia kuna muda unahitaji tendo la ndoa. Pesa ya kununua dada poa haipo, pesa ya kumpeleka mdada lodge haipo.Anaishia kujichua.

Akiangalia waliofeli darasa la saba, wapo mtaani na viduku na vidread kichwani wanaendesha bodaboda zao kwa furaha na kutamba elimu sio kitu.

Ndugu yangu; Ukipata nafasi ya kumshika kijana mmoja mkono na kumuinua juu, usisite. Vijana tunapitia mengi. Mungu atakulipa.

Kuna vijana wengi wasomi ila watoto wao hawatakwenda shule. Hawaamini tena kwenye elimu, kwa uelekeo wa vijana wasomi wanavyoongezeka na kuaminishwa kwenye kazi za ujanja ujanja taifa litaanza kujenga magereza mengi sana siku zijazo.
Aisee! Umeandika kweli ila kwa machungu mno. Pole broo.
Ninawaangalia vijana wengi hata siwaelewi.
Hivi kweli vijana wanaijua hali yao ilivyo na mustakabali wa maisha yao ya sasa na baadaye? Mbona wamekaza fuvu e.g. wanaambiwa Ajira hakuna mjiajiri wenyewe, lakini bado wanalilia ajira.
1. Vijana wanadanganyana eti mjini ndo mambo yote. Sasa hapo mjini mmefungiwa hapo hamwezi kutoka? Nendeni huko vijijini makajaribu kujitafuta huko.
2. Vijana mliosoma na kufuzu vizuri na cheti mkapata. It is OK. Lakini wakati unasubiri labda fursa itapatikana, jaribuni fursa nyingine. Zipo fursa za kukopa. Sio lazima ukakope pesa-Hapana. Kopa vitu Physical e.g. unaweza kujaribu "Kauli mali" au kukopa shamba kwa muda n.k. Shida ya vijana hapa ni uvivu, uoga na ule uthubutu wa kujaribu. Huku vijijini fursa ni nyingi lakini vijana waliosoma wanajisemea "Why should I go to venture in those dubious activities with my degree? A graduate can't engage in indigenous chicken production......... or tilling the land......... they are selective." Kwa hiyo kaeni na Kiingereza chenu halafu kitaeleweka.
 
Shida mfumo wetu wa elimu unamuandaa mtu kwaajili ya kuajiriwa wanafunzi wengi wanawaza "nitasoma kwa bidii then nitapa ajira nzuri alaf nitajenga nyumba ya kuishi na kununua gari" hawawazi nje ya hapo. Mzazi kaa na mwanao umuelekeze jinsi maisha yalivyo hakikisha unaondoa mindset yake ya kuajiriwa.
soma comment #26 badili mtazamo wako.

Acha kulialia dunia hii hakuna wa kukuonea huruma.

Acha kuwasikiliza wanasiasa maisha ni vile unayaendea🤝
 
Aisee! Umeandika kweli ila kwa machungu mno. Pole broo.
Ninawaangalia vijana wengi hata siwaelewi.
Hivi kweli vijana wanaijua hali yao ilivyo na mustakabali wa maisha yao ya sasa na baadaye? Mbona wamekaza fuvu e.g. wanaambiwa Ajira hakuna mjiajiri wenyewe, lakini bado wanalilia ajira.
1. Vijana wanadanganyana eti mjini ndo mambo yote. Sasa hapo mjini mmefungiwa hapo hamwezi kutoka? Nendeni huko vijijini makajaribu kujitafuta huko.
2. Vijana mliosoma na kufuzu vizuri na cheti mkapata. It is OK. Lakini wakati unasubiri labda fursa itapatikana, jaribuni fursa nyingine. Zipo fursa za kukopa. Sio lazima ukakope pesa-Hapana. Kopa vitu Physical e.g. unaweza kujaribu "Kauli mali" au kukopa shamba kwa muda n.k. Shida ya vijana hapa ni uvivu, uoga na ule uthubutu wa kujaribu. Huku vijijini fursa ni nyingi lakini vijana waliosoma wanajisemea "Why should I go to venture in those dubious activities with my degree? A graduate can't engage in indigenous chicken production......... or tilling the land......... they are selective." Kwa hiyo kaeni na Kiingereza chenu halafu kitaeleweka.
Mikopo haitakufikisha mahali sanasana itakufilisi,tafuta ujuzi hakuna mtu mwenye ujuzi analia njaa.

Soma post #26 hujachelewa chukua hatua.

#kupanga ni kuchagua.
 
Bro maisha ni mapambano sasa vijana wa leo wakiona mtu yupo kwenye kazi ana drive wanadhani maish ni lelemama .mimi niliweka digrii pembeni nikaingia mtaani.


Leohii mtu akiniona anahisi sijapitia mambo magumu kiss mwili soft na kakitambi kadogo.

Takuja kuandika historia yangu humu ilikuwafundisha vijana maisha yalivyo na wajue kuwa na digrii suo kufanikiwa kimaisha
mi niliingia migodini huko kuchimba, nilisahau mengine kwanza, ikawa ni kukomaa kusaka mtaji,....... maisha hakika ni safari ndefu🙏🙏
 
Unakuta kijana ana miaka 30+, ametumia miaka 28 au zaidi shuleni hadi kuhitimu shahada yake ya udaktari.

Anarudi nyumbani bila ajira. Hana mtaji na hana ujuzi zaidi ya alichosomea. Wazazi nao hawakuwa na ajira rasmi, walikuwa wanaungaunga tu ili mtoto wao apate elimu aje kuwaokoa. Kijana anaamka anakuta baba na mama hawana nguvu tena ya kumsapoti na yeye hana nguvu ya kuwasapoti. Kila akiwaangalia wazazi anapata stress.

Kijana huyo akienda kwenye vibarua vya kusaidia mafundi anaonekana hajui lolote hivyo watu wanamkwepa.

Akisema aende mjini kama kariakoo, kutafuta cha kufanya. Anaishia kuzurula na anakosa hata 500 ya maji. Anaishia kutamani hata kuomba maji kwa mtu.

Hawezi kuuza simu ili aanze biashara maana kwenye simu ndipo ajira zinatangazwa. Na kuna muda anapitwa na fursa kwasababu ya kukosa bando.

Siku akipata elfu 1 yake anunue kifurushi, anakutana na kelele za motivational speaker wakimwambia kuwa kukaa kutegemea ajira ni uzembe. Utakufa masikini.
Anazidi kuchanganyikiwa.

Kijana huyu alikuwa na girlfriend wake, lakini ameachwa kwasababu future yake haionekani. Kijana huyu anahisia na mwili wake pia kuna muda unahitaji tendo la ndoa. Pesa ya kununua dada poa haipo, pesa ya kumpeleka mdada lodge haipo.Anaishia kujichua.

Akiangalia waliofeli darasa la saba, wapo mtaani na viduku na vidread kichwani wanaendesha bodaboda zao kwa furaha na kutamba elimu sio kitu.

Ndugu yangu; Ukipata nafasi ya kumshika kijana mmoja mkono na kumuinua juu, usisite. Vijana tunapitia mengi. Mungu atakulipa.

Kuna vijana wengi wasomi ila watoto wao hawatakwenda shule. Hawaamini tena kwenye elimu, kwa uelekeo wa vijana wasomi wanavyoongezeka na kuaminishwa kwenye kazi za ujanja ujanja taifa litaanza kujenga magereza mengi sana siku zijazo.
Kwanza hakuna serikali inayo weza kuajili wananchi wake wote lakini lingine watanzania tujitahidi kuwa waaminifu tukiajiriwa ,nimesikiliza clip moja ya muwekeza aliye ajiri vijana kwenye mashamba yake matokeo yake vijana wanatumia matrekta yake kufanya kazi za nje kwa wizi hadi yameharika, sasa nani atawaajiri nyie kwa tabia za wizi hizi?
 
soma comment #26 badili mtazamo wako.

Acha kulialia dunia hii hakuna wa kukuonea huruma.

Acha kuwasikiliza wanasiasa maisha ni vile unayaendea🤝
Sawa vijana wanatakiwa kuongeza ujuzi ila ukikosa ujuzi kuhusu fedha na jinsi gani utaitumia kuongeza pesa hata kama umesoma veta na macourse mengine bado utaona maisha magumu.
 
Sawa vijana wanatakiwa kuongeza ujuzi ila ukikosa ujuzi kuhusu fedha na jinsi gani utaitumia kuongeza pesa hata kama umesoma veta na macourse mengine bado utaona maisha magumu.
Endelea kujiliza hapo subiri wanasisa waje kukufariji, yaani kijana mzima unataka ufundishwe budgeting na how to maximize profit hivi huko shule mlienda kukariri ujinga😀😀😀

Sasa kama application ya hesabu zile za form 4 au lasaba hauwezi maana mimi nakumbuka form 4 enzi zetu tulifundishwa hesabu ambazo ndo nazitumia mpaka leo maishani. Pia darasa la saba mwalimu wangu wa hesabu alikuwa anasistiza ni bora mtu ujue hesabu utakuwa hata Kondakta akimaanisha ukiijua hesabu wewe pesa haitakusumbua.

Vijana wa leo bure kabisa!! mmebemendwa nadhani, yaani mmelelewa kimayaimayai hambebeki😬😬😬

#Kijana endelea kusubiri embe chini ya mnazi!!!!
 
Watu wasiolia njaa ni wale wenye ujuzi wa kufanya pesa izalishe pesa nyingine vingine ni vya ziada.
Wewe ni muumini wa miujiza,hauna imani kuwa mafanikio ni mchakato.

Nakushauri ungana na matahira wale wa KAWE ukapakwe mafuta ya bukubuku huwenda ndoto zako zikatimia.

#kupanga ni kuchagua!!!
 
SHTUKENI ACHENI KUWATAJIRISHA WENYE MASHULE YA ENGLISH MEDIUM,PELEKENI WATOTO VETA,MTAOKOA MUDA,PESA NA KUPUNGUZA MALALAMIKO.

TATIZO WATANZANIA WENGI WANAISHI KWA KUIGANA(FASHION LIFESTLE)KITAWARAMBA SANA!!!!😄😄😄 MNAONA UFAHARI KWENDA KUTUPA MAMILIONI HUKO ENGLISH MEDIUM.

MTOTO ANAMALIZA SHULE KITU PEKEE ANARUDI NACHO NYUMBANI NI BROCKEN ENGLISH🤣🤣🤣 NA KARATASI( CHETI) AMBACHO KWA MUDA HUU HAKITAMSAIDIA CHOCHOTE.MAANA HANA EXPERIENCE WALA SKILLS ZOZOTE NA MTAANI WENYE ELIMU WAPO WENGI NA WANAAJIRIWA KWA UJIRA WA NYANYA😄😄😄.

KUNIELEWA ZAIDI PITIA COMMENT YANGU #26

#LEARN OR PERISH!!!!
ENglish muhimu mkuu. Huoni watu wanavyoangaika kwenye interview au kupata connection ya kufanya kazi na wazungu. Ata kupata fursa nje ya nchi kuzamia marekani, Uarabuni bila kiingereza maisha ni magumu. Bila hiyo lugha ujasiri wa kutoka nje ya mpka kutafta fursa unaupata wap. Tuulize sisi tuliozamia Sauzi enzi za kikwete ujue umuhimu wa hiyo lugha
 
Endelea kujiliza hapo subiri wanasisa waje kukufariji, yaani kijana mzima unataka ufundishwe budgeting hivi huko shule mlienda kukariri ujinga😀😀😀

Sasa kama application ya hesabu zile za form 4 au lasaba hauwezi maana mimi nakumbuka form 4 enzi zetu tulifundishwa hesabu ambazo ndo nazitumia mpaka leo maishani. Pia darasa la saba mwalimu wangu wa hesabu alikuwa anasistiza ni bora mtu ujue hesabu utakuwa hata Kondakta akimaanisha ukiijua hesabu wewe pesa haitakusumbua.

Vijana wa leo bure kabisa!! mmebemendwa nadhani, yaani mmelelewa kimayaimayai hambebeki😬😬😬

#Kijana endelea kusubiri embe chini ya mnazi!!!!
Mkuu ujuzi wa kufanya pesa ikufanyie kazi haina uhusiano wowote na hisabati. Na ni wachache sana wana ujuzi huu kwakuwa haufundishwi mashuleni na pia ujuzi huu unamfanya mtu aingize pesa bila kujichosha.

Make money work for you.
Soma kitabu cha the RICHEST MAN IN BABYLON utanielewa.
 
Unakuta kijana ana miaka 30+, ametumia miaka 28 au zaidi shuleni hadi kuhitimu shahada yake ya udaktari.

Anarudi nyumbani bila ajira. Hana mtaji na hana ujuzi zaidi ya alichosomea. Wazazi nao hawakuwa na ajira rasmi, walikuwa wanaungaunga tu ili mtoto wao apate elimu aje kuwaokoa. Kijana anaamka anakuta baba na mama hawana nguvu tena ya kumsapoti na yeye hana nguvu ya kuwasapoti. Kila akiwaangalia wazazi anapata stress.

Kijana huyo akienda kwenye vibarua vya kusaidia mafundi anaonekana hajui lolote hivyo watu wanamkwepa.

Akisema aende mjini kama kariakoo, kutafuta cha kufanya. Anaishia kuzurula na anakosa hata 500 ya maji. Anaishia kutamani hata kuomba maji kwa mtu.

Hawezi kuuza simu ili aanze biashara maana kwenye simu ndipo ajira zinatangazwa. Na kuna muda anapitwa na fursa kwasababu ya kukosa bando.

Siku akipata elfu 1 yake anunue kifurushi, anakutana na kelele za motivational speaker wakimwambia kuwa kukaa kutegemea ajira ni uzembe. Utakufa masikini.
Anazidi kuchanganyikiwa.

Kijana huyu alikuwa na girlfriend wake, lakini ameachwa kwasababu future yake haionekani. Kijana huyu anahisia na mwili wake pia kuna muda unahitaji tendo la ndoa. Pesa ya kununua dada poa haipo, pesa ya kumpeleka mdada lodge haipo.Anaishia kujichua.

Akiangalia waliofeli darasa la saba, wapo mtaani na viduku na vidread kichwani wanaendesha bodaboda zao kwa furaha na kutamba elimu sio kitu.

Ndugu yangu; Ukipata nafasi ya kumshika kijana mmoja mkono na kumuinua juu, usisite. Vijana tunapitia mengi. Mungu atakulipa.

Kuna vijana wengi wasomi ila watoto wao hawatakwenda shule. Hawaamini tena kwenye elimu, kwa uelekeo wa vijana wasomi wanavyoongezeka na kuaminishwa kwenye kazi za ujanja ujanja taifa litaanza kujenga magereza mengi sana siku zijazo.
Washa ibadilisha Betting kama Proffession utawaambia nn
 
Kwanza hakuna serikali inayo weza kuajili wananchi wake wote lakini lingine watanzania tujitahidi kuwa waaminifu tukiajiriwa ,nimesikiliza clip moja ya muwekeza aliye ajiri vijana kwenye mashamba yake matokeo yake vijana wanatumia matrekta yake kufanya kazi za nje kwa wizi hadi yameharika, sasa nani atawaajiri nyie kwa tabia za wizi hizi?
Hao mnaita wawekezaji ni makanjanja,mtu anaanzisha mradi anaajiri watu wa hovyohovyo ili awalipe kidogo.Hakuna upuuzi kama huo ajiri watu serious wenye ujuzi husika pia walipe vizuri weka management uone kama ptoject yako haitaenda vizuri.

Ila unaokoteza huko warugaruga unawafanya mashamba boy wako lazima kikurambe tu😄😄😄.

Mafanikio ni mchakato,hakuna shortcut kwenye maisha. Bisha kikurambe!!!

#kupanga ni kuchagua!!!!
 
Back
Top Bottom