Serikali kuja na mradi wa Dola bilioni 1.9 kutatua tatizo Umeme

Waziri Makamba amesema wanakuja na mradi wa Dola billioni 1.9 kutatua tatizo.

Nauliza huu mradi ameukuta ofisini au umebuniwa ndani ya hii miezi yake 4.

Kama hajaukuta umepitishwa na bajeti ipi?
Ukwel Ni huu jm amechoka kabisa, kunasiku atatuambia anakuja na umeme wa hewa hyu...
 
Magufuli alipoutupilia mbali mradi wa gesi uliitisha kumkataaa??.
Magufuli alitoa sababu,kuwa gesi pamoja na kuwa yetu tunainunua kwa bei kubwa Maana iliisha uzwa zamani, Ndio Maana kaamua kuanzisha mradi mwingine wa kutupatia umeme wa kutosha tena kwa bei nafuu.Sasa hawa majambazi wanaturudisha kule tulikokuwa tuna pakimbia.Mungu atawapiga raana tu acha watuibie tu.
 
Acha waibe ila tuishi kwa uhuru, tumeishi miaka 5 ya mateso huku tunaibiwa na kupigwa juu. Bora waibe sisi tuishi maisha ya amani, haya wanayoiba hawaendi nayo peponi.
 
Waziri Makamba amesema wanakuja na mradi wa Dola billioni 1.9 kutatua tatizo.

Nauliza huu mradi ameukuta ofisini au umebuniwa ndani ya hii miezi yake 4.

Kama hajaukuta umepitishwa na bajeti ipi?
Shida yako wewe ni nini hasa? Unachotaka mradi utatue changamoto au Una nongwa zako?
 
Kwani kuna tatizo la umeme?

Si kasema jana tu kuwa hii katakata ni "service" tu ambayo haikuwahi kufanyika kwa miaka mitano.

Nadhani hii wizara inahitaji mtu serious siyo watu wa porojo sampuli ya Makamba.
 
Shida hawataki kuukamilisha kwa kuwa ulianza kutekelezwa na Magufuli.
 
Waziri Makamba amesema wanakuja na mradi wa Dola billioni 1.9 kutatua tatizo.

Nauliza huu mradi ameukuta ofisini au umebuniwa ndani ya hii miezi yake 4.

Kama hajaukuta umepitishwa na bajeti ipi?
Si umesema mwenyewe "...serikali kuja na mpango wa $1.9bn kutatua tatizo la umeme...?"

Sasa swali la "...kwa bajeti ipi..." linaingiaje ingiaje hapo?

Maana hiyo ni "future tense". Inawezekana ukawa mpango wa mwaka kesho au mwaka kesho kutwa...

Usipende kutanguliza toroli mbele punda au farasi....!!
 
Huyu kijana wamtoe Kalemani arudi au.Muhongo au hata Lukuvi
Huyu ni famba, bure kabisaa
Sukuma gang wanahangaika kuonyesha Kalemani alifanya kazi, alikuwa anafanya utapeli tu na hatarudi, hata uzalishe umeme kiasi gani, kama hauna miundombinu ya kuufikisha kwa wateja ni kazi bure, kwa Sasa lazima kazi maalum ifanyike kulifuta kundi la sukuma gang na mawakala wake, nashauri Idara za usalama zijipe miaka kumi au ishirini kufuta kabisa kundi hili linalohatarisha usalama wa nchi na utangamano. Dola haijawahi kushindwa na itawadhibiti na kuwafuta wote
 
Unaanza mpango Kisha utekelezaji, akili za michembe zitakufikisha wapi
 
Waziri Makamba amesema wanakuja na mradi wa Dola billioni 1.9 kutatua tatizo.

Nauliza huu mradi ameukuta ofisini au umebuniwa ndani ya hii miezi yake 4.

Kama hajaukuta umepitishwa na bajeti ipi?
Tanesco inauhab wa nishati yeye anataka mijizija huko ni kutawanya pesa za shiriki ili wakusanya mabilioni ya shilingi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jiwe aliipekelesha Tanesco kama tawi la CCM..sasa matokeo yake ni haya.

Tutaambiwa mengi...nasubiri tuambiwe wananchi tukajaze maji kwenye vyanzo vya maji kwa ndoo kichwani ili umeme upatikane.

Matatizo mengi ya nchi hii yanaletwa na sisi wenyewe., haiwezekani miaka 60 ya uhuru - maji ni 30% nchi nzima, umeme 40%, elimu 20%, kilimo 5%, viwanda 20%

Hivi sisi tupo serious kweli ??? Tunajua tunapotaka kwenda ?
 
Ondoa huyu Jamaa haraka..., naona sasa sio kutukosesha tu umeme bali kutoboa mifuko yetu....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…