Serikali kuondoa udhibiti wa sukari kutoka nje kisheria. Bashe adai anaenda kuwatikisa 'Big Boys'

Serikali kuondoa udhibiti wa sukari kutoka nje kisheria. Bashe adai anaenda kuwatikisa 'Big Boys'

Wakafie mbele huko. Kama ni syndicate ya kututesa wananchi kwa kulangua sukari acha ife tu. Tunduma sukari ni 2500/- lakini ukifika Mbeya mjini ni 4800. Kwa nini watu wateseke? Wafungue mipaka sukari ya Zambia na Malawi ije kwa wingi bei zishuke.
Ina maana Malawi na Zambia hakuna mvua?
 
Inafikirisha sana Waziri wa Kilimo anaapa kabisa lazima aiue sekta Fulani ya Kilimo?
Huyu waziri inabidi afutwe kazi ameshindwa kudeal na chanzo cha tatizo la kupanda.bei ya sukari
Si kwamba waziri anataka kuiua sekta fulani.

Waziri anawaambia watu wa kwenye hiyo sekta waache kupenda kubebwa na protectionism, ni muda kwa kushindana na bei ya sukari kutoka nje.

Waliosoma uchumi wanajua kitu kinaitwa "competitive advantage".

Anachosema Bashe ni kwamba, kama Tanzania hatuna competitive advantage katika sukari, sukari yetu ina gharama ya juu zaidi kuizalisha, tuseme labda tunazalisha kilo moja kwa shilingi 6,000, wakati wenzetu wanaweza kuzalisha kilo hiyo kwa shilingi 3,000, hapo labda inawezekana ikawa busara kuacha kuzalisha sukari, tuagize ya nje, na hiyo ardhi ya kulima sukari tulime mpunga.

Hapo hatuna "competitive advantage" katika kutengeneza sukari.

Kauli hii pia inaweza kuwa silaha ya kisiasa, kwa mfano, ikiwa waziri anajua kuwa wafanyabiashara wa sukari wanapandisha bei kwa hila, na wanaweza kabisa kupunguza bei ikawa sawa na ile ya sukari kutoka nje ya shilingi 3,000 , kwa kupunguza gharama za uzalishaji na kuondoa upandishaji bei wa kiholela wa kutafuta faida tu, kauli hii inaweza kutumika kulazimisha wadau wa sekta ya sukari kupunguza bei.

Bei ya sukari Tanzania haipo juu naturally, ipo juu artificially. Ndiyo maana sukari ya nchi jirani kama Malawi bei yake iko chini zaidi.

Serikali inafanya kitu sahihi kuruhusu sukari ya nje ije kushindana na ya ndani kwenye soko.

Hili jambo lilitakiwa kufanyika zamani sana. Naona kama wamechelewa.
 
Kwani waziri wa Viwanda na Biashara anasemaje?

Yawezekana Tatizo ni kubwa zaidi🐼

Hoarding ni sabotage kwny uchumi.
Nchi nyingi duniani swala hilo ni sawa na uhujumu uchumi.

Wanacho kifanya hao wenye viwanda ni kupunguza uzalishaji, ama ku'store mzigo ghalani au vyote ili kutengeneza artificial scarcity kwa ajili ya kupandisha bei.

Mawili, la kwanza tokeni hapo kwny dawati lenu muache kwanza kazi ya kuwachamba wapinzani mwende kuwa expose wafanya biashara wanaoficha sukar pamoja na viwanda.

La pili, serikali iruhusu uingizaji wa sukari nchini bila kibali kwa hati ya dharura hadi wenye viwanda watoke mafichoni na kusema watashushaje bei ili ilingane na nchi zingine majirani, Maana sijui kwann Tanznia bara tu ndiyo sukar aghali lakn zenj, nchi jirani zote sukari bei ni ndogo.
 
Chain ya sukari imebeba watu wengi ikiwemo wasio na makosa. Bashe hawezi kuharibu maisha yao kisa Serikali kushindwa kutimiza wajibu wao wa kudhibiti bei. Anajigamba kabisa mwaka mmoja mashamba yote yatakufa, hamna mtu hapo..
Yaan kazingua, tuwe tegemezi nje hata Kwa sukari? Siku wakiamua hao wa nje hatutoi sukari tunywe chai bila sukari?

Binafsi naona kazingua. Serikali ingejikita katika viwanda vyake na mashamba kama JPM alivyoanza na kiwandà Cha Mkulazi ambapo wao saiz baada ya kufa mwamba wanatafuta mbia, muwekezaji.
 
Si kwamba waziri anataka kuiua sekta fulani.

Waziri anawaambia watu wa kwenye hiyo sekta waache kupenda kubebwa na protectionism, ni muda kwa kushindana na bei ya sukari kutoka nje.

Waliosoma uchumi wanajua kitu kinaitwa "competitive advantage".

Anachosema Bashe ni kwamba, kama Tanzania hatuna competitive advantage katika sukari, sukari yetu ina gharama ya juu zaidi kuizalisha, tuseme labda tunazalisha kilo moja kwa shilingi 6,000, wakati wenzetu wanaweza kuzalisha kilo hiyo kwa shilingi 3,000, hapo labda inawezekana ikawa busara kuacha kuzalisha sukari, tuagize ya nje, na hiyo ardhi ya kulima sukari tulime mpunga.

Hapo hatuna "competitive advantage" katika kutengeneza sukari.

Kauli hii pia inaweza kuwa silaha ya kisiasa, kwa mfano, ikiwa waziri anajua kuwa wafanyabiashara wa sukari wanapandisha bei kwa hila, na wanaweza kabisa kupunguza bei ikawa sawa na ile ya sukari kutoka nje ya shilingi 3,000 , kwa kupunguza gharama za uzalishaji na kuondoa upandishaji bei wa kiholela wa kutafuta faida tu, kauli hii inaweza kutumika kulazimisha wadau wa sekta ya sukari kupunguza bei.

Bei ya sukari Tanzania haipo juu naturally, ipo juu artificially. Ndiyo maana sukari ya nchi jirani kama Malawi bei yake iko chini zaidi.

Serikali inafanya kitu sahihi kuruhusu sukari ya nje ije kushindana na ya ndani kwenye soko.

Hili jambo lilitakiwa kufanyika zamani sana. Naona kama wamechelewa.

Mawaziri na mamlaka husika zinajua hatua ya kuchukua, nnacho ona ni kuwa wanaweza wawe kwny malipo kutoka kwa wenye viwanda.
 
Always talking the Talk... lakini sishangai huwezi ku-walk the walk kama hatuna Dira....
 
Bashe hawezi kupambana na hawa jamaa hiyo cartels kubwa yenye mapapa
Anaweza akang’ooka yeye !
Jamaa mmoja aliongea kwenye Radio moja kwenye malumbano ya hoja kwamba hao ma-cartels wa Sukari ni kama wa Ngada ! So powerful !
 
Chain ya sukari imebeba watu wengi ikiwemo wasio na makosa. Bashe hawezi kuharibu maisha yao kisa Serikali kushindwa kutimiza wajibu wao wa kudhibiti bei. Anajigamba kabisa mwaka mmoja mashamba yote yatakufa, hamna mtu hapo..
Akifanya atakua kafanya Jambo zuri,uhuru wa manyani
 
Mawaziri na mamlaka husika zinajua hatua ya kuchukua, nnacho ona ni kuwa wanaweza wawe kwny malipo kutoka kwa wenye viwanda.
Kwa Bashe anachofanya ni tofauti na anachotakiwa kufanya mtu aliye kwenye malipo kutoka kwa wenye viwanda.

Kwa sababu Bashe anataka kufungua soko zaidi ili wenye viwanda wapate ushindani zaidi kutoka sukari ya nje.
 
Anaweza akang’ooka yeye !
Jamaa mmoja aliongea kwenye Radio moja kwenye malumbano ya hoja kwamba hao ma-cartels wa Sukari ni kama wa Ngada ! So powerful !
Hili linawezekana,KAGERA sugar,kilombero, bakhressa nk.. powerful
 
Kwa Bashe anachofanya ni tofauti na anachotakiwa kufanya mtu aliye kwenye malipo kutoka kwa wenye viwanda.

Kwa sababu Bashe anataka kufungua soko zaidi ili wenye viwanda wapate ushindani zaidi kutoka sukari ya nje.

Kwahiyo anasema hadharani hayo ili kuwatisha wenye viwanda ili wamwone au waongeze dau, kwa maana ya kwann asichukue hatua at first place ili wakilalamika yy ndiyo aje na haya majibu?
 
Bashe anaongea ongea tu ila anajuq kabisa moyoni Hana atakaolifanya
 
Yaan kazingua, tuwe tegemezi nje hata Kwa sukari? Siku wakiamua hao wa nje hatutoi sukari tunywe chai bila sukari?

Binafsi naona kazingua. Serikali ingejikita katika viwanda vyake na mashamba kama JPM alivyoanza na kiwandà Cha Mkulazi ambapo wao saiz baada ya kufa mwamba wanatafuta mbia, muwekezaji.
Mtibwa,kilombero, KAGERA vilikua vya serikali..wazalishaji sukari nje wengi,hakuna wa kusema hatuletei sukari,kuwabana wadau wa ndani imeshindika a
 
Kwahiyo anasema hadharani hayo ili kuwatisha wenye viwanda ili wamwone au waongeze dau, kwa maana ya kwann asichukue hatua at first place ili wakilalamika yy ndiyo aje na haya majibu?
Hatua gani!?..kupeleka miswada maana yake kishaandaa,hawatishi
 
Kwahiyo anasema hadharani hayo ili kuwatisha wenye viwanda ili wamwone au waongeze dau, kwa maana ya kwann asichukue hatua at first place ili wakilalamika yy ndiyo aje na haya majibu?
Anasema anapeleka muswada bungeni kuruhusu sukari ya nje kwenye soko.

Sasa, wewe huna haki ya kumtuhumu hilo unalomtuhumu mpaka akishindwa kupeleka huo muswada bungeni.

Mfanyie haki ya kumpa muda kwanza akosee, ashindwe anachosema atafanya, akikosea, akishindwa, hapo utakuwa na haki ya kumsakama na kusema alitaka kidau kipande tu.

Ukimsakama kabla hajapeleka muswada bungeni, utakuwa unafanya tabia zenu za kulalamika kishamba tu kwa conspiracy theories bila ushahidi wala mantiki.

Wewe una tatizo la bei ya sukari. Waziri kakwambia anatatua hilo tatizo kwa kuruhusu sukari kutoka nje. Kakupa na muda maalum wa kutatua hilo tatizo, kwamba atapeleka muswada wa kubadili sheria kwenye bunge la bajeti.

Kwa nini hungojei hilo bunge la bajeti uone kitakachotokea?

Kwa nini unapenda kulalamika kwa conspiracy theories wakati jibu la uhakika utalipata kwenye bunge la bajeti?
 
Back
Top Bottom