Tetesi: Serikali mbioni kuchapisha noti mpya, kuna hatari ya kuelekea kwa Mugabe, harufu ya tenda za kifisadi zatawala

Tetesi: Serikali mbioni kuchapisha noti mpya, kuna hatari ya kuelekea kwa Mugabe, harufu ya tenda za kifisadi zatawala

Mkuu,umenikumbusha kitabu fulani kinaitwa 'His Excellence The Head Of The State' humo ndani humo mwanamama kwa jina la Nelly Takida

Kuna mtawala alitaka kuchapisha fedha Nelly Takida akagoma kwa kumshauri asichapishe tena alimpa formula za kiuchumi mwishowe mwanamama Nelly Takida alipuuzwa na kiongozi wa nchi yake (Kilitania) ali-print noti nyingi sana na kuwapa tenda rafiki zake bila kufuata taratibu za zabuni za ununuzi...gues what happened then!!!!!!?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwel bado kinatumika a level, always literature reflects what is happening in our society
 
BAADA ya uchumi wa nchi kuyumba na maisha ya wananchi kuwa magumu, Rais John Magufuli anahaha kufyatua noti mpya.

SAUTI KUBWA inatambua kwamba tayari serikali imeshaanza mradi wa ufyatuaji wa noti hizo.

Hata hivyo, mradi huo umekwama kwa muda kwa sababu ya kugubikwa na sintofahamu kati ya rais na washauri wake; na miongoni mwa kampuni zilizoingia katika mchakato huo.

Kampuni za kimataifa ambazo zimetambulika kuingia katika mzozo huo ni De la Rue International, Oberthur Fiduciare, na M/s Crane Currency.

Vyanzo vinataja ufisadi katika mchakato kama sababu mojawapo iliyosababisha mzozo huo. SAUTI KUBWA inafuatilia habari za kina kuhusu mzozo huo.

Baadhi ya washauri wa serikali wanapinga ufyatuaji wa noti mpya wakidai utaongeza mfumuko wa bei, utashusha zaidi thamani ya shilingi ya Tanzania; na utafanya maisha ya wananchi yawe magumu zaidi.

Baadhi ya wachambuzi na wachumi waliozungumza na SAUTI KUBWA wanasema iwapo serikali itachapisha noti hizo nchi inaweza kukumbwa na mdororo wa kiuchumi kama uliokumba Zimbabwe katika utawala wa Robert Mugabe.

Mchambuzi mmoja amesema: “Itasababisha mfumuko wa bei za kila kitu kwa namna itakayoifanya shilingi yetu isiwe na thamani kabisa. Hiki ndicho alichokifanya Mugabe miaka ya nyuma baada ya kunyang’anya wazungu mashamba yao na vitega uchumi kutoka nje kukauka.

“Matokeo yake ni kwamba Zimdollar ilipoteza thamani hadi ikabidi ifutwe kabisa. Leo Zimbabwe haina sarafu yake yenyewe, na wananchi wanalazimika kutumia dola ya Marekani na rand ya Afrika Kusini kwa ajili ya manunuzi ya kila aina. Huko ndiko Magufuli anapotaka kupeleka Tanzania. Ataharibu kila kitu kilichobaki.”

Mchumi mmoja anayeheshimika nchini, ambaye SAUTI KUBWA haitataja jina lake, amezungumzia mfumuko wa bei na mzunguko wa fedha. Anasema:

“Mfumuko wa bei uko chini ya asilimia nne (4%). Si mbaya sana. Mzunguko wa hela ni kidogo. Hii ni mbaya. Kuchapisha hela ni uamuzi mbaya kiuchumi. Ujazo wa fedha katika uchumi lazima uendane na kiwango cha shughuli za uzalishaji katika uchumi. Kuchapisha hela ni njia ya ‘kiswahili’ ya kukabiliana na changamoto ya kiuchumi.”

Uamuzi wa Magufuli kuagiza ufyatuaji wa noti mpya, unaakisi kituko cha Idi Amini (dikteta wa Uganda 1971-1979) ambaye alipoelezwa juu ya upungufu wa fedha katika mzunguko, aliamuru benki kuu: “fyatua nyingi zaidi.”

Akijadili hali hii, mhadhiri wa uchumi anayeishi Marekani, anasema kwa kirefu:

Kwanza, tuanze na kujua sababu za lazima za kuchapa pesa. Hii ni kweli kuwa serikali haina fedha za kuendesha shughuli zake na kulipa madeni.

Pili, ni kwa nini serikali haina fedha? Kwa kawaida, ukiacha misaada, serikali ina vyanzo vikubwa viwili vya mapato: (1) Kodi, (2) kuuza dhamana au bonds.

Kwa hiyo, yawezekana ukusanyaji wa mapato ya kodi umepungua Ila serikali haisemi ukweli ili kijipatia sifa za kijinga.

Pia dhamana za serikali huenda haziuziki kama ilivyokuwa awali.

Mambo yote mawili, kupungua kwa mapato ya kodi na dhamana hutokea iwapo uchumi umesinyaa: hakuna uzalishaji wa kutosha kutokana na kudorora kwa uzalishaji kiuchumi.

Nini hufanyika? Serikali ingeweza kukopa zaidi. Huenda wakopeshaki hawapo tayari kwa kuwa kiwango cha uaminifu wa serikali kimeshuka. Utakupunga credit rating ya Tanzania imeshuka sana kwa sasa.

Pia, serikali ingeweza kubana zaidi matumizi yake. Lakini hili nalo Ni gumu sana kwa sasa kwa kuwa tayari imebana hadi ukomo wake. Kumbuka pia kubana matumizi ya serikali hupunguza ukuaji wa uchumi. Kudorora kwa sekta binafsi ni matokeo ya serikali kupana matumizi.

Nini matokeo ya kuchapa pesa? Uchapaji fedha huwa na madhara hasi kiuchumi iwapo uzalishaji haukui. Yaani, kutakuwa na fedha zaidi kwenye mzunguko zisizo na thamani. Matokeo yake ni mfumuko mkubwa wa bei. Kumbuka kilichotokea Zimbabwe kwa utawala wa Mugabe.

Mfumo wa bei usioendana na kipato halisi cha watu, utapunguza uwezo wa kutumia (purchasing power) na matumizi (consumption). Hapo uchumi utaendelea kuelekea shimoni zaidi.View attachment 853999View attachment 854386
Magufuli ni rais wa hovyo kabisa na mikononi mwake hii nchi inaenda kutumbukia shimoni,acha wajjnga kama magonjwa mtambuka,jingalao,Barbarosa,mudawote na wengineo wamshangilie huyu Dikteta lakini ukweli itafika mahali kila mtu atalia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
uchumi alianza kuuharibu jk
huyu alikuwa na nafasi ya kuurekebisha,bahati mbaya badala awaachie wachumi yeye mchmi maganda korosho akawa ndio mshauri mkuu wa kiuchumi,tena majukwaani!!!!
 
Hehe, nacheka kama mazuri vile.

Kumbe magufuli ashafikwa na maji ya shingo? Haya ni matunda ya kiburi na ujuaje wake mwingi usio na faida.

Anyway, tutembee vifua mbere tuko kwenye laiti tlaki.

Mapaka ya lumumba hoyeee (cocochanel, thetallest, nyani ngabu, pohamba, kibst, magonjwa mtambuka, stroke & co.)

Sent using Mikoyan MiG-29
Naomba day and night afanye haraka Ku print hizi note ili tuone hayo mapaka yatasemaje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna tatizo moja ambalo tunashindwa hapa
Kuna wasomi wa uchumi ambao wapo wengi mpaka mawaziri wastaafu lakini wanashindwa hata kulizungumzia au kutoa rai mbele ya camera au kwa simu.

Wanaoongea nao wanaogopa kutajwa that's a shame

Bado tuko nyuma sana likifika suala la kuelezea mambo makubwa na ya msingi katika taifa.
Huku wenzetu waandishi wa habari watawatafuta wahusika au mpaka wastaafu na kuwauliza kuhusu chochote kinachotokea na huwezi kukuta hata mmoja anajibu eti mimi sio msemaji wa serikali

Watu wanajibu wanachoelewa na ni rai tu na uelewa wao kutokana na wanachokijua.

Hela zipo ila zinaelekezwa kwenye miradi mikubwa lakini mradi unaweza ukaenda polepole na huku hela zingine zinatumika kwa kulipa mishahara nk huku tukitafuta zingine kwa kuendeleza miradi

Kuchapisha hela sio suluhu ila kuzalisha zaidi na kupeleka bidhaa nje kwa wingi ndio sehemu nzuri ya kupambana
Kama livestock wanapelekwa kwa wingi nje ni kuongeza maradufu na tujifunze pia kusafirisha matunda yetu na mboga kwa wingi nchi za maghribi na middle East

Hilo tumefeli sana siwasifii Kenya ila wako vizuri kwa hili na May kilichompeleka huko ni mambo kama haya akifikiria brexit itakuwaje anaanza kujiandaa

Ifike mahali tuwe aggressive likifika suala la kujitanua kibiashara na tuache uswahili mwingi

Sent from my SM using Tapatalk
Mkuu huyu ni rais pumbavu kuwahi kutokea,wakiongea mbele ya camera watatekwa ,wataitwa wasaliti wasioitakia mema nchi,wanajua Dikteta hatari yupo ikulu,Magufuli hana tofauti na Idd Amin,tofauti zao ni kidogo mno.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwan Tulipobadilisha Elfu Kumi ya Blue kuingia Elfu kumi nyekundu Uchumi ulidodora.

Hizo Ramli Chonganishi zimekaa kijuha-Juha
Mimi si Mchumi ila nitakusaidia hili kulingana na Wataalamu wa Uchumi wa Jf walivyojibu.

Suala lipo hivi, Rais anataka kuchapa noti hizi hizi zinazotumika sasa hivi kwa maana aziongezee ujazo ziwe nyingi kwenye mzunguko. Wataalamu wa Uchumi wanasema huko ni kudidimiza uchumi, kwa sababu uchumi unabidi ujiendeshe wenyewe. Kuongeza idadi ya noti kwenye mzunguko pesa zitakuwa nyingi ila hazitosadifu ule mzunguko unaotakikana yaani kama umeu' pump mzunguko.

Matokeo yake pesa zitakuwa nyingi kwenye mzunguko ila hazito akisi thamani halisi ya kitu, ili ziendane na thamani ya kitu wenye bidhaa wataongeza bei. Kitakachofuata kwenye manunuzi itaongezwa idadi ya noti ili kujaza lile gap la thamani halisi. Kwa hiyo, kama manunuzi ya kitu flani yalikuwa ni 10,000 ili iendane na thamani halisi ya mambo yalivyo, wata' pump nao bei. Kwaa mantiki hiyo, bidhaa ya namna hiyo inaweza uzwa 30,000 mpaka 40,000.

Kwa hiyo, thamani ya pesa imeshuka.
 
Wakuu nafikri wanaomshauri Rais wetu ama wanamuogopa au hawamwambii ukwel, ama vyote viwili...

Hebu tuanze na kudolola kwa uchumi(tuachane na takwim za kiuchumi ambazo huwa za kisiasa) ni kwel kunakuyumba kwa uchumi kwa kiwango kikubwa na hasa kutokana na sector binafsi kutokupewa kipaumbele..

Nitoe mfano mdogo tu, kipindi cha awam ya nne, serikal za mitaa,(halimashauri, miji na majiji) yalipewa mamlaka ya kukusanya fedha, yakitumia makampun binafsi au wenyewe, hii ilipelekea kuwepo kwa mzunguko wa moja kwa moja fedha kwa kuwa fedha zilipatikana na kuzisaidia haljmashauri..

Isitoshe wasaidizi wa halimashauri(makampuni) yaliajiri watu wengi na hvyo nao kupitia mfumo huo wakapata fedha....

Sasa basi mfumo huo ukaja ukaonekana unashida kubwa si kwenye ukusanyaji bali kwenye matumizi na usimamizi, hii ilipelekea serikali kuzizuia halimashauri kwa aina furani ya tenda kutokuzitangaza..

Bila kujari matokea, halimashairi zikanyang,anywa mapato na kupelekea kuyumba sana... Wakiwa bado wanatafakari ikaja kubwa kuliko yote kuwa sasa si ukusanyaji tu lkn pesa zote ziwe kwenye mfuko mmoja, ili kulinda zisiibiwe..

Hapo ndipo mdololo umekuwa mkubwa sana, sasa hebu jiulize jambo moja ni familia ngap zilikuwa zinapata pesa kwa kutegemea hayo makampun ambayo sasa hayafanyi kazi na taasisi za serikali,

Ok, tufanye kwamba tatzo limetatatuliwa, la wizi na udhibiti wa matumizi ya fedha, je ni kwel kwamba hyo ndyo ilikuwa njia sahihi?

Huenda tulitumia njia ya kuchoma msitu kwa kuwa kuna nyoka ameingia msituni, na kweli tukafanikiwa kumuuwa, je tumepoteza viumbe asili vingapi kwa sabab ya kuongia kwa nyoka msituni?

Hapo ndipo mm nafikiri washauri wa rais walipaswa kumwambia ukwel Rais, kuwa hoja si kuzuia mapato kukusanywa na serikali, hoja ni kuhakikisha tunatengeneza mfumo imara wa usimamizi na ukaguzi ili kuziba minya ya pesa....


Ikumbukwe kwa sasa kunaupungufu mkubwa wa pesa hasa kwa wananchi wa chini, ambae alitegemea auze maandazi, vitumbua, matunda, mitumba n.k

Hii inamaana ipi?
Tunakwenda kwenye kuimalisha nchi ya viwanda tukuwa na wananchi ambao hawako tayri kuingia kwenye huo uchumi, tujue tu kuwa kwa kuwa hatuna katiba Ambayo inamsingi mzuri siku akitokea Rais mwingine ambae si wa sasa.(baada ya miaka ya uchaguzi)atakuja na kuubadili kabisa mfumo uliopo sasa,

Kwa maana hyo tutakuwa tumechelewa kwa miaka 10, lakini pia itatulazim tuanza na muundo mwingine kwa miaka 10tena.. Matokeo yake tutakuwa tunasafri kwa hatua kumi tunarudi kwa hatua 7, halafu tena tunaanza hatua za kwenda mbele..


Jambo la msingi kwa sasa Rais ashauriwe vizr ya kwamba huku chini bado hapako vzr, nia yake ni njema kabisa(sina shaka nayo) ila ajitahidi kuimalisha sector binafsi



Mwiaho niseme hiki, uchumi wa nchi hautegemei mtu mmoja au taasisi, uchumi wa nchi unamtegemea kila mtu, wajibu wa serikal ni kuweka mazingira rafiki, si shindani ili kuwawezesha watu wake kufaidi na kuijenga nchi yao...

Kwa pamoja tutajenga

Mr Bonny...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu,umenikumbusha kitabu fulani kinaitwa 'His Excellence The Head Of The State' humo ndani humo mwanamama kwa jina la Nelly Takida

Kuna mtawala alitaka kuchapisha fedha Nelly Takida akagoma kwa kumshauri asichapishe tena alimpa formula za kiuchumi mwishowe mwanamama Nelly Takida alipuuzwa na kiongozi wa nchi yake (Kilitania) ali-print noti nyingi sana na kuwapa tenda rafiki zake bila kufuata taratibu za zabuni za ununuzi...gues what happened then!!!!!!?

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji16][emoji16]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom