Serikali na Hatima ya Tamthilia za kigeni zilizo lugha ya Kiswahili kwa Kizazi Chetu

Serikali na Hatima ya Tamthilia za kigeni zilizo lugha ya Kiswahili kwa Kizazi Chetu

CONSISTENCY

Senior Member
Joined
Feb 16, 2023
Posts
135
Reaction score
309
Binafsi nasikitika kuona Tamthilia hizi za Kituruki, kihindi, kikorea, kichina, kiarabu n.k zilizotafsiriwa kwa lugha yetu ya Taifa kiswahili zinazooneshwa sana muda mwingi katika chanel zetu maarufu nchini hasa Azam kila nikiingia nyumbani, saloon, bar, hotel n.k.

Serikali hasa Wizara ya sanaa na michezo tunaomba simamisheni kuonesha hizi Tamthilia sababu hakuna faida ya hizi Tamthilia kwa jamii yetu na kama Kuna faida za kimapato au kimaadili tunaomba jamii ielezwe.

Kwanza kinachoonesha kwenye hizo Tamthilia hakiendani kabisa na Mila, desturi, utamaduni wetu n.k kuanzia mazingira, location, nidhamu, mavazi n.k kinachoonesha katika hizo Tamthilia ni kuifanya jamii ya kitanzania iamini kwamba maisha wanayoishi hao watu ni Bora na ya maana kuliko maisha ya kitanzania mfano mtoto mdogo atataka kuiga tabia za mtoto wa kwenye Tamthilia kuliko kufuata kile anachoambiwa na wazazi wake.

Kwa kifupi hizo Tamthilia zinasababisha mmonyoko mkubwa wa maadili kwa jamii nzima, kitu kibaya zaidi hizo Tamthilia zinaoneshwa mda wote kuanzia asubuhi Hadi usiku, utasikia hiki ndio kipindi haya ni marudio n.k ila zinaoneshwa siku nzima.

Serikali Kuna mambo mengi yakuonesha jamii kwenye chanel zetu ikiwemo kilimo, biashara, ufundi, fursa nje ya nchi n.k

Hata kama jamii inapenda lakini mda mwingine inawezekana jamii inapenda sababu ya nguvu inayotumika kuonesha kwamba hizo Tamthilia zina maana kumbe ni ujinga mtupu.

Wito wangu kwa serikali simamisheni hivyo vipindi sababu havina faida yeyote kwa jamii.
 
No offense, ila broh unasound kama dingi mwenye itikadi za kikoloni au kikuda. Yani unataka tv zioneshe habari za kilimo au ufundi muda wote? Nini maana ya burudani?

Alaf usichojua, kwenye ulimwengu huru Kila mtu anachagua anachopenda. Wewe unahisi tv muda wote zinaonesha tamthilia kwavile hizo ndizo sehemu unazo tune wewe, ila vipindi vipo vingi tu, Kila mtu na interest zake.
 
No offense, ila broh unasound kama dingi mwenye itikadi za kikoloni au kikuda. Yani unataka tv zioneshe habari za kilimo au ufundi muda wote? Nini maana ya burudani?
Bado haujaelewa, Kuna nguvu kubwa inayotumika kutangaza hivyo vipindi ila jamii iamine ni vipindi vizuri.

Unajua kitu kinaitwa culture transmission?

Au unaweza kutuambia faida ya hivyo vipindi kwenye jamii yetu?
 
Bado haujaelewa, Kuna nguvu kubwa inayotumika kutangaza hivyo vipindi ila jamii iamine ni vipindi vizuri.
Unajua kitu kinaitwa culture transmission?
Au unaweza kutuambia faida ya hivyo vipindi kwenye jamii yetu?
Yani mkuu unaongelea culture transmission na kulaumu vipindi vya TV, wakati huo huo 24/7 mnashindwa TikTok n other social medias.
 
Unachoongea ni kweli ila ume exaggerate sana.

Japo hata mimi niliwahi kuwaza kama wewe hasa katika nyanja ya kuathiriwa kitamaduni.

Vibinti vingi vimekuwa brainwashed na tamthilia hadi vinakataa utu wao kiafrika na kuona kuwa mwafrika ni laana, wengi wanatamani kuwa na watoto weupe na huwapa majina ya kituruki.

Yaani jamii ishakuwa brainwashed sana, nadhani tamthilia za hapa nyumbani zingepewa kipaumbele maana zinagusa dhima halisi ya maisha ya kitanganyika.

Mfano wa tamthilia bora kwangu ni hii MTAA WA KAZAMOYO na ZAHANATI YA KIJIJI
 
Sasa nyie wasanii wa bongo tamthilia zenu zipo chini ya kiwango unataka watu wafanyeje? Boresheni kazi zenu acheni majungu.
Ni sahihi, ila hizo Tamthilia hazina faida yeyote kwa jamii yetu
 
Unachoongea ni kweli ila ume exaggerate sana
Japo hata mimi niliwahi kuwaza kama wewe hasa katika nyanja ya kuathiriwa kitamaduni
Vibinti vingi vimekuwa brainwashed na tamthilia hadi vinakataa utu wao kiafrika na kuona kuwa mwafrika ni laana, wengi wanatamani kuwa na watoto weupe na huwapa majina ya kituruki
Hehe kuna trend ya kutoa majina ya watoto siku hizi siielewi,,,tamthilia kweli zina nguvu
 
This is Rubbish and nonsense.

Hizi tamthilia zimeenea kwa sababu pia ya kupendwa na majority.

Tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa wenzetu kupitia hizi tamtilia na ni lazima ziendelee kuhamasishwa. Unataka mda wote chanel ziwe zinaonesha kilimo biashara na ufundi? Huo ni ukoloni kuna muda wa burudani pia.

Uwekezaji na support ya serikali katika tamtilia za ndani ni poor, ndyo maana hakuna ubunifu wowote katika hizi tamtilia na kuna maudhui machache sana ya kujifunza huko. Acha tutizame za kimataifa, binafsi nipo nimetulia hapa nacheki Golden Boy.
 
SERIKALI IRUDISHE MASOMO YA KILIMO NA BIASHARA MASHULENI.ACHANA NA HZO TAMTHLIA
Hilo wazo zuri sana, Serikali inatakiwa kuwa na dira kijamii, kiuchumi, kisiasa, kiteknolojia n.k kuliko hizo Tamthilia ambazo zinapoteza mda na kuharibu jamii
 
This is Rubbish and nonsense.

Hizi tamthilia zimeenea kwa sababu pia ya kupendwa na majority.
Tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa wenzetu kupitia hizi tamtilia na ni lazima ziendelee kuhamasishwa. Unataka mda wote chanel ziwe zinaonesha kilimo biashara na ufundi?? Huo ni ukoloni kuna muda wa burudani pia.

Uwekezaji na support ya serikali bkatika tamtilia za ndani ni poor ndyo maana hakuna ubunifu katika tamtilia mengi na kuna maudhui machache sana ya kujifunza huko. Acha tutizame za kimataifa, binafsi nipo nimetulia hapa nacheki Golden Boy.
Your an idiot with inferiority complex
 
Hehe kuna trend ya kutoa majina ya watoto siku hizi siielewi,,,tamthilia kweli zina nguvu
Kwa kesi kama hiyo ndo utaona siku zikianza kuingizwa ajenda mbaya za nje jamii itaathirika sana nadhani tunapaswa kuulinda utambulisho wetu kama watanzania hizi tamthilia za nje zimezidi sana siku hizi ukiwa na mtoto mweusi atatengwa
Ukizaa mweupe utasikia "katoto kako kazuri kama mturuki au mkorea"

Vibinti vya siku hizi haviamini unaweza kuwa mbantu na ukawa mrembo
 
Back
Top Bottom