Serikali na Hatima ya Tamthilia za kigeni zilizo lugha ya Kiswahili kwa Kizazi Chetu

Hii ni hatari sana ndugu, ila nafikiri Azam analipwa pesa nyingi kwa kuonesha hizo Tamthilia
 
familia zetu zinapaswa kupata chakula bora, mavazi na maradhi, ili kujenga kizazi bora kijacho, hili ni jukumu la baba, mama na wanajamii
 
Azam ni mfanyabiashara na mfanyabiashara anajali faida tu, Lakini lazima ana baraka za serikali kupitia wizara husika.
Inawezekana, hawa jamaa wanatumika sana na kufanya Dili chafu kwenye jamii.
Ukianzia kwenye energy drink, Tamthilia n.k ni hatari tupu
 
familia zetu zinapaswa kupata chakula bora, mavazi na maradhi, ili kujenga kizazi bora kijacho, hili ni jukumu la baba, mama na wanajamii
Umesahau kwamba kwenye kujenga maadili na serikali inahusika kutokana na utandawazi jinsi ulivyo
 
Bongo muvi mnazingua ndiomana hatupendi kuwaangalia, jini linavuka barabara huku linatazama kushoto na kulia kweli??
 
Maadili ya kitanzania ni kujiepusha na maadili ya hovyo kama ushoga, kuwa na heshima kwa wazazi n.k
Kwanini iwe heshima kwa wazazi na isiwe kuheshimiana kati ya watu wote?vile vikundi vya ngoma vinavyochezaga nusu uchi, wasanii especially wa kike wanaovaa nusu uchi, vipi hayo ni maadili ya kitanzania na kama sio kwanini yamehalalishwa?
 
Bongo muvi mnazingua ndiomana hatupendi kuwaangalia, jini linavuka barabara huku linatazama kushoto na kulia kweli??
Upo sahihi, ila huu uzi hauhusiani na bongo movie.
 
Kwanini iwe heshima kwa wazazi na isiwe kuheshimiana kati ya watu wote?vile vikundi vya ngoma vinavyochezaga nusu uchi, wasanii especially wa kike wanaovaa nusu uchi, vipi hayo ni maadili ya kitanzania na kama sio kwanini yamehalajishwa?
Ni jamii ngapi za kitanzania zinafanya hilo jambo ukiacha watu wenye asili ya pwani kama wazaramo, wakwere, waruguru?
Unajua kwamba hizo Tamthilia za kigeni zinaangaliwa nchi nzima kwenye TV?
 
yana madhara makubwa kwa jami
Sure ndugu yangu, athari ni kubwa mno, watu wengi wana focus kwenye hizo tamthilia hata taarifa ya habari hawana haja nayo .

Kijana wa makamo anakuelezea mwelekeo wa tamthilia kwa ufasaha lakini hana taarifa yoyote ya kitaifa.

Juzi tu kijana mmoja wa kike hajui kama sera mpya ya elimu ipoa imesha anza kazi kwamba elimu ya msingi sasa ni miaka kumi, hilo hajui ila anakuelezea barabara tamthilia za kituruki kana alikua miongoni mwa walio iandaa!
 
Sorry umeandika elimu ya msingi ni miaka sita au kumi?
 
Ni jamii ngapi za kitanzania zinafanya hilo jambo ukiacha watu wenye asili ya pwani kama wazaramo, wakwere, waruguru?
Unajua kwamba hizo Tamthilia za kigeni zinaangaliwa nchi nzima kwenye TV?
Apana! Bila shaka utakua unazungumzia vigodoro lakini mimi simanishi hivo japo navyo ni kichefuchefu. Kuna vile vikundi ambavyo hata mgeni wa heshima akija katika nchi hupokelewa na vikundi hivyo vya ngoma airport.Vilevile tuna wasanii wetu wa kike wanavaa nusu uchi na wasanii wetu wa kiume wanatoboa pua, kuvaa hereni, kusuka nywele, kuvaa nguo za kina dada n. k , hayo yote yanachigiza hayo mambo ya ushoga na tabia zingine chafu. Huoni kwamba kabla ya kutaka tamthilia za nje zikemewe tuanzie ndani kwanza?
 
Ndo nia kuu ya huu uzi kujadili ushoga, kwan mashoga wote hawa walianza kwa kutazama tamthilia?

Huwa hamna hoja nyingine?
 
Maadili ya kitanzania ni kujiepusha na maadili ya hovyo kama ushoga, kuwa na heshima kwa wazazi n.k
Yaan nia yako kupinga ushoga, jamani ushoga hata hauenezwi na tamthilia, polee wee
 
Upo sahihi kwa upande huo ila hayo mambo yanamatokeo mabaya kidogo kwa sababu jamii haioni kila siku.

Hizo Tamthilia nazungumzia sababu jamii inaona kila siku kuanzia asubuhi Hadi usiku hivyo imegeuka kama ndio mtindo wa maisha wa Kitanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…