Serikali na Wadau wa afya sikieni kilio hiki cha NHIF

Serikali na Wadau wa afya sikieni kilio hiki cha NHIF

Siku Moja katika pita pita zangu nlikutana na Jamaa mmoja anitwa NHIF ,huyu jamaa ni mdau mkubwa sana wa Afya kwa kifupi ni kajitolea kuwatunzia pesa zao Watu kwa Ajiri ya Matibabu yao baadae .

Wakati napita alikuwa mlangoni nlimsikia akilia kwa Nguvu sana akisema Ooh God ,thank you for another day nkamsalimia nikamuuliza mbona Unahuzuni na masikitiko makubwa ? Alinijibu yafuatayo :-

1.Pesa za Watu wangu zinachukuliwa na kwenda kulipa huduma ambazo hazipo kwenye makubaliano kama Watu wanachukua Maji ya kunywa,Mafuta ,Vipodozi na vingine vingi kupitia bima kunyume na Taaribu .

2.Pesa za watu wangu zinachukuliwa na kwenda kulipa Wateja feki

3.Pesa za watu wangu zinachukuliwa zinakwendakulipa vipimo na upasuaji ambao haujafanyi mfano mtu Anapusuaji Jipu anaandika katoa Uvimbe mkubwa .

4.Pesa za watu wangu zinachuliwa kwenda kulipa Dawa za Bei kubwa huku dawa iliyotolewa ni ya Bei Ndogo sana .

5.Pesa za watu wangu zinachukuliwa zinapelekwa kulipa malipo ya matibabu kwa watu ambao sio Hata wanachama .

6.Kibaya zaidi Serikali na Bodi ya Wakurugenzi NHIF wamefanya pesa hizi kama mali yao wanatumia kwa starehe zao na matumizi yao binafsi .

Alilia sana akasema sio muda nitaishiwa pesa ,watu hawatanielewa watakosa huduma Bora watapata BORA HUDUMA na hawatanipenda tena .Nikamuacha nikamuahidi ntafikisha kilio Chake .

Hivyo Serikali na Watoa huduma za Afya sikieni kilio cha NHIF .​
Tulikubaliana tunaifungua nchi na kila mmoja ale kwa urefu wa kamba yake, kelele za nini?
 
  • Thanks
Reactions: RNA
Kiufupi NHIF ni suala la muda tu inapenda kufa soon, watoa huduma wengi hasa private wamekaa kiupigaji sana ni muda muafaka serikali ichukue hatua kwa hivi vituo kabla mambo hayajawa mabaya.
 
Bongo kuongeza chumvi kwingi. Kwanza polyclinic nyingi zipo mjini sehemu ambazoo uelewa ni mkubwa na specialist wanajulikana sana. Yaani mgonjwa aje kutibiwa kwa gyno specialist x halafu amkute MD na akubali tu kirahisi tu kupata huduma. Halafu kwenye Polyclinic si specialist tu wapo kuna MD pia. Kwa sehemu kubwa makubaliano huwa ni kuwa kwa kila specialist anapewa sehemu ya fedha kwa kila mgonjwa anayemuona. Sasa itakuwaje umlipe MD halafu kwa mgonjwa huyohuyo umlipe specialist anayekuja ku-sign fomu! Kwa sababu consultation inayolipwa na NHIF ni Tshs.15,000 kwa mgonjwa.
Haya mambo yapo pia
 
Mkuu, wewe ni daktar
Umeongea vizuri
Watanzania ujuaji ni mwingi, tunajikuta wataalam Kwenye Kila sekta.
Consultation fee ya G. P ni 7000/=
Consultation fee ya specialized M. O ni 15000/=
Hawafanyi double consultation for the same pt at the same day, kwenye hizi polyclinic.
NHIF ndio wanaongoza kureject claims za Malipo zinazowasilishwa kwao, yaani huwezi kwenda kudai million 10 halafu ulipwe zote, ni lazima wazipunguze
Mimi nadhani NHIF ndio wezi kuliko hao watoa hudumq
Hakika
 
Namna pekee ya kuunusuru huu mfuko usife, nikuongeza wanachama wapya ambao hawaumwi. Mfuko upambane kusajili watoto karibu wote kwenye shule za msingi na sekondari wawe na NHIF, vyuo vikuu vyote na vyuo vya Kati NHIF iwe lazima. Lakini pia mfuko uongeze siku za kuwa mwanachama Kwa watu wazima kutoka siku 30 hadi 120 (Wekeza,Najali, na Timiza Afya) hii itasaidia kuwepo Kwa uelewa wa pamoja kujiunga na NHIF bila kusubiri uumwe.

Pamoja na mambo yote niliyoshauri hapo juu, mfuko usiruhusu usajili mpya kwenye polyclinic zilizo karibu karibu Kwa sababu unachochea fraud kutokana na kwamba, wagonjwa wanakuwa wachache kwenye vituo vyao na kuwalazimu kupika madai ili waweze kumuda kuendesha. Lakini vituo vikiwa mbalimbali, Dr akawa anapata wagonjwa Kwa wastani wa 20 Kwa wakatimoja anakuwa busy na kupunguza ujanjaujanja wa + or - ambazo pengine wanafanya Kwa lengo la adjustment ili makato yakifanyika wasiweze kuingia hasara kubwa Kwa sababu NHIF na wenyewe wanawakata Sana na wakati mwingine sababu za msingi wanakuwa hawana. Naomba niishie hapo Kwa sasa niweze kuendelea na majukumu mengine asante.

Suala la usajili wa polyclinic siyo issue, tumeona matumizi ya live registration unatumika. Hizi hizi za live registration/electronic bado wagonjwa ni walewale wengi. Ingawa NHIF pia walikuwa na wasiwasi, ukipeleka wanakwambia " mbona folio nyingi, wagonjwa mnatoa wapi??". Polyclinic moja inaona watu 80-100 kwa siku, huku imezungukwa na vituo vya serikali. Kuna vitu ambavyo vinafanya watu wageukie polyclinic:

1: Huduma zisizotoshereza kwenye baadhi ya vituo vya afya, ikiwemo vya serikali. Ukimuuliza mgonjwa ka nini haujaenda pale, wakati ni karibu ukamleta mgonjwa kama huyu huku mbali? anakwambia mimi pale sipaelewielewi.

Mfano: mtoto ana homa kali au amebanwa kifua, unamweleza mgonjwa ni vizuri kwanza angepatahuduma pale karibu na anapoishi.

2: Wagonjwa wa NHIF kuwa halfly treated kwa watu kuogopa makato.

Mgonjwa ana kikohozi na mafua. Anapewa dawa ya kikohozi na mafua unanikata mojawapo. Kesho akija atapewa mojawapo, mfano: atapewa ya mafua au kikohozi tu. Ili kukwepa makato.

Akiona mambo yanaendelea, anaenda kufanya consultation kwaajili ya dawa ya mafua yaliyoachwa bila kutibiwa. Na hasa haya ya sasa ni kisilani kweli.

Ingawa kuna self limiting flue and cough, lakini kama mtaalamu kafikia kumpa then wewe ukiwa ofisini unakata tu.
Ukiulizwa kwa nini mmekata: Unajibu, nadhani mlikuwa na dawa zinakaribia ku-expire mkaamua kuzitoa au mnatoa sana dawa za mafua(mtu hajui haya magonjwa ni seasonal).

Unashauriwa: tafuta cough mixture yenye multipurpose, of which ziko more expensive.

3: Tunang'ang'ana na STG kama msahafu wakati hutufanyi resistance patterns ya dawa kwenye jamii yetu ili kuwa objective and scientific. Unapataje STG kwa kukusanya tu matabibu bila data zozote kutengeneza muongozo? Hivyo, watu tunanaogelea humo blindly. At least tungefanya zonal wise ili tuwe na ushauri unaoendana na hali halisi. Ukifanya wewe C/S, mnafanya vipimo sana?? Kumbe wewe umetibia na mtu amerufi bila better response.

4: Wagonjwa kutokufanyiwa vipimo wakati mwingine hata kama wanastahili kwa kuogopa makato. Mgonjwa anaelekezwa kituo Y kufanya vipimo kwa sababu kituo B wanaogopa wakifanya vipimo wataishia kukatwa.

5: Wagonjwa kuambiwa hapa hutapata huduma kwa sababu jana mtoto/mgojwa huyu alitibiwa hapa jana.

6: Unapata mgonjwa ana fangusi na muwasho, unampatia combined(antifungal na antipruritus), mtu anakata.

Maana ya:
1: Huyu mtu umpe antifungal peke yake? Kesho ataenda kutafuta dawa ya muwasho??
2: Umwandikie separate tubes antifungal na antipruritus of which is very expensive.

7: Hili litaenda kuumiza tena kwenye form 2C kwa wazee ambao ni DM na HTN au long term/life long illnesses. Kwani wakikosa dawa hizo obviously watakuwa wanafanya multiple shopping ili mpaka watimize idadi ya dawa zao. Hii itakuwa shida sana kwa wagonjwa wenye magonjwa ya kudumu mgano yule ambaye ni DM and HTN aje ku-refill, mpaka abahatike kupata sehemu moja yenye dawa zote. Ni ngumu kuamini kuna hospitali itakuwa na dawa zote za Bp, Dm, Osteoporosis, Pumu, Kifafa nk. Labda kama kila mara utazibadili, kitu ambacho si practice.

Mgonjwa atakuja ana hitaji la dawa ya level S kwenye Polyclinic au Zahanati, kosa la nani hapo? Wakati huo, CO, AMO na MO hawaruhusiwi ku-refill.
Na wao hawajui levels za dawa.

NB: Wagonjwa wengi wataendelea kuzurula mahospitalini kwa expense za hela iliyoko kwenye mfuko. Multiple consultation ili apate dawa zake zote. 🤔🤔🤔

Kuna mambo NHIF inafanya, ni kama kukata mti uliokalia.
 
Nadhani huyu mdau inabidi ajiangalie mwenyewe kwanza:

1: Utaratibu wa kupata na kutumia kwa kiasi gani uko ndani ya mifumo yake.

2: Yeye ndiye anaehakiki kila anachokitoa kwa mtoa huduma, hivyo kama hana uhakika na anacholipa basi ajitafakari kwa nini analipa watu ili kuhakiki anacholipa huko.

3: Ukipewa advance, ukaona una hela nyingi na kuongeza matumizi ya ndani ya himaya yako kabla ya yule alitekupa advace, ujue kuna siku utakwama tu.

4: Ukipewa advance nawe ukaona una hela nyingi, ukamkopesha jirani ambaye huna uhakika wa kurudisha kwake ujue unatwanga maji kwenye kinu kuna siku utatafuta mchawi tu.

5: Ukianzisha miradi bila upembuzi yakinifu, kwa kufuata sauti za jirani, ujue kuna siku utatafuta mchawi tu, mahitaji yanatofautiana siyo kila ukiambiwa unawekeza hata kwa wenye mahitaji makubwa ili umridhishe jirani tu.

Simamia mifumo yako vizuri kabla ya kutoka nje, kwani haya yote ya watoa huduma yanaanzia kwako mwenyewe kushindwa kuwasimamia ndo shimo lake. Wasimamie vyema kwa mjibu wa sheria na taratibu, hatakuja mwingine kusimamia kazi zako.
1 mpaka 5 anayoyalalamikia yapo ndani ya himaya yake. Ni kushindwa kuwajibika tu.
 
Suala la usajili wa polyclinic siyo issue, tumeona matumizi ya live registration unatumika. Hizi hizi za live registration/electronic bado wagonjwa ni walewale wengi. Polyclinic moja inaona watu 80-100 kwa siku, huku imezungukwa na vituo vya serikali. Kuna vitu ambavyo vinafanya watu wageukie polyclinic:

1: Huduma zisizotoshereza kwenye baadhi ya vituo vya afya, ikiwemo vya serikali. Ukimuuliza mgonjwa anakwambia mimi pale sipaelewielewi.

2: Wagonjwa wa NHIF kuwa halfly treated kwa watu kuogopa makato. Tunang'ang'ana na STG kama msahafu wakati hutufanyi resistance patterns ya dawa kwenye jamii yetu ili kuwa objective and scientific.

3: Wagonjwa kutokufanyiwa vipimo wakati mwingine hata kama wanastahili kwa kuogopa makato. Mgonjwa anaelekezwa kituo Y kufanya vipimo kwa sababu kituo B wanaogopa wakifanya vipimo wataishia kukatwa.

4: Wagonjwa kuambiwa hapa hutapata huduma kwa sababu jana mtoto/mgojwa huyu alitibiwa hapa jana.

5: Hili litaenda kuumiza tena kwenye form 2C kwa wazee ambao ni DM na HTN. Kwani wakikosa dawa hizo obviously watakuwa wanafanya multiple shopping ili mpaka watimize idadi ya dawa zao. Hii itakuwa shida sana kwa wagonjwa wenye magonjwa ya kudumu. Ni ngumu kuamini kuna hiapitali itakuwa na dawa zote za Bp, Dm, Osteoporosis, Pumu, Kifafa nk. Labda kama kila mara utazibadili, kitu ambacho si practice.

Mgonjwa atakuja ana hitaji la dawa ya level S kwenye Polyclinic, kosa la nani hapo?
Na wao hawajui levels za dawa.

NB: Wagonjwa wengi wataendelea kuzurula mahospitalini kwa expense za hela iliyoko kwenye mfuko. Multiple consultation ili apate dawa zake zote. 🤔🤔🤔
Umewasilisha vizuri mkuu
NHIF Ina matatizo mengi ya kiutawala kuliko hayo madai ya kua wanaibiwa na watoa Huduma.
Mkurugenzi anawahimiza auditing/control officers wakat Malipo kwa hali na Mali, wakiwa wanakagua form wanachoangalia ni wapi PA kukata
Ajabu ni kwamba hawa control officers ni madaktar lakini madudu wanayoyafanya
Daktar anakata dawa ya kikohozi ile mucolyn kisa imetolewa pamoja nq Cetirizine au loratadine
Hua najiuliza, hivi huyu daktar akiwa amebanwa na mafua hasa na kikohozi, akipewa mucolyn pekee ataridhia au huwa wanafanya hivi kukomoana?
Ila kwa vile Wagonjwa wenyewe ni ndio kama Hawa wajuaji wasio jua wanataka nini haswa basi sawa
 
Umewasilisha vizuri mkuu
NHIF Ina matatizo mengi ya kiutawala kuliko hayo madai ya kua wanaibiwa na watoa Huduma.
Mkurugenzi anawahimiza auditing/control officers wakat Malipo kwa hali na Mali, wakiwa wanakagua form wanachoangalia ni wapi PA kukata
Ajabu ni kwamba hawa control officers ni madaktar lakini madudu wanayoyafanya
Daktar anakata dawa ya kikohozi ile mucolyn kisa imetolewa pamoja nq Cetirizine au loratadine
Hua najiuliza, hivi huyu daktar akiwa amebanwa na mafua hasa na kikohozi, akipewa mucolyn pekee ataridhia au huwa wanafanya hivi kukomoana?
Ila kwa vile Wagonjwa wenyewe ni ndio kama Hawa wajuaji wasio jua wanataka nini haswa basi sawa
Uko sawa
 
Namna pekee ya kuunusuru huu mfuko usife, nikuongeza wanachama wapya ambao hawaumwi. Mfuko upambane kusajili watoto karibu wote kwenye shule za msingi na sekondari wawe na NHIF, vyuo vikuu vyote na vyuo vya Kati NHIF iwe lazima. Lakini pia mfuko uongeze siku za kuwa mwanachama Kwa watu wazima kutoka siku 30 hadi 120 (Wekeza,Najali, na Timiza Afya) hii itasaidia kuwepo Kwa uelewa wa pamoja kujiunga na NHIF bila kusubiri uumwe.

Pamoja na mambo yote niliyoshauri hapo juu, mfuko usiruhusu usajili mpya kwenye polyclinic zilizo karibu karibu Kwa sababu unachochea fraud kutokana na kwamba, wagonjwa wanakuwa wachache kwenye vituo vyao na kuwalazimu kupika madai ili waweze kumuda kuendesha. Lakini vituo vikiwa mbalimbali, Dr akawa anapata wagonjwa Kwa wastani wa 20 Kwa wakatimoja anakuwa busy na kupunguza ujanjaujanja wa + or - ambazo pengine wanafanya Kwa lengo la adjustment ili makato yakifanyika wasiweze kuingia hasara kubwa Kwa sababu NHIF na wenyewe wanawakata Sana na wakati mwingine sababu za msingi wanakuwa hawana. Naomba niishie hapo Kwa sasa niweze kuendelea na majukumu mengine asante.
Umeongea mambo ya maana sana kam MD wa NHIF ataweza kupitia hapa .
 
Nchi ya majizi hii, nawe jitahidi tu kukwapua hapo ulipo….. hakuna namna.
 
Back
Top Bottom