Serikali na Wadau wa afya sikieni kilio hiki cha NHIF

Serikali na Wadau wa afya sikieni kilio hiki cha NHIF

Na wagonjwa siku hizi tuna-google, ukinitibu hivyo nakuona hufai kwenye taaluma yako na wewe ni kajanja! Nikija kwenye kituo chako na dawa fulani nikakosa najua kituo ni cha wababaishaji, sitajua kuwa haiwezekani kituo kikawa na dawa zote zinazohitajika kwa matibabu. Nikikukuta zahanati au kituo cha afya ukashindwa kunipa pantoprazole nitakushangaa (kumbe inatakiwa kutolewa na MD na wewe ni CO), ukiniambia basi kanunue au lipia unisaidie napiga simu NHIF nawaambia kituo kinanitoza pesa ili kiniibie! Nikija na kidonda Polyclinic na ukakataa kunifanyia dressing napiga simu NHIF kuwaambia mmekataa kunipa huduma mnataka pesa yangu (kumbe dressing haipo kwenye kitita kwa polyclinic).

Mtandao wa NHIF ukisumbua mkaniambia hebu subiri utengamae ili unipe huduma nasonya na kuwaambia nyie ni wababaishaji! halafu napiga simu NHIF kulalamika, NHIF wanakuwa wakali na kutaka mimi na wenzangu tupewe huduma ila tuache kadi. Lahaula tukiondoka na mtandao ukarudi unakuta mimi au mwenzangu kadi zetu zimekuwa rejected na tumeshatibiwa, kama umepata hasara shauri yako NHIF hawatakulipa.

Halafu kuna madaraja ya wagonjwa hatujui, nikija kutibiwa na akaja mwanachama wa fast track kama BOT, NMB au TRA anapitiliza moja kwa moja kwa daktari maalum huku nikiwa nimepanga foleni na wenzangu (naanza kulaumu jinsi watoa huduma walivyo na upendeleo na kujali rushwa) hee, kumbe mwongozo wa NHIF fasttrack anatakiwa apewe upendeleo maalum kwa sababu alilipa NHIF mpunga mrefu! Ghafla naona analazwa chumba cha peke yake na mimi nipo wodi ya jumuiya, nalalamika kwa daktari kwa nini aniweke wodi ya jumuiya wakati mteja mwingine wa NHIF kawekwa private ward. Hatari!!

😂😂😂Wewe utakuwa si mgonjwa umeamua kwenda kununua ugomvi tu kituo cha afya.

1: Ingawa suala la Polyclinic kunyimwa dressing!!?? Sijawahi elewa.

2: Pantoprazole, hiyo utaambiwa kwani hakuna Omeprezole (mgonjwa usichague dawa bali daktari ndiye hukuandikia).
 
Siku Moja katika pita pita zangu nlikutana na Jamaa mmoja anitwa NHIF ,huyu jamaa ni mdau mkubwa sana wa Afya kwa kifupi ni kajitolea kuwatunzia pesa zao Watu kwa Ajiri ya Matibabu yao baadae .

Wakati napita alikuwa mlangoni nlimsikia akilia kwa Nguvu sana akisema Ooh God ,thank you for another day nkamsalimia nikamuuliza mbona Unahuzuni na masikitiko makubwa ? Alinijibu yafuatayo :-

1.Pesa za Watu wangu zinachukuliwa na kwenda kulipa huduma ambazo hazipo kwenye makubaliano kama Watu wanachukua Maji ya kunywa,Mafuta ,Vipodozi na vingine vingi kupitia bima kunyume na Taaribu .

2.Pesa za watu wangu zinachukuliwa na kwenda kulipa Wateja feki

3.Pesa za watu wangu zinachukuliwa zinakwendakulipa vipimo na upasuaji ambao haujafanyi mfano mtu Anapusuaji Jipu anaandika katoa Uvimbe mkubwa .

4.Pesa za watu wangu zinachuliwa kwenda kulipa Dawa za Bei kubwa huku dawa iliyotolewa ni ya Bei Ndogo sana .

5.Pesa za watu wangu zinachukuliwa zinapelekwa kulipa malipo ya matibabu kwa watu ambao sio Hata wanachama .

6.Kibaya zaidi Serikali na Bodi ya Wakurugenzi NHIF wamefanya pesa hizi kama mali yao wanatumia kwa starehe zao na matumizi yao binafsi .

Alilia sana akasema sio muda nitaishiwa pesa ,watu hawatanielewa watakosa huduma Bora watapata BORA HUDUMA na hawatanipenda tena .Nikamuacha nikamuahidi ntafikisha kilio Chake .

Hivyo Serikali na Watoa huduma za Afya sikieni kilio cha NHIF .​
Kheri yake kuliko mwenzake NSSF ambaye pesa za watu wanagawana barabarani na wafanyakazi wanazichota huku serikali na viongozi wanajengea makasri na kununua magari huku wenyenazo wakizisikia kwa mbali.
 
Hii itasaidia sana ikiunganishwa na live registration/authorization na finger print pia ni njia mwafaka ya kuhakiki gharama halisi za matibabu, maana wahudumiwa wanaonyesha kutokujali sana. Hasa kwa sababu kwenye mfumo wa sasa wanasaini kuandikishwa na si kuthibitisha gharama husika.

Nadhani kwa mfumo wa sasa wa electronic, ilitakiwa kuwepo namna zile gharama kwa kuwa ni electronic basi mtu asaini mwishoni akiwa anaona jumla ya gharama na si kuthibitisha kujisajili.
Kimsingi hawa Bima(NHIF) wanatakiwa waje na mfumo imara na madhubuti wenye kunyumbua kila kitu na kila mtu ajue/awekwe wazi juu ya huduma aliyopata na aliyotoa.

Huo mfumo umuwezeshe mgonjwa kuondoka na nakala ya gharama ya huduma aliyopata na nakala nyingine kama hiyo ndio iende Bima(yaani Claimed folio na Health facility).

Mfumo inabidi uweze kunyumbulisha level dawa vs prescriber, yaani CO akilog in aweze kuaccess dawa zake pekee bila kuforce kuandika hovyo hovyo kama sasa.

Mfumo pia uweze kuamua aina ya huduma kulingana na jinsia ya la mgonjwa, detail za mgonjwa zikiwa zinasoma ni Ke aweze kupatiwa huduma ya C/S na wala si Me kama CAG alivyogundua. Ishu kama hizi udanganyifu hautakuwepo.

Serikali hii ina mfumo thabiti wa Payroll lakini mfumo wa NHIF ni hovyo kiasi hiki hadi tuanze kunyimwa huduma kizembe hivi. Yaani serikali inamua mfumo gani uwe imara/mzuri na mwingine uwe hovyo hovyo, Daah majanga
 
Malalamiko country...sisi tunaendelea Sana uzuzu kikundi Cha wachache kinafanya watakavyo tunaangalia tu.
 
Na wagonjwa siku hizi tuna-google, ukinitibu hivyo nakuona hufai kwenye taaluma yako na wewe ni kajanja! Nikija kwenye kituo chako na dawa fulani nikakosa najua kituo ni cha wababaishaji, sitajua kuwa haiwezekani kituo kikawa na dawa zote zinazohitajika kwa matibabu. Nikikukuta zahanati au kituo cha afya ukashindwa kunipa pantoprazole nitakushangaa (kumbe inatakiwa kutolewa na MD na wewe ni CO), ukiniambia basi kanunue au lipia unisaidie napiga simu NHIF nawaambia kituo kinanitoza pesa ili kiniibie! Nikija na kidonda Polyclinic na ukakataa kunifanyia dressing napiga simu NHIF kuwaambia mmekataa kunipa huduma mnataka pesa yangu (kumbe dressing haipo kwenye kitita kwa polyclinic).

Mtandao wa NHIF ukisumbua mkaniambia hebu subiri utengamae ili unipe huduma nasonya na kuwaambia nyie ni wababaishaji! halafu napiga simu NHIF kulalamika, NHIF wanakuwa wakali na kutaka mimi na wenzangu tupewe huduma ila tuache kadi. Lahaula tukiondoka na mtandao ukarudi unakuta mimi au mwenzangu kadi zetu zimekuwa rejected na tumeshatibiwa, kama umepata hasara shauri yako NHIF hawatakulipa.

Halafu kuna madaraja ya wagonjwa hatujui, nikija kutibiwa na akaja mwanachama wa fast track kama BOT, NMB au TRA anapitiliza moja kwa moja kwa daktari maalum huku nikiwa nimepanga foleni na wenzangu (naanza kulaumu jinsi watoa huduma walivyo na upendeleo na kujali rushwa) hee, kumbe mwongozo wa NHIF fasttrack anatakiwa apewe upendeleo maalum kwa sababu alilipa NHIF mpunga mrefu! Ghafla naona analazwa chumba cha peke yake na mimi nipo wodi ya jumuiya, nalalamika kwa daktari kwa nini aniweke wodi ya jumuiya wakati mteja mwingine wa NHIF kawekwa private ward. Hatari!!
Kumbe kuna kitita cha Fasttrack a.k.a VIP mko kimya hamsemi...

Hili la mtandao kuzingua mara nyingi inakuwa ni kituo husika kutokuwa na internet imara(limeliona kwa vituo kadhaa vya Afya) ila ukienda vituo vingine au Pharmacy za Bima kule unakuta network iko imara na huduma zinaenda fast.
 
Malalamiko country...sisi tunaendelea Sana uzuzu kikundi Cha wachache kinafanya watakavyo tunaangalia tu.
Sisi ni waoga sana.

Nimeona clips kule Twitter wanaume wa Sri Lanka wanaenjoy kwenye Ikulu yao baada kuivamia, wengine wamejilaza kwenye makochi, wapo wanajikaribisha kwenye kiti maalum cha Rais, wengine wanaoga bafuni,wengine wanapika jikoni, wengine wanaogelea kwenye swimming pool, hawajaishia hapo wengine wakaenda kupiga sarakasi kwenye kitanda Waziri Mkuu. Yaani nimecheka sana, wananchi wanajipooza na machungu yote wanayoyapitia kwa kusherehekea hivyo.

Huku sisi tunaendelea kuchezewa shere na wachache na tuko kimya tu.
 
Hili taifa malalamiko yamezidi kwanini msichukue hatua, hao wahuni wako mnawaona kwanini msiamue liwalo na liwe tu. Nchi hii bila kukinukisha hakutakaa kuwe na nafuu ya maisha hata siku 1 yani. Lazima tusimame kama taifa kupinga ushenzi tunaofanyiwa na viongozi walafi wasio na huruma na mtanzania maskini. ~~Alisikika mlevi mmoja toka jamhuri ya twitter 😀😀😀

Mbona huwa tunaandamana sana humu JF ila kutoka barabarani ndio shughuli..
 
NHIF inapigwa peupe, nimempeleka dogo hosp anabima natumiwa msg na NHIF eti jumla ya matibabu ni tshs. 34,000 ilibd nicheke dawa zenyewe za mafua mbili ambazo pharmacy haizid 10k
emoji23.png
emoji23.png
.

Kuna haja serikali kuunda mfumo bora lasivyo watapigwa sana.
Hahahahah
Mbona huwa tunaandamana sana humu JF ila kutoka barabarani ndio shughuli..
 
NHIF inapigwa peupe, nimempeleka dogo hosp anabima natumiwa msg na NHIF eti jumla ya matibabu ni tshs. 34,000 ilibd nicheke dawa zenyewe za mafua mbili ambazo pharmacy haizid 10k[emoji23][emoji23].

Kuna haja serikali kuunda mfumo bora lasivyo watapigwa sana.
Tatizo la watanzania wanadhani matibabu ni dawa , pekee ,consultants, vipimo kwao sio matibabu
 
  • Thanks
Reactions: RNA
Sisi ni waoga sana.

Nimeona clips kule Twitter wanaume wa Sri Lanka wanaenjoy kwenye Ikulu yao baada kuivamia, wengine wamejilaza kwenye makochi, wapo wanajikaribisha kwenye kiti maalum cha Rais, wengine wanaoga bafuni,wengine wanapika jikoni, wengine wanaogelea kwenye swimming pool, hawajaishia hapo wengine wakaenda kupiga sarakasi kwenye kitanda Waziri Mkuu. Yaani nimecheka sana, wananchi wanajipooza na machungu yote wanayoyapitia kwa kusherehekea hivyo.

Huku sisi tunaendelea kuchezewa shere na wachache na tuko kimya tu.
Sisi tutafika huko Kama kizazi Cha 80-2000 kipite kwanza
 
Kheri yake kuliko mwenzake NSSF ambaye pesa za watu wanagawana barabarani na wafanyakazi wanazichota huku serikali na viongozi wanajengea makasri na kununua magari huku wenyenazo wakizisikia kwa mbali.
Hakuna mwenye afadhali hapo
 
Back
Top Bottom