Serikali na Wasafi TV mlitakiwa muwe mmeshakuchukua hatua za kinidhamu kwa Makonda na Oscar. Ukimya wenu unamaanisha mmebariki udhalilishaji huo?

Serikali na Wasafi TV mlitakiwa muwe mmeshakuchukua hatua za kinidhamu kwa Makonda na Oscar. Ukimya wenu unamaanisha mmebariki udhalilishaji huo?

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Inapotokea mfanyakazi wa taasisi fulani amefanya kosa mbele za umma na akaonywa mbele za umma pia, tunatarajia taasisi anayofanyia kazi kuwajibika, kwanza kwa kukubali kuwa kosa limefanywa, kuomba radhi kwa umma, na kuchukua hatua za kinidhamu kama kanuni za maadili zinavyowaelekeza kulingana na taasisi hiyo.

Kilichofanywa na Oscar Oscar pamoja na Makonda ni udhalilishaji na uvunjivu wa haki za binadamu, Wasafi na Serikali kwanza walitakiwa kukubali kwanza kilichofanyika sio sawa na Serikali kama mtetezi mkuu wa haki za binadamu pamoda na Wasafi kama wadau wanaotetea haki za binadamu ilibidi watoe neno na kumtaka aliyefanya ukiukaji huu aombe radhi kwa umma pamoja na kuwachukulia hatua za kinidhamu.

Lakini inashangaza Oscar Oscar hajatoa neno kuomba radhi na taasisi inayomsimamia nayo imekaa kimya wala haijajigusa. Vivyo hivyo kwa Makonda, amedhalilisha mtu afu anakuja kujitapa hawa wananipiga kelele tu nizidi kusonga mbele na kuwashughulikia wajinga. Hakuna mtu anayekubali uzembe, rushwa wala ubadhilifu, lakini unatakiwa kutumia njia sahihi kufanya hivyo.

Ni aibu, huzuni inatia hasira na kinyaa kwamba mpaka sasa serikali haijatoa tamko lolote kumkanya Makonda na kuomba radhi kwa jambo alilofanya. Mnajenga viongozi wa namna gani? Leo Makonda kafanya hili limenyamaziwa kesho litafanyanika kubwa zaidi, ndio mnataka hii iwe norm? Kwakuwa mtu ana mamlaka basi afanye atakavyo?

Mnakuja na hoja za kijinga na kipumbavu kabisa, eti mbona kuna matukio yalitokea nyuma hayakupigiwa kelele, kwahiyo hilo linafanya jambo alilofanya Makonda kuwa sawa? Kwahivyo kila mtu akidhalilishwa hii ndio itakuwa scapegoat (upenyo wa kuchomokea) na kuhalalisha kosa ulilofanya?

Embu tuweni serious basi, serikali msituangushe tukazidi kupoteza imani na nyie zaidi ya hapa tulipofikia, mnatengeneza bomu ambalo hamtaweza kulitegua mbeleni.

====

Pia soma:
-
LHRC yamuonya Makonda kwa kumdhalilisha Mtumishi wa Kike mbele ya Umati wa Wananchi
- Makonda ashtakiwe kwa udhalilishaji alioufanya kwa mwanakamati huyu
 
Hakuna mtu anayekubali uzembe, rushwa wala ubadhilifu, lakini unatakiwa kutumia njia sahihi kufanya hivyo.
Ingekuwa hakuna mtu anayekubali mambo hayo basi yasingekuwepo humo maofisini na sehemu nyingine za kazi.

Rushwa, uzembe, ufisadi, wizi, nk vimetawala kwa sababu mnabikubali, na kuvijengea kinga kwa kuvitetea kama unavyofanya wewe hapa.

Hatuwezi kuondokana navyo kwa kuteteana na kuoneana haya kwa namna hii.
Hao wanaodai kudharirishwa waende mahakamani wakadai haki zao huko.
 
Ingekuwa hakuna mtu anayekubali mambo hayo basi yasingekuwepo humo maofisini na sehemu nyingine za kazi.
Rushwa, uzembe, ufisadi, wizi, nk vimetawala kwa sababu mnabikubali...
Kabla ya aliyedhalilishwa chombo/taaisisi inatakiwa kutake accountability juu ya kilichofanywa. Mambo hayo kufanyanyika haifanyi hili lililofanywa kuwa sawa, hili limeona zaidi na kupigiwa kelele iwe njia ya kurekebisha na mengine, sio kufumbia mambo na kuendelea kufanya ushenzi
 
Inapotokea mfanyakazi wa taasisi fulani amefanya kosa mbele za umma na akaonywa mbele za umma pia, tunatarajia taasisi anayofanyia kazi kuwajibika, kwanza kwa kukubali kuwa kosa limefanywa, kuomba radhi kwa umma, na kuchukua hatua za kinidhamu kama kanuni za maadili zinavyowaelekeza kulingana na taasisi hiyo...
Paul kasema hivi mambo ambayo hayana maana wananchi wanayashadadia na wakati mama yenu, mwenye watoto na familia alipotukananwa asubui jion mlikua kimya tu.
 
Watz wengi ni wapumbavu tu, Kila siku CAG anakuja na ripoti ma trillion yanaibia watu wako kimya tu, watu wanapiga mabilioni kwa miradi ya kijinga watu wapo kimya tu, bima za afya zinafutwa na kupandishwa Bei kiholela ziii watu wapo kimya tu, nape alikuja na mradi wa zaidi ya bilioni 150 kuweka sijui vibao vya mtaa ambavyo karibia nusu vishavunjika au kufutika majina na havijawahi hata kua msaada wowote watu wapo kimya

Ila Leo Kwa kuwa mtu anaambiwa aache kubana pua kama anaongea na baby wake na kutoa maelezo pesa za walipa Kodi zimeenda wapi ndo watu wanatoka usingizini na kuanza kuhaha Kila kona
 
Achani nogwa
Kwakuwa hakuhusu au haujafanyiwa wewe haimaniishi ni sahihi. Kama huna cha maana cha kusema unakaa kimya tu Mkuu, au mpaka mtu auliwe ndio utahesabu kama ni kosa?

Kila ambacho sio sawa kinatakiwa kukemewa kwa nguvu zote. Inaweza isikukute wewe lakini ikamkuta mume ama mke wako, mama au baba yako, utaendelea kufurahi watendewe hivyo kwakuwa tu alifanya hivyo ana mamlaka ya kufanya hivyo au sababu unamkubali sana aliyetenda ubaya huo?
 
Paul kasema hivi mambo ambayo hayana maana wananchi wanayashadadia na wakati mama yenu, mwenye watoto na familia alipotukananwa asubui jion mlikua kimya tu.
Na mimi nakuuliza, wao kukaa kimya wakati 'mama' yao anatendewa hivyo inahalalisha hili alilotendewa yule dada au upuuzi anaofanya oscar. Kwakuwa kesi fulani ya ubakaji haikufanywa vyema basi watu waendelee kubaka?
 
Na mimi nakuuliza, wao kukaa kimya wakati 'mama' yao anatendewa hivyo inahalalisha hili alilotendewa yule dada au upuuzi anaofanya oscar. Kwakuwa kesi fulani ya ubakaji haikufanywa vyema basi watu waendelee kubaka?
Kamuulize yeye Paul maan mim sitetei ujinga nina watoto pia, nimesema tu alichosema hakuna mana ya kua nakubaliana nae.
 
Kwakuwa hakuhusu au haujafanyiwa wewe haimaniishi ni sahihi. Kama huna cha maana cha kusema unakaa kimya tu Mkuu, au mpaka mtu auliwe ndio utahesabu kama ni kosa? Kila ambacho sio sawa kinatakiwa kukemewa kwa nguvu zote. Inaweza isikukute wewe lakini ikamkuta mume ama mke wako, mama au baba yako, utaendelea kufurahi watendewe hivyo kwakuwa tu alifanya hivyo ana mamlaka ya kufanya hivyo au sababu unamkubali sana aliyetenda ubaya huo?
Kichwa panzi wewe, unamuandikia nani gazeti?
 
Inapotokea mfanyakazi wa taasisi fulani amefanya kosa mbele za umma na akaonywa mbele za umma pia, tunatarajia taasisi anayofanyia kazi kuwajibika, kwanza kwa kukubali kuwa kosa limefanywa, kuomba radhi kwa umma, na kuchukua hatua za kinidhamu kama kanuni za maadili zinavyowaelekeza kulingana na taasisi hiyo.

Kilichofanywa na Oscar Oscar pamoja na Makonda ni udhalilishaji na uvunjivu wa haki za binadamu, Wasafi na Serikali kwanza walitakiwa kukubali kwanza kilichofanyika sio sawa na Serikali kama mtetezi mkuu wa haki za binadamu pamoda na Wasafi kama wadau wanaotetea haki za binadamu ilibidi watoe neno na kumtaka aliyefanya ukiukaji huu aombe radhi kwa umma pamoja na kuwachukulia hatua za kinidhamu.

Lakini inashangaza Oscar Oscar hajatoa neno kuomba radhi na taasisi inayomsimamia nayo imekaa kimya wala haijajigusa. Vivyo hivyo kwa Makonda, amedhalilisha mtu afu anakuja kujitapa hawa wananipiga kelele tu nizidi kusonga mbele na kuwashughulikia wajinga. Hakuna mtu anayekubali uzembe, rushwa wala ubadhilifu, lakini unatakiwa kutumia njia sahihi kufanya hivyo.

Ni aibu, huzuni inatia hasira na kinyaa kwamba mpaka sasa serikali haijatoa tamko lolote kumkanya Makonda na kuomba radhi kwa jambo alilofanya. Mnajenga viongozi wa namna gani? Leo Makonda kafanya hili limenyamaziwa kesho litafanyanika kubwa zaidi, ndio mnataka hii iwe norm? Kwakuwa mtu ana mamlaka basi afanye atakavyo?

Mnakuja na hoja za kijinga na kipumbavu kabisa, eti mbona kuna matukio yalitokea nyuma hayakupigiwa kelele, kwahiyo hilo linafanya jambo alilofanya Makonda kuwa sawa? Kwahivyo kila mtu akidhalilishwa hii ndio itakuwa escape goat (upenyo wa kuchomokea) na kuhalalisha kosa ulilofanya?

Embu tuweni serious basi, serikali msituangushe tukazidi kupoteza imani na nyie zaidi ya hapa tulipofikia, mnatengeneza bomu ambalo hamtaweza kulitegua mbeleni.

====

Pia soma:
-
LHRC yamuonya Makonda kwa kumdhalilisha Mtumishi wa Kike mbele ya Umati wa Wananchi
- Makonda ashtakiwe kwa udhalilishaji alioufanya kwa mwanakamati huyu
Chadema hamnaga kazi ya kufanya mkiamka mnapayuka payuka mpaka jua lizame. Hivi hoja kama hizi zinawaongezeaje kura?
 
If someone hates you can figure something small to prove you guilt ,ukiangalia hii taarifa wala Makonda alikuwa hana lengo la kumzalilisha yule dada, isipokuwa ni namna yule dada injinia alivyokuwa anajibu kwa kutokua serious kwa mambo yanayo wahusu wananchi as if anaongea mambo ya kitchen party au wanatongozana na ndio maana Makonda akaongea vile.
 
Back
Top Bottom