Serikali ondoeni haraka tozo hizi za matengenezo ya nyumba wakati huu wa mvua

Serikali ondoeni haraka tozo hizi za matengenezo ya nyumba wakati huu wa mvua

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Yamenikuta najuta kuwa na kibanda, wiki iliyopita mvua ilinyesha usiku na kubomoa choo cha nyumba yangu cha mtindo wa pasipoti sasa hivi, asubuhi kulipokucha nikaenda kununua simenti na matofali na kuamua kukijenga upya, hamadi serikali ya mtaa kumbe nao wanajua watatupata, wakanidaka.

Baada ya kunifikisha ofisini kwa nikidhani naenda kupewa msaada nikaambiwa ninajenga bila kibali!

Nikajiuliza hiyo mvua imebomoa bila amri ya mahakama mimi naamniwa adhabu yangu nilipe shilingi laki mbili! Sijui nitazitoa wapi huku nikiwaza kwanini wao wasinipe msaada huo lakini jamaa hawna utani nilipe hizo hela.

Hili limenikuta lakini je, ni watanzania wote waliobomokewa na nyumba zao watalipa pesa za kibali cha ujenzi au bahati yangu mimi kuiingizia mapato serikali wakati huu wa mvua?

Nimesimamisha ujenzi na sina choo inabidi nitumie cha jirani wakati wa mchana na usiku kuna lile kopo letu la jadi maarufu kwa jina la sululu.
 
Huna hata panga au sime ndani kwako? Wanataka ukajisaidie wapi kama si kukudhalilisha!
Yaani niwagongee mlango wanifungulie niingie chooni wao wamesimama mlangoni wanasubiri nitoke nawapita mlangoni huku nanukia kale kapafyumu ka vyoo vyetu kisha wafunge mlango wao! Sitawatendea haki.
 
Ujenzi wa choo hauhitaji kibar cha serikali. Labda kama ni ujenzi mwingine
Matengenezo yoyote yale yanahitaji kibali, nenda ofisini kwao utaambiwa hivyo. Hata hivyo ningebomokewa nyumba ingenibidi nilale nje nasubiri kibali, na wale wanaosaidiwa kujengewa baada ya kubomokewa nani anawaombea kibali.
 
Mtaani kwetu mtendaji amewema maspy kila kona. Ukionekana na kakoleo tu au umemwaga mchanga wajomba wanatia timu.
Kujenga fensi, flemu, kupaka rangi au kufanya boresho lolote achilia mbali ujenzi kabisa sharti ulipie kibali, Tena kama ni marekebisho lifespan ya kibali ni mwezi tu baada ya hapo kama ujenzi unaendelea basi utakat na kulipia kipya.

Hatare sana.
 
Mtaani kwetu mtendaji amewema maspy kila kona. Ukionekana na kakoleo tu au umemwaga mchanga wajomba wanatia timu.
Kujenga fensi, flemu, kupaka rangi au kufanya boresho lolote achilia mbali ujenzi kabisa sharti ulipie kibali, Tena kama ni marekebisho lifespan ya kibali ni mwezi tu baada ya hapo kama ujenzi unaendelea basi utakat na kulipia kipya.

Hatare sana.
Mimi nilienda serikali ya mtaa nikawapa 50 wakanipa karatasi lao la kwenda manispaa halafu wakaniambia unaweza kuanza tu. wao ndo masinitch ukishawapa ela imeisha hiyo.
 
We usipate shida,uwe unaenda kuoga na kumaliza haja kwa mwenyekiti.

Usiwe na vurugu kuwampole na kuwaomba mwenyewe ataomba poo
 
We usipate shida,uwe unaenda kuoga na kumaliza haja kwa mwenyekiti.

Usiwe na vurugu kuwampole na kuwaomba mwenyewe ataomba poo
Hili tatizo si kwangu tu, ni wengi mvua zimewaharibia nyumba zao, ila marekebisho yoyote kwa kilichoharibiwa na mvua ni neema kwa serikali.
 
wenyeviti na wajumbe wa serikali za miras ndio chanzo kikubwa cha migogoro ya viwanja na sehemu za wazi hasa sasa hivi karibu na uchaguzi wa serikali za mitaa!
Wanauza sehemu za wazi mpaka sehemu za barabara ili wapate fedha kwani wanaamini wakati huu serikali macho yake yako kwenye uchaguzi na sio kulinda sheria!
Bila kuwathibi sehemu nyingi zitavamiwa na hawa wahuni.
Mfano hai ni Mwenyekiti na wajumbe wa Mbezi Beach “ A”
 
Si wanasema nyumba ni choo, imekuwaje Tena.
Waambie wewe unafanya ukarabati walipize Kama Wana kibali cha ukarabati.
 
Hili suala la kibali serikali iweke mambo sawa hasa huku kwetu uswazi kwa sababu imekuwa kero kubwa sana,ikiwezekana hivyo vibali vya kukarabati hizi nyumba zetu za uswazi vitolewe palepale serikali ya mtaa kwa bei ya kawaida tu ikiwezekana iwe 20,000 au 30,000 tu kuliko ilivyo sasa ambapo unatakiwa uende manispaa ndipo upate kibali baada ya mizunguko mingi isiyokuwa na sababu hali ambayo inaleta usumbufu na kusababisha rushwa.
 
Yamenikuta najuta kuwa na kibanda, wiki iliyopita mvua ilinyesha usiku na kubomoa choo cha nyumba yangu cha mtindo wa pasipoti sasa hivi, asubuhi kulipokucha nikaenda kununua simenti na matofali na kuamua kukijenga upya, hamadi serikali ya mtaa kumbe nao wanajua watatupata, wakanidaka.

Baada ya kunifikisha ofisini kwa nikidhani naenda kupewa msaada nikaambiwa ninajenga bila kibali!

Nikajiuliza hiyo mvua imebomoa bila amri ya mahakama mimi naamniwa adhabu yangu nilipe shilingi laki mbili! Sijui nitazitoa wapi huku nikiwaza kwanini wao wasinipe msaada huo lakini jamaa hawna utani nilipe hizo hela.

Hili limenikuta lakini je, ni watanzania wote waliobomokewa na nyumba zao watalipa pesa za kibali cha ujenzi au bahati yangu mimi kuiingizia mapato serikali wakati huu wa mvua?

Nimesimamisha ujenzi na sina choo inabidi nitumie cha jirani wakati wa mchana na usiku kuna lile kopo letu la jadi maarufu kwa jina la sululu.
Mkuu wewe uko mitaa ipi mimi najipanga kwenda kubadilisha roof yangu nilipigwa na kitu kizito nikauziwa zile mbao za rangi za mikeka sasa wadudu wemefanya makao ikifika usiku unatamani kukuche wanavokereza. Sijajua kama mitaa yangu nako wameshabana kiasi hicho
 
Kumbe mjini kuna haya tena? Mmmhh bora niemdelee kukaa mpigamiti yangu,huku hakuna haya mambo
 
Mkuu wewe uko mitaa ipi mimi najipanga kwenda kubadilisha roof yangu nilipigwa na kitu kizito nikauziwa zile mbao za rangi za mikeka sasa wadudu wemefanya makao ikifika usiku unatamani kukuche wanavokereza. Sijajua kama mitaa yangu nako wameshabana kiasi hicho
Hiyo ni sheria ya manispaa, chochote utakachofanya kuhusu nyumba yako pamoja na hilo kasoro kupiga deki na kufagia lazima upate kibali vinginevyo faini, kwa mvua hizi manispaa itavuna sana kupita kiwango.
Nenda serikali ya mtaa upate kibali vinginevyo faini inakusubiri.
 
Back
Top Bottom