Serikali tatu iko kinyume na natural law of equilibrium

Serikali tatu iko kinyume na natural law of equilibrium

Unafaa kivipi? Ziliungana nchi mbili - Zanzibar na Tanganyika. Halafu zikazaa Tanzania. Kinachoshangaza ghafla Tanganyika ikawa Tanzania Bara lakini Zanzibar ikabaki Zanzibar. Kwanini haikuwa Tanzania Visiwani ili jina Zanzibar nalo life? Sasa ama tuwe na Tanzania Bara na Visiwani au Tanganyika na Zanzibar halafu JMT.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums


Kwahiyo wewe shida yako ni jina tu? Tanganyika imepoteza nini embu nikuulize? Logically muungano wa serikali tatu hauwezekani pasipo muungano kuvunjika. Hatuwezi kuwa na sovereign state ya tanganyika pasipo kuleta mgawanyiko hivi vitu viko in perfect harmony. Hauwezi kuiondoa zanzibar kwenye muungano Tanganyika ikabaki salama na kinyume chake ni sahihi. Hivi vitu viko deep sana mpaka utafakari kwa kina ndio utakapo pata ukweli. Mwalimu nyerere alikuwa yuko sahihi. Na kama tusipo msikiliza tutapata tabu. Believe me you must have spiritual insight to understand this. Lakini sio wajibu wangu kukuaminisha; wajibu wangu kusema ukweli na nimeusema kama mtauchukua au mtaukataa ni juu yenu..
 
Kwa wanaodai serikali tatu naomba watambue iko kinyume na natural law of equlibrium hakuna uwezekano wowote serikali hizo kufanya kazi bila muungano kuvunjika. Hakutakuwepo ''balance of power'' Collision itakuwepo kati ya raisi wa Tanganyika NA YULE WA MUUNGANO. Hakutakuwa na harmonization yeyote. Wanaodai serikali tatu either ni wajinga au wana ajenda ya kuvunja muungano wanaogopa kuiweka wazi. Tatizo litakalo zuia balance hii of power ni udogo wa zanzibar, ingekuwa kenya na Tanzania zimeungana Muungano wa serikali tatu ungekuwa possible. Kwahiyo nakubaliana na muungano uliopo kwa asilimia zote kwakuwa unagusa mantiki ya fikra.

I thought kwamba ungeileta tu hoja yako kiungwana ili waungwana tuijadili kistaarabu tu kwa kila mtu kutoa sababu za kuunga au kupinga muundo huo kwani mwisho wa siku lolote laweza kupita......pengine hichohicho kinachoaminiwa na unaowaita wajinga!!.....Kwako wewe hata kina Warioba na wenzake wote ktk tume na wale wote waliootoa maoni yao ktk tume na kuuona kuwa na muundo wa serikali 3 ni mwafaka kwa sasa ni WAJINGA na hawautakii mema Muungano!!

Lakini wewe kuwaita walio kinyume na wewe/mawazo/mtazamo wako kuwa ni WAJINGA ni kulazimisha mambo kwa interest zako na maana hiyo binafsi sitakuwa na makosa kusema kuwa wewe pia ni MJINGA TU TENA ZAIDI kwa sababu tu unaamini ktk hicho unachoaamini kinyume na wengine!!!

Tushindane kwa HOJA si kwa kubezana na kwa matusi,THAT'S MY POINT!.
 
I thought kwamba ungeileta tu hoja yako kiungwana ili waungwana tuijadili kistaarabu tu kwa kila mtu kutoa sababu za kuunga au kupinga muundo huo kwani mwisho wa siku lolote laweza kupita......pengine hichohicho kinachoaminiwa na unaowaita wajinga!!.....Kwako wewe hata kina Warioba na wenzake wote ktk tume na wale wote waliootoa maoni yao ktk tume na kuuona kuwa na muundo wa serikali 3 ni mwafaka kwa sasa ni WAJINGA na hawautakii mema Muungano!!




Lakini wewe kuwaita walio kinyume na wewe/mawazo/mtazamo wako kuwa ni WAJINGA ni kulazimisha mambo kwa interest zako na maana hiyo binafsi sitakuwa na makosa kusema kuwa wewe pia ni MJINGA TU TENA ZAIDI kwa sababu tu unaamini ktk hicho unachoaamini kinyume na wengine!!!

Tushindane kwa HOJA si kwa kubezana na kwa matusi,THAT'S MY POINT!.


Kwanza ujinga sio tusi nataka ujue ni kutokuwa na ufahamu wa kutosha kuhusu jambo fulani kila mtu ana ujinga katika jambo fulani. Mimi sifahamu kila kitu. Kwahiyo napenda ujue hivyo ujinga sio tusi ni kukosa maarifa kuhusu jambo fulani.
 
Asichoelekea kuelewa ndugu yetu mleta mada ni kwamba,hakuna kati yetu,akiwemo yeye,ambaye ni mmiliki wa ''ukweli'' ikiwemo hata mada hii kwa kuwa imetawala siasa za Tanzania kwa miongo kadhaa na wala hakuna dalili kwamba mjadala utakoma mara baada ya ''Katiba Mpya'' .Anadai,mahali fulani,kwamba "nitausimamia ukweli"!!Hata hivyo 'ukweli''hutafutwa na hutafutwa kwa kushindanisha mawazo na hoja,wakati mwingine hata zile zisizovutia masikioni.Wengine tunaaamini katika ''serikali tatu'' kama jawabu la umbali mafupi,kwa lengo la kuweka mazingira ya ''serikali moja'', kama jawabu la umbali mrefu.
Tunamuhimiza mleta mada wetu na wengine wenye mawazo kama yake,kwamba aendelee na mawazo ya kale ya ''kuushikilia na kuusimamia ukweli'' wake!Sisi wengine ''tunashikilia na kusimamia maoni na mitazamo'' yetu.Sasa,kama tayari wengine wana ''ukweli'' wao,kuna haja gani,basi,ya kuendelea kujadili?Ili iweje?Kama umedhamiria kuleta hoja jamvini tafsiri rahisi ni kwamba umeingia katika shughuli nzito na pevu ya ''kuusaka ukweli''.Ingefaa mno tukumbuke kwamba hakuna mwenye ''kweli'' yote.Socrate hakuimaliza kazi ya kuisaka kweli.Wala Aristotle hakuihitimisha kazi hiyo.
Mwisho,sifa moja muhimu ya kushiriki mijadala ya namna hii ni utayari wa kuheshimu mawazo ya watu wengine.
 
Kwa wanaodai serikali tatu naomba watambue iko kinyume na natural law of equlibrium hakuna uwezekano wowote serikali hizo kufanya kazi bila muungano kuvunjika. Hakutakuwepo ''balance of power'' Collision itakuwepo kati ya raisi wa Tanganyika NA YULE WA MUUNGANO. Hakutakuwa na harmonization yeyote. Wanaodai serikali tatu either ni wajinga au wana ajenda ya kuvunja muungano wanaogopa kuiweka wazi. Tatizo litakalo zuia balance hii of power ni udogo wa zanzibar, ingekuwa kenya na Tanzania zimeungana Muungano wa serikali tatu ungekuwa possible. Kwahiyo nakubaliana na muungano uliopo kwa asilimia zote kwakuwa unagusa mantiki ya fikra.
Shayu usiache kuangalia hoja na maswali ambayo niliuliza kwenye thread hii: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...wa-nchi-mbili-mojawapo-haipo.html#post6882313 , ningependa kujua mawazo yako kwa hoja hii unayouisema.
 
Asichoelekea kuelewa ndugu yetu mleta mada ni kwamba,hakuna kati yetu,akiwemo yeye,ambaye ni mmiliki wa ''ukweli'' ikiwemo hata mada hii kwa kuwa imetawala siasa za Tanzania kwa miongo kadhaa na wala hakuna dalili kwamba mjadala utakoma mara baada ya ''Katiba Mpya'' .Anadai,mahali fulani,kwamba "nitausimamia ukweli"!!Hata hivyo 'ukweli''hutafutwa na hutafutwa kwa kushindanisha mawazo na hoja,wakati mwingine hata zile zisizovutia masikioni.Wengine tunaaamini katika ''serikali tatu'' kama jawabu la umbali mafupi,kwa lengo la kuweka mazingira ya ''serikali moja'', kama jawabu la umbali mrefu.
Tunamuhimiza mleta mada wetu na wengine wenye mawazo kama yake,kwamba aendelee na mawazo ya kale ya ''kuushikilia na kuusimamia ukweli'' wake!Sisi wengine ''tunashikilia na kusimamia maoni na mitazamo'' yetu.Sasa,kama tayari wengine wana ''ukweli'' wao,kuna haja gani,basi,ya kuendelea kujadili?Ili iweje?Kama umedhamiria kuleta hoja jamvini tafsiri rahisi ni kwamba umeingia katika shughuli nzito na pevu ya ''kuusaka ukweli''.Ingefaa mno tukumbuke kwamba hakuna mwenye ''kweli'' yote.Socrate hakuimaliza kazi ya kuisaka kweli.Wala Aristotle hakuihitimisha kazi hiyo.
Mwisho,sifa moja muhimu ya kushiriki mijadala ya namna hii ni utayari wa kuheshimu mawazo ya watu wengine.

Naomba uniambie serikali hizi tatu zitafanyaje kazi, njoo na structure ya muungano huo wa serikali tatu utakavyofanya kazi bila kusababisha serikali ya muungano kuanguka.
 
Kwa wanaodai serikali tatu naomba watambue iko kinyume na natural law of equlibrium hakuna uwezekano wowote serikali hizo kufanya kazi bila muungano kuvunjika. Hakutakuwepo ''balance of power'' Collision itakuwepo kati ya raisi wa Tanganyika NA YULE WA MUUNGANO. Hakutakuwa na harmonization yeyote. Wanaodai serikali tatu either ni wajinga au wana ajenda ya kuvunja muungano wanaogopa kuiweka wazi. Tatizo litakalo zuia balance hii of power ni udogo wa zanzibar, ingekuwa kenya na Tanzania zimeungana Muungano wa serikali tatu ungekuwa possible. Kwahiyo nakubaliana na muungano uliopo kwa asilimia zote kwakuwa unagusa mantiki ya fikra.

Mimi nadai serikali tatu lakini nakuhakikishia si mjinga bali nahisi wewe ni zumbukuku. Hebu ona hiyo hapo kwenye Bold, huo ndio upeo wa fikira zako? Kwani unazungumzia ukoloni au Muungano?
 
mjomba umesema kweli wanaotaka serikali tatu hawana nia njema, ni wabinafsi.

Naam ni ubinafsi wa kitaifa ndio maana huyo msomi juu akashindwa kuelewa maana ya muungano.
 
Watanganyika mnapenda muungano kuliko kitu chochote hata kama muungano huo hauna faida yoyote lakini mutaupenda,mliuzika hai utaifa wenu kwa kupenda muungano na mpo tayari kuigawa ardhi yenu kwa kupenda muungano,hivi mnapata faida gani kwenye haya mazingaombwe ya muungano huu?

Huwa najiuliza kila siku nini hasa faida ya muungano huu ikiwa kila upande unalalamika? Kwa roho radhi mwenye kuzijuwa faida zilizopo atumwagie hapa huenda tukabadili mitazamo!
 
Kwahiyo wewe shida yako ni jina tu? Tanganyika imepoteza nini embu nikuulize? Logically muungano wa serikali tatu hauwezekani pasipo muungano kuvunjika. Hatuwezi kuwa na sovereign state ya tanganyika pasipo kuleta mgawanyiko hivi vitu viko in perfect harmony. Hauwezi kuiondoa zanzibar kwenye muungano Tanganyika ikabaki salama na kinyume chake ni sahihi. Hivi vitu viko deep sana mpaka utafakari kwa kina ndio utakapo pata ukweli. Mwalimu nyerere alikuwa yuko sahihi. Na kama tusipo msikiliza tutapata tabu. Believe me you must have spiritual insight to understand this. Lakini sio wajibu wangu kukuaminisha; wajibu wangu kusema ukweli na nimeusema kama mtauchukua au mtaukataa ni juu yenu..

Kwani muungano ni chuma, gogo au metal gani kuwa lazima uvunjike kwa kukosa balance? Muungano ni will na hadi sasa upo si kwa kuwa kuna balance lakini bado ipo will, na iwapo hakuna will miongoni mwetu basi hauna faida kwani binaadamu hufanya kitu kwa faida.Iwapo utavunjika haitokuwa wa kwanza kwani hata Taifa kubwa la Urusi lilipitia hilo na tena for the best ever!
 
Kwanza ujinga sio tusi nataka ujue ni kutokuwa na ufahamu wa kutosha kuhusu jambo fulani kila mtu ana ujinga katika jambo fulani. Mimi sifahamu kila kitu. Kwahiyo napenda ujue hivyo ujinga sio tusi ni kukosa maarifa kuhusu jambo fulani.

Kitaturu uko sahihi, iwapo yeye anahisi ni sifa kuambiwa mjinga, lakini bwana Shayu wakati mwwengine binaadamu hatuna sifa moja hivyo hiyo sifa nzuri ya ujinga haipaswi kupewa sote, bakia nayo mwenyewe!
 
Naomba uniambie serikali hizi tatu zitafanyaje kazi, njoo na structure ya muungano huo wa serikali tatu utakavyofanya kazi bila kusababisha serikali ya muungano kuanguka.

Kwani hii ya mtazamo wako imesimama? mjadala wa nini basi kama kitu kimesimama sawsawa?
 
Kwa nini watanganyika hawawezi kuungana na nchi nyengine zaidi ya zanzibr?
 
Kwa wanaodai serikali tatu naomba watambue iko kinyume na natural law of equlibrium hakuna uwezekano wowote serikali hizo kufanya kazi bila muungano kuvunjika. Hakutakuwepo ''balance of power'' Collision itakuwepo kati ya raisi wa Tanganyika NA YULE WA MUUNGANO. Hakutakuwa na harmonization yeyote. Wanaodai serikali tatu either ni wajinga au wana ajenda ya kuvunja muungano wanaogopa kuiweka wazi. Tatizo litakalo zuia balance hii of power ni udogo wa zanzibar, ingekuwa kenya na Tanzania zimeungana Muungano wa serikali tatu ungekuwa possible. Kwahiyo nakubaliana na muungano uliopo kwa asilimia zote kwakuwa unagusa mantiki ya fikra.

Soma hii mada. link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/334649-tundu-lissu-na-kiinimacho-cha-muungano.html Pia soma hili andiko : Tume ya Warioba imefanya madudu kwa kuleta rasimu ya Katiba yenye kupendekeza serikali tatu.

Mwaka 1994, Mwasisi wa muungano alisema haya:

Kwa kweli hata kesho Nchi za Afrika ya Mashariki zikiamua kuungana, na Tanzania ikawa ni mshiriki, naamini kuwa ni rahisi zaidi kushirikisha Tanzania yenye Serikali Mbili - ya Zanzibar na ya Tanganyika - kuliko Tanzania yenye Serikali Mbili, ya Tanzania na ya Zanzibar.Uk 11-12 link Uongozi Wetu Na Hatma Ya Tanzania (by Nyerere) Unaweza kusoma uk 10-12 ili kupata maarifa zaidi.
Hatuhitaji serikali ya Muungano wala katiba ya Muungano.

Tunachokihitaji ni serikali ya Tanganyika na katiba ya Tanganyika tu.
Mwalimu alisharidhia kuuvunja muungano kwa njia ya kistaarabu.
Mamlaka kamili kwa Tanganyika(Tanganyika huru) na mamlaka kamili kwa Zanzibar (Zanzibar huru). Mkutano,muungano,ushirikiano, udugu, ujomba na ushangazi ni kupitia SADC, EAC, UN na baadae kwenye Shirikisho la Afrika Mashariki.

Nini kinatupelekea kupoteza muda na fedha za walalahoi kwa kujadili Katiba ya Muungano ambayo haina umuhimu wowote?
 
Nitaerndelea kujadili kama mtakubali ku argue bili kutumia emotional...Law of equilibrium ziko nyingi una nishangaza kwakuwa wewe ni daktari khalafu una reason namna hiyo.

kati ya hizo laws of equilibrium nyingi ,which one has direct relevance to the union?
 
AuB=n(A)+n(B)-n(AnB)'
where AUB= Muungano
B= zenji
A= Tanganyika
n(AnB)= tanganyika na zenji
hence muungano wa serikali tatu unawezekana
 
Back
Top Bottom