Serikali, TFF, Bodi ya Ligi na TAKUKURU; Kwa uhuni huu wa GSM ile "Fair Competition" inayotakiwa na FIFA ipo wapi?

Utopolo acheni kuwapa hela wachezaji wa timu inayocheza na Simba ili wavunje wachezaji wa Simba tafuteni Ubingwa kwa Fair Play sio kutoa rushwa
 
"GSM wanawapa timu ndogo hela ili wawakazie Simba", alisikika Great Thinker wa jf.

Pia Jwaneng Galaxy walipewa mbinu na Manara ili wawafunge Simba, dah nchi ngumu hii.
Manara ndio alimwambia Wawa asiwe anapiga mipira ya kichwa? Simba tulieni msuke kikosi. Pia dhambi ya kuwaweka benchi Kagere na Ajibu itawatafuna sana.
 
Achana nao hawana akili Hawa. Ndio maana mwenyekiti wao (ismael Aden Rage) akiwahi kuwaita Mbumbumbu
 
Kimeumana
 
Tunachosikitika ni kukamiwa kwa kufanyiwa rafu nyingi sana.
Ona rafu aliyofanyiwa Kapombe na Kibu Dennis.
Kila mechi lazima Wachezaji wa Simba waumizwe vibaya.
Kama kukamiwa kwa soka la fair play haina shida kabisa.
Mechi tano tayari kuna majeruhi ya hatari sita.
 
Unawivu wa kike ndugu, punguza wivu upate afya
 
Hili bandiko io la Kindezi sana baada kushindwa mpira sasa mnatafuta pa kutokea

GSM Inaithamini kupigwa product yake hii ni biashara, kama sport pesa, Emirates na kadhalika.

Bakharesa anamiliki timu hapo hapo anadhamini ligi kwa ujumla wake hilo hujaliona, acheni wivu usio na mashiko

Hata simba mkitaka GSM inaweza kuwadhini Simba

Mini nafikiri angalieni mahali timu yenu inapokosea kuliko kupoteza muda kuisakama Yanga.
 
Ama kweli Aden Rage hakukosea aliposema mashabiki wa Makolo ni Mbumbumbu:-

GSM hawajaanza kudhamini hivyo vilabu leo, sasa hiyo fair competition imeanza sasa?

Halafu eti wamefanya udhamini kwa siri...

Ingekuwa siri, media zingeripoti?!

Kusoma hujui, ina maana hatapicha za logo za GSM huzioni kwenye jezi?!

Unadhamini vipi kwa siri halafu hapo hapo unaweka logo yakoopenly ?

Btw, hivi unatakiwa kukumbushwa kwamba pamoja na udhamini huo wa GSM, bado Yanga msimu uliopita walipigwa na Coastal, tena kwenye mechi muhimu kweli kweli?!

Au wewe ni mfuatiliaji wa soka la Instagram?
Hao walioko serikalini sio mbumbumbu kama mashabiki wa Makolo!
Povu na matusi yote ya nini, Kolo?!

Azam Media wana Content Contract na Yanga...

Azam FC na Azam Media ni baba mmoja, mama mmoja...

Nini Kolo kinakufanya uone GSM kudhamini Yanga na Coastal ni Upumbavu unaofumbiwa macho lakini unaona sawa kwa Azam kufanya kitu kile kile?! Au kwa sababu na Makolo mnanufaika na Azam?

Kweli we Kolo...

Kwahiyo Azam Media iliyoingia mkataba wa content na Yanga, hapo Yanga wamehongwa?!
Kama GSM kweli walikuwa na nia ya Kuvidhamini Vilabu vya Ligi Kuu ya Tanzania NBC PREMIER LEAGUE walikuwa wapi Kujitokeza pale TFF na Bodi ya Ligi walipokuwa wanatafuta Wadhamini?
Umeanza lini kufuatilia soka kiasi kwamba unashindwa kutofautisha kati ya mdhamini wa ligi na mdhamini wa vilabu?
Ndo tatizo la kuwa na Think Tank Shaffii Dauda
Hapa ndo umethibitisha ile kauli ya Aden Rage...

Dhambi ni kuhonga wachezaji au kuhonga waamuzi ili wahujumu mchezo lakini hakuna dhambi yoyote kuwapa motisha wachezaji...

Btw, mechi mbili mlipata goli dakika ya 99 kwa sababu wachezaji wa timu pinzani waliahidiwa pesa na GSM; vipi kuhusu zile 3 mlizotandikwa pale Mkapa na timu ambayo nchini kwao ligi imemesimama kwa zaidi ya miezi 18?

Hivi kule Morocco ambako mliweka kambi, mkafikia kucheza hadi na timu ya daraja la 3; mlishinda mechi ngapi kule?

Msimu uliopita mlishinda mechi ngapi ambazo Chama hakuwepo uwanjani?

GSM wameshaiharibu Ligi Kuu ya NBC.
Ina maana GSM ndo anawafanya muwe mnashinda kwa mbinde, au?

Ni GSM nde anawafanya mfungaji wenu pekee mnayemtegemea muwe mnamuingiza dakika 30 za mwisho, au?

Au ndo nyie ambae Think Tank wenu ni Shaffi Dauda?!

Nimekuwekea hapo YouTube link inayoonesha GSM amekuwa akividhamini hivyo vilabu tangu msimu uliopita, lakini kwavile watu wenyewe nyinyi ni "hoya hoyaa" ndo mnazadhani huo udhamini umeanza mwaka huu, huku bila aibu ukisema eti kawadhamini kisirisiri!!
 
Kwahiyo hayo Makolo yatajipanga vizuri kupitia hoja zipi?

Kwamba wamekamiwa na timu zinazodhaminiwa na GSM, au?!

Dah... nilikuwa sifahamu kwamba Shabiki wa Makolo ni Janga la Taifa!!
 
 
Kwa mtu anaeujua mpira hawezi kusema SIMBA ni mbovu. Ni kauli za wale mashabiki vitumbua.

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…