ozone layer
JF-Expert Member
- Oct 27, 2021
- 471
- 1,935
Polisi wangeweza kutowafanya kitu, ila kumpora mtu simu yake akipata mwanasheria mzuri akiunganisha na vingine ulimpora, kutumua ofisi yako kama tegesheo la kupora watu vitu basi ingekuwa kesi kubwa au anehonga sana zaid ya hiyo 1mKwani ungepeleka hizo details police ndio wangekuja kuwafanya Nini hao jamaa?Kuwatishia/kuwafunga au?
Mpakistani hakupi 1mil kizembe namna hio.
Kazi yako ni ubishi tu . Soma ueleweKwani ungepeleka hizo details police ndio wangekuja kuwafanya Nini hao jamaa?Kuwatishia/kuwafunga au?
Mpakistani hakupi 1mil kizembe namna hio.
Tuma salamu kwa watu watatu tafadhali.Kazi yako ni ubishi tu . Soma uelewe
Ninachojuwa Mimi gari used kitu muhimu sana ni engine na body, jitahidi kumlipa Fundi mkweli uende naye kununuwa gari kuna technical kadhaa za kuangalia.Serikali itupie macho uhuni unaofanywa na hawa wafanyabiashara wa magari wenye asili ya Pakistan.
Jana mida ya saa sita mchana tulienda na rafiki yangu kwenye moja ya maduka (yard) ya kuuzia magari. Rafiki yangu alikuwa anataka Toyota Probox kwa ajili ya kubebea mizigo yake Kariakoo na kwenye godown yake.
Tukafika hiyo saa sita tukakuta magari ndiyo yanapangwa. Walivyomaliza tukaomba kukagua gari moja. Kijana akaitwa akaja mbio na funguo za gari zikiwa mkononi kwake.
Nikakaa kwenye usukani na rafiki yangu pembeni. Nilipoiweka gari switch on nikakuta odometer inasoma gari imetembea kilometa 219,551. Bei milioni 16
Tukashauriana tukasema hapana hili gari halifai. Tukaendelea duka jingine na jingine na jingine.
By saa tisa tukafudi tena kwenye ile Probox, tukakuta ishachezewa odometer, sasa inaonekana imetembea kilometa 46,755.
Nilikuwa nimeoiga picha chasis namba mlangoni na dashboard. Nikipowauliza mbona hii gari mmeichezea kilometa, nikawaonyesha na picha wakakasirika sana wakapora simu yangu. Nikawaambia kaeni nayo, leo mtalala polisi.
Nikawa naondoka kulekea kwenye gari tuliyokuja nayo hapo yard, ndipo mmoja ya wafanyabiashara wale akaja mbio huku akinibembeleza nifute zile picha watatupa million moja.
Hela tamu, tukakubali kufuta picha, tukabeba milioni yetu. Tukaondoka.
Lakini backyard ya hizo yard zote kuna mafundi wako busy wanayaweka sawa mamikweche hayo.
Kingine tulichogundua ni kwamba kwenye minada ya magari, magari ya nauzwa kwa classes. Hawa wanachagua class duni kabisa, yakifika hapa wanaongea vizuri na wakaguzi, wanatolewa bandarini.
Kwa somo hili tulilojifunza jana rafiki yangu amekata tamaa kabisa na magari haya. Sasa kaona bora aagize kutoka Japan 🗾 asubiri siku 45 abebe mwana wake wa uhakika
Hata mleta mada kasema alifika saa sita akarudi tisaKurudisha Odometer sio zoezi la saa moja. Ni zoezi la muda kidogo.
Jan Motors wao hawa gari zao utaikuta kama ilivyo na bei zao ziko chini, hivyo watu huenda kwao wananunua afu wanaenda uza tena
Hapo kwa wewe kupewa mil 1 ni uongo...wewe una price tag gan? Ungekuwa na price tag kubwa usinge enda kuulizia gari low classes kama hizo. Acha uongo!Kila mtu ana price tag yake. Hata Waswahili wanausemi:-
Vidole havifanani
Wa mbili havai moja.
Ukiwa cheap wewe ni wa hivyo hivyo tu
Hata ndani ya hayo masaa motor haiwezi rudisha km 170,000 nyumaHata mleta mada kasema alifika saa sita akarudi tisa
Huo mkwanja alilamba baada ya wadosi kugundua kuwa kuchukua simu ya mtu ni jinai, mbona mnakuwa wagumu kuelewa? Chukulia alikuwa na Samsung ZHapo kwa wewe kupewa mil 1 ni uongo...wewe una price tag gan? Ungekuwa na price tag kubwa usinge enda kuulizia gari low classes kama hizo. Acha uongo!
Haya basi tufanye kuwa hawarudishi kilometa nyumaHata ndani ya hayo masaa motor haiwezi rudisha km 170,000 nyuma
Magufuli alipendaga kuita vita vya kiuchumi.😀😀Hapo kwa wewe kupewa mil 1 ni uongo...wewe una price tag gan? Ungekuwa na price tag kubwa usinge enda kuulizia gari low classes kama hizo. Acha uongo!
JABA ilikuwa ya Ditopile kama sikosei.Aisee, mi sijui kwanini kuanzia enzi za JABA, baba alioouziwa gari bovu magari ya yard nayaogopa sana
Haina shida ya crankshaft sema walimuuzia imechoka hivyo anarekebisha hiki kinaharibika hikiHajachonga crankshaft bado?
LC hilo litaishi umri wa mtu mzima,Ni uhakika.Haina shida ya crankshaft sema walimuuzia imechoka hivyo anarekebisha hiki kinaharibika hiki
Ndo magari Yao wazee hawataki sedanLC hilo litaishi umri wa mtu mzima,Ni uhakika.
AiseeKurudisha Odometer sio zoezi la saa moja. Ni zoezi la muda kidogo.
Jan Motors wao hawa gari zao utaikuta kama ilivyo na bei zao ziko chini, hivyo watu huenda kwao wananunua afu wanaenda uza tena
Basi iko vizuri sana, najua gari ikianza kuchongwa crankshaft engine ndio imefika Kigoma mwisho wa reliHaina shida ya crankshaft sema walimuuzia imechoka hivyo anarekebisha hiki kinaharibika hiki
😄😄 Wengi wanaonaga SUV Ni Gari za heshima/kifahari, saloon zote wanaonaga Ni Taxi tu.Ndo magari Yao wazee hawataki sedan