Serikali ya Ghana yamuiga Rais Samia kuanzisha Tozo ya Miamala. Wabunge watwangana Makonde

Serikali ya Ghana yamuiga Rais Samia kuanzisha Tozo ya Miamala. Wabunge watwangana Makonde

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Hii ndo maana sahihi ya Muongoza njia. Hatimaye Serikali ya Ghana imemuiga Mama asiye na maneno mengi bali matendo mengi, asiye na mbwembwe za kujitangaza hovyo na promo za kijinga anayependa vitu kwenda kwa usahihi na kupata matokeo sahihi, Si mwingine ni Rais Wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha tozo ya miamala ya simu

Piga kazi Samia. Unayofanya Tanzania sasa yanaanza kuigwa nje. Afrika bila kujitoa Kweli hatuwezi kufika. Hata Ghana tozo zinapingwa na upinzani Ila Serikali wameona ndo njia sahihi.

Lazima tulipe kodi kwa maendeleo yetu!

922EE760-B66C-4C3F-956F-5CE72BAFADB2.jpeg


-===========

Wabunge nchini Ghana wamelazimika kutwangana makonde bungeni baada ya kutokea ubishani wakati wa mjadala juu ya sheria ya tozo ya miamala ya kidigitali.

Ugomvi huo ulianza baada ya Mbunge wa Upinzani kumzuia Msaidizi wa Spika kunyanyuka kwenda kupiga kura. Chama cha Upinzani cha NDC kinapinga mapendekezo ya tozo ya 1.75% kwa miamala ya kidigitali kikidai kuwa tozo hizo zitaathiri watu wa kipato cha chini.

Waziri wa Fedha wa nchi hiyo amesema tozo hizo zitasaidia kuongeza makusanyo ya kodi kufikia cedi bilioni 6.9 (zaidi ya Tsh. trilioni 2.3). Kikao cha bunge kililazimika kuahirishwa baada ya vurugu hizo kutokea.
 
Nabii hakubaliki kwao. Tuna raisi bora, mwenye maono, mpenda maendeleo na mtatuaji wa kero na shida za Watanzania. Ila kuna kundi la wavuta bangi, wanywa gongo na viloba wanajaribu kumchafua na kujifanya hawayaoni mazuri anayoyafanya, kisa tu mshika akili wao kawekwa ndani.
 
Hii ndo maana sahihi ya Muongoza njia. Hatimaye Serikali ya Ghana imemuiga Mama asiye na maneno mengi bali matendo mengi, asiye na mbwembwe za kujitangaza hovyo na promo za kijinga anayependa vitu kwenda kwa usahihi na kupata matokeo sahihi, Si mwingine ni Rais Wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha tozo ya miamala ya simu

Piga kazi Samia. Unayofanya Tanzania sasa yanaanza kuigwa nje. Afrika bila kujitoa Kweli hatuwezi kufika. Hata Ghana tozo zinapingwa na upinzani Ila Serikali wameona ndo njia sahihi.

Lazima tulipe kodi kwa maendeleo yetu!

View attachment 2052727
Tanzania sio nchi ya kwanza kuwa na tozo za miamala. Huko Cameroon wanatoza siku nyingi. Congo Brazzaville pia
 
Hii ndo maana sahihi ya Muongoza njia. Hatimaye Serikali ya Ghana imemuiga Mama asiye na maneno mengi bali matendo mengi, asiye na mbwembwe za kujitangaza hovyo na promo za kijinga anayependa vitu kwenda kwa usahihi na kupata matokeo sahihi, Si mwingine ni Rais Wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha tozo ya miamala ya simu

Piga kazi Samia. Unayofanya Tanzania sasa yanaanza kuigwa nje. Afrika bila kujitoa Kweli hatuwezi kufika. Hata Ghana tozo zinapingwa na upinzani Ila Serikali wameona ndo njia sahihi.

Lazima tulipe kodi kwa maendeleo yetu!

View attachment 2052727
Baada ya Mwendazake kuingiza nchi kwenye mzigo wa madeni,Samia hakua na options zaidi ya tozo ..

Ghana nayo iko hoi kwa madeni kwa hiyo lazima walipe.Hali iko hivi 👇

Screenshot_20211113-134557.png
 
Nabii hakubaliki kwao. Tuna raisi bora, mwenye maono, mpenda maendeleo na mtatuaji wa kero na shida za Watanzania. Ila kuna kundi la wavuta bangi, wanywa gongo na viloba wanajaribu kumchafua, kisa tu mshika akili wao kawekwa ndani.
Wanaomchafua Samia Sio hao unaodhani, hao unaodhani wengi wao wanamuunga mkono! Samia anachafuliwa na waliokuwa wafuasi wa Marehemu, ambao wanalazimisha Samia atawale "exactly" kama alivyokuwa anatawala jamaa yao, jambo ambalo haliwezekani
 
Baada ya Mwendazake kuingiza nchi kwenye mzigo wa madeni,Samia hakua na options zaidi ya tozo ..

Ghana nayo iko hoi kwa madeni kwa hiyo lazima walipe.Hali iko hivi [emoji116]

View attachment 2052739
Ikiwa nchi ina madeni makubwa imekuwaje tena Samia ndani ya muda mfupi kakopa sana, tena kwa miezi 7 kakopa nusu ya alichokopa jiwe
 
Back
Top Bottom