Serikali ya Kenya imepiga marufuku shule za bweni kwa ngazi ya msingi, sisi ndiyo kwanza tunakumbatia

Serikali ya Kenya imepiga marufuku shule za bweni kwa ngazi ya msingi, sisi ndiyo kwanza tunakumbatia

Kupeleka mtoto mdogo boarding ni kumtenga, kumnyanyapaa

Wazazi tusikwepe majukumu yetu ya kulea watoto.

Boarding school sio mbaya lakini basi angalau ianzie secondary level

Unapeleka mtoto boarding eti akafundishwe na mwalimu kupiga mswaki, afundishwe kuoga, sujui nini, hapo bado mtoto hajaumwa eti mwalimu ndo akae na mtoto, hivi nyie mnaotetea watoto wadogo kwenda boarding school ni wendawazimu kabisa..

Kibaya zaidi hao watoto hawajakutana na watoto wenzao watukutuku wakawafanyia michezo mibaya.

Kaeni na watoto wenu waleeni, wapeni malezi ya baba na mama kwa ukaribu jueni tabia zao, mapendeleo yao na mengine mengi

Wazazi wa siku hizi wanaobebea watoto mbele badala ya mgongoni ndo wanakaza fuvu kuwatupa watoto wao boarding school

Kwa hili nampongeza ruto, japo namkubali ODINGA
 
naunga mkono asilimia 99, ijapokuwa kuna waajiriwa /wafanyabiashara wanaosafiri sana na wanapata shida kuwaachia watoto wadada/kaka /ndugu wa karibuu mida hawapo homendo

naunga mkono asilimia 99, ijapokuwa kuna waajiriwa /wafanyabiashara wanaosafiri sana na wanapata shida kuwaachia watoto wadada/kaka /ndugu wa karibuu mida hawapo home
Ndio maana kuna useja. Kama huwezi kujilelea watoto haukulidhi vigezo vya kuzaa.
 
MPAKA SASA KUNA WATU WANA AMINI KULIPA GHARAMA KUBWA ZA BOARDING NDIO ISHARA YA UBORA WA HUDUMA!
JE UMEWAHI FANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HUKO ANAKO SOMA MTOTO WAKO?
KAMA MTOTO WA KWENDA NA KURUDI NA BADO ANABAKWA NA WATU WAZIMA WAWILI KWA MIEZI MINGI BILA MZAZI KUJUA , JE WA HUKO BWENI WANA USALAMA GANI?

NINA USHUHUDA WA KWELI, NDUGU WA KARIBU ALIPELEKA MTOTO WAKE WA MIAKA 4!KUSOMA SHULE YA BWENI HAPA DSM, SHULE IKO MBAGALA NA INA JINA KUBWA TU YA MAMA MCHUNGAJI.SABABU BABA YUKO BIZE NA MAMA YUKO BIZE PIA NA WANA FEDHA. NA WAKATI ULE SHULE ILIKUWA NA JINA KUBWA KIASI ILIONEKANA NI SIFA MTOTO KUMPELEKA PALE.
BAADA YA MWAKA, MTOTO ALIHAMISHWA KWA SBB WATOTO WAKUBWA, WANA WAINGILIA WATOTO WADOGO WANAO LALA NAO!
KAMA UNA SBB ZOZOTE ZA KUWA MBALI NA MALEZI YA WATOTO, BASI VYEMA UKAACHA KUZAA!
ZAMA ZINA KUJA WATOTO WA KIUME WATAONA KUWA NA MADUNGU NI KOSA LA KIUFUNDI!
 
Actually kupeleka mtoto chini ya miaka 12 boarding ni bad parenting.

Kenya wako mbele sana kwenye kufikiri, ni ukabila tu unawatia doa.

Hata mtaala wa elimu ni wa aina yake, sio huu wa kwetu wa kukomalia ufaulu tuu.

Wakenya wakiwa kitu kimoja ni rahisi kutawala Afrika mashariki.
Kenya ya Sasa na katiba waliyo nayo ukabila imeshapitwa na wakati.
Tanzania Kwa Sasa ukabila Upo mkubwa sana. Kinachotusaidia ni dini mbili kubwa uislam na Ukristo ambao mara nyingine udini unavuruga ukabila. Yaani dini inakua ni kabila jipya katikati.

Uchaguzi wa Juzi Kenya umethibitisha kuwa Kenya hakuna ukabila. Siku zote ukabila na udini unajengwa na watawala kwenye katiba kama tuliyo nayo. Ukiwa na katiba ya hovyo na ya kidikteta lazima uwe mkabila au mdini Vinginevyo usalama wako Utakua mdogo.

Ukabila unajitokeza Kwa sababu ya mtu mmoja kuwa na nguvu za teuzi. Kama katiba haimbani mwenye mamlaka ya kuteua ni lazima apendelee wa kwao mana ndio namna ya kuwasaidia Kwa kuwapa nafasi zenye maslahi. Kama ana mtoto Jeshini lazima ampe cheo Cha juu au mtu wa kabila au dini yake ili apate Taarifa za ndani. Ukiwa na katiba ya kifalme halafu ukataka kuwafurahisha wote basi nchi itagubikwa na ubadhirifu kila Kona mana utaogopa kuwatumbua watu na watakua wanakutisha .

Wakenya wameshajikomboa kwenye ukabila na hata udini mana kila mtu sasa ana uhuru wa kumlalamikia yeyote anapoona Kuna uonevu. Kabila Fulani wanaweza kuandamana Kupinga kubaguliwa na isiwe ni uchochezi.

Tanzania hata kama Kuna harufu za udini au ukabila ni kosa la uchochezi Kwa mwananchi wa kawaida kusimama na Kupinga viashiria vya udini au ukabila.

Tundu Lisu alipigwa Risasi baada ya kusema kuwa Serikali ya awamu Ile ilizuia viongozi kusafiri nje ya nchi isipokuwa Roma peke yake na alisema kuwa Roma haikuzuiwa Kwa sababu Rais wa awamu hiyo alikua ni Mroma. Haikupita siku tatu Lisu alipigwa Risasi. Watu wakajidanganya kuwa alipigwa Risasi Kwa sababu sijui za makinikia sijui maelekezo sijui Nini . Hapana kauli ya Kupinga viashiria vya udini vilimponza mana Kuna watu wanaonufaika na upendeleo wa kidini au kikabila. Hawapendi jambo Hilo litoke mana kwao ni faidi kwenye teuzi.
Hapo Mtawala Wala hahusiki ila Chawa ndio wanajichukulia SHERIA mikononi ili kulinda ulaji wao.

Kwa katiba mbovu Kuna watu wanasema Tanzania uongozi uwe wa kupokezana kati ya Waislam na wakristo . Yote ni sababu ya Fursa za uteuzi na kupeana ulaji bila sifa.
Watu wanateuana kama fadhila na kama mashinikizo .
Leo hii Rais wa awamu hii ni muislam Kuna mambo inabidi ayaache yaende hivyo hivyo ili TU asija akalaumiwa kuwa ni mdini.
Kuna wakristo wengi wangepaswa kutumbuliwa na kupelekwa gerezani lakini akifanya hivyo watapenyeza uongo kuwa wanaonewa Kwa sababu ni Wakristo.

Pakiwa Katiba inayopunguza mamlaka ya Rais kuteua kila mtu itawafanya watu waadilifu tuu kuteuliwa bila kujali dini zao.
Kama sio mwadilifu ujue kubaki madarakani kutakupelekea kifungo.
Leo watu wanaiba Mali za umma wanakimbilia kujenga nyumba za Ibada na kutoa masadaka Mengi . HALI INAYOWAFANYA KUONEKANA KUWA NI WATU WA MAANA SANA KWENYE DINI ZAO.
HALIKADHALIKA KWENYE MAKABILA MTU ANAIBA SERIKALINI HALAFU ANAPELEKA JIMBONI KWAKE ANAONEKANA NI WA MAANA SANA. UKIMTUMBUA UNAAMBIWA UTAUA CHAMA MANA JIMBO LAKE BILA CHAMA HAKIPATI KURA NA WATU WANALETA fitina kuwa anatumbuliwa mana ni kabila Fulani na mkubwa ana chuki na kabila Hilo . Ukabila unachukua nafasi ya utetezi na sio uzalendo Tena.
 
Naunga mkono asilimia 99, ijapokuwa kuna waajiriwa /wafanyabiashara wanaosafiri sana na wanapata shida kuwaachia watoto wadada/kaka /ndugu wa karibuu mida hawapo home.
Ila huko shule unako wapelekaaa?
 
Kenya ya Sasa na katiba waliyo nayo ukabila imeshapitwa na wakati.
Tanzania Kwa Sasa ukabila Upo mkubwa sana. Kinachotusaidia ni dini mbili kubwa uislam na Ukristo ambao mara nyingine udini unavuruga ukabila. Yaani dini inakua ni kabila jipya katikati.

Uchaguzi wa Juzi Kenya umethibitisha kuwa Kenya hakuna ukabila. Siku zote ukabila na udini unajengwa na watawala kwenye katiba kama tuliyo nayo. Ukiwa na katiba ya hovyo na ya kidikteta lazima uwe mkabila au mdini Vinginevyo usalama wako Utakua mdogo.

Ukabila unajitokeza Kwa sababu ya mtu mmoja kuwa na nguvu za teuzi. Kama katiba haimbani mwenye mamlaka ya kuteua ni lazima apendelee wa kwao mana ndio namna ya kuwasaidia Kwa kuwapa nafasi zenye maslahi. Kama ana mtoto Jeshini lazima ampe cheo Cha juu au mtu wa kabila au dini yake ili apate Taarifa za ndani. Ukiwa na katiba ya kifalme halafu ukataka kuwafurahisha wote basi nchi itagubikwa na ubadhirifu kila Kona mana utaogopa kuwatumbua watu na watakua wanakutisha .

Wakenya wameshajikomboa kwenye ukabila na hata udini mana kila mtu sasa ana uhuru wa kumlalamikia yeyote anapoona Kuna uonevu. Kabila Fulani wanaweza kuandamana Kupinga kubaguliwa na isiwe ni uchochezi.

Tanzania hata kama Kuna harufu za udini au ukabila ni kosa la uchochezi Kwa mwananchi wa kawaida kusimama na Kupinga viashiria vya udini au ukabila.

Tundu Lisu alipigwa Risasi baada ya kusema kuwa Serikali ya awamu Ile ilizuia viongozi kusafiri nje ya nchi isipokuwa Roma peke yake na alisema kuwa Roma haikuzuiwa Kwa sababu Rais wa awamu hiyo alikua ni Mroma. Haikupita siku tatu Lisu alipigwa Risasi. Watu wakajidanganya kuwa alipigwa Risasi Kwa sababu sijui za makinikia sijui maelekezo sijui Nini . Hapana kauli ya Kupinga viashiria vya udini vilimponza mana Kuna watu wanaonufaika na upendeleo wa kidini au kikabila. Hawapendi jambo Hilo litoke mana kwao ni faidi kwenye teuzi.
Hapo Mtawala Wala hahusiki ila Chawa ndio wanajichukulia SHERIA mikononi ili kulinda ulaji wao.

Kwa katiba mbovu Kuna watu wanasema Tanzania uongozi uwe wa kupokezana kati ya Waislam na wakristo . Yote ni sababu ya Fursa za uteuzi na kupeana ulaji bila sifa.
Watu wanateuana kama fadhila na kama mashinikizo .
Leo hii Rais wa awamu hii ni muislam Kuna mambo inabidi ayaache yaende hivyo hivyo ili TU asija akalaumiwa kuwa ni mdini.
Kuna wakristo wengi wangepaswa kutumbuliwa na kupelekwa gerezani lakini akifanya hivyo watapenyeza uongo kuwa wanaonewa Kwa sababu ni Wakristo.

Pakiwa Katiba inayopunguza mamlaka ya Rais kuteua kila mtu itawafanya watu waadilifu tuu kuteuliwa bila kujali dini zao.
Kama sio mwadilifu ujue kubaki madarakani kutakupelekea kifungo.
Leo watu wanaiba Mali za umma wanakimbilia kujenga nyumba za Ibada na kutoa masadaka Mengi . HALI INAYOWAFANYA KUONEKANA KUWA NI WATU WA MAANA SANA KWENYE DINI ZAO.
HALIKADHALIKA KWENYE MAKABILA MTU ANAIBA SERIKALINI HALAFU ANAPELEKA JIMBONI KWAKE ANAONEKANA NI WA MAANA SANA. UKIMTUMBUA UNAAMBIWA UTAUA CHAMA MANA JIMBO LAKE BILA CHAMA HAKIPATI KURA NA WATU WANALETA fitina kuwa anatumbuliwa mana ni kabila Fulani na mkubwa ana chuki na kabila Hilo . Ukabila unachukua nafasi ya utetezi na sio uzalendo Tena.
This is true
 
Hiyo sheria ni kwa shule zipi za Serikali au private?
Kama inahusisha private schools ni hopeless decision

Mambo mengine washirikishwe wazazi kuamua kipi kiwe kipi sio kukaa ofisini tu na kuamua bila kushirikisha wazazi
kwa hiyo waliokaa ofisini na kuamua sio wazazi?
 
Kenya kuna vitu akili hawana kabisa wajinga sifuri

Mtu mume na mke wote mfano wote wanajeshi mume mwanajeshi yuko kikosi cha Kenya kilichoko Somalia

Mwingine mwanajeshi mwanamke mkewe yuko Kikosi cha jeshi cha Kenya kilichoko kongo

Mtoto wao unapotaka kuwa awe na wazazi wake asiwe bweni asome wapi congo au Somalia day school?

Wakenya kwa hili hopeless kabisa

Unakuta mfano mama changudoa malaya anajiuza chumba anakitumia kujiuza humo humo wanachokaa na mtoto anaishi na mtoto uwanja wa fisi kwa malaya usalama wa huyo mtoto ni bweni

Factors za kupeleka watoto bweni ziko nyingi mno mojawapo ni kuhakikisha mtoto anaondoka eneo hatarishi kwa mtoto

Kuna day mtoto anasafiri umbali mrefu mno kwenda shule

Pia kuna wafugaji huhama hama kutoka eneo moja kwenda lingine ambalo hata shule hizo za day hazipo solution yao ya watoto wao kusoma ilikuwa bweni

Kuna Wakenya Diaspora mume na mke wako nje watoto husomesha Bweni Kenya sababu hawawezi afford kusomesha watoto wao nchi waliko Anataka wasome day ipi? Uamuzi wa kijinga Ruto na serikali yake wa wamefanya

Kenya wamefanya uamuzi wa kijinga sana .Tanzania tusije kuiga.uamuzi huo Utamlipukia puani Ruto sio muda mrefu utelekezaji ukianza.Mark my words.
Kama serikali ndio ineweka utaratibu huo, basi hao wanajeshi wataitaarifu hali yao na watafikiriwa. Hakuna shida ya mazungumzo/taarifa.
Katika Kenya nzima utapata wangapi wenye suala kama hili, ni wachache.
 
Watanzania sio copy cat kwa taarifa yako huo uamuzi wa Kenya wa kijinga na utaleta vurugu Kenya muda si mrefu utelekezaji ukianza tutaheshimisna kuwa Tanzania tuna akili na huwa hatuigi vitu kibwege.

Subiri waanze implementation ndipo utatujua Watanzania tukisema kitu no tuna uhakika.

Ruto hilo kachemka yeye na serikali yake maamuzi ya kukurupuka.
Tulichonacho Tz juu ya elimu ya watoto, kwa kiasi kikubwa tumeiga kutoka Kenya. Hatuna ubunifu.
 
Kama serikali ndio ineweka utaratibu huo, basi hao wanajeshi wataitaarifu hali yao na watafikiriwa. Hakuna shida ya mazungumzo/taarifa.
Katika Kenya nzima utapata wangapi wenye suala kama hili, ni wachache.
Vipi kuhusu watanzania wanaosomesha watoto wao shule za bweni za msingi Kenya?
 
Kwa nini haiwezekani?
Kwanza ni.kuua ushiriki wa sekta binafsi ya elimu kwa shule za msingi za bweni ambazo watu wamewekeza sana kuanzia miundombinu ya chekechea hadi primary

Fikiria from nowhere kiafisa cha serikali ambacho hakijawahi fanya mradi wowote hara wa kuuza fungu la nyanya kimekaa kwenye kiti ofisini unaamka asubuhi kinaaua biashara yako ya shule ya bweni kirahisi tu

Pumbafu kabisa
 
To each their own!

Wanangu watasoma boarding primary haijalishi yatasemwa mangapi.
 
Back
Top Bottom