Serikali ya Mkapa ilipouza NBC Mwalimu Nyerere alilengwa na machozi

Serikali ya Mkapa ilipouza NBC Mwalimu Nyerere alilengwa na machozi

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
20,654
Reaction score
35,887
Heshima sana wanajamvi,

Leo naomba tujikite katika mjadala wa athari za uuzwaji wa NBC kwa kampuni ya ABSA ya Afrika kusini.Miaka ya 90s NBC ilikuwa moja ya bank kubwa sana kusini mwa jangwa la sahara ikimilikiwa na serekali ya Tanzania.Kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali bank hii ilikuwa ikitengeneza faida kubwa sana na si hilo tu bali ilikuwa kikwazo kikubwa kwa bank za nje zilizotaka kufanyabiashara Tanzania.

Moja ya faida kubwa ya NBC ilikuwa ni kuisaidia serekali wakati ilipokuwa ikiitaji fedha kwaajili ya uendeshaji wa shughuli zake za kawaida na hata kugharamia baadhi ya miradi mikubwa.

Mara baada ya Mwl Nyerere kupata taarifa kwamba NBC ipo mbioni kuuzwa alijaribu bila mafanikio kuzuia uuzwaji wa bank hiyo kubwa lakini alifanikiwa walau kuanzishwa kwa bank ya NMB ambayo serekali ina hisa nyingi.

Ni wazi NBC ilikuwa chanzo kikubwa cha mapato ya serekali ya awamu ya kwanza na pili ya Mzee Ruksa kabla ya Rais B Mkapa kuamua kuiza kwa bei ya kutupwa tena kwa kampuni ya nje (mjadala mrefu unatakiwa).

Baada ya chanzo hiki muhimu kuondolewa na Rais wa awamu ya nne je athari zake kwa serekali ya Kikwete ni zipi ?.

Mimi naweka moja ambalo sasa lipo wazi kabisa.Serekali ya Kikwete baada ya kukosa chanzo hiki muhimu cha mapato imevamia mifuko ya hifadhi ya jamii (NSSF,PPF......)Matokeo yake umri wa kustaafu umeongezwa kutoka miaka 55 hadi miaka 60 na sheria nyingine ipo mbioni ambayo italazimisha wafanyakazi watakaoacha kazi au kufukuzwa kazi hawatalipwa mpaka watakapofikisha miaka 60.Mifuko hii ipo taabani kifedha kwakuwa fedha zake nyingi zinanyakuliwa na serekali bila kurejeshwa matokeo yake wachangiaji wa mifuko hii ni kulipwa fedha zisizo endana na hali halisi ya maisha.

Unaweza kuongeza athari nyingine kadri uonavyo.
 
Hiyo mifuko nayo iko mbioni kubinafsishwa ili iwe mali ya mtu/watu fulani na wengine mbakie kuwa wachangiaji tu wa mifuko.
Ila sakata la uuzwaji wa NBC unasura 2 mosi wafanyakazi wa NBC walichangia sana kuifilisi ile benki, mfano unakuta kila baada ya miezi 6 nyumba za wafanyakzai zilikuwa zinabadilishwa fenicha, wafanyakzai walianza kuajiri watu wasiokuwa na sifa kisa tu undugu au mtu kaoa mke hajasoma basi anatafutiwa kazi hadi za usadizi wa mahesabu nk.
Pili Serikali ilipotaka kuuza haikufanya utafiti wa kina future ya mabenki na uchumi wa nchi ulipokuwa unaelekea. Na kulikuwa na harufu ya ufisadi ndani ya uuzwaji wa benki hiyo.


Heshima sana wanajamvi,

Leo naomba tujikite katika mjadala wa athari za uuzwaji wa NBC kwa kampuni ya ABSA ya Afrika kusini.Miaka ya 90s NBC ilikuwa moja ya bank kubwa sana kusini mwa jangwa la sahara ikimilikiwa na serekali ya Tanzania.Kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali bank hii ilikuwa ikitengeneza faida kubwa sana na si hilo tu bali ilikuwa kikwazo kikubwa kwa bank za nje zilizotaka kufanyabiashara Tanzania.

Moja ya faida kubwa ya NBC ilikuwa ni kuisaidia serekali wakati ilipokuwa ikiitaji fedha kwaajili ya uendeshaji wa shughuli zake za kawaida na hata kugharamia baadhi ya miradi mikubwa.

Mara baada ya Mwl Nyerere kupata taarifa kwamba NBC ipo mbioni kuuzwa alijaribu bila mafanikio kuzuia uuzwaji wa bank hiyo kubwa lakini alifanikiwa walau kuanzishwa kwa bank ya NMB ambayo serekali ina hisa nyingi.

Ni wazi NBC ilikuwa chanzo kikubwa cha mapato ya serekali ya awamu ya kwanza na pili ya Mzee Ruksa kabla ya Rais B Mkapa kuamua kuiza kwa bei ya kutupwa tena kwa kampuni ya nje (mjadala mrefu unatakiwa).

Baada ya chanzo hiki muhimu kuondolewa na Rais wa awamu ya nne je athari zake kwa serekali ya Kikwete ni zipi ?.

Mimi naweka moja ambalo sasa lipo wazi kabisa.Serekali ya Kikwete baada ya kukosa chanzo hiki muhimu cha mapato imevamia mifuko ya hifadhi ya jamii (NSSF,PPF......)Matokeo yake umri wa kustaafu umeongezwa kutoka miaka 55 hadi miaka 60 na sheria nyingine ipo mbioni ambayo italazimisha wafanyakazi watakaoacha kazi au kufukuzwa kazi hawatalipwa mpaka watakapofikisha miaka 60.Mifuko hii ipo taabani kifedha kwakuwa fedha zake nyingi zinanyakuliwa na serekali bila kurejeshwa matokeo yake wachangiaji wa mifuko hii ni kulipwa fedha zisizo endana na hali halisi ya maisha.

Unaweza kuongeza athari nyingine kadri uonavyo.
 
Sijaona hoja ya maana kwenye andiko lako mkuu.
 
Hiyo mifuko nayo iko mbioni kubinafsishwa ili iwe mali ya mtu/watu fulani na wengine mbakie kuwa wachangiaji tu wa mifuko.
Ila sakata la uuzwaji wa NBC unasura 2 mosi wafanyakazi wa NBC walichangia sana kuifilisi ile benki, mfano unakuta kila baada ya miezi 6 nyumba za wafanyakzai zilikuwa zinabadilishwa fenicha, wafanyakzai walianza kuajiri watu wasiokuwa na sifa kisa tu undugu au mtu kaoa mke hajasoma basi anatafutiwa kazi hadi za usadizi wa mahesabu nk.
Pili Serikali ilipotaka kuuza haikufanya utafiti wa kina future ya mabenki na uchumi wa nchi ulipokuwa unaelekea. Na kulikuwa na harufu ya ufisadi ndani ya uuzwaji wa benki hiyo.

be realistic man..
usisahau wadeni sugu waliokuwa wanadaiwa MABILIONI. WATAJE AKINA REGINALD MENGI
 
Daa,Nyerere alikuwa na uchungu na mali ya umma. Sasa hivi imeingiliwa na majambazi,manyang'au,maharamia,mafisadi nk yanashinda angani kama mbayuwayu,yamekuwa yakitoa hukumu ya kipilato,yamejigeuza kuwa mahakama kwa kutoa misamaha ya wezi nk.
So sad!
1.Kara Jeremiah-Waambieni
2.Roma mktoliki-Mr President,Tanznia ee mwanangu kuwa uyaone
 
Hiyo mifuko nayo iko mbioni kubinafsishwa ili iwe mali ya mtu/watu fulani na wengine mbakie kuwa wachangiaji tu wa mifuko.
Ila sakata la uuzwaji wa NBC unasura 2 mosi wafanyakazi wa NBC walichangia sana kuifilisi ile benki, mfano unakuta kila baada ya miezi 6 nyumba za wafanyakzai zilikuwa zinabadilishwa fenicha, wafanyakzai walianza kuajiri watu wasiokuwa na sifa kisa tu undugu au mtu kaoa mke hajasoma basi anatafutiwa kazi hadi za usadizi wa mahesabu nk.
Pili Serikali ilipotaka kuuza haikufanya utafiti wa kina future ya mabenki na uchumi wa nchi ulipokuwa unaelekea. Na kulikuwa na harufu ya ufisadi ndani ya uuzwaji wa benki hiyo.


wafanyakazi hawahusiki kabisa katika hili,sema tu serikali ilishindwa kulisimamia ipasavyo.utaajirije mtu hana sifa?serikali iko wapi?
 
Heshima sana wanajamvi,

Leo naomba tujikite katika mjadala wa athari za uuzwaji wa NBC kwa kampuni ya ABSA ya Afrika kusini.Miaka ya 90s NBC ilikuwa moja ya bank kubwa sana kusini mwa jangwa la sahara ikimilikiwa na serekali ya Tanzania.Kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali bank hii ilikuwa ikitengeneza faida kubwa sana na si hilo tu bali ilikuwa kikwazo kikubwa kwa bank za nje zilizotaka kufanyabiashara Tanzania.

Moja ya faida kubwa ya NBC ilikuwa ni kuisaidia serekali wakati ilipokuwa ikiitaji fedha kwaajili ya uendeshaji wa shughuli zake za kawaida na hata kugharamia baadhi ya miradi mikubwa.

Mara baada ya Mwl Nyerere kupata taarifa kwamba NBC ipo mbioni kuuzwa alijaribu bila mafanikio kuzuia uuzwaji wa bank hiyo kubwa lakini alifanikiwa walau kuanzishwa kwa bank ya NMB ambayo serekali ina hisa nyingi.

Ni wazi NBC ilikuwa chanzo kikubwa cha mapato ya serekali ya awamu ya kwanza na pili ya Mzee Ruksa kabla ya Rais B Mkapa kuamua kuiza kwa bei ya kutupwa tena kwa kampuni ya nje (mjadala mrefu unatakiwa).

Baada ya chanzo hiki muhimu kuondolewa na Rais wa awamu ya nne je athari zake kwa serekali ya Kikwete ni zipi ?.

Mimi naweka moja ambalo sasa lipo wazi kabisa.Serekali ya Kikwete baada ya kukosa chanzo hiki muhimu cha mapato imevamia mifuko ya hifadhi ya jamii (NSSF,PPF......)Matokeo yake umri wa kustaafu umeongezwa kutoka miaka 55 hadi miaka 60 na sheria nyingine ipo mbioni ambayo italazimisha wafanyakazi watakaoacha kazi au kufukuzwa kazi hawatalipwa mpaka watakapofikisha miaka 60.Mifuko hii ipo taabani kifedha kwakuwa fedha zake nyingi zinanyakuliwa na serekali bila kurejeshwa matokeo yake wachangiaji wa mifuko hii ni kulipwa fedha zisizo endana na hali halisi ya maisha.

Unaweza kuongeza athari nyingine kadri uonavyo.

Mkuu lakini Nyerere ndiye aliyempigia Mkapa kampeni kwa nguvu nchi nzima kuwa ndiye msafi aliyebaki CCM
 
Hii benki kwa hali ilivyofikia ingekufa tu, usimamizi ulikuwa zero kila mwenye cheo ndani ya benki hiyo alikuwa anaamua lolote atakalo, na mbaya zaidi serikali iliigeuza kuwa ndio shamba lake la kuvuna bila kupanda. Tatizo kubwa ni mchakato wenyewe wa uuzwaji serikali haikuchanganua wala kufikria kwa kina, yaani naweza kusema ilikurupuka tu bila kutafakari. Lakini ilikuwa lazima iuzwe.
 
serikali haiwezi kufanya biashara na benki ile ni ya biashara, isingeweza kusimamia benk ile baada ya kukubali soko huria labda kama tungekuwa na sheria kama za china kuwaadabisha watendaji ndio benk ile ingeweza endeshwa na serikali.
 
Mkuu Dr. Ngongo.

Hoja ni nini Mkapa kuiuza NBC wakati wa Nyerere au serikali kuchukuwa pesa kwenye mifuko ya fedha.

Kama suala serikali kuchukuwa pesa kwenye mifuko ya fedha kwa matumizi yake mpaka hata wakati wa Nyerere, NBC ilikuwepo lakini bado serikali ilikuwa inachukuwa pesa kwenye mifuko kama PPF, na mashirika ya umma kama BIMA, POSTA na mengineyo mpaka yakafirisika.

Kigezo cha kuongeza umri wa kustaafu mimi nadhani akina uhusiano na kuuzwa NBC.
 
Last edited by a moderator:
Ndio maana Mwl Nyerere alikufa kabla ya wakati wake.

Mkuu lakini Nyerere ndiye aliyempigia Mkapa kampeni kwa nguvu nchi nzima kuwa ndiye msafi aliyebaki CCM
 
Ndio maana Mwl Nyerere alikufa kabla ya wakati wake.
Kali zaidi iikuwa ni KIWANDA CHA SIGARA, kiliuzwa kwa 700m bei ambayo hata adhi tu inayokaliwa na majengo ya kiwanda hicho ilkwa inazidi hiyo 700m. Ama kweli MKAPA, alichangia kumuua Nyerere, mapema zaidi!!!
 
Kipindi hicho TISS walikujana na kauli mbiu ya kuwaadaa waTanganyika "Mr Clean" kumbe alikuwa bomu la maangamizi ya ustawi wa wananchi.

Kali zaidi iikuwa ni KIWANDA CHA SIGARA, kiliuzwa kwa 700m bei ambayo hata adhi tu inayokaliwa na majengo ya kiwanda hicho ilkwa inazidi hiyo 700m. Ama kweli MKAPA, alichangia kumuua Nyerere, mapema zaidi!!!
 
wakati ule ukiondoa mengi na diallo wakopaji wengine walikuwa wahindi na waarabu tu.
 
Back
Top Bottom