Serikali ya Tanzania yasema Nemes Tarimo alihukumiwa miaka 7 jela, akafariki akiwa vitani

Hujuwi kilicho nyuma ya pazia Bora ukae kimya tetesi ni nyingi kuliko unayo yasikia. Why tetesi? Ask deep state
Sasa mkuu.. nyuma ya pazia kwamba katumwa na serikali ya Tanzania au ni vip?

Ama labda alilazimishwa kuingia Wagner?

Tujaribu kuwa objective kidogo kwenye hii issue..

Mbona Ukraine mpaka Navy Seal wa marekani kauawa na wala hatuoni wamarekani wakianza kujiuliza.

Sasa huyu wetu hakuwahi hata kuwa mwanajeshi huku kwetu.. kwanini iwe issue?
 
Huyo Jamaa alikuwa yupo mahabusu before kuambiwa salama yake iloyopo nukujiunga na Hilo jeshi uchwara.
Hili watu wengi wanaonekana kulipinga ikiwemo familia yake pia

Inavyoonekana huko waafrika wanalazimishwa kwenda vitani na inapotokea bahati mbaya wameuwawa, wanatoa taarifa kuwa alikuwa mfungwa

Fatilia kifo cha yule kibopa wa Malawi sijui Zambia alivyokufa ripoti ni ile ile kama hii

Bado kuna m-algeria mwingine naye alidanja vitani kwa tuhuma hizo hizo
 
Sure, ni kutaka kukuza mambo tu kwa watu wa ulaya na Us.

Wanaopigana Kongo na kufa mbona hawapewi airtime?
 
Hizi ni made up stories... ushahidi kwamba wanalazimishwa upo wapi?... mimi sitetei upande wowote.. ila nachotaka hapa ni watu tuwe objective
 
Kifo ni haki ya kila binadamu.. Huyo Nemes sijui ashukuru tu hata kutangazwa na serikali na kuagwa huko urusi. Hata angerudi mzima huenda Angekuwa Kama DK Shika...
 
Hizi ni made up stories... ushahidi kwamba wanalazimishwa upo wapi?... mimi sitetei upande wowote.. ila nachotaka hapa ni watu tuwe objective
Ingekuwa ni madeup stories serikali za Zambia isingedai kupewa majibu zaidi ya ile taarifa waliyo publish moscow

Waafrica wengi waishio huko wameripoti kubaguliwa pamona na kulazimishwa kwenda vitani

Hata kile kipindi Ukraine ihamishe raia, waafrika walikuwa wanatupwa nje ya treni.

Sasa kama unaona ni stori za kutungwa jaribu kwenda
 

Kwani mpaka sasa kuna Watanzania/Waafrika wangapi ndani ya Urusi, na wangapi wamelazimishwa kwenda vitani...
 
Serikali inalaumiwa kwa kutoiwajibisha Russia hasa balozi wake hapa Tz atoe maelezo kwa nini jamaa ambaye alikuwa mfungwa kwenye jela za serikali ya urusi achukuliwe na kuandikishwa kupigana nchini Ukraine kwa kupitia kikundi cha wanamgambo kiitwacho Wagner?Je sheria za kimataifa zinazolinda haki za wafungwa zinaruhusu kitu hicho
 
Kwani mpaka sasa kuna Watanzania/Waafrika wangapi ndani ya Urusi, na wangapi wamelazimishwa kwenda vitani...
Mi siyo karani wa sensa wa urusi

Nayoyaandika ni yale nayokutana nayo kwenye habari za huko Russia watu wakisimulia mikasa wanayokumbana nayo
 
Huyo Jamaa alikuwa yupo mahabusu before kuambiwa salama yake iloyopo nukujiunga na Hilo jeshi uchwara.
Kwanini vijana wengi wa kiafrika waliopo Urusi wanafungwa sana?! Nini kipo nyuma ya hili jambo?! Wanafanya uhalifu au wanabambikiwa kesi na kufungwa ili kuipa fursa Urusi kuwalazimisha kujiunga na jeshi lake la kimamluki?
 
Sahihi
 
Chadema inapeleka watu wake mafunzoni, wanafia huko, wanajigamba kwamba watu wao makamanda, wanapimwa field,wanakufia huko, trainers wanasema nyie badooo kwa JWTZ
 
Apumzike tu kwa amani. Namna yake ya kuondoka Duniani ilipangwa hivyo. Amekamilisha aliyoumbiwa
 
Ni kinyume na katiba ya nchi mtanzania kujiunga na kikubdi cha kijeshi au jeshi nje ya tz
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…