Serikali ya Wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(DARUSO) waomba radhi

Serikali ya Wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(DARUSO) waomba radhi

Hilo Tangazo limelazimishwa na Ndarichako kwenda kwa Mkuu wa chuo akalazimisha pia viongozi waliobaki waweke wagonge mhuri..
Bado vijana wanasisitiza kupewa chao
IMG_20191219_112736.jpg

 
Watambue wapi, wamepangwa waombe radhi ili kuhadaa umma kwamba wamejiona wana makosa. Ukweli ni kuwa kama wasingetishia kuandamana wasingepata kitu. Bila kupanga maandamano ingekuwa kwao. Haki haiombwi bali hudaiwa.
Kama hawajatambua waingie barabarani tuone
 
!
!
DARUSO hii misheni waliikosea tangu mwanzo. Walitakiwa kufanya harakati hizi kupitia kwa mkuu wa mkoa wa dar au tawi la sisiemu vyuo vikuu. Wao wameamua kutumia DARUSO Tena bila kuanza na utetezi kwa Mtukufu.
 
Upuuzi umewajaa hawa watoto,nadhani sasa wameanza kupevuka kiakili,huwezi kuipa 72 hrs serikali inayokusomeshwa na kukugharamia kila kitu,huu ni ujangili ,pongezi kwa government yetu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watambue wapi, wamepangwa waombe radhi ili kuhadaa umma kwamba wamejiona wana makosa. Ukweli ni kuwa kama wasingetishia kuandamana wasingepata kitu. Bila kupanga maandamano ingekuwa kwao. Haki haiombwi bali hudaiwa.
Msiwatishe wanafunzi serikali imetoa fedha na Rais alishasema hakuna kucheleweshea wanafunzi mikopo yao...halafu kuna toyboy mmoja anatumia madaraka yake vibaya kwa kutamka wanafunz wafukuzwe chuo. ...
 
Yaani madogo mnatia hasira kweli mwenzenu kawatetea mpaka wameanza kuwashughulikia wamemtimua chuo hamna hata habari naye eti mnaomba msamaha kwa kudai haki yenu pathetic kwa viongozi kama hawa wangekuwepo enzi hizo za utumwa mpaka leo tungekuwa tumetawaliwa

Hiyo barua sio ya hao vijana, imeandikwa na hao hao waliogoma kutoa vyuma, ole wa hao wanafunzi waseme hawaijui hiyo barua lazima waelee kwenye viroba hapo beach.
 
Watoto wa sahivi ni wasela mavi, wanavuta bangi zao gizani wanakuja kutishia baba mwenyenyumba anayewalisha.
 
Wamechelewa sana, inasikitisha baada ya wezao kusimamishwa, waliobaki kwenye serikali ya wanafunzi wamewasaliti wezao Rais wa chuo akiwemo.
Hii migomo ya vyuoni kama watumwa. Wakifukuzwa baadhi ya viongozi waliobaki wanafuata matakwa ya chuo na kusalita malengo.
 
Yaani madogo mnatia hasira kweli mwenzenu kawatetea mpaka wameanza kuwashughulikia wamemtimua chuo hamna hata habari naye eti mnaomba msamaha kwa kudai haki yenu pathetic kwa viongozi kama hawa wangekuwepo enzi hizo za utumwa mpaka leo tungekuwa tumetawaliwa
madogo wase/nge sana aisee, yaani ni usaliti wa hali ya juu
 
Back
Top Bottom