Tetesi: Serikali yadaiwa kumvua uraia Padri wa Kanisa Katoliki

kama wewe ni mtanzania,huwezi kushindwa kuonesha walipozikwa wazee wako,muite Helsinki nae awe mkimbizi wa kiuchumi
Kwani viongozi walio tangulia hawakuwa wanawajua kuwa ni warundi?mbona kuna wasomali wamejaa lkn hamuwaandami kiasi hicho?
 
Zamani makaburi yalikuwa hayajengewe kama sasa. Utakuta wameshajenga majumba ama shamba la mazao. Kwa wale wenyeji wa Arusha ilipo stand ndogo ilikuwa eneo la makaburi ya serikali kwa sasa ni stand ya vihaice pamoja na maduka ukute sasa babu yako alizikwa hapo sijui utaonyesha nini
 
Kigoma ni lazima iangaliwe kwa jicho pevu kwa sababu ni sehemu muhimu sana kwa usalama wa nchi yetu. Tusilaumu tu kwa sababu za kisiasa. Usalama wa Tanzania ni mihimu kuliko chochote ukijuacho. Tanzania inazungukwa na nchi jirani za Msumbiji, Malawi, Zambia, DR Congo, Burundi, Rwanda, Uganda na Kenya. Lakini kati ya hizo zote Burundi na Congo ziko kwenye hali tete kiusalama na zote hizo ziko karibu sana na mkoa wa Kigoma. Hapo unaweza kuona umuhimu wa kiusalama kwa mkoa wa Kigoma. Lakini pia Kigoma ndo mkoa pekee wenye lango linalounganisha nchi tatu za nje ambazo ni Burundi, Congo na Zambia hivyo kuwa na uwezekano mkubwa wa kuwa na wageni wengi wasio raia. Hivyo basi kwa kila raia wa Tanzania anayetoka Kigoma lazima uwe nae makini sana kwani anaweza kuwa katoka nje ya nchi akajifanya anatoka Kigoma.

Lakini pia mkoa wa Kigoma unapakana na nchi zenye matatizo ya kiuchumi kiasi kwamba raia wengi wa nchi hizo hupenda sana kukimbilia Kigoma kutafuta kazi na vibarua vya kufanya kukidhi mahitaji yao. Ni kama ilivyo kwa South Africa inavyovutia wahamiaji wengi kutoka nchi zote za kusini mwa Africa.
Mimi ni mzaliwa wa Kigoma nafahamu maisha ya huko. Mara nyingine kumtofautisha muha wa Muyama kwetu na Kayogoro au Makamba Burundi inakuwa vigumu sana. Ama kumtofautisha Mbembe wa Helembe, Sunuka, Sibwesa na Mbembe wa Moba, Baraka na hata Kalemii au Uvira Congo inakuwa vigimu.

Ni kwa misingi hiyo kama nchi huru tunapaswa kuwa waangalifu kwenye uraia wa wananchi wetu.
Watu wa Kigoma sisi kama raia halal wa nchi hii tunao wajibu wa kuilinda mipaka yetu na kuwachunguza watu wasio raia miongoni mwetu.
Hatuna nchi nyingine Tanzania ndo nchi yetu.
Nchi jirani nao wana utaratibu wao wa kuwashughulikia watu wasio raia wa nchi zao.
Kigoma tusigombanishwe na serikali yetu na wajinga wachache kwamba serikali haitupendi. Tuendelee kuipenda na kuilinda nchi yetu kuanzia Mashariki mpaka Mafharibi na kutoka Kusini mpaka Kaskazini.

Karibuni kijijini kwetu Muyama mpakani kabisa na Burundi.
Aksante.
 
Unafikiri nani anatakiwa kulaumiwa juu ya hilo, wavamizi au watendaji wa serikali?
Uhamiaji walikuwa wapi hadi hao watu wanaingia nchini hadi kupata nafasi ya kuwa viongozi wa kiroho?
 
Inauma miongoni mwa Mapadre ninaowapenda na kuwakubali sana Ni katibu Mkuu Padre Raymond Saba inauma sana unafiki wa baadhi ya Maaskofu wakatoliki kuficha na kushindwa kuusema ukweli huyo anaeagiza wahoji uraia ni raia wa wapi
SIKU MOJA DINI ZITAKUFA NA NDIPO DUNIA ITAKUWA SALAMA.
 
Inauma miongoni mwa Mapadre ninaowapenda na kuwakubali sana Ni katibu Mkuu Padre Raymond Saba inauma sana unafiki wa baadhi ya Maaskofu wakatoliki kuficha na kushindwa kuusema ukweli huyo anaeagiza wahoji uraia ni raia wa wapi
Warundi wanawafukuza watanzania nchini kwao
 
Kila likija hili swala la uraia najaribu kwenda kutembelea walipolala babu na bibi zangu (makaburini) ili nisije kupasahau .
 
Msaidie kupata asylum nae aishi huko ughaibuni!
nitakuwa wa mwisho kuamini kwamba upo sawa kichwani wewe. kichwa kimejaa usaha kama wale wabunge kina waitara wanaohama vyama kisa tu ya kumkomoa mbowe bila kusahau kuwa wengine waliwachagua bila hata kuwa na vyama. jitafakari mkuu. hata kama uligelezea mitihani lakink ficha kudesa kwako huku kwenye mitandao
 
Niwakati muafaka kwenda kulitafuta na kuliimarisha kaburi la Babu.
 
Huyu mh t atawamaliza wenzao ila walisema wachaga in watu wa baya
 

Na kama siyo raia kweli serikali imekosea nini???!!!
 
Wengine hat kuwa na utaratibu wa jujengea makaburi, yale matuta yamesha titia. Tutainyesha nini?
 
unaweza kua sahihi,lakini huyo padri ni mrundi,hapo hata akipiga novena itamrudia hakuna dhulma hapo,ametendewa haki
Tanzania ndio nchi pekee dunia,mgeni anaweza kujichanganya na raia,akapata pasi na kadi ya kura akajifanya mtanzania
Mlijua lini kuwa ni Mrundi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…